Nimekusikia bungeni waziri ukisema mtajitahidi kufanya kila linalowezekana kupata wataalamu wa Counselling
Kwa taarifa yako baadhi ya walimu wamesomea unasihi yaani counselling mimi nikiwa mmoja wao nina shahada lakini hata hivyo tulipoleta vyeti tukaambiwa shahada yenu haitambuliki. Hivyo tunahesabiwa kama hatukusoma.
Baada ya kuona hivyo baadhi ya walimu wameacha kazi na kwenda kufanya kazi kwenye mashirika mbalimbali. Counselling ni muhimu sana katika jamii hasa mashuleni, hospitalini, katika majeshi, katika jamii nk. Leo hii vijana wanaiga mambo kwa vile tu wamekosa kujiamini, hivyo wanajiingiza katika ulevi, umalaya nk kumbe counsellors wanaouwezo wa kuwasaidia na kupata jamii iliyo bora.
Matatizo mengi ya jamii hutokana na matatizo ya kisaikolojia. Hivyo waziri agiza shahada zetu zitambuliwe ili tufanyie kazi taaluma hii muhimu maana kwa sasa tumekaa kimya wala hatutumii taaluma hizo.
Kwa taarifa yako baadhi ya walimu wamesomea unasihi yaani counselling mimi nikiwa mmoja wao nina shahada lakini hata hivyo tulipoleta vyeti tukaambiwa shahada yenu haitambuliki. Hivyo tunahesabiwa kama hatukusoma.
Baada ya kuona hivyo baadhi ya walimu wameacha kazi na kwenda kufanya kazi kwenye mashirika mbalimbali. Counselling ni muhimu sana katika jamii hasa mashuleni, hospitalini, katika majeshi, katika jamii nk. Leo hii vijana wanaiga mambo kwa vile tu wamekosa kujiamini, hivyo wanajiingiza katika ulevi, umalaya nk kumbe counsellors wanaouwezo wa kuwasaidia na kupata jamii iliyo bora.
Matatizo mengi ya jamii hutokana na matatizo ya kisaikolojia. Hivyo waziri agiza shahada zetu zitambuliwe ili tufanyie kazi taaluma hii muhimu maana kwa sasa tumekaa kimya wala hatutumii taaluma hizo.