Waziri wa afya kikaangoni!

Waziri wa afya kikaangoni!

Usifikiri uko peke yako hapa Dodoma hakuna kitu unachotuambia labda kama unataka kuongeza namba ya thead zako
 
David Mwakyusa ilimshinda pamoja na uprofesa wake katika fani ya tiba ndio iwe ajabu kwa Dr Haji Mponda.. Wizara hii ni ngumu na wakati mwingine unarithi matatizo ya watangulizi wako.
 
kimsingi ni lazima mtu awajibike,wananchi wameteseka na kufa kwa sababu ya uzembe wake.

Migogoro ya wizara hii haitokani na uongozi peke yake. Tunaweza kubadilisha viongozi hata mara 100 bila mafanikio ni budi tuangalie kwa mapana yake.
 
Migogoro ya wizara hii haitokani na uongozi peke yake. Tunaweza kubadilisha viongozi hata mara 100 bila mafanikio ni budi tuangalie kwa mapana yake.
Sasa Raia Mwema unashauri nini? Hiyo wizara iachwe iendelee hivyo?
 
Jairo ameingia lini kwenye fani ya udaktari? anzisha thread ya Jairo.

Mbona unatumia nguvu kubwa kiasi hiki?una maslahi gani kwenye sakata hili?ila hongera unajitahidi sana katika kupambana.
 
Mbona wamekuwa vigeugeu juzi walikuwa wamemkaba shingo Dr. Kigwangwala leo waziri?
Kuna umuhimu wa Lowasa kuchukua nchi 2015

huyo lowasa mzushi tu anatafuta umaarufu kila siku yupo bungeni lakini haongelei matatizo ya vijana,akienda kwenye harambee za makanisa ndio anaanza kulalama hayo mabomu yanayosubiri kulipuka
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Mh Hadji abaki ila blandina, Nkya na mtasiwa waondoke
 
Kwanini tusiache mambo yatokee (hasa linapokuja suala la ccm na watu wake) kuliko kutabiri vitu ambavyo baadae inaonekana ni porojo tu?
Tukaambiwa habari za Kigwangala, ikawa upuuzi tu, hii ni kuifanya JF kuwa kijiwe cha watu wenye akili za Sheikh Yahya!
 
Migogoro ya wizara hii haitokani na uongozi peke yake. Tunaweza kubadilisha viongozi hata mara 100 bila mafanikio ni budi tuangalie kwa mapana yake.
migogoro ya wizara hii inatokana na nini?
 
Kama sababu za kiutendaji zipo za kumuondoa madarakani basi ataondoka,yuko wapi Jairo leo?? hakuteuliwa na wabunge yule... Ilianza tu kwa hoja ya Beatrice Shelukindo,lolote laweza kutokea....tusubiri!

Nafikiri kama sio public outcry, watu bado wangekuwa wanalisukuma gari la Jairo.
 
Nafikiri kama sio public outcry, watu bado wangekuwa wanalisukuma gari la Jairo.

Hii ya madaktari ni zaidi ya Jairo sana EMT....wakisikiliza wananchi wao,wabunge watampa wakati mgumu sana JK,manake itambidi pia kumuondoa na Katibu Mkuu anayelalamikiwa sana na pengine hata waziri mkuu mwenye kutoa majibu mepesi kwenye masuala magumu sana na yanayotesa wananchi wengi!
 
Jitahid bwana ila nahsi hawana lolote wauaji wakubwa hao.
 
Kumfukuza waziri haitasaidia chochote, turudi nyuma na kuangalia mfumo mzima wa AFYA na ELIMU nchini. Mtasema weee mkiukwepa ukweli lakini swala litabakia pale pale. Uongozi wa JK umeshindwa ktk ngazi zote za uongozi kwa sababu mfumo mzima wa kiutawala unakumbatia UFISADI na yeyote utakayemweka ktk nafasi hizo atajua hawajibiki.. Tukubali sote tumeshindwa na tunataka mwanzo mpya. tunataka mabadiliko - CHANGE, na hakuna atakayeweza kuyaleta mabadiliko haya isipokuwa wewe, mimi na Watanzania wengine wote ambao wanaipenda nchi yao kwanza.

Najua sana kwamba mara nyingi hutofautiana na watu wengi na wengine huniona mpuuzi lakini ukweli umesimama kwamba tatizo ni sisi wananchi na suluhu ni sisi wananchi kuweka Uzalendo mbele ya kila kitu..Na bahati mbaya natambua taratibu kwamba hata wasomi wetu wamesoma sana lakini hawaelewi maana zaidi ya Unafiki mbele. Sidhani kama kuna mtu hapa anaweza kunambia kwa nini mwaka 1992 ktk kura za maoni wananchi wengi walipinga mfumo wa vyama vingi wakati rohoni mwao walitaka kuwepo kwa vyama vingi?..

Jamani tuache unafiki tuippende nchi yetu na tuwe tayari kujitoa mhanga ktk kutetea maslahi ya Taifa na sii kutazama rangi zetu...
 
Kama sababu za kiutendaji zipo za kumuondoa madarakani basi ataondoka,yuko wapi Jairo leo?? hakuteuliwa na wabunge yule... Ilianza tu kwa hoja ya Beatrice Shelukindo,lolote laweza kutokea....tusubiri!

ndugu usijidanganye, issue ya jairo na hili la waziri wa afya ni mmbo mawili tofauti kabisa. La waziri liko bungenu na kamwe ccm haiwezi kujivua nguo ndani ya bunge. walijaribu hivyo kwa EL wakaaibika sana. Jiulize why hawataki kutekeleza maazimio ya mwakayembe hadi leo?

Kwa magamba ni heri watu wafe lakini sio kukimaliza chama ndani ya bunge!
 
Magamba tokea lini wakawa seriouz na maswala yanayohusu maslahi ya taifa.Yaliyotokea kipindi kile kwa EL ilikuwa ni maslahi binafsi kwa kundi la kina Sita ,wakitaka kukomoana kuwa kundi gani lina nguvu.
 
Pinda yeye alichodhani, kwa akili yake, ni kwamba mkwara ungesaidia madokta kutenda kazi, kumbe hali ndo imekuwa mbovu kabisa. Alisahau kale kamsemo kuwa unaweza kumburuza ng'ombe hadi mtoni lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji.......ni hiari yake
 
Kubadrisha sura ya mtu kwa matatizo ambayo yanatokana na utawala mbovu ni kupoteza muda wa kujiuzuru ni kinara wa dora nchi imekuwa mzigo kwake.
 
Back
Top Bottom