Waziri Nape kwanini husemi ni vigezo gani ambavyo Starlink hawajatimiza? Au wamegoma sharti la kuzima mtandao muda wowote mkiamua?

Cute Wife

Senior Member
Nov 17, 2023
176
486
Akiwa anahojiwa kutoka katika televisheni ya Wasafi (Wasafi TV) Waziri Nape amesema kuwa serikali haina matatizo na Starlink, kinachofanya washindwe kutoa huduma zao nchini ni sababu hawajakamilisha masharti, na kama wakikamilisha basi wataruhusiwa kutoa huduma nchini.

Msikilize hapa


====
"Nimezungumza hapa, kama nchi tunamchakato wa kuwa na Satelite ambao tutaukamilisha mapema tu, iwe ni alternative yah hizi cable. The best ni cables lakini satellite ni njia mojawapo, na Starlink ni kama watoa huduma wengine ambao wanaleta huduma za mawasiliano walikuja wakaomba leseni.

"Sasa mfumo wetu wa lesseni unaoingia kwenye mtandao kidijitali unajaza taarifa mbalimbali, sasa baadhi ya nyaraka walikuwa hawana, kwahiyo walipoenda wakafika mahali wakagota na nyaraka zile hawana, sisi tuliwaambia kamilisheni. Wakikamilisha maombi yao na yakaletwa mezani kwangu siku hiyo hiyo nasaini, hatuna matatizo nao.

"Nasikia watu wanasema wamezuiwa, hatujazuia mtu. Tumewaambia kamilisheni utaratibu. Hatuwezi kubadilisha taratibu tulizoziweka ambazo watoa huduma wote wamezifuata kwasababu ya mtu mmoja ambaye hana cheti chake cha form four sijui cha wapi. Fuateni utaratibu tu na kila kitu kipo mtandaoni wala hauitaji kwenda kusoma. Kwahiyo wakikamilisha watakuja.

"Lakini hata baadhi ya nchi ambazo wanapata huduma hiyo ya Starlink na wenzake ni katika nchi zilizoathirika. Kwahiyo kwenda kudanganyana kwamba eti ndio suluhu la mwisho kabisa, tunadanganyana. Mimi najua katika nchi 11 karibia nchi 2..3 zinapata huduma na zimeathirika."
====

Ni masharti gani hayo yanayosemwa kila mara kuwa Starlink hawajatimiza? Yaani Nape anataka kutuamisha kabisa kuwa Starlink wamekosa cheti cha kutoa hudumu nchini?

Wameweza kukamilisha documents kwa nchi nyingine halafu ndio washindwe kukamilisha kutoa documents Tanzania, nchi ndogo ambayo inajikongoja kwenye karibu kila kitu?

Nape tuambie ukweli, acha kuzunguka zunguka, ukiangalia uchaguzi mkuu upo puani na historia imetufundisha vyema vile mnatufanyia wananchi linapokuja suala la mtando.

Kwa ninavyoona Serikali itakuwa imetoa sharti kwa Starlink na Elon Musk kuzima mtandao kila serikali itakapotoa agizo hilo, na kwakuwa Elon ni champion wa uhuru wa kujieleza akawatolewa nje basi na nyie serikali mkashupaza shingo.

Inaonesha mwakani ngoma nzito kiasi kwamba mko tayari hata kuacha taifa liingie hasara ya mabilioni ya pesa sababu ya kukosekana kwa internet ili tu mjihakikishie kuendelea kubaki madarakani.

Wakuu, maonaje kuhusu hili? Sababu hii ina mashiko? Kama haina mashiko unafikiri ni sababu gani au document gani ambayo Sterlink wameshindwa kutimiza ili wapewe leseni ya kuhuduma ya mtandao nchini?
 
Starlink ni ghali.

Huko Kenya gharama za kununua vifaa ni sawa na Tsh1.7m

Kifururushi cha chini kabisa Tsh130k/mwezi

Ipo Kenya karibia mwaka ila wanaotumia hawafiki 3000. Sasa utatobokaje mfuko wakati providers wengine kama zuku wanakupa huduma kwa bei che?

Mimi naona Nape atakua anashirikiana na kina voda ambao hawataki kupoteza wateja wao wakubwa, starlink itawaiba hao maskini hawatoimudu
 
starl.PNG


starlink.PNG


Mleta mada unatakiwa kufahamu kila nchi inataratibu zake

ebu jionee taarifa katika mtandao wao rasmi...

jiulize mbona wengine wamewahi? na wengine wamechelewa kama sisi?


Afrika ina Nchi zaidi ya 50, ni nchi chache sana zimeingia mkataba wa huduma
1. Kenya
2. Rwanda
3. Msumbiji
4. Malawi
5. Zambia
6. Nigeria nk

tunachakujifunza kutoka katika hizo nchi kwa tukio lililotokea hivi karibuni... je starlink alisaidia? na takwimu zinasemaje? ghrama katika hizo nchi zipoje? mikataba katika hizo nchi je? ilitufahamu kama huyu mwamba anamikataba ya kibeberu na usalama wa nchi je?

je tuna haja ya kufata njia ya china kutengeneza setellite zetu katika eneo hili? au tuemdelee kuwa tegemezi? na kumlilia muwekezaji?

wananchi tunatakiwa kujua tunataka nini? tuendelee kuishi utumwani misri au tuendelee na safari kuelekea nchi ya ahadi (ya maziwa na asali)??


 
View attachment 2990761

View attachment 2990762

Mleta mada unatakiwa kufahamu kila nchi inataratibu zake

ebu jionee taarifa katika mtandao wao rasmi...

jiulize mbona wengine wamewahi? na wengine wamechelewa kama sisi?


Afrika ina Nchi zaidi ya 50, ni nchi chache sana zimeingia mkataba wa huduma
1. Kenya
2. Rwanda
3. Msumbiji
4. Malawi
5. Zambia
6. Nigeria nk

tunachakujifunza kutoka katika hizo nchi kwa tukio lililotokea hivi karibuni... je starlink alisaidia? na takwimu zinasemaje? ghrama katika hizo nchi zipoje? mikataba katika hizo nchi je? ilitufahamu kama huyu mwamba anamikataba ya kibeberu na usalama wa nchi je?

je tuna haja ya kufata njia ya china kutengeneza setellite zetu katika eneo hili? au tuemdelee kuwa tegemezi? na kumlilia muwekezaji?

wananchi tunatakiwa kujua tunataka nini? tuendelee kuishi utumwani misri au tuendelee na safari kuelekea nchi ya ahadi (ya maziwa na asali)??
Kama umesikiliza video hiyo ya Nape vyote hivyo ulivyoandika hapa sio tatizo, shida ni hiko ambacho hawajatimiza, je ni nini? Kwanini hakisemwi?
 
View attachment 2990761

View attachment 2990762

Mleta mada unatakiwa kufahamu kila nchi inataratibu zake

ebu jionee taarifa katika mtandao wao rasmi...

jiulize mbona wengine wamewahi? na wengine wamechelewa kama sisi?


Afrika ina Nchi zaidi ya 50, ni nchi chache sana zimeingia mkataba wa huduma
1. Kenya
2. Rwanda
3. Msumbiji
4. Malawi
5. Zambia
6. Nigeria nk

tunachakujifunza kutoka katika hizo nchi kwa tukio lililotokea hivi karibuni... je starlink alisaidia? na takwimu zinasemaje? ghrama katika hizo nchi zipoje? mikataba katika hizo nchi je? ilitufahamu kama huyu mwamba anamikataba ya kibeberu na usalama wa nchi je?

je tuna haja ya kufata njia ya china kutengeneza setellite zetu katika eneo hili? au tuemdelee kuwa tegemezi? na kumlilia muwekezaji?

wananchi tunatakiwa kujua tunataka nini? tuendelee kuishi utumwani misri au tuendelee na safari kuelekea nchi ya ahadi (ya maziwa na asali)??
Ukifika nchi ya ahadi niite nitakuja. Chini ya hapo ni pwagu na pwaguzi tuuu.
 
Starlink ni ghali.

Huko Kenya gharama za kununua vifaa ni sawa na Tsh1.7m

Kifururushi cha chini kabisa Tsh130k/mwezi

Ipo Kenya karibia mwaka ila wanaotumia hawafiki 3000. Sasa utatobokaje mfuko wakati providers wengine kama zuku wanakupa huduma kwa bei che?

Mimi naona Nape atakua anashirikiana na kina voda ambao hawataki kupoteza wateja wao wakubwa, starlink itawaiba hao maskini hawatoimudu
Kama shida ingekuwa gharama Nape angesema, huoni its strange wanasema hawajatimiza mashari lakini hawasemi masharti ambayo hawajatimiza? Mara nyingi wizara mbalimbali zimetoa taarifa na kulinganisha gharama za huduma ili kutetea hoja zao, sasa gharama iwe kubwa kwa Stralink nido washindwe kuweka hilo wazi?
 
Kama umesikiliza video hiyo ya Nape vyote hivyo ulivyoandika hapa sio tatizo, shida ni hiko ambacho hawajatimiza, je ni nini? Kwanini hakisemwi?
Starlink pia wananafasi ya kusema kwa upande wao!

tunaweza wauliza wapi wamekwama tuwasaidie kupaza sauti! maana inaonekana tunawaitaji kuliko wanavyotuitaji

 
Kama shida ingekuwa gharama Nape angesema, huoni its strange wanasema hawajatimiza mashari lakini hawasemi masharti ambayo hawajatimiza? Mara wizara mbalimbali zimetoa taarifa na kulinganisha gharama za huduma ili kutetea hoja zao, sasa gharama iwe kubwa kwa Stralink nido washindwe kuweka hilo wazi?
Kinachoogopwa hapo ni dhahiri ile control ya mtandao watakuwa hawana sababu server zitakuwa Marekani😂! Hizo blah blah za masharti ya kipuuzi ni kukwamisha zoezi tu. Kingine huduma itakuwa stable kuliko huduma zao za kinyonyaji za mitandao ya simu.
 
Kama shida ingekuwa gharama Nape angesema, huoni its strange wanasema hawajatimiza mashari lakini hawasemi masharti ambayo hawajatimiza? Mara wizara mbalimbali zimetoa taarifa na kulinganisha gharama za huduma ili kutetea hoja zao, sasa gharama iwe kubwa kwa Stralink nido washindwe kuweka hilo wazi?
labda tuseme ni usalama wa nchi bwana Elon anatakiwa kutupa uhakika katika eneo hilo... mtandao wake ukiruhusiwa hautaleta uvunjifu wa amani nk...

je wewe unamaoni gani hapa katika sharti kama hili?

tunataka taarifa za watumiaji wako kila mwezi kila mwaka! ili tujue na mienendo yao mitandaoni

hapo una mawazo gani...?

au serikali inataka bando iwe linganifu na taasisi au watoaji wengine wa huduma kama ttcl ambao wanauza huduma kama hiyo nchi, serikali imewekeza mahela mengi huko pia

wewe una maoni gani?

 
Nape anataka waweke mitambo ya ku intercept traffic Tz, siyo US
sizani kama jambo baya kwa maslahi ya taifa au wewe unaonaje?

 
Kinachoogopwa hapo ni dhahiri ile control ya mtandao watakuwa hawana sababu server zitakuwa Marekani😂! Hizo blah blah za masharti ya kipuuzi ni kukwamisha zoezi tu. Kingine huduma itakuwa stable kuliko huduma zao za kinyonyaji za mitandao ya simu.
Kweli kabisa Mkuu
 
Starlink ni ghali.

Huko Kenya gharama za kununua vifaa ni sawa na Tsh1.7m

Kifururushi cha chini kabisa Tsh130k/mwezi

Ipo Kenya karibia mwaka ila wanaotumia hawafiki 3000. Sasa utatobokaje mfuko wakati providers wengine kama zuku wanakupa huduma kwa bei che?

Mimi naona Nape atakua anashirikiana na kina voda ambao hawataki kupoteza wateja wao wakubwa, starlink itawaiba hao maskini hawatoimudu
Hii starlink tunapiga makelele tu hapa, cost za kununua vifaa zipo juu sana
 
Kinachoogopwa hapo ni dhahiri ile control ya mtandao watakuwa hawana sababu server zitakuwa Marekani😂! Hizo blah blah za masharti ya kipuuzi ni kukwamisha zoezi tu. Kingine huduma itakuwa stable kuliko huduma zao za kinyonyaji za mitandao ya simu.
China hawana habari na ndio kwanza wanaendelea na project kama hiyo ya Elon... labda kwa kuwa sisi ni marafiki na China tuna tegemea kupata kitu bora na huku tukiendelea na mchakato wa kuwa na setellite yetu wenyewe

hili unalionaje? hasa unapoingia mkataba wa kinyonyaji kuwa hatakiwi mtoa huduma mwingine kama yeye. je unaweza kukubali masharti kama hayo?


:D
 
Back
Top Bottom