Pasco,
VUTA-NKUVUTE,
..Prof.Muhongo anatakiwa aache lugha za kibabe.
..huyu ni Professor mwandamizi, sasa sielewi kwanini anashindwa "kuwasomesha" na kuwashawishi wananchi wa Mtwara mpaka wakaunga mkono mradi wa gesi.
Ndugu yangu.....
Nadhani na wewe unatambua hili;
Kwamba katika sakata la GESI INATOKA AMA HAITOKI NTWARA kuna pande 3
Upande wa Kwanza ni wa serikali,unasema GESI ITOKE kwa sababu ni rasilimali ya Taifa zima,ingawaje inajali kwamba walio katika eneo gesi inakotoka watafaidishwa kwa mpango maalumu....na imetoa Elimu hiyo kwa Wana Ntwara
Upande wa pili ni wa Wana Ntwara,ambao wao wanasikiliza maneno toka pande mbili,yaani serikali inawaambia nini,na wakati huo huo wanasikiliza upande wa tatu nitakaoutaja.....
Upande wa tatu ni wa Wanaharakati na Wanasiasa,ambao malengo yao ni mchanganyiko na hawako Organised...wengine wanataka kuwatetea wana Ntwara ili wapate kipande chao...na wengine ,hasa Wanasiasa,wanataka watimize malengo yao kwa kupitia mgongo wa kujifanya wanawatetea Wana Ntwara.....Kundi hili pia wapo wanaharakati ambao wao pia kutokana na kulobiwa/kupumpiwa na "maadui"(Taasisi,watu binafsi,makampuni makubwa) ambao wanaona hatari ya wao "kutokupata faida kutokana na uwepo wa bomba hilo la gesi"(maadui wa ndani na nje ya Nchi),basi wanapaza sauti za kuhakikisha kwamba mgogoro huu hauishi kama ambavyo SERIKALI NA WANA NTWARA wangelitaka.
Hivyo basi....Professor ana Kazi ngumu kwani kuweza kuwatimizia haja zao,hasa hawa wa Kundi la tatu ni ngumu sana...na hawa ndio "wanaongea lugha za Kijiweni zinazowapa mshawasha wana ntwara kujua kweli wanatetewa".....kUMBE WATU WANAPATA AJIRA KWA KUFUKISHA MGOGORO....WATU WANAPATA KURA KWA KUFUKISHA MGOGORO.....
Lakini pia,tunawashukuru wale ambao kwa Moyo wa Ukweli wanawaamusha wana Mtwara waweze kujua namna ya kuibana serikali ili mkataba uwe wa win-win formation....