Waziri Muhongo: Gesi ya Mtwara itatoka!

Waziri Muhongo: Gesi ya Mtwara itatoka!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Waziri wa Nishati na Madini,Profesa Sospeter Muhongo amekaririwa leo akisema kuwa gesi asilia ya Mtwara itatoka na Serikali itaendelea kutekeleza mipango yake kama ilivyopangwa.

Waziri Muhongo ameyasema hayo baada ya Serikali kutia saini Mkataba wa Uzalishaji wa Umeme na Kampuni moja ya nchini China leo hii.Uzalishaji huo wa umeme utafanyika katika eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Waziri Muhongo amewataka wananchi kuwapuuza wale wote wanaopinga kutumika kwa gesi asilia ya Mtwara.

Bomba la kusafirisha gesi hiyo litaanza kujengwa wakati wowote kuanzia sasa.'Hadi kufikia mwisho wa mwaka ujao,Tanzania itakuwa inauza umeme nchi za nje' aliongeza Waziri Muhongo.

Wananchi wa Mtwara wameshasikilizwa au ndio wamepuuzwa?

Chanzo: Mimi mwenyewe na East Africa Radio

Cc THE BIG SHOW na Sizinga

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
hili tulishalimaliza.....na gesi tiari ishatoka
 
mi nilisema yale maandamano ni kaupepo tu katapita watu wakanipuuza
 
Nina mashaka na the motive behind taarifa hii!.
Uchochezi!.
Mimi ni ssupporter mkubwa wa gesi ya Mtwara lazima itoke!.
Pasco

Tunajua kwanja ulilipokea wakati wa uzinduzi pale kinyerezi sio la kitoto ndio maana unakuwa na kibri cha kusema hayo

Shame on you

na tunajua wewe na yule wa TBCCM Muro kama sijakosea jina mmewekwa koposha watu mjadala utakaposhika kasi
mark my words Pasco na Muro
 
Last edited by a moderator:
Pasco, VUTA-NKUVUTE,

..Prof.Muhongo anatakiwa aache lugha za kibabe.

..huyu ni Professor mwandamizi, sasa sielewi kwanini anashindwa "kuwasomesha" na kuwashawishi wananchi wa Mtwara mpaka wakaunga mkono mradi wa gesi.
Ni lecturer wa Savimbi nasikia?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hao wanajeshi wataweka kambi ya milele pale Mtwara na kweny hiyo pipe mpaka gesi itakapoisha huko ardhini ndiyo wataondoka.
Kama ni garasa kweli tulilipata la Bagamoyo Originali.
 
Yale ya Delta state Nigeria! We learn from history that we learn nothing from history. Qoute Bernard Shaw
 
kinauche,

..sipendi kabisa viongozi wanaofokea wananchi.

..binafsi naamini angetumia lugha ya kistaarabu na kuelewesha hali isingekuwa mbaya kama ilivyo sasa hivi.
 
Last edited by a moderator:
Nina mashaka na the motive behind taarifa hii!.
Uchochezi!.
Mimi ni ssupporter mkubwa wa gesi ya Mtwara lazima itoke!.
Pasco
jitu zima ka litoto ama kutumia ID nyingi unajisahau unatumia ipi? Hapa uchochezi upo wapi? Bora utumie ile ID nyingine... ulishaadhilika na posho mwandishi njaa
 
jitu zima ka litoto ama kutumia ID nyingi unajisahau unatumia ipi? Hapa uchochezi upo wapi? Bora utumie ile ID nyingine... ulishaadhilika na posho mwandishi njaa
Nakuruhusu itaje na wala sitakushitaki kwa name calling!. Humu jf tupo Pasco wawili tuu tunaofanana, yule mwenyewe halisi in his real name tena akiwa ni verified user na mimi Pasco wa jf!. No more no less!.
Pasco
 
Tunajua kwanja ulilipokea wakati wa uzinduzi pale kinyerezi sio la kitoto ndio maana unakuwa na kibri cha kusema hayo

Shame on you

na tunajua wewe na yule wa TBCCM Muro kama sijakosea jina mmewekwa koposha watu mjadala utakaposhika kasi
mark my words Pasco na Muro

Du!.Mimi Pasco huwa najitolea tuu na kiukweli silipwi!, unless unazungumzia zile overheads za utekelezaji!.
P.
 
Nina mashaka na the motive behind taarifa hii!.
Uchochezi!.
Mimi ni ssupporter mkubwa wa gesi ya Mtwara lazima itoke!.
Pasco

Hakuna anayepinga kutoka gesi mtwara bali aina ya utokaji na manufaa yake yawekwe wazi ili kila mmoja ajue nini kinaendelea.
Juzi tuliambiwa gesi iende Dar ili izalishe umeme ambao hatukuambiwa nani atauzalisha, Leo mkataba tena na mchina kuzalisha. Tumekopa kuchimba na kusafirisha gesi, ikishafika dar anamiliki mchina tena sisi tusubiri bili mwisho wa mwezi, Hivi hii ni faida ya aina gani? Kwa nini hizo plants zisinunuliwe na serikali?. Si bora wangemwambia huyo mchina atoe gesi mtwara hadi Dar halafu akizalisha umeme sisi tununue uniti ili tujue ni biashara tu. Hapa nadhani ni mchezo wa TRL unaendelea. Kitu ambacho watanzania hatukitaki.

Kipindi chote cha Mwl, alikataa nguzo kuu za uchumi kuwekezwa kwa watu wa nje, kwani kiongozi hatokuwa na uwezo wa kudhibiti masuala kadhaa ya uchumi wa nchi. Mathalani kushusha bei/gharama za umeme bila ruzuku kitu ambacho kitaendelea kutuua zaidi badala ya kutusaidia.
 
Back
Top Bottom