Waziri Muhongo: Gesi ya Mtwara itatoka!

Waziri Muhongo: Gesi ya Mtwara itatoka!

Yea, watu walimwagia mafisa hapa.

Kiongozi mzuri siyo lazima profesa.

Sometimes, ni shida pia kuanza siasa ukubwani.
sifa huwa zinatesa sana mkuu.... wanasemaga "Mgema akisifiwa......", na nyingine "ngoma ikivuma sana inapasuka", ndo haya tunayoyashuhudia.
Uongozi haukurupushwi..... unatakiwa uwiwe..... hasa na unaowaongoza....
sikatai kuna muda ambao kama kiongozi unatakiwa ufanye maamuzi magumu kwa wananchi.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Waziri wa Nishati na Madini,Profesa Sospeter Muhongo amekaririwa leo akisema kuwa gesi asilia ya Mtwara itatoka na Serikali itaendelea kutekeleza mipango yake kama ilivyopangwa.

Waziri Muhongo ameyasema hayo baada ya Serikali kutia saini Mkataba wa Uzalishaji wa Umeme na Kampuni moja ya nchini China leo hii.Uzalishaji huo wa umeme utafanyika katika eneo la Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Waziri Muhongo amewataka wananchi kuwapuuza wale wote wanaopinga kutumika kwa gesi asilia ya Mtwara.

Bomba la kusafirisha gesi hiyo litaanza kujengwa wakati wowote kuanzia sasa.'Hadi kufikia mwisho wa mwaka ujao,Tanzania itakuwa inauza umeme nchi za nje' aliongeza Waziri Muhongo.

Wananchi wa Mtwara wameshasikilizwa au ndio wamepuuzwa?

Chanzo: Mimi mwenyewe na East Africa Radio

Cc THE BIG SHOW na Sizinga

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Wananchi wa Mtwara hawakaidi kutoka gas wanachokaidi ni kwa nini Kinyerezi na sio Mtwara? Kwa nini serikali inaingia gharama kubwa na isiyo na msingi wa kuweka mabomba hivi sasa ya gesi wakati hakukuwa na sababu na hizo pesa zingetumika kuboresha mazingara ya Mtwara na kuweka mitambo ya umeme Mtwara. Au ni kwa sababu huu ni mradi wa Jakaya Kikwete kupendelea kinyerezi ambako ni nyumbani kwake? Je, kila rais anayekuja aboreshe kule anakotoka kwa mtaji wa Watanzania wengine?

Nafahamu Jakaya kwa sababu ni dhaifu hawezi kujibu haya maswali na wala CCM hawawezi kujibu kwa sababu ni ma-cowards. Siku inakuja jiulizeni nini kiliwapata Sadam Hussein, Gaddafi, Mobutu, Bokasa et al.
 
Back
Top Bottom