Waziri Muhongo anasa bil. 400/-

Waziri Muhongo anasa bil. 400/-

Kama hata 400billion tunalalamika hamna shida tuwafukuze hao wawekezaji then tuchimbe wenyewe kama sasa. Maake hata kama ni yetu si tumeshindwa kuizalisha hiyo gas maake tutaishia kulalamika wakati hatuna uwezo.Try to imagine una shamba lakini vifaa vya kulimia na pembejeo then mtu anakuja kukodi shamba lako analima anapata gunia 100 anakupa gunia 20 unalalamika kama ulikuwa unahitaji 100 si ungelima mwenyewe asingekusaidia huyo hata tu gunia 20 si ungekufa njaa
 
Kosa lipo na nimeshauri kwamba rate ya capital gains ipandishwe toka 20% hadi 50% na siyo kila rasilimali zetu ziuzwe kwa kampuni za nje, kwanini tusiingie nao ubia wa 50/50? Makosa yale yale yaliyofanywa na Mkapa kwenye dhahabu yanaendelea hadi hii leo hakuna lolote tulilojifunza kutokana na makosa yale ambayo yanasababisha nchi kupoteza mapato mengi Sana ambayo yangesaidia kuboresha sekta mbali mbali nchini kama elimu, afya, umeme, maji n.k.

Si ndio nakuuliza waliuza kwa kiasi gani? Na kama kuna kosa basi twende kwenye kubadili sheria kwa kuwa Muhongo alichofanya ni kusimamia utekelezaji washeria...

Badala ya kulalamikia case moja moja tunatakiwa tuweke institutions za kuondoa hizi lawama...

Wewe una propose tuchaji kiasi gani na kwa reference ipi? Wengine wanachaji kiasi gani?
 
Na wanasahau kuwa target yetu ni ku gain thru tax na loyalty na si capital gains....kwa kuwa si lazima watu wa change ownerships

Tushaambiwa production inatarajiwa 2020...tutulie tuone kama tutapata enough tax na loyalty ndio tuanze kulalamika...



Unajua nimegundua kwamba watu wengi hawafahamu vizuri haya mambo jinsi yanavyoenda...kimsingi wala hakuna tulichopteza ingawaje watu wanadhani tumepoteza. Kwenye sharing Agreement, Tanzania inapata 65% ya mapato ya gesi....kwahiyo hata wauziane mmoja baada ya mwingine lakini sisi 65% yetu ipo pale pale; sana sana tutakuwa tunachukua kodi yetu kila wanapouziana.

Labda watu wanapojichanganya ni kwamba wanachukulia uuzaji huu unafanana kama ilivyopata kufanyika kwa Sheraton Hotel and the like ambao kimsingi investor anauza; kisha anasepa wakati uuzaji wa aina hii ya sasa ni wa investor kuuza kwa ajili ya ku-accumulate capital....ni kama walivyofanya Swala Energy ambao wame-opt kuuza hisa DSE, hawa Ophir wame-opt kuuza hisa kwa one big investor.
 
WAMEONA SHIDA SANA KUANDIKA KICHA CHA HABARI KAZI NZURI YA ZZK YAANZA KUTOA MATUNDA.

habari hii inamaanisha hata kama waziri angekuwa ni vuai au kagasheki bado hizo pesa tungezipata, hivyo sifa ni za aliyesababisha hiyo sheria kuwepo na si waziri aliyenuafaika na kazi waliyoshindwa kuifanya kwa miaka 50 ya UHURU wa Taifa letu.

MSIFIENI TUU HATA KAMA ANAMATATIZO NA HAO WANACHADEMA WENZAKE KAMA SI WENZANGU.
 
Tusiwe watu watu wa kulalamika tu 400bil ni badget ya wizara jamani hizi hela kwa Transaction moja ni nyingi hizi tujiulize nani anaweza kufanya biashara ya hasara na lazima tukubali achievement inayofikiwa taratibu tutafika tu wapendwa juzi hatukupata kitu jana tukaambulia millioni 32 kwa kampuni 5 kwa miaka zaidi ya kumi leo tumepata 400 billion kwa transaction moja kwanini kesho tusipate trillions
 
Hao wanaopinga gawio la hisa walitaka iweje ?????? Wana tamani vitu vya kufikirika ?
 
Hapana banaaa hauko sawa kabisa kwanini tupate royalties tu na sio capital gains? Kwa maneno yako hata hii bilioni 400 tusingeambulia chochote. Kumbuka capital gains ilikuwa introduced nchini baada ya Serikali kutoambulia hata senti moja baada ya India airtel kuununua kampuni moja ya simu nchini na Serikali kukosa mapato ya $308 million kwa kuwa TRA ilikuwa haicharge capital gains, ndiyo katika mjadala mzito hapa jamvini Zitto akachukua hilo wazo la capital gains toka katika mjadala ule na kuupeleka bungeni na sheria kupitishwa kuiruhusu TRAkuanza kucharge CG.

Na wanasahau kuwa target yetu ni ku gain thru tax na loyalty na si capital gains....kwa kuwa si lazima watu wa change ownerships

Tushaambiwa production inatarajiwa 2020...tutulie tuone kama tutapata enough tax na loyalty ndio tuanze kulalamika...
 
Nachosema biashara ya kuuza na kununua si lengo kuu; kwani shell toka wamekuwepo nigeria muda gani? Nakubali kuwa ni kitu kizuri kucharge ila kumbuka kuwa ukisema unacharge 50% hapo nia itakuwa si kuongeza pato ila ni ku discourage sales na maana yake ni kuwa unataka wasio na uwezo wa kuendesha walazimishe kuendesha hivyo vitalu kwa sababu kuviuza ni hasara...

Capital gain ni ya msimu tax na loyalty ni continuous ndio maana nasema hiyo charge iangalie yote isije ikalazimisha makampuni uchwara kuendelea kuhodhi vitalu kwa kuwa kuviuza hakulipi...hapo tutakosa tax na loyalty


Hapana banaaa hauko sawa kabisa kwanini tupate royalties tu na sio capital gains? Kwa maneno yako hata hii bilioni 400 tusingeambulia chochote. Kumbuka capital gains ilikuwa introduced nchini baada ya Serikali kutoambulia hata senti moja baada ya India airtel kuununua kampuni moja ya simu nchini na Serikali kukosa mapato ya $308 million kwa kuwa TRA ilikuwa haicharge capital gains, ndiyo katika mjadala mzito hapa jamvini Zitto akachukua hilo wazo la capital gains toka katika mjadala ule na kuupeleka bungeni na sheria kupitishwa kuiruhusu TRAkuanza kucharge CG.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Lengo la kuongeza rate ya capital gains ni kuhakikisha kwamba Watanzania tunafaidika na rasilimali zetu kwa kiwango cha juu kabisa. Kwa mfano hebu angalia tofauti ya hazina kuvuna shilingi 1.04 Trillioni na bilioni 400. Pia ni kupunguza hawa matapeli kuingia nchini na kununua vitalu kwa bei ya kutupa kisha kuuza kwa faida kubwa sana kisha kusepa nchini. Tukiweza hili basi yale makampuni yenye nia ya kweli ya kushiriki katika uvunaji wa rasilimali zetu ndiyo yatakayoingia nchini na kampuni za kitapeli zinazotaka kutengeneza faida ya haraka haraka zitacheza mbali na Tanzania. Makosa kama haya ya kuuza rasilimali za nchi hayatokei kwenye nchi nyingi duniani sasa hivi ubia wa 50/50 ndio mwendo wa kwenda mbele kwa mbele siye bado tunakurupuka sana na kuikosesha nchi mapato mengi sana.


Nachosema biashara ya kuuza na kununua si lengo kuu; kwani shell toka wamekuwepo nigeria muda gani? Nakubali kuwa ni kitu kizuri kucharge ila kumbuka kuwa ukisema unacharge 50% hapo nia itakuwa si kuongeza pato ila ni ku discourage sales na maana yake ni kuwa unataka wasio na uwezo wa kuendesha walazimishe kuendesha hivyo vitalu kwa sababu kuviuza ni hasara...

Capital gain ni ya msimu tax na loyalty ni continuous ndio maana nasema hiyo charge iangalie yote isije ikalazimisha makampuni uchwara kuendelea kuhodhi vitalu kwa kuwa kuviuza hakulipi...hapo tutakosa tax na loyalty
 
Biashara hii ni complicated kuliko unavyofikiria kwani mikataba hii ilisainiwa under kitu kinaitwa PSA. Maelezo hayo hapo juu kama yangekuwa sahihi Tanzania ingepata pesa nyingi kuliko tulizoambiwa kwy article.
Tanzania itaendelea kuibiwa sana kama itaendelea kuwaficha wananchi(wenye mali) wake mikataba wanayosaini.

gas iliyouzwa kwa mujibu wa NYSE commodity market ina thamani ya $ 60 billions wao wameuza kwa dola bilioni 1.3 that is very questionable NASDAZ. Wameuza kwa almost 90% off ya thamani ya gas hiyo. Gas ni ya kwetu tunaambulia dola milioni 260 which is less than 1% ya thamani ya gas inayouzwa halafu unaita hii ni kufaidika come on ???

inabidi ufanye assumption nyingi sana ili kuamini kuwa nchi imepata faida lazima ukubali kuwa bei ya dola 1.3 bilioni ni sahihi na pili je serikali ilishirikishwa ktk mapatano ya bei hiyo?? ne je serikali haikuona haja ya wao wenyewe kutafuta mnunuzi mwingine atakayelipa pesa zaidi ya hizi hasa ukizingatia ndiye mwenye hisa kubwa?? je muhongo alishauri nini serikali ktk kukubali bei hii ?? je alifanya research kuakiki bei hii au alichukua 10% na hakuwa na haja ya kufanya uchunguzi wa bei wala nini kama wengine wanavyofanya?? cha msingi kama nilivyokuwambia thamani ya gas iliyouzwa ni dola bilioni 60 wewe unaambuliwa makusanyo ya capital gain tax ya dola milioni 260 . i am very skeptical na hili deal inawezekana muhongo amefaidika kuliko nchi yetu.
Sina hakika kama nimekuelewa hususani hapo uliposema $ 60 billion...labda ungeweka hiyo source hapa tukaisoma vizuri ndipo tungejadili vizuri. Hata hivyo, ngoja nijaribu kukujibu kama nilivyokuelewa.

Kwanza kabisa nikukumbushe ni hiyo Production Sharing Agreement(PSA) ndiyo inayotoa 65% kwa serikali(kupitia TPDC) na 35% Kwa investor. Arrangement iliyopo ni kwamba, mwenye leseni ya vitalu ni TPDC..so, mwekezaji anaenda kwa TPDC na (assume no ufisadi) ku-prove ana uwezo wa kufanya kazi; financially and in terms of technology among other things. Sina hakika mwenzangu una PSA ya mwaka gani lakini the latest PSA, ime-include payments on signing license, ambayo zamani haikuwapo, na pia imeongoza Royalty Fee. Na kingine kilichobadilika ni training fee kwa locals ambayo imepanda kutoka $ 150,000/ to 500,000/ kwa mwaka.

Hivyo basi, investor akishapata vitalu, either solely or in partnership kama ilivyokuwa kwa Ophir na BG; vile vile kuna room kwa TPDC ku-share production costs...but all in all; mwisho wa cku, TPDC anachukua 65% ya profit na mwekezaji anachukua 35%. Hii ndiyo latest PSA.

Sasa tukirudi kwenye hoja ya hapo juu ni kwamba, origin partnership ni ya Ophir 40% na GB 60%. Hii maana yake ni nini, profit share ya BG ni 60% ya hiyo 35% ambayo ni 21% wakati Ophir ni 40% ya hiyo 35% ambayo ni 14% ambapo aggregate profiti sharing itakuwa TPDC 65% + 21%+14%=100%.

Hata hivyo, Ophir ameuza 20% ya share zake. Kama reference yetu ni among investors, ni kwamba wameuza 20% ya ile 40% ambayo itakuwa ni 8% na mwenyewe kubakiwa 32% na hatimae inakuwa BG 60%+Ophir 32% + Pavillion 8%. Lakini linapokuja suala la Profit sharing (assuming profit sharing itatokana na umiliki wa mradi), maana yake ni kwamba Ophir ameuza 20% ya 21% ambayo ni 4.2% na mwenyewe kubakiwa na 16.8%...so, the whole sharing itabadilika na kuwa TPDC 65%+BG 21%+Ophir 11.2% + Pavillion 2.8%=100%. So, in either way, percentage ya TPDC inabaki palepale.

Sasa hoja hapa ni hiyo 20% ya 40% ambayo Ophir ameuza. Kama nilivyosema hapo awali, nimeshindwa kabisa kukuelewa uliposema "gas iliyouzwa ina thamani ya $60billion." Je, unamaanizisha kwamba hiyo 20% ya share zake ameuza kwa $ 60 billion? Ungeweka hapa hiyo link ingekuwa vizuri. Lakini hata kama ndicho unachokimaanisha, bado nami ndicho hicho hicho nilichokisema hapo kabla. Nisome hapa chini kwenye RED
Ni jambo la kujivunia kuwa tunae waziri ambae ni msomi na muelewa wa mambo ya utawala na maendeleo. Na hakika amepewa wizara ambayo inafanana na professional yake na kwa bahati mbaya amewabana sana makanjanaja na matapeli wa mjin mpaka imekuwa nongwa.
Soma vizuri,Mhe. Zitto Zuberi Kabwe ndie aliyeanzisha hii kitu ikawa sheria,sio waziri. All kudos to Mr ZZK
Hizi siasa za kugombea fito Watanzania sijui sitatufikisha wapi! Hapo kila mmoja ame-play role yake vizuri! Zitto, kama mbunge ametekeleza wajibu wake na ameleta mswada wenye maslahi kwa taifa! Lakini Muhongo na wenzake nao wame-play part yao vizuri...kusimamia uuzaji na kuhakikisha taifa linapata stahiki yake. Hao wengine wasiolipa kodi si kwamba hakuna sheria; zipo na hawalipi. KImsingi hapa hoja sio hiyo mnayoshindana nayo nyie; hoja ni kwamba je, hizo 20% ambazo Ophir wameuza kwa USD 1.3 Billion, kweli hiyo ndiyo thamani waliyouza? Let me keep it this way ili mpate kunielewa. Assume unanunua gari Japan kwa USD 250 million. Lakini unafahamu wazi kwamba, hiyo gari ya USD 250 million, TRA watachukua nyingi sana za kwao. Ili kukwepa panga zito la TRA, unaamua ku-collude na Seller na kisha anaandika Stakabadhi mbili; moja anaandika USD 250 million(hii unabaki nayo) na nyingine anaandika USD 100million (ndiyo unayoenda kuonesha TRA). Hii ilikuwa inafanyika sana; tena sana hadi TRA walipoamua kuanza kufanya evaluation wenyewe! Sasa basi, kodi ambayo ilibidi itokane na USD 250million, will eventually come from USD 100 million! Meaning that, at the end of story, TRA watachukua chini ya 50% ya kodi halisi!!

Hivyo basi, kama hakuna ushenzi wowote(Watanzania kutokana na kutopea uhalifu, mnaita "ujanja") na kwamba ni kweli kabisa Ophir wameuza hisa husika kwa USD 1.3 billion; then congrats to all waliohakikisha national interest zinazingatia hata kama ni wajibu wao kufanya hivyo...coz' they're being paid to do so.

inabidi Pamoja na yote, ningefurahi sana kuona hiyo reference inayosema wameuza kwa $ 60 billion. Am so concerned coz' ikiwa 2.8% of total project is equivalent to $ 60 billion, this means the the whole project ni more than $ 200 billion! Does it bring any sense? Think about it bila kusahau kwamba hata Wall Street Journal nao wameripoti $1.3 Billion...nanukuu "Ophir Energy PLC has sold a share of a giant natural-gas discovery off the coast of Tanzania to state-owned Pavilion Energy Pte. Ltd. of Singapore for $1.3 billion, U.K.-based Ophir said Thursday." source: http://online.wsj.com/news/articles/SB10001424052702303289904579197193769425338 . Sasa mbona hiyo difference ni kubwa sana wakati NYSE na Wall Street Journals wote ni watu wanaohusika na masuala ya investments? Au hiyo $ 60 billion yako wewe inaelezea nini hasa?
 
Hao wanaopinga gawio la hisa walitaka iweje ?????? Wana tamani vitu vya kufikirika ?

wanacholalamikia ni kwamba kwa mujibu wa NYSE COMMODITY EXCHANGE MARKET GAS ILE INA THAMANI YA DOLA BILLIONI 60 ORPHIL IMEUZA KWA DOLA BILLION 1.3 ASSUME KWAMBA BEI HII NDIO BEI KAMILI ILIYOUZWA NA SIYO ZAIDI YA HAPO KWA MUJIBU WA SOKO LA DUNIA ?? NA JE SERIKALI KAMA MBIA MKUBWA ILIJARIBU KUTAFUTA SOKO MWINGINE AMBAYE ANGEWEZA KUTOA ZAIDI YA HIYO (KOSA LA MUHONGO LIPO HAPA) AU amechukua 10% na kuchukua bei in face value bila ya kufanya market anaysis ya kampuni nyingine yenye uwezo wa kulipa zaidi ya bei hiyo.

tuliambulia hapa ni capital gain tax ya 20% ya 1.3 ambayo ni dola milioni 260 ambayo ni less than 1% ya thamani ya gas?? should we rely on the Government that the price is good or we should rely on free market?? some of us have more faith on free market than what the gov. is telling to be the truth.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kusema ukweli hizi mada mi nazisoma humu humu (sijawa na muda wa kusoma policy)

Lakini si nimesikia tuna 65/45...more than 50/50....au niko misinformed?

Kwa kweli lazima tuwe wabia wakubwa wa gesi otherwise itakuwa ni upuuzi...nchi nyingi zinazofanya vizuri kama Botswana na Ghana serikali ina ubia mkubwa. Unajua Ashanti ilikuwa ya serikali ya Ghana kabla ya kuingia ubia na Anglo America na kuzaa AngloGold Ashanti. Imagine wakati mgodi wa Geita unanunuliwa mnunuzi alikuwa serikali ya Ghana chini ya Ashanti Gold ... kwa nini Ghana isiendelee...mipango, mipango, policy.....

Nilikuwa najua serikali kwa kuwa haina ela imeamua baada ya wawekezaji kumaliza kulipa cost za investments zao basi tunaanza 65% kwa 45%....nielimisheni


Lengo la kuongeza rate ya capital gains ni kuhakikisha kwamba Watanzania tunafaidika na rasilimali zetu kwa kiwango cha juu kabisa. Kwa mfano hebu angalia tofauti ya hazina kuvuna shilingi 1.04 Trillioni na bilioni 400. Pia ni kupunguza hawa matapeli kuingia nchini na kununua vitalu kwa bei ya kutupa kisha kuuza kwa faida kubwa sana kisha kusepa nchini. Tukiweza hili basi yale makampuni yenye nia ya kweli ya kushiriki katika uvunaji wa rasilimali zetu ndiyo yatakayoingia nchini na kampuni za kitapeli zinazotaka kutengeneza faida ya haraka haraka zitacheza mbali na Tanzania. Makosa kama haya ya kuuza rasilimali za nchi hayatokei kwenye nchi nyingi duniani sasa hivi ubia wa 50/50 ndio mwendo wa kwenda mbele kwa mbele siye bado tunakurupuka sana na kuikosesha nchi mapato mengi sana.
 
Kwani wameuza gesi au wameuza vitalu (deposits)...kama ni vitalu jua kuna cost ya uchimbaji; hiyo amount ni estimation ya deposits...gesi inategemea kuanza kupatikana 2020

wanacholalamikia ni kwamba kwa mujibu wa NYSE COMMODITY EXCHANGE MARKET GAS ILE INA THAMANI YA DOLA BILLIONI 60 ORPHIL IMEUZA KWA DOLA BILLION 1.3 ASSUME KWAMBA BEI HII NDIO BEI KAMILI ILIYOUZWA NA SIYO ZAIDI YA HAPO KWA MUJIBU WA SOKO LA DUNIA ?? NA JE SERIKALI KAMA MBIA MKUBWA ILIJARIBU KUTAFUTA SOKO MWINGINE AMBAYE ANGEWEZA KUTOA ZAIDI YA HIYO (KOSA LA MUHONGO LIPO HAPA) AU amechukua 10% na kuchukua bei in face value bila ya kufanya market anaysis ya kampuni nyingine yenye uwezo wa kulipa zaidi ya bei hiyo.

tuliambulia hapa ni capital gain tax ya 20% ya 1.3 ambayo ni dola milioni 260 ambayo ni less than 1% ya thamani ya gas?? should we rely on the Government that the price is good or we should rely on free market?? some of us have more faith on free market than what the gov. is telling to be the truth.
 
kwako NASDAZ,
Napenda sana unavyojaribu kuwaelimisha wabongo kuhusu hii biashara ya gas lakini nigependa kukufanulia yafuatayo katika mikataba ya PSA .
hiyo asilimia 65 au 75 mnayogawana ni ya profit na siyo mapato kwani ktk mapato inabidi utoe gharama za uzalishaji halafu kilichobakia ndiyo hilo panga la hizo asilimia linapigwa. utata namba wani unakuwa ktk hili lifuatalo hatujui serikali ilichosaini kwenye kitu kinaitwa kitaalamu AFE hapo ndipo mara nyingi huwa serikali na nchi nyingi husika zinapopigwa bao. forget about profit, forget about revenue, forget about anything the most important document is AFE full stop
Ofcourse ni profit, sijui nilikuwa nafikiria nini hadi nikawa naandika mapato...ni profit.
 
wanacholalamikia ni kwamba kwa mujibu wa NYSE COMMODITY EXCHANGE MARKET GAS ILE INA THAMANI YA DOLA BILLIONI 60 ORPHIL IMEUZA KWA DOLA BILLION 1.3 ASSUME KWAMBA BEI HII NDIO BEI KAMILI ILIYOUZWA NA SIYO ZAIDI YA HAPO KWA MUJIBU WA SOKO LA DUNIA ?? NA JE SERIKALI KAMA MBIA MKUBWA ILIJARIBU KUTAFUTA SOKO MWINGINE AMBAYE ANGEWEZA KUTOA ZAIDI YA HIYO (KOSA LA MUHONGO LIPO HAPA) AU amechukua 10% na kuchukua bei in face value bila ya kufanya market anaysis ya kampuni nyingine yenye uwezo wa kulipa zaidi ya bei hiyo.

tuliambulia hapa ni capital gain tax ya 20% ya 1.3 ambayo ni dola milioni 260 ambayo ni less than 1% ya thamani ya gas?? should we rely on the Government that the price is good or we should rely on free market?? some of us have more faith on free market than what the gov. is telling to be the truth.
Mkuu politiki,
UNgetoa hiyo link ili tuweze kujadili vizuri coz' there's something missing kwenye hiyo $60 billion. Je, hiyo $60billion ni equivalent to what Ophir owned before (14%) or equivalent to total project? Take it from me, there's something missing.
 
Last edited by a moderator:
Kusema ukweli hizi mada mi nazisoma humu humu (sijawa na muda wa kusoma policy)

Lakini si nimesikia tuna 65/45...more than 50/50....au niko misinformed?

Kwa kweli lazima tuwe wabia wakubwa wa gesi otherwise itakuwa ni upuuzi...nchi nyingi zinazofanya vizuri kama Botswana na Ghana serikali ina ubia mkubwa. Unajua Ashanti ilikuwa ya serikali ya Ghana kabla ya kuingia ubia na Anglo America na kuzaa AngloGold Ashanti. Imagine wakati mgodi wa Geita unanunuliwa mnunuzi alikuwa serikali ya Ghana chini ya Ashanti Gold ... kwa nini Ghana isiendelee...mipango, mipango, policy.....

Nilikuwa najua serikali kwa kuwa haina ela imeamua baada ya wawekezaji kumaliza kulipa cost za investments zao basi tunaanza 65% kwa 45%....nielimisheni
Profit sharing ni kwamba, serikali inachukua 65-75% na 25-35% inaenda kwa investor. Hiyo 65-75% inategemeana na location ya project husika na kuna factors zingine wanaangalia.
 
Sina hakika kama nimekuelewa hususani hapo uliposema $ 60 billion...labda ungeweka hiyo source hapa tukaisoma vizuri ndipo tungejadili vizuri. Hata hivyo, ngoja nijaribu kukujibu kama nilivyokuelewa.

Kwanza kabisa nikukumbushe ni hiyo Production Sharing Agreement(PSA) ndiyo inayotoa 65% kwa serikali(kupitia TPDC) na 35% Kwa investor. Arrangement iliyopo ni kwamba, mwenye leseni ya vitalu ni TPDC..so, mwekezaji anaenda kwa TPDC na (assume no ufisadi) ku-prove ana uwezo wa kufanya kazi; financially and in terms of technology among other things. Sina hakika mwenzangu una PSA ya mwaka gani lakini the latest PSA, ime-include payments on signing license, ambayo zamani haikuwapo, na pia imeongoza Royalty Fee. Na kingine kilichobadilika ni training fee kwa locals ambayo imepanda kutoka $ 150,000/ to 500,000/ kwa mwaka.

Hivyo basi, investor akishapata vitalu, either solely or in partnership kama ilivyokuwa kwa Ophir na BG; vile vile kuna room kwa TPDC ku-share production costs...but all in all; mwisho wa cku, TPDC anachukua 65% ya profit na mwekezaji anachukua 35%. Hii ndiyo latest PSA.

Sasa tukirudi kwenye hoja ya hapo juu ni kwamba, origin partnership ni ya Ophir 40% na GB 60%. Hii maana yake ni nini, profit share ya BG ni 60% ya hiyo 35% ambayo ni 21% wakati Ophir ni 40% ya hiyo 35% ambayo ni 14% ambapo aggregate profiti sharing itakuwa TPDC 65% + 21%+14%=100%.

Hata hivyo, Ophir ameuza 20% ya share zake. Kama reference yetu ni among investors, ni kwamba wameuza 20% ya ile 40% ambayo itakuwa ni 8% na mwenyewe kubakiwa 32% na hatimae inakuwa BG 60%+Ophir 32% + Pavillion 8%. Lakini linapokuja suala la Profit sharing (assuming profit sharing itatokana na umiliki wa mradi), maana yake ni kwamba Ophir ameuza 20% ya 21% ambayo ni 4.2% na mwenyewe kubakiwa na 16.8%...so, the whole sharing itabadilika na kuwa TPDC 65%+BG 21%+Ophir 11.2% + Pavillion 2.8%=100%. So, in either way, percentage ya TPDC inabaki palepale.

Sasa hoja hapa ni hiyo 20% ya 40% ambayo Ophir ameuza. Kama nilivyosema hapo awali, nimeshindwa kabisa kukuelewa uliposema "gas iliyouzwa ina thamani ya $60billion." Je, unamaanizisha kwamba hiyo 20% ya share zake ameuza kwa $ 60 billion? Ungeweka hapa hiyo link ingekuwa vizuri. Lakini hata kama ndicho unachokimaanisha, bado nami ndicho hicho hicho nilichokisema hapo kabla. Nisome hapa chini kwenye RED

Hizi siasa za kugombea fito Watanzania sijui sitatufikisha wapi! Hapo kila mmoja ame-play role yake vizuri! Zitto, kama mbunge ametekeleza wajibu wake na ameleta mswada wenye maslahi kwa taifa! Lakini Muhongo na wenzake nao wame-play part yao vizuri...kusimamia uuzaji na kuhakikisha taifa linapata stahiki yake. Hao wengine wasiolipa kodi si kwamba hakuna sheria; zipo na hawalipi. KImsingi hapa hoja sio hiyo mnayoshindana nayo nyie; hoja ni kwamba je, hizo 20% ambazo Ophir wameuza kwa USD 1.3 Billion, kweli hiyo ndiyo thamani waliyouza? Let me keep it this way ili mpate kunielewa. Assume unanunua gari Japan kwa USD 250 million. Lakini unafahamu wazi kwamba, hiyo gari ya USD 250 million, TRA watachukua nyingi sana za kwao. Ili kukwepa panga zito la TRA, unaamua ku-collude na Seller na kisha anaandika Stakabadhi mbili; moja anaandika USD 250 million(hii unabaki nayo) na nyingine anaandika USD 100million (ndiyo unayoenda kuonesha TRA). Hii ilikuwa inafanyika sana; tena sana hadi TRA walipoamua kuanza kufanya evaluation wenyewe! Sasa basi, kodi ambayo ilibidi itokane na USD 250million, will eventually come from USD 100 million! Meaning that, at the end of story, TRA watachukua chini ya 50% ya kodi halisi!!

Hivyo basi, kama hakuna ushenzi wowote(Watanzania kutokana na kutopea uhalifu, mnaita "ujanja") na kwamba ni kweli kabisa Ophir wameuza hisa husika kwa USD 1.3 billion; then congrats to all waliohakikisha national interest zinazingatia hata kama ni wajibu wao kufanya hivyo...coz' they're being paid to do so.


kwako NASDAZ,
Kuhusu source ya thamani ya dola bilioni 60 nilishaitoa kwy maelezo yangu ya awali kwamba ni NYSE Commodity exchange market. na nikasema Tanzania imeambulia Capital gain tax ya 20% ya 1.3 billion. nataka kujua ni nani aliyefanya market analysis ya bei hiyo ya 1.3 billion ??? na je kulikuwa na somesort of bidding na hiy 1.3 ikawa ndiyo ya highest bidder?? huwezi kusema fulani yaani Tanzania imepata faida kama hujui thamani ya kitu unachokiuza ?? ukilinganisha thamani ya gas na pesa tunayopata ya dola milioni 260 mabayo ni less than 1% ya thamani ya kile tunachopata hii ni hasara kwani biashara za gas faida kamili ni between 6 to 8% profit margin hii ni hasara .

swali langu kwako ni kwamba je pavillion italipa tax again baada ya kulipa capital gain tax ya 20% ?? na kama watalipa hii si ndio double taxation tunayojaribu ku avoid ?? ninavyofahamu mimi ni kwamba 75% ni ya profit inayopatikana mara baada ya kutoa gharama zote za uzalishaji kumbuka serikali ta Tanzania haina uwezo wa kuchangia chochote kwenye gharama za exploration, appraisal, development wala production wanasubiri baada ya pesa kuanza kuingia wawekezaji watoe gharama zao halafu baadae ndio faida waje wagawane kwa percentage hizo ulizozitaja

asante kwa maelezo yako mazuri NASDAZ
 
Back
Top Bottom