Waziri Muhongo anasa bil. 400/-

Waziri Muhongo anasa bil. 400/-

Change hiyo heading kuwa watz watapata bil.400,hela za raslimali ni za kuboresha ustawi wa jamii na miundo mbinu(shule,afya,barabara,nishati,mawasiliano,chakula bora,etc.). Huu uwe mwanzo wa kuigeuza nchi yetu kuwa first world.
 
Mwanzo mzuri...tunahitaji more governance katika hii sector kama tunataka kutoka....

Tukichemsha kwenye gesi basi tutakuwa masikini daima....
 
Nchi yetu ina sifa zote muhimu za kuifanya iendelee...

Tuna strong state and stable democracy (si kama Nigeria, DRC, Msumbiji, Uganda na nchi nyingi za Sub Saharan Afrika) kwa maana kuwa nchi yote inatawaliwa na serikali....hii pekee ni nguzo kubwa sana kwa maendeleo kwa nchi yenye rasilimali nyingi kama yetu kwa kuwa serikali ikiwa makini itatumia pato la rasilimali kuendeleza sector nyingine tofauti na hao wenzetu ambao kila mtu ana tax natural resources (DRC, Nigerian militants))


Ndio maana inabidi tuwe wakali sana kwenye gesi hakuna kuleta u namjua fulani, basi nipe tender...ni ushindani baaasi.

Nilikuwa nasoma kitabu fulani 'Why Nations Fail" kumbe Egypt walikuwa na mawaziri wafanya biashara...yani mfanya biashara mkubwa kwenye sector ya mawasiliano ndio kapewa wizara husika, utalii same, natural resources same.... Kilichofuata ni kuwa walitengeneza oligopoly ya nguvu ya economic and political elites. Ambao walihakikisha wanazuia makampuni ya kigeni kuwekeza Egypt ili kuondoa ushindani; lakini hao hao wazawa hawakuwasaidia chochote walala hoi wa Egypt bali walijenga matabaka ya wenye nacho (washikaji wa karibu wa Mubarak) na wasio nacho...kulikuwa na matajiri wakubwa 30 nchi nzima wote well connected na rais au watoto wa rais....kilichofuta ndio hiyo arab spring...

Hiki kitabu ni noma wametaja majina ya hao vigogo 30 mpaka bei walizokuwa wanauziana state owned corporations pale walipoamua ku liberalize economy (SAP). Hayo makampuni yote yalikuwa ya serikali before hayajauzwa kwa bei ya kugawa kwa washikaji wa rais wa Egypt
 
Ezekiel Kamwaga | Raia Mwema - Toleo la 331 | 25 Dec 2013


TANZANIA inatarajia kupata mgawo wa takribani shilingi bilioni 400 kutokana na mauzo ya hisa yaliyofanywa na kampuni ya Ophir kwa kampuni ya Pavillion katika vitalu vya gesi vilivyopo nchini, Raia Mwema limeambiwa.

Kampuni ya Ophir inamiliki asilimia 40 ya hisa katika vitalu namba 1, 3 na 4 huku asilimia nyingine 60 ikimilikiwa na kampuni ya BG, lakini Ophir wameamua kuuza hisa zao 20, mwaka huu.


Mauzo ya hisa hizo yanatarajiwa kuiingizia Ophir kiasi cha dola bilioni 1.3 (shilingi trilioni mbili) na kutokana na mauzo hayo, Tanzania itapata kiasi cha dola milioni 260 (shilingi bilioni 400) kama kodi.


Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufaidika na mauzo ya hisa za rasilimali zake kupitia Kodi ya Ongezeko la Mtaji (Capital Gain Tax) ambayo ilipitishwa na Bunge mwaka jana.

Kodi hiyo ilipitishwa na Sheria ya Fedha (Finance Act) ya mwaka 2012 baada ya kuwasilishwa kama mapendekezo binafsi na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe na kisha Bunge kuridhia.

Katika miaka ya nyuma, Tanzania haikuwa ikifaidika na mauzo yoyote ya hisa kwa makampuni yanayouziana rasilimali zake kwa sababu Kodi hiyo ya Ongezeko la Mtaji haikuwepo.


Kwa sababu mauzo hayo ya hisa yana thamani ya dola hizo bilioni 1.3, serikali ya Tanzania inatakiwa kupata asilimia 20 ya kiasi hicho ambayo ni dola milioni 260.

Akizungumza na Raia Mwema wiki hii, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, alisema wanatarajia kupata fedha hizo wakati wowote mauzo hayo yatakapopitishwa.

“Inategemea na namna hao wanaouziana hisa watakavyokubaliana lakini sisi tunafahamu tu kwamba wakimalizana, yetu itakuwa asilimia 20. Kwa vyovyote vile, inaonekana mauzo yanaweza kufanyika kwenye robo ya kwanza ya mwaka ujao wa 2014,” alisema Simbachawene.

Ophir ina makao yake makuu katika miji ya London, Uingereza na Perth nchini Australia na kwa mujibu wa tovuti yake, ilianzishwa mwaka 2004. Kampuni ya Pavillion Energy inamilikiwa na serikali ya Singapore.


Vitalu ambayo vimeuzwa katika uuzianaji huo vinaelezwa kuwa na ujazo wa mita za ujazo trilioni 15 na mauzo hayo pia yameenda sambamba na uuzaji wa hisa nyingine 17.6 katika makampuni yatakayokuwa yakifanya biashara za gesi hiyo hapa nchini.


Kwa mujibu wa Simbachawene, makampuni hayo matatu ni Ruvuma Pipeline Company Limited, Mzalendo Gas Processing Company Limited na Fahari Marketing Limited.


Simbachawene alisema nia ya serikali kwa sasa ni kutaka kutumia fedha hizo kwa ajili ya kulipa madeni na kuliboresha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ingawa alisema itategemea pia na mahitaji mengine yatakayokuwepo wakati fedha hizo zitakapopatikana.


“Hizi ni fedha za Watanzania wote na si za wizara yetu pekee. Tunataka kuliwezesha shirika letu la umeme ili lifanye kazi vizuri na kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa watu wengi zaidi.


“Hata hivyo, sisemi kwamba ni hela zote zitatumika kwa kazi hiyo au la lakini kuna mawazo hayo. Mambo mengine serikali itaamua kutokana na wakati fedha hizo zitakapopatikana. Huwezi kujua kutakuwa na nini wakati huo,” alisema Naibu Waziri huyo.


Alisema kwa miaka ya nyuma, Tanzania isingepata kitu kutokana na sheria zilizokuwepo na akasema serikali itajitahidi kuboresha sheria zake ili kuhakikisha inafaidika na utajiri uliokuwepo.


Mmoja wa wachambuzi wa masuala ya gesi aliyehojiwa na mtandao wa Bloomberg kuhusiana na uuzaji huu wa hisa, Tony Regan wa kampuni ya Tri Zen Inc alisema uamuzi wa kununua hisa hizo ni wa “roho ngumu” kwa sababu Tanzania ni eneo bichi kwenye sekta ya gesi.


“Mpaka sasa hakuna sheria rasmi iliyopitishwa kuhusiana na masuala ya gesi na hivyo Singapore inaingia katika eneo bichi kabisa katika sekta hii. Kumbuka pia kwamba gesi ya kwanza itaanza kuvunwa mwaka 2020 kutoka kwenye vitalu hivyo na utaona kwamba huu ni uamuzi mzito,” alisema.

CHANZO
: Raia Mwema - Waziri Muhongo anasa bil. 400/-
Waliouza viwanja kariakoo kwa bei waliyodhani wameula,leo hii wakiangalia bei za viwanja kariakoo wanaishia kupata maumivu ya vichwa,
Ningefurahi kusikia serikali ndo imeuza hisa au vitalu hivyo kwa fedha hizo badala ya kuwagawia wajanja wakauza afu
serikali ikapewa kodi tukashangilia kama mazuzu.
 
Ni jambo la kujivunia kuwa tunae waziri ambae ni msomi na muelewa wa mambo ya utawala na maendeleo. Na hakika amepewa wizara ambayo inafanana na professional yake na kwa bahati mbaya amewabana sana makanjanaja na matapeli wa mjin mpaka imekuwa nongwa.
Soma vizuri,Mhe. Zitto Zuberi Kabwe ndie aliyeanzisha hii kitu ikawa sheria,sio waziri. All kudos to Mr ZZK
Hizi siasa za kugombea fito Watanzania sijui sitatufikisha wapi! Hapo kila mmoja ame-play role yake vizuri! Zitto, kama mbunge ametekeleza wajibu wake na ameleta mswada wenye maslahi kwa taifa! Lakini Muhongo na wenzake nao wame-play part yao vizuri...kusimamia uuzaji na kuhakikisha taifa linapata stahiki yake. Hao wengine wasiolipa kodi si kwamba hakuna sheria; zipo na hawalipi. KImsingi hapa hoja sio hiyo mnayoshindana nayo nyie; hoja ni kwamba je, hizo 20% ambazo Ophir wameuza kwa USD 1.3 Billion, kweli hiyo ndiyo thamani waliyouza? Let me keep it this way ili mpate kunielewa. Assume unanunua gari Japan kwa USD 250 million. Lakini unafahamu wazi kwamba, hiyo gari ya USD 250 million, TRA watachukua nyingi sana za kwao. Ili kukwepa panga zito la TRA, unaamua ku-collude na Seller na kisha anaandika Stakabadhi mbili; moja anaandika USD 250 million(hii unabaki nayo) na nyingine anaandika USD 100million (ndiyo unayoenda kuonesha TRA). Hii ilikuwa inafanyika sana; tena sana hadi TRA walipoamua kuanza kufanya evaluation wenyewe! Sasa basi, kodi ambayo ilibidi itokane na USD 250million, will eventually come from USD 100 million! Meaning that, at the end of story, TRA watachukua chini ya 50% ya kodi halisi!!

Hivyo basi, kama hakuna ushenzi wowote(Watanzania kutokana na kutopea uhalifu, mnaita "ujanja") na kwamba ni kweli kabisa Ophir wameuza hisa husika kwa USD 1.3 billion; then congrats to all waliohakikisha national interest zinazingatia hata kama ni wajibu wao kufanya hivyo...coz' they're being paid to do so.
 
Last edited by a moderator:
Waliouza viwanja kariakoo kwa bei waliyodhani wameula,leo hii wakiangalia bei za viwanja kariakoo wanaishia kupata maumivu ya vichwa, Ningefurahi kusikia serikali ndo imeuza hisa au vitalu hivyo kwa fedha hizo badala ya kuwagawia wajanja wakauza afu serikali ikapewa kodi tukashangilia kama mazuzu.
Nadhani hujafahamu vizuri jinsi haya mambo yanavyoenda. Tanzania haijapoteza chochote hapo, sana sana ime-gain.
 
Tatizo letu watanzania hatupendi kuambiwa ukweli hasa na watanzania wenzetu. tumekuwa watu wa siasa wakati wote hata kwenye mambo ambayo siyo ya kisiasa. tunahitaji watu wa kutuambia hard truth ituume na mwisho tuifanyie kazi na siyo kulalama tu wakati dunia inakimbia kama usain bolt

hivi wewe Tanzania tunakimbia au tunatambaaa?tunatambaa chini ya swaga na ulaghai wa ccm,ufisadi na ubinafsi wa mawaziri wa chama chakavu ndo wanasainishana mikataba mibovu huku wakiramba ten /cnt zao nyie mnasema mnakimbia,kama sisi tunakimbia tueleze tunakimbiaje? Labda tunakimbia kwa riverse!
 
sisi vitalu tuliwapa kwa how much?
Ipo hivi. Assume mimi nina kiwanja 100mx100m=10,000 square meters City Centre. Unfortunately, sina uwezo wa kuendeleza au kuweka investment ya maana kutokana na eneo husika. Kisha, wewe unakuja na mwenzako (BG+Ophir) na kusema mna uwezo wa kuendeleza kiwanja husika kwa kujenga hiki na kile. Hapo nawaambia kwamba, mkitaka kiwanja changu, basi mradi ukikamilika mimi inabidi nipate 65% na nyinyi mchukue 35% ya mapato lakini. Lakini pamoja na hayo, nawaambia kwamba hicho kiwanja unachokiona leo; nimefanya hiki na kile; nimelipa watu kung'oa visiki; kulikuwa na dampo kubwa sana; nikalipa watu kulifukia kwahiyo ni lazima mnilipe kwanza hizo gharama! Hii maana yake ni nini? Kiwanja sitawauzia lakini gharama zilizofanikisha kiwanja kuwa hapo kilipo ni lazima mlipie.

Kumbuka kwamba, wewe umekuja na mwenzako ambao kwa ujumla wenu mtakuwa mnamiliki 35%...sasa assume katika hiyo 35%, wewe yako hapo ni only 25% ya hiyo 35%! Lakini ili muanze ujenzi, ni kwamba wewe na mwenzako mnabidi mchangie gharama za huo mradi. Sasa, inawezekana ukaona mfuko wako umepwaya kwahiyo wewe kama wewe unaamua kuuza sehemu ya umiliki wako wa ile 25% ya 35%(kuu ya wawili). Mzee mzima nakuibukia tena; nasema kwavile umeuza portion ya umiliki wako, nataka kodi yangu hapo hapo! Kwahiyo unanipa changu kwa roho safi, kisha mnaendelea na mambo yenu huku mkikumbuka kwamba 65% yangu ipo pale pale! Kwahiyo ikiwa mkataba ni kugawana vyumba kisha mkajenga jengo la vyumba 100, nabeba vyumba vyangu 65, nawaachia 35 vyenu.

Trust me, kama isingekuwa donda ndugu la ufisadi na wizi, deal la gesi lingeifikisha TZ level ya juu sana...wadau hawataki kabisa kuniunga mkono katika Approved Dictatorship Governance! Hii ndiyo njia pekee itakayopunguza ufisadi kwa kiasi kikubwa!
 
Ulifuatilia ITV jana kuhusu tathmini ya kisiasa na kiuchumi ya mwaka 2013. Hizo ni pea nut ulilinganisha na deposit za gas. Ni sawa na mikataba ya ma-chief wetu wa zamani waliodanganywa na wakoloni. Professor Mhongo hana tofauti na hao ma-chief ambao hawakujua kusoma na kuandika
 
Watu wenye uwezo finyu wa kuelewa wanaruka huku na kule kushangilia eti tumepata sh bilioni 400 out of $1.3 billion * 1,600= Shilingi 2,080,000,000,000 kwa maana nyingine rasilimali yetu imeifaidisha kampuni ya nje na kuweza kujizolea shilingi 1,680,000,000,000 (Trillioni 1.68) kweli wajinga ndio waliwao. Ushauri wangu capital gains iongezwe na kufikia 50% ili tufaidike zaidi badala 20%, ingekuwa capital gains ni 50% badala ya 20% basi nchi ingepata Shilingi Trilioni 1.04, shilingi bilioni 600 zaidi na ushee.

Acha niende barabarani nikatafute sheli inayojaza mafuta ya ndege. Most of us are like that, kama hiyo ni kodi aliyeuza kavuta ngapi? nngu kama mtu wa Mungu kimbia kamuombe Mungu wako atusaidie watanzania na vizazi vijavyo vinginevyo jidunge na valuer
 
BAK usiangalie muuzaji kauza kiasi gani kwa kuwa ni wazi kuwa hatukumpa bure hivyo vitalu....

Unless unambie faida alopata baada ya kutoa ela ya ununuzi na any additional investments ndio u conclude kuwa tumepata kidogo...still there is nothing we can do kwani ndio haki yetu kisheria

Hata wewe hapo ukiuza gari si unatakiwa ulipe kodi...unataka kunambia serikali itakuwa imekutendea haki ikichukua zaidi ya say 50% ya ela ulopata?


Mimi naona hiki kipato ni cha kujisifia kwa kuwa ndio haki yetu kisheria...sasa ukitaka kulalamika muuzaji kapata ngapi; basi tururdi bungeni kurekebisha sheria less than that tutakuwa wanyang'anyi...



Watu wenye uwezo finyu wa kuelewa wanaruka huku na kule kushangilia eti tumepata sh bilioni 400 out of $1.3 billion * 1,600= Shilingi 2,080,000,000,000 kwa maana nyingine rasilimali yetu imeifaidisha kampuni ya nje na kuweza kujizolea shilingi 1,680,000,000,000 (Trillioni 1.68) kweli wajinga ndio waliwao.
 
Yaliyofanyika hapa ni makosa makubwa sana ambayo yamelikosesha Taifa pesa nyingi sana. Tuambie Serikali imeuza kwa hivyo vitalu kwa bei gani? Mfano wa kuuza gari na kuuza rasilimali hauna mantiki hata kidogo. Kwanini capital gains iwe 20% badala ya 50%?

BAK usiangalie muuzaji kauza kiasi gani kwa kuwa ni wazi kuwa hatukumpa bure hivyo vitalu....

Unless unambie faida alopata baada ya kutoa ela ya ununuzi na any additional investments ndio u conclude kuwa tumepata kidogo...still there is nothing we can do kwani ndio haki yetu kisheria

Hata wewe hapo ukiuza gari si unatakiwa ulipe kodi...unataka kunambia serikali itakuwa imekutendea haki ikichukua zaidi ya say 50% ya ela ulopata?


Mimi naona hiki kipato ni cha kujisifia kwa kuwa ndio haki yetu kisheria...sasa ukitaka kulalamika muuzaji kapata ngapi; basi tururdi bungeni kurekebisha sheria less than that tutakuwa wanyang'anyi...
 
Kimsingi, Tanzania hapo haijapoteza chochote...kwenye hii mikataba, TPDC/Tanzania wanakuwa na 65% na mwekezaji anakuwa na 35%. So, unapoambiwa kwamba BG wana hisa 60%, maana yake ni kwamba ni 60% ya total 35% share. Maana yake ni kwamba, ikiwa project value ni sh. 100; TPDC zake ni sh. 65 na BG+Ophir zao ni sh 35. Sasa 60% ya sh. 35 ndiyo ya BG na inayobaki ndiyo ya Ophir(pamoja na Pavillion). Hiyo maana yake ni kwamba, aliyepungukiwa hapo ni Ophir ambae ameuza hisa lakini Tanzania hajakuwa affected in any way; sana sana wameanza kuvuna kabla ya wakati!

Biashara hii ni complicated kuliko unavyofikiria kwani mikataba hii ilisainiwa under kitu kinaitwa PSA.
Maelezo hayo hapo juu kama yangekuwa sahihi Tanzania ingepata pesa nyingi kuliko tulizoambiwa kwy article.
Tanzania itaendelea kuibiwa sana kama itaendelea kuwaficha wananchi(wenye mali) wake mikataba wanayosaini.

gas iliyouzwa kwa mujibu wa NYSE commodity market ina thamani ya $ 60 billions wao wameuza kwa dola bilioni 1.3 that is very questionable NASDAZ. Wameuza kwa almost 90% off ya thamani ya gas hiyo. Gas ni ya kwetu tunaambulia dola milioni 260 which is less than 1% ya thamani ya gas inayouzwa halafu unaita hii ni kufaidika come on ???

inabidi ufanye assumption nyingi sana ili kuamini kuwa nchi imepata faida lazima ukubali kuwa bei ya dola 1.3 bilioni ni sahihi na pili je serikali ilishirikishwa ktk mapatano ya bei hiyo?? ne je serikali haikuona haja ya wao wenyewe kutafuta mnunuzi mwingine atakayelipa pesa zaidi ya hizi hasa ukizingatia ndiye mwenye hisa kubwa?? je muhongo alishauri nini serikali ktk kukubali bei hii ?? je alifanya research kuakiki bei hii au alichukua 10% na hakuwa na haja ya kufanya uchunguzi wa bei wala nini kama wengine wanavyofanya?? cha msingi kama nilivyokuwambia thamani ya gas iliyouzwa ni dola bilioni 60 wewe unaambuliwa makusanyo ya capital gain tax ya dola milioni 260 . i am very skeptical na hili deal inawezekana muhongo amefaidika kuliko nchi yetu.
 
Ezekiel Kamwaga | Raia Mwema - Toleo la 331 | 25 Dec 2013


TANZANIA inatarajia kupata mgawo wa takribani shilingi bilioni 400 kutokana na mauzo ya hisa yaliyofanywa na kampuni ya Ophir kwa kampuni ya Pavillion katika vitalu vya gesi vilivyopo nchini, Raia Mwema limeambiwa.

Kampuni ya Ophir inamiliki asilimia 40 ya hisa katika vitalu namba 1, 3 na 4 huku asilimia nyingine 60 ikimilikiwa na kampuni ya BG, lakini Ophir wameamua kuuza hisa zao 20, mwaka huu.


Mauzo ya hisa hizo yanatarajiwa kuiingizia Ophir kiasi cha dola bilioni 1.3 (shilingi trilioni mbili) na kutokana na mauzo hayo, Tanzania itapata kiasi cha dola milioni 260 (shilingi bilioni 400) kama kodi.


Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufaidika na mauzo ya hisa za rasilimali zake kupitia Kodi ya Ongezeko la Mtaji (Capital Gain Tax) ambayo ilipitishwa na Bunge mwaka jana.

Kodi hiyo ilipitishwa na Sheria ya Fedha (Finance Act) ya mwaka 2012 baada ya kuwasilishwa kama mapendekezo binafsi na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe na kisha Bunge kuridhia.

Katika miaka ya nyuma, Tanzania haikuwa ikifaidika na mauzo yoyote ya hisa kwa makampuni yanayouziana rasilimali zake kwa sababu Kodi hiyo ya Ongezeko la Mtaji haikuwepo.


Kwa sababu mauzo hayo ya hisa yana thamani ya dola hizo bilioni 1.3, serikali ya Tanzania inatakiwa kupata asilimia 20 ya kiasi hicho ambayo ni dola milioni 260.

Akizungumza na Raia Mwema wiki hii, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, alisema wanatarajia kupata fedha hizo wakati wowote mauzo hayo yatakapopitishwa.

“Inategemea na namna hao wanaouziana hisa watakavyokubaliana lakini sisi tunafahamu tu kwamba wakimalizana, yetu itakuwa asilimia 20. Kwa vyovyote vile, inaonekana mauzo yanaweza kufanyika kwenye robo ya kwanza ya mwaka ujao wa 2014,” alisema Simbachawene.


Ophir ina makao yake makuu katika miji ya London, Uingereza na Perth nchini Australia na kwa mujibu wa tovuti yake, ilianzishwa mwaka 2004. Kampuni ya Pavillion Energy inamilikiwa na serikali ya Singapore.


Vitalu ambayo vimeuzwa katika uuzianaji huo vinaelezwa kuwa na ujazo wa mita za ujazo trilioni 15 na mauzo hayo pia yameenda sambamba na uuzaji wa hisa nyingine 17.6 katika makampuni yatakayokuwa yakifanya biashara za gesi hiyo hapa nchini.


Kwa mujibu wa Simbachawene, makampuni hayo matatu ni Ruvuma Pipeline Company Limited, Mzalendo Gas Processing Company Limited na Fahari Marketing Limited.


Simbachawene alisema nia ya serikali kwa sasa ni kutaka kutumia fedha hizo kwa ajili ya kulipa madeni na kuliboresha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ingawa alisema itategemea pia na mahitaji mengine yatakayokuwepo wakati fedha hizo zitakapopatikana.


“Hizi ni fedha za Watanzania wote na si za wizara yetu pekee. Tunataka kuliwezesha shirika letu la umeme ili lifanye kazi vizuri na kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa watu wengi zaidi.


“Hata hivyo, sisemi kwamba ni hela zote zitatumika kwa kazi hiyo au la lakini kuna mawazo hayo. Mambo mengine serikali itaamua kutokana na wakati fedha hizo zitakapopatikana. Huwezi kujua kutakuwa na nini wakati huo,” alisema Naibu Waziri huyo.


Alisema kwa miaka ya nyuma, Tanzania isingepata kitu kutokana na sheria zilizokuwepo na akasema serikali itajitahidi kuboresha sheria zake ili kuhakikisha inafaidika na utajiri uliokuwepo.


Mmoja wa wachambuzi wa masuala ya gesi aliyehojiwa na mtandao wa Bloomberg kuhusiana na uuzaji huu wa hisa, Tony Regan wa kampuni ya Tri Zen Inc alisema uamuzi wa kununua hisa hizo ni wa “roho ngumu” kwa sababu Tanzania ni eneo bichi kwenye sekta ya gesi.


“Mpaka sasa hakuna sheria rasmi iliyopitishwa kuhusiana na masuala ya gesi na hivyo Singapore inaingia katika eneo bichi kabisa katika sekta hii. Kumbuka pia kwamba gesi ya kwanza itaanza kuvunwa mwaka 2020 kutoka kwenye vitalu hivyo na utaona kwamba huu ni uamuzi mzito,” alisema.

CHANZO
: Raia Mwema - Waziri Muhongo anasa bil. 400/-

kama naiona minjino ya watu inavochelekea. naomba tujue hizo hela zitawanufaisha vipi watanzania!
 
Si ndio nakuuliza waliuza kwa kiasi gani? Na kama kuna kosa basi twende kwenye kubadili sheria kwa kuwa Muhongo alichofanya ni kusimamia utekelezaji washeria...

Badala ya kulalamikia case moja moja tunatakiwa tuweke institutions za kuondoa hizi lawama...

Wewe una propose tuchaji kiasi gani na kwa reference ipi? Wengine wanachaji kiasi gani?


Yaliyofanyika hapa ni makosa makubwa sana ambayo yamelikosesha Taifa pesa nyingi sana. Tuambie Serikali imeuza kwa hivyo vitalu kwa bei gani? Mfano wa kuuza gari na kuuza rasilimali hauna mantiki hata kidogo. Kwanini capital gains iwe 20% badala ya 50%?
 
BAK usiangalie muuzaji kauza kiasi gani kwa kuwa ni wazi kuwa hatukumpa bure hivyo vitalu....

Unless unambie faida alopata baada ya kutoa ela ya ununuzi na any additional investments ndio u conclude kuwa tumepata kidogo...still there is nothing we can do kwani ndio haki yetu kisheria

Hata wewe hapo ukiuza gari si unatakiwa ulipe kodi...unataka kunambia serikali itakuwa imekutendea haki ikichukua zaidi ya say 50% ya ela ulopata?


Mimi naona hiki kipato ni cha kujisifia kwa kuwa ndio haki yetu kisheria...sasa ukitaka kulalamika muuzaji kapata ngapi; basi tururdi bungeni kurekebisha sheria less than that tutakuwa wanyang'anyi...
Unajua nimegundua kwamba watu wengi hawafahamu vizuri haya mambo jinsi yanavyoenda...kimsingi wala hakuna tulichopteza ingawaje watu wanadhani tumepoteza. Kwenye sharing Agreement, Tanzania inapata 65% ya mapato ya gesi....kwahiyo hata wauziane mmoja baada ya mwingine lakini sisi 65% yetu ipo pale pale; sana sana tutakuwa tunachukua kodi yetu kila wanapouziana.

Labda watu wanapojichanganya ni kwamba wanachukulia uuzaji huu unafanana kama ilivyopata kufanyika kwa Sheraton Hotel and the like ambao kimsingi investor anauza; kisha anasepa wakati uuzaji wa aina hii ya sasa ni wa investor kuuza kwa ajili ya ku-accumulate capital....ni kama walivyofanya Swala Energy ambao wame-opt kuuza hisa DSE, hawa Ophir wame-opt kuuza hisa kwa one big investor.
 
Ipo hivi. Assume mimi nina kiwanja 100mx100m=10,000 square meters City Centre. Unfortunately, sina uwezo wa kuendeleza au kuweka investment ya maana kutokana na eneo husika. Kisha, wewe unakuja na mwenzako (BG+Ophir) na kusema mna uwezo wa kuendeleza kiwanja husika kwa kujenga hiki na kile. Hapo nawaambia kwamba, mkitaka kiwanja changu, basi mradi ukikamilika mimi inabidi nipate 65% na nyinyi mchukue 35% ya mapato lakini. Lakini pamoja na hayo, nawaambia kwamba hicho kiwanja unachokiona leo; nimefanya hiki na kile; nimelipa watu kung'oa visiki; kulikuwa na dampo kubwa sana; nikalipa watu kulifukia kwahiyo ni lazima mnilipe kwanza hizo gharama! Hii maana yake ni nini? Kiwanja sitawauzia lakini gharama zilizofanikisha kiwanja kuwa hapo kilipo ni lazima mlipie.

Kumbuka kwamba, wewe umekuja na mwenzako ambao kwa ujumla wenu mtakuwa mnamiliki 35%...sasa assume katika hiyo 35%, wewe yako hapo ni only 25% ya hiyo 35%! Lakini ili muanze ujenzi, ni kwamba wewe na mwenzako mnabidi mchangie gharama za huo mradi. Sasa, inawezekana ukaona mfuko wako umepwaya kwahiyo wewe kama wewe unaamua kuuza sehemu ya umiliki wako wa ile 25% ya 35%(kuu ya wawili). Mzee mzima nakuibukia tena; nasema kwavile umeuza portion ya umiliki wako, nataka kodi yangu hapo hapo! Kwahiyo unanipa changu kwa roho safi, kisha mnaendelea na mambo yenu huku mkikumbuka kwamba 65% yangu ipo pale pale! Kwahiyo ikiwa mkataba ni kugawana vyumba kisha mkajenga jengo la vyumba 100, nabeba vyumba vyangu 65, nawaachia 35 vyenu.

Trust me, kama isingekuwa donda ndugu la ufisadi na wizi, deal la gesi lingeifikisha TZ level ya juu sana...wadau hawataki kabisa kuniunga mkono katika Approved Dictatorship Governance! Hii ndiyo njia pekee itakayopunguza ufisadi kwa kiasi kikubwa!

kwako NASDAZ,
Napenda sana unavyojaribu kuwaelimisha wabongo kuhusu hii biashara ya gas lakini nigependa kukufanulia yafuatayo katika mikataba ya PSA .
hiyo asilimia 65 au 75 mnayogawana ni ya profit na siyo mapato kwani ktk mapato inabidi utoe gharama za uzalishaji halafu kilichobakia ndiyo hilo panga la hizo asilimia linapigwa. utata namba wani unakuwa ktk hili lifuatalo hatujui serikali ilichosaini kwenye kitu kinaitwa kitaalamu AFE hapo ndipo mara nyingi huwa serikali na nchi nyingi husika zinapopigwa bao. forget about profit, forget about revenue, forget about anything the most important document is AFE full stop
 
Back
Top Bottom