Waliouza viwanja kariakoo kwa bei waliyodhani wameula,leo hii wakiangalia bei za viwanja kariakoo wanaishia kupata maumivu ya vichwa,Ezekiel Kamwaga | Raia Mwema - Toleo la 331 | 25 Dec 2013
TANZANIA inatarajia kupata mgawo wa takribani shilingi bilioni 400 kutokana na mauzo ya hisa yaliyofanywa na kampuni ya Ophir kwa kampuni ya Pavillion katika vitalu vya gesi vilivyopo nchini, Raia Mwema limeambiwa.
Kampuni ya Ophir inamiliki asilimia 40 ya hisa katika vitalu namba 1, 3 na 4 huku asilimia nyingine 60 ikimilikiwa na kampuni ya BG, lakini Ophir wameamua kuuza hisa zao 20, mwaka huu.
Mauzo ya hisa hizo yanatarajiwa kuiingizia Ophir kiasi cha dola bilioni 1.3 (shilingi trilioni mbili) na kutokana na mauzo hayo, Tanzania itapata kiasi cha dola milioni 260 (shilingi bilioni 400) kama kodi.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufaidika na mauzo ya hisa za rasilimali zake kupitia Kodi ya Ongezeko la Mtaji (Capital Gain Tax) ambayo ilipitishwa na Bunge mwaka jana.
Kodi hiyo ilipitishwa na Sheria ya Fedha (Finance Act) ya mwaka 2012 baada ya kuwasilishwa kama mapendekezo binafsi na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe na kisha Bunge kuridhia.
Katika miaka ya nyuma, Tanzania haikuwa ikifaidika na mauzo yoyote ya hisa kwa makampuni yanayouziana rasilimali zake kwa sababu Kodi hiyo ya Ongezeko la Mtaji haikuwepo.
Kwa sababu mauzo hayo ya hisa yana thamani ya dola hizo bilioni 1.3, serikali ya Tanzania inatakiwa kupata asilimia 20 ya kiasi hicho ambayo ni dola milioni 260.
Akizungumza na Raia Mwema wiki hii, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, alisema wanatarajia kupata fedha hizo wakati wowote mauzo hayo yatakapopitishwa.
Inategemea na namna hao wanaouziana hisa watakavyokubaliana lakini sisi tunafahamu tu kwamba wakimalizana, yetu itakuwa asilimia 20. Kwa vyovyote vile, inaonekana mauzo yanaweza kufanyika kwenye robo ya kwanza ya mwaka ujao wa 2014, alisema Simbachawene.
Ophir ina makao yake makuu katika miji ya London, Uingereza na Perth nchini Australia na kwa mujibu wa tovuti yake, ilianzishwa mwaka 2004. Kampuni ya Pavillion Energy inamilikiwa na serikali ya Singapore.
Vitalu ambayo vimeuzwa katika uuzianaji huo vinaelezwa kuwa na ujazo wa mita za ujazo trilioni 15 na mauzo hayo pia yameenda sambamba na uuzaji wa hisa nyingine 17.6 katika makampuni yatakayokuwa yakifanya biashara za gesi hiyo hapa nchini.
Kwa mujibu wa Simbachawene, makampuni hayo matatu ni Ruvuma Pipeline Company Limited, Mzalendo Gas Processing Company Limited na Fahari Marketing Limited.
Simbachawene alisema nia ya serikali kwa sasa ni kutaka kutumia fedha hizo kwa ajili ya kulipa madeni na kuliboresha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ingawa alisema itategemea pia na mahitaji mengine yatakayokuwepo wakati fedha hizo zitakapopatikana.
Hizi ni fedha za Watanzania wote na si za wizara yetu pekee. Tunataka kuliwezesha shirika letu la umeme ili lifanye kazi vizuri na kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa watu wengi zaidi.
Hata hivyo, sisemi kwamba ni hela zote zitatumika kwa kazi hiyo au la lakini kuna mawazo hayo. Mambo mengine serikali itaamua kutokana na wakati fedha hizo zitakapopatikana. Huwezi kujua kutakuwa na nini wakati huo, alisema Naibu Waziri huyo.
Alisema kwa miaka ya nyuma, Tanzania isingepata kitu kutokana na sheria zilizokuwepo na akasema serikali itajitahidi kuboresha sheria zake ili kuhakikisha inafaidika na utajiri uliokuwepo.
Mmoja wa wachambuzi wa masuala ya gesi aliyehojiwa na mtandao wa Bloomberg kuhusiana na uuzaji huu wa hisa, Tony Regan wa kampuni ya Tri Zen Inc alisema uamuzi wa kununua hisa hizo ni wa roho ngumu kwa sababu Tanzania ni eneo bichi kwenye sekta ya gesi.
Mpaka sasa hakuna sheria rasmi iliyopitishwa kuhusiana na masuala ya gesi na hivyo Singapore inaingia katika eneo bichi kabisa katika sekta hii. Kumbuka pia kwamba gesi ya kwanza itaanza kuvunwa mwaka 2020 kutoka kwenye vitalu hivyo na utaona kwamba huu ni uamuzi mzito, alisema.
CHANZO: Raia Mwema - Waziri Muhongo anasa bil. 400/-
Ni jambo la kujivunia kuwa tunae waziri ambae ni msomi na muelewa wa mambo ya utawala na maendeleo. Na hakika amepewa wizara ambayo inafanana na professional yake na kwa bahati mbaya amewabana sana makanjanaja na matapeli wa mjin mpaka imekuwa nongwa.
Hizi siasa za kugombea fito Watanzania sijui sitatufikisha wapi! Hapo kila mmoja ame-play role yake vizuri! Zitto, kama mbunge ametekeleza wajibu wake na ameleta mswada wenye maslahi kwa taifa! Lakini Muhongo na wenzake nao wame-play part yao vizuri...kusimamia uuzaji na kuhakikisha taifa linapata stahiki yake. Hao wengine wasiolipa kodi si kwamba hakuna sheria; zipo na hawalipi. KImsingi hapa hoja sio hiyo mnayoshindana nayo nyie; hoja ni kwamba je, hizo 20% ambazo Ophir wameuza kwa USD 1.3 Billion, kweli hiyo ndiyo thamani waliyouza? Let me keep it this way ili mpate kunielewa. Assume unanunua gari Japan kwa USD 250 million. Lakini unafahamu wazi kwamba, hiyo gari ya USD 250 million, TRA watachukua nyingi sana za kwao. Ili kukwepa panga zito la TRA, unaamua ku-collude na Seller na kisha anaandika Stakabadhi mbili; moja anaandika USD 250 million(hii unabaki nayo) na nyingine anaandika USD 100million (ndiyo unayoenda kuonesha TRA). Hii ilikuwa inafanyika sana; tena sana hadi TRA walipoamua kuanza kufanya evaluation wenyewe! Sasa basi, kodi ambayo ilibidi itokane na USD 250million, will eventually come from USD 100 million! Meaning that, at the end of story, TRA watachukua chini ya 50% ya kodi halisi!!Soma vizuri,Mhe. Zitto Zuberi Kabwe ndie aliyeanzisha hii kitu ikawa sheria,sio waziri. All kudos to Mr ZZK
Nadhani hujafahamu vizuri jinsi haya mambo yanavyoenda. Tanzania haijapoteza chochote hapo, sana sana ime-gain.Waliouza viwanja kariakoo kwa bei waliyodhani wameula,leo hii wakiangalia bei za viwanja kariakoo wanaishia kupata maumivu ya vichwa, Ningefurahi kusikia serikali ndo imeuza hisa au vitalu hivyo kwa fedha hizo badala ya kuwagawia wajanja wakauza afu serikali ikapewa kodi tukashangilia kama mazuzu.
Tatizo letu watanzania hatupendi kuambiwa ukweli hasa na watanzania wenzetu. tumekuwa watu wa siasa wakati wote hata kwenye mambo ambayo siyo ya kisiasa. tunahitaji watu wa kutuambia hard truth ituume na mwisho tuifanyie kazi na siyo kulalama tu wakati dunia inakimbia kama usain bolt
Ipo hivi. Assume mimi nina kiwanja 100mx100m=10,000 square meters City Centre. Unfortunately, sina uwezo wa kuendeleza au kuweka investment ya maana kutokana na eneo husika. Kisha, wewe unakuja na mwenzako (BG+Ophir) na kusema mna uwezo wa kuendeleza kiwanja husika kwa kujenga hiki na kile. Hapo nawaambia kwamba, mkitaka kiwanja changu, basi mradi ukikamilika mimi inabidi nipate 65% na nyinyi mchukue 35% ya mapato lakini. Lakini pamoja na hayo, nawaambia kwamba hicho kiwanja unachokiona leo; nimefanya hiki na kile; nimelipa watu kung'oa visiki; kulikuwa na dampo kubwa sana; nikalipa watu kulifukia kwahiyo ni lazima mnilipe kwanza hizo gharama! Hii maana yake ni nini? Kiwanja sitawauzia lakini gharama zilizofanikisha kiwanja kuwa hapo kilipo ni lazima mlipie.sisi vitalu tuliwapa kwa how much?
Acha niende barabarani nikatafute sheli inayojaza mafuta ya ndege. Most of us are like that, kama hiyo ni kodi aliyeuza kavuta ngapi? nngu kama mtu wa Mungu kimbia kamuombe Mungu wako atusaidie watanzania na vizazi vijavyo vinginevyo jidunge na valuer
Watu wenye uwezo finyu wa kuelewa wanaruka huku na kule kushangilia eti tumepata sh bilioni 400 out of $1.3 billion * 1,600= Shilingi 2,080,000,000,000 kwa maana nyingine rasilimali yetu imeifaidisha kampuni ya nje na kuweza kujizolea shilingi 1,680,000,000,000 (Trillioni 1.68) kweli wajinga ndio waliwao.
BAK usiangalie muuzaji kauza kiasi gani kwa kuwa ni wazi kuwa hatukumpa bure hivyo vitalu....
Unless unambie faida alopata baada ya kutoa ela ya ununuzi na any additional investments ndio u conclude kuwa tumepata kidogo...still there is nothing we can do kwani ndio haki yetu kisheria
Hata wewe hapo ukiuza gari si unatakiwa ulipe kodi...unataka kunambia serikali itakuwa imekutendea haki ikichukua zaidi ya say 50% ya ela ulopata?
Mimi naona hiki kipato ni cha kujisifia kwa kuwa ndio haki yetu kisheria...sasa ukitaka kulalamika muuzaji kapata ngapi; basi tururdi bungeni kurekebisha sheria less than that tutakuwa wanyang'anyi...
Kimsingi, Tanzania hapo haijapoteza chochote...kwenye hii mikataba, TPDC/Tanzania wanakuwa na 65% na mwekezaji anakuwa na 35%. So, unapoambiwa kwamba BG wana hisa 60%, maana yake ni kwamba ni 60% ya total 35% share. Maana yake ni kwamba, ikiwa project value ni sh. 100; TPDC zake ni sh. 65 na BG+Ophir zao ni sh 35. Sasa 60% ya sh. 35 ndiyo ya BG na inayobaki ndiyo ya Ophir(pamoja na Pavillion). Hiyo maana yake ni kwamba, aliyepungukiwa hapo ni Ophir ambae ameuza hisa lakini Tanzania hajakuwa affected in any way; sana sana wameanza kuvuna kabla ya wakati!
Inawezekana mimi sijui ila katika Trillion 2 ya mali yetu tunaambulia Bil 400?
Am I dumb or what? Nisaidieni kunielimisha hapa sijaelewa kabisa!
Ezekiel Kamwaga | Raia Mwema - Toleo la 331 | 25 Dec 2013
TANZANIA inatarajia kupata mgawo wa takribani shilingi bilioni 400 kutokana na mauzo ya hisa yaliyofanywa na kampuni ya Ophir kwa kampuni ya Pavillion katika vitalu vya gesi vilivyopo nchini, Raia Mwema limeambiwa.
Kampuni ya Ophir inamiliki asilimia 40 ya hisa katika vitalu namba 1, 3 na 4 huku asilimia nyingine 60 ikimilikiwa na kampuni ya BG, lakini Ophir wameamua kuuza hisa zao 20, mwaka huu.
Mauzo ya hisa hizo yanatarajiwa kuiingizia Ophir kiasi cha dola bilioni 1.3 (shilingi trilioni mbili) na kutokana na mauzo hayo, Tanzania itapata kiasi cha dola milioni 260 (shilingi bilioni 400) kama kodi.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kufaidika na mauzo ya hisa za rasilimali zake kupitia Kodi ya Ongezeko la Mtaji (Capital Gain Tax) ambayo ilipitishwa na Bunge mwaka jana.
Kodi hiyo ilipitishwa na Sheria ya Fedha (Finance Act) ya mwaka 2012 baada ya kuwasilishwa kama mapendekezo binafsi na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe na kisha Bunge kuridhia.
Katika miaka ya nyuma, Tanzania haikuwa ikifaidika na mauzo yoyote ya hisa kwa makampuni yanayouziana rasilimali zake kwa sababu Kodi hiyo ya Ongezeko la Mtaji haikuwepo.
Kwa sababu mauzo hayo ya hisa yana thamani ya dola hizo bilioni 1.3, serikali ya Tanzania inatakiwa kupata asilimia 20 ya kiasi hicho ambayo ni dola milioni 260.
Akizungumza na Raia Mwema wiki hii, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, alisema wanatarajia kupata fedha hizo wakati wowote mauzo hayo yatakapopitishwa.
Inategemea na namna hao wanaouziana hisa watakavyokubaliana lakini sisi tunafahamu tu kwamba wakimalizana, yetu itakuwa asilimia 20. Kwa vyovyote vile, inaonekana mauzo yanaweza kufanyika kwenye robo ya kwanza ya mwaka ujao wa 2014, alisema Simbachawene.
Ophir ina makao yake makuu katika miji ya London, Uingereza na Perth nchini Australia na kwa mujibu wa tovuti yake, ilianzishwa mwaka 2004. Kampuni ya Pavillion Energy inamilikiwa na serikali ya Singapore.
Vitalu ambayo vimeuzwa katika uuzianaji huo vinaelezwa kuwa na ujazo wa mita za ujazo trilioni 15 na mauzo hayo pia yameenda sambamba na uuzaji wa hisa nyingine 17.6 katika makampuni yatakayokuwa yakifanya biashara za gesi hiyo hapa nchini.
Kwa mujibu wa Simbachawene, makampuni hayo matatu ni Ruvuma Pipeline Company Limited, Mzalendo Gas Processing Company Limited na Fahari Marketing Limited.
Simbachawene alisema nia ya serikali kwa sasa ni kutaka kutumia fedha hizo kwa ajili ya kulipa madeni na kuliboresha Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ingawa alisema itategemea pia na mahitaji mengine yatakayokuwepo wakati fedha hizo zitakapopatikana.
Hizi ni fedha za Watanzania wote na si za wizara yetu pekee. Tunataka kuliwezesha shirika letu la umeme ili lifanye kazi vizuri na kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme kwa watu wengi zaidi.
Hata hivyo, sisemi kwamba ni hela zote zitatumika kwa kazi hiyo au la lakini kuna mawazo hayo. Mambo mengine serikali itaamua kutokana na wakati fedha hizo zitakapopatikana. Huwezi kujua kutakuwa na nini wakati huo, alisema Naibu Waziri huyo.
Alisema kwa miaka ya nyuma, Tanzania isingepata kitu kutokana na sheria zilizokuwepo na akasema serikali itajitahidi kuboresha sheria zake ili kuhakikisha inafaidika na utajiri uliokuwepo.
Mmoja wa wachambuzi wa masuala ya gesi aliyehojiwa na mtandao wa Bloomberg kuhusiana na uuzaji huu wa hisa, Tony Regan wa kampuni ya Tri Zen Inc alisema uamuzi wa kununua hisa hizo ni wa roho ngumu kwa sababu Tanzania ni eneo bichi kwenye sekta ya gesi.
Mpaka sasa hakuna sheria rasmi iliyopitishwa kuhusiana na masuala ya gesi na hivyo Singapore inaingia katika eneo bichi kabisa katika sekta hii. Kumbuka pia kwamba gesi ya kwanza itaanza kuvunwa mwaka 2020 kutoka kwenye vitalu hivyo na utaona kwamba huu ni uamuzi mzito, alisema.
CHANZO: Raia Mwema - Waziri Muhongo anasa bil. 400/-
Yaliyofanyika hapa ni makosa makubwa sana ambayo yamelikosesha Taifa pesa nyingi sana. Tuambie Serikali imeuza kwa hivyo vitalu kwa bei gani? Mfano wa kuuza gari na kuuza rasilimali hauna mantiki hata kidogo. Kwanini capital gains iwe 20% badala ya 50%?
Unajua nimegundua kwamba watu wengi hawafahamu vizuri haya mambo jinsi yanavyoenda...kimsingi wala hakuna tulichopteza ingawaje watu wanadhani tumepoteza. Kwenye sharing Agreement, Tanzania inapata 65% ya mapato ya gesi....kwahiyo hata wauziane mmoja baada ya mwingine lakini sisi 65% yetu ipo pale pale; sana sana tutakuwa tunachukua kodi yetu kila wanapouziana.BAK usiangalie muuzaji kauza kiasi gani kwa kuwa ni wazi kuwa hatukumpa bure hivyo vitalu....
Unless unambie faida alopata baada ya kutoa ela ya ununuzi na any additional investments ndio u conclude kuwa tumepata kidogo...still there is nothing we can do kwani ndio haki yetu kisheria
Hata wewe hapo ukiuza gari si unatakiwa ulipe kodi...unataka kunambia serikali itakuwa imekutendea haki ikichukua zaidi ya say 50% ya ela ulopata?
Mimi naona hiki kipato ni cha kujisifia kwa kuwa ndio haki yetu kisheria...sasa ukitaka kulalamika muuzaji kapata ngapi; basi tururdi bungeni kurekebisha sheria less than that tutakuwa wanyang'anyi...
Ipo hivi. Assume mimi nina kiwanja 100mx100m=10,000 square meters City Centre. Unfortunately, sina uwezo wa kuendeleza au kuweka investment ya maana kutokana na eneo husika. Kisha, wewe unakuja na mwenzako (BG+Ophir) na kusema mna uwezo wa kuendeleza kiwanja husika kwa kujenga hiki na kile. Hapo nawaambia kwamba, mkitaka kiwanja changu, basi mradi ukikamilika mimi inabidi nipate 65% na nyinyi mchukue 35% ya mapato lakini. Lakini pamoja na hayo, nawaambia kwamba hicho kiwanja unachokiona leo; nimefanya hiki na kile; nimelipa watu kung'oa visiki; kulikuwa na dampo kubwa sana; nikalipa watu kulifukia kwahiyo ni lazima mnilipe kwanza hizo gharama! Hii maana yake ni nini? Kiwanja sitawauzia lakini gharama zilizofanikisha kiwanja kuwa hapo kilipo ni lazima mlipie.
Kumbuka kwamba, wewe umekuja na mwenzako ambao kwa ujumla wenu mtakuwa mnamiliki 35%...sasa assume katika hiyo 35%, wewe yako hapo ni only 25% ya hiyo 35%! Lakini ili muanze ujenzi, ni kwamba wewe na mwenzako mnabidi mchangie gharama za huo mradi. Sasa, inawezekana ukaona mfuko wako umepwaya kwahiyo wewe kama wewe unaamua kuuza sehemu ya umiliki wako wa ile 25% ya 35%(kuu ya wawili). Mzee mzima nakuibukia tena; nasema kwavile umeuza portion ya umiliki wako, nataka kodi yangu hapo hapo! Kwahiyo unanipa changu kwa roho safi, kisha mnaendelea na mambo yenu huku mkikumbuka kwamba 65% yangu ipo pale pale! Kwahiyo ikiwa mkataba ni kugawana vyumba kisha mkajenga jengo la vyumba 100, nabeba vyumba vyangu 65, nawaachia 35 vyenu.
Trust me, kama isingekuwa donda ndugu la ufisadi na wizi, deal la gesi lingeifikisha TZ level ya juu sana...wadau hawataki kabisa kuniunga mkono katika Approved Dictatorship Governance! Hii ndiyo njia pekee itakayopunguza ufisadi kwa kiasi kikubwa!