PreGE2025 Waziri mkuu: Serikali tutahakikisha uchaguzi unakuwa wa amani na utulivu, Tume huru ya uchaguzi wametuambia watausimamia kwa uhuru, haki na uwazi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
"2025 huu ni mwaka wa uchaguzi, sisi kama serikali, kama wadau wa uchaguzi, pindi tume huru ya uchaguzi watatoa ratiba tunatarajia nyie ndiyo mtalieleza taifa (Wanahabari) na sisi ushiriki wetu ni kuhakikisha kwamba yale yaliyo muhimu ya kuufanya uchaguzi huu kuwa wa usalama, na kila mmoja atakwenda kushiriki kwa usalama wake.. Na watu wa tume huru ya uchaguzi wametuambia kwamba uchaguzi huu watausimamia kwa uhuru na haki na uwazi. Na sisi serikali kama wadau wa uchaguzi tunataka tuwahakikishie kuwa uchaguzi huu utakuwa ni wa amani na utulivu" -

Waziri mkuu Kassim Majaliwa ameyasema hayo katika Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, (World Press Freedom Day 2025) yaliyofanyika jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 kwenye Hoteli ya Gran Melia

Your browser is not able to display this video.
 
Unaweza kudanganya watu kwa muda fulani, lakini siyo siku zote.

Mwaka jana 2024 walisema hivyo hivyo, halafu Mchengerwa na genge lake kwa kushirikiana na hao Tume "Huru" wakaiba uchaguzi wote, uchaguzi mzima..
Eti ccm wakashinda kwa 99.9% !!

Hawa hawana hata haya, hawajui kuwa ukila na kipofu unambakizia angalau kidogo, wao wanakomba na kumaliza kabisa!!!

Huu uhuni ndo umeibua kaulimbiu ya 'No Reforms No Election', ambayo sasa inakubalika na kutakiwa na wananchi wengi ili kurejesha heshima ya sanduku la kura iliyonajisiwa na watawala
 
Maneno haya haya yamekuwa yakitamkwa kila uchafuzi. maneno ya kijinga kabisa kuwaona watu wajinga wataupokea ujinga huo!
Mnastahili adhabu kali toka kwa Mungu wa Mbinguni
 
It is not a matter of kuhakikisha kama nyinyi kama serikali, NO, A BIG NO!. It should be a matter of kuweka sytems ambazo ni impartial/independent approved by all stakeholders, NOT CCM ALONE!
 
huyu naye kwa sasa yupoyupo tu alimradi cku ziende,mdomo hauna ushirikiano na ubongo kwa anachokiongea
 
Hakupaswa kuwepo katika nafasi hiyo huyu ndio wanaoiba na kubaka haki ya kuchaguliwa. Alipita bila kupingwa.
 
Kwani miaka yote wakiiba na kuchafua michakato ya uchaguzi walisema wataiba? Inahitaji akili ya mwenda wazimu kuiamini serikali ya CCM na vyombo vyake.
 
Hawa jamaa wanavyo ongea kwa madaha na kwa kujiamini, unaweza ukafikiri wako kwenye dunia ya peke yao. Yaani watu wanataka hivi, wenyewe wanaleta story tofauti kabisa! Sijui ni kwa nini wana kiburi, kejeli na dharau kiasi hiki.
Bila kupata vijana wazalendo aina ya Captain Ibrahim Traore ndani ya JWTZ nchi hii haitakaa ipate maendeleo daima.
 
Ewee bwana Majaliwa, muwe mnaona AIBU basi hata kidogo..MMEROGWA na nani??..bila marekebisho ya Katiba na tume ya Uchaguzi, hizi ni PORoJO tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…