Waziri Mkuu aagiza daktari akamatwe baada ya wananchi kusimamisha msafara wake na kulalamika

Waziri Mkuu Majaliwa Kassim ameagiza Daktari wa Kituo cha Afya Mahuta Mtwara akamatwe, ni baada ya Wananchi kudai anahusika na wizi wa dawa kunakosababisha Wagonjwa kukosa dawa

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo baada ya Wananchi kusimamisha msafara wake [HASHTAG]#MillardAyoUPDATES[/HASHTAG]


Je alichofanya waziri mkuu ni sahihi? Je kama wananachi hawakuwa sahihi si atakuwa kamfedhehesha huyo daktari?
d61ccab0ac5475cad5ef96860b267222.jpg
Kama uhakiki utaonyesha hakuiba atafidiwaje? Na hao wananchi watafanywaje,? Naona kama bado tuko kwenye kipindi cha kampeni.
 
Wizi wa dawa na waganga wa Zahanati mkuu ni janga la taifa,kama lilivyo tatizo la matumizi mabaya ya fedha za Halimashauri na Wakurugenzi wa Wilaya.Naamini wananchi hawakukurupuka.Akamatwe tu.
Hili si swala la imani. Lazima uthibitishe kabla ya kuchukua hatua. WM angeamuru uhakiki ufanywe halafu mhusika akamatwe ikithibitika.
 
Wizi wa dawa na waganga wa Zahanati mkuu ni janga la taifa,kama lilivyo tatizo la matumizi mabaya ya fedha za Halimashauri na Wakurugenzi wa Wilaya.Naamini wananchi hawakukurupuka.Akamatwe tu.
una ushahidi kama kaiba au zinaibiwa,
 
Sawa we mkubwa,hivi si kuna registers zinazoonesha kiasi cha dawa kilichoingia na kutolewa(kutumika), je hao wananchi wana access kwa hizo taarifa au PM amejiridhisha kwa kuangalia hizo registers kisha kutoa hili agizo la daktari kukamatwa?


Unataka kuniambia hizo registers zama za Kikwete zikikuwa hazipo? Jibu ni zilikuwepo always na bado jamaa wakawa wanakula njama kuhujumbu nchi kwa kuuziana dawa. Nilipokuwa nafanya kazi katika almashauri (jina kapuni) moja ya kazi zangu ilikuwa ni ukusanyaji data kama hizi na michezo michafu tuliijuwa na kutonya viongozi wetu. Kwa bahati mbaya hata viongozi wetu nao walihusika na ushenzi huu wa kuidanganya serikali.
 
Hivi mnakumbuka serikali hii wakati inaingia madarakani,Pm aliwahi kumsimamisha Dr mbele ya watu huko Mtwara na kuamuru akamatwe kwa madai amepokea pesa kwa mgonjwa ikiaminika ni rushwa.Mlishajiuliza ile kesi iliishia wapi?.
 
Huyo daktari kaonewa tu. Hawezi kuiba dawa hata siku moja. Tatizo ni serikali yenyewe ambayo haisambazi dawa za kutosha mahospitalini na kwenye vituo vya afya.
 
Huyu naye hajifunzi?

Kuna wakati alikurupuka na kumsimamisha daktari bingwa kwa madai amemwomba mgonjwa rushwa ya laki 1 kumbe ndiyo cost sharing iliyopangwa na hospitali kwa huduma ya upasuaji.

Baadaye wakaishia kumwomba msamaha daktari ambaye ndiye alikuwa daktari pekee bingwa wa upasuaji kwenye hospitali ya mkoa. Akawagomea.

Watanzania wengi ni waongo, watu wenye roho za husda, tena waliojawa na mioyo ya umaskini. Mtu yeyote wakiona ana kitu, wazo lao la kwanza, ni mwizi.

Kiongozi huwezi kutoa maamuzi barabarani kwa kitu ambacho hakijafanyiwa uchunguzi.

PM alikuwa na uafadhali lakini naona naye ameanza kuambukizwa tabia za kukurupuka. Pathetic!
 
Hao wananchi wanafikra Duni hasa!! Huwajui kuwa hakuna kitu toka juu!! Heri wangejua!! Huyo Dr ataondoka na hakuna dawa milele wapambane kuvyao hali zao! Heri wangesema mbolea hakuna sio dawa
 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim ameagiza Daktari wa Kituo cha Afya Mahuta Mtwara akamatwe, ni baada ya Wananchi kudai anahusika na wizi wa dawa kunakosababisha Wagonjwa kukosa dawa

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo baada ya Wananchi kusimamisha msafara wake [HASHTAG]#MillardAyoUPDATES[/HASHTAG]


Je alichofanya waziri mkuu ni sahihi? Je kama wananachi hawakuwa sahihi si atakuwa kamfedhehesha huyo daktari?
d61ccab0ac5475cad5ef96860b267222.jpg
Hii serikali ya awamu ya tano imethibitisha kuwa haina uwezo, ila inachofanya ni "show tu". Unamsimamishaje mtumishi wa umma kwa tuhuma za kutolewa barabarani? Sawa inawezekana tuhuma hzo zikawa na ukweli (labda?), lakini kufanya kilichofanywa na PM ni kukaribisha vurugu na kudhalilishana, jambo ambalo linapunguza tija katika utendaji kazi. PM amefungua ukurasa ambapo mwananchi, kwa chuki zake tu, anaweza kumtuhumu mtumishi wa umma.
 
Huyu naye kaanza kuambukizwa ujinga. Umemsikia mganga amesemaje? Mnawadekeza wananchi kijinga halafu mnadhalilisha taaluma za watu. Pathetic!
 
First uchunguzi ungefanyika akibainika kama kuna ukweli angechukuliwa hatua stahiki
 
Unataka kuniambia hizo registers zama za Kikwete zikikuwa hazipo? Jibu ni zilikuwepo always na bado jamaa wakawa wanakula njama kuhujumbu nchi kwa kuuziana dawa. Nilipokuwa nafanya kazi katika almashauri (jina kapuni) moja ya kazi zangu ilikuwa ni ukusanyaji data kama hizi na michezo michafu tuliijuwa na kutonya viongozi wetu. Kwa bahati mbaya hata viongozi wetu nao walihusika na ushenzi huu wa kuidanganya serikali.
inaonesha una hasira sana na kikwete!
 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim ameagiza Daktari wa Kituo cha Afya Mahuta Mtwara akamatwe, ni baada ya Wananchi kudai anahusika na wizi wa dawa kunakosababisha Wagonjwa kukosa dawa

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo baada ya Wananchi kusimamisha msafara wake [HASHTAG]#MillardAyoUPDATES[/HASHTAG]


Je alichofanya waziri mkuu ni sahihi? Je kama wananachi hawakuwa sahihi si atakuwa kamfedhehesha huyo daktari?
d61ccab0ac5475cad5ef96860b267222.jpg
Hayo ni majukumu ya taasisi zenye mamlaka za kiuchunguzi juu yake, ila waziri mkuu kama mtendaji mkuu wa serikali, alichokifanya yuko sahihi. Ni mwanakijiji gani atakayependa daktari wao mzuri, mwenye weledi na maadili aondolewe?
 
Back
Top Bottom