robinson crusoe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2020
- 831
- 1,379
Hali ya Tanzania kwa sasa ufisadi hakuna sababu ya kusema kuna ufisadi, kwa sababu ni kama imeruhusiwa na viongozi wa nchi, lakini ni vibaya sana kwa tunaoona yanyaofanyika kunyamaza bila sababu pia.
Waziri Mkenda anaendelea kung'ang'ania sula la Samia scholarship kwa kisingizio cha kuinua sayansi nchini. Sayansi haiwezi kuinuka kwa kuwapa upendeleo wanafunzi waliosoma shule za upendeleo na kupata matokeo mazuri, huku ukiwaacha maeffu ktk shule za serikali wakiwa hawana waalimu.
Lakini kibaya zaidi, sasa wanafunzi wanachaguliwa kwa kufuata familia zao na uwezo wa kuhonga watendaji wa Wizara. Kuna wanafunzi ambao wana ushindi mzuri, lakini wameachwa. Ujinga mkubwa unakuta wananfunzi wametoka shule moja, lakiniu aliyewazidi kwa ushindi anaachwa, anachukuliwa mwingine.
Hii ni wizara eti waziri ni profesa, katibu mkuu naye eti ni profesa, na yote haya yanafanyika wakiyapa baraka.
Waziri Mkenda anaendelea kung'ang'ania sula la Samia scholarship kwa kisingizio cha kuinua sayansi nchini. Sayansi haiwezi kuinuka kwa kuwapa upendeleo wanafunzi waliosoma shule za upendeleo na kupata matokeo mazuri, huku ukiwaacha maeffu ktk shule za serikali wakiwa hawana waalimu.
Lakini kibaya zaidi, sasa wanafunzi wanachaguliwa kwa kufuata familia zao na uwezo wa kuhonga watendaji wa Wizara. Kuna wanafunzi ambao wana ushindi mzuri, lakini wameachwa. Ujinga mkubwa unakuta wananfunzi wametoka shule moja, lakiniu aliyewazidi kwa ushindi anaachwa, anachukuliwa mwingine.
Hii ni wizara eti waziri ni profesa, katibu mkuu naye eti ni profesa, na yote haya yanafanyika wakiyapa baraka.