Waziri Mbarawa azidi kulikoroga miradi ya Maji

Waziri Mbarawa azidi kulikoroga miradi ya Maji

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
17,547
Reaction score
28,494
20191203_183312.jpg

Nipashe leo 3 Dec 2019.

Waziri wa Maji Mh. Prof Makame Mbarawa ameamua kuachana na makandarasi.
Eti sasa atajenga miradi ya Maji kwa Force Account.

Hiki kiutendaji ni kichekesho na upotezaji wa fedha ya umma.

Hakuna asiyeona kwa macho mabomba yanayotiririka kwa siku kadhaa kabla DAWASA, MWAUWASA, MORUWASA su Ma ...UWASA mengine hawajastuka.
Eti watendaji wa Wizara walioshindwa kuwasimamia ma consultants na makandarasi sasa watatekeleza miradi wenyewe.
Siye tupo tupo tunamtakia heri, lakini kesha jipalia lawama.
 
Hizo bangi sijui huwa mnavutia wapi?Kwa kifupi kila kazi ina alternatives zake.
 
Dogo wakuoe wewe tukuone maana unajifanya unajua sana kukosoa
 
Nafikiri Mbarawa hajaona malalamiko ya Waziri Mkuu Majaliwa au Profesa mwenziwe Ndalichako juu ya TBA na Force account zao.
 
Kwenu wanaokosoa wanaolewa?
Pole ndo maana hamuendelei.

Naona huyo uliyemquote hakutaka kusema uolewe bali spelling error badala ya wakupe likawa wakuoe. Hilo tatizo naliona sana unapoondika neno hilo wakupe.
 
Sawa serekali inataka kufanya kila kitu sawa
 
Kituko ni wewe mlalamikaji ukiona bomba limepasuka hutoi taarifa.
Elewa maana ya miradi na maintainance.
Tatizo kila kiongozi hata akiwa profesa kujidai kujua tasnia ya ujenzi, kumbe ukweli hawajui kitu maana sio tu hawakusomea bali hawachukui ushauri wa wataalam wa ujenzi.
 
Mkuu Jidu, kwa matumizi ya Force Account katika utekelezaji wa miradi, Prof. Mbarawa yuko right 100%, utaratibu huu uta save time, money and resources.

Kwa kawaida miradi inatekelezwa na makampuni ya makandarasi, makandarasi hao kuleta quotations za gharama kubwa ikiwemo consultancy fee kubwa, watekelezaji wa ujenzi ni local funds ambao watalipwa fedha mdogo tuu kama vibarua, kazi ya mkandarasi ni kugundua vifaa kwa bei ya juu baada ya kuweka cha juu, kisha kuwasimamia local fundis ambao ndio wanafanya all donkey jobs.

Matumizi ya Force Account ni kuiruhusu kuwa engage hawa local fundis directly na kusimamiwa na regional engineers, hivyo kununua vifaa locally na kuanza kujenga fasta bila lengthy tendering process, na ku save money kwenye makandarasi ambao huweka cha juu kikubwa, gharama zao za juu, kupelekea mradi kuwa ghali wakati ukitumia local fundis gharama ni nusu tuu.

Changamoto pekee za utaratibu huu ni 3.
1. Sheria zinataka miradi fulani ya thamani fulani lazima isimamiwe na contractors wa viwango fulani, mfano consulting engineer, structural engineers, electrical engineers, quantity engineers, etc, sasa hawa regional engineers wanaweza?.
2. Vifaa vya quality, lengo la local fundis ni saving money not quality, vifaa quality vya ujenzi ni gharama na vinapatika maduka mahsus huku Wachina wame flood cheap counterfeit products maduka ya mitaani, ambayo kwa local fundis ndio their best option.
3. Miongoni mwa cost kubwa za contractors ni guarantee na insurance, when things go wrong, kwa kutumia local fundis, there is no guarantee na no insurance likitokea la kutokea hivyo there is nobody to cover the losses.

P
 
Nafikiri hiyo ndio sababu ya Serikali kuunda Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA). Kupitia RUWASA kama ilivyo TANROAD wizara inaweza kusimamia miradi kama habari inavyojieleza hapo juu.

Nimejaribu sana kuwafuatilia hawa jamaa wa RUWASA nimeona wamejipanga na wana kitu cha kufanya katika kutatua changamoto na kero za maji. Kabla ya kulalamika tujipe muda wa kufuatilia mabadiliko mbali mbali ya kiufundi na kimuundo ktk wizara zetu. Tuwape muda tuone ni kwa namna gani mamlaka hii itakuja na majibu ya maswali ya watanzania wengi kuhusu upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama bombani na si visimani na mitoni.
 
Back
Top Bottom