Waziri Masha ajikanganya?

Unajua Masha alizani kwa lile bit Mengi angenywea.
Anazani ni zama zile kiongozi akipiga bit unanywea sasa Mengi kakomaa Masha kaamua anywee.
Iyo ni fundisho as next time hatorudia tena kupiga bit watu wazima na akili zao
 
Haikubaliki si Tanzania wala penginepo kwa kiongozi kama Waziri kutoa kauli ambazo hawezi kuzisimamia au hamaanishi anachokisema. Kwa kiongozi yoyote au Masha kufanya alichofanya Masha au kifananacho na hicho ina maana ya kati ya haya hapa chini:
- Hakuwa serious na kauli aliyoitoa, hivyo anatania umma wa Watanzania; au
- Hawezi kusimamia maamuzi yake - he therefore dont mean business;
How can we take him seriously next time anatoa statement au agizo?
 
Haikubaliki si Tanzania wala penginepo kwa kiongozi kama Waziri kutoa kauli ambazo hawezi kuzisimamia au hamaanishi anachokisema. Kwa kiongozi yoyote au Masha kufanya alichofanya Masha au kifananacho na hicho ina maana ya kati ya haya hapa chini:
- Hakuwa serious na kauli aliyoitoa, hivyo anatania umma wa Watanzania; au
- Hawezi kusimamia maamuzi yake - he therefore dont mean business;
How can we take him seriously next time anatoa statement au agizo?

Hapo umegusa kwenye mhimili wa hoja yenyewe. Kwa maana hiyo ameidhalilisha ofisi ya Waziri wa Mambo ya ndani. Sasa baada ya hapo anabaki na uwaziri wa nini? Hapa hakuna mchezo wa watoto wa kidali po! Ama unafanya kazi (you mean business) au unawaachia wengine wanakusaidia. Wapo wengi wenye uwezo hata kama si wana mtandao. Lakini kama atang'ang'ania basi inabidi aogopwe kama ukoma. Kwani akikutana na mnyonge atamsulubisha msalabani. Nao hao ndio tuko wengi.
 
masha bwana alikurupuka tu,yeye na aam malima ndo wana huo mpango wa kumfilisi mengi.

kimsingi hafai kuwa waziri wa wizara nyeti kama anayooongoza.anashindwa hata na mrema ambaye kamwe alikuwa harudi nyuma kwenye maamuzi yake.

huyu masha ni kijana wa mjini tu anashinda rose gadeni anakunywa bia.hamuwezi mengi mtoto mdogo sana huyu.
 
Unajua ndugu yangu kuna Wizara ambazo ukimpa kijana chini ya miaka 50 umechemsha.

King'eng'e kuna kitu kama vile: 'nothing, nothing beats experience!' Hatu uwe na digrii saba lakini kama huna experience kuna kazi zingine mtu hastahili kuzishika, maana baada ya muda si mrefu atatokota tuu!
 
Unajua ndugu yangu kuna Wizara ambazo ukimpa kijana chini ya miaka 50 umechemsha.

King'eng'e kuna kitu kama vile: 'nothing, nothing beats experience!' Hatu uwe na digrii saba lakini kama huna experience kuna kazi zingine mtu hastahili kuzishika, maana baada ya muda si mrefu atatokota tuu!

Hii sikubaliani nayo...wamerekani wangemchangua Mcain kama kigezo ni umri!
 
Mkuu Mwanakijiji, kupima upepo wa kasheshe lenyewe ndio ukubwa.Masha atapata credits kwa kukaa kumya baada ya kuona sakata lenyewe halimsaidii kwa vyovyote,sana sana litamharibia.Waswahili walisema"funika kombe wa....... wapite"

Basi ni bora Masha asahihishe kauli yake ya awali ya vitisho kwa mengi la sivyo awajibike kwa kutishia raia wakati yeye ndio wa kumlinda.
 
Hivi ile sheria ambayo inayo mkataza mtu mmoja kutomiliki RAdio,TV na Gazeti kwa wakati mmoja itaanzishwa TAnzania..?

Nahisi ni wakati muafaka sasa kuianzisha kabla suala hili halijaleta madhara makubwa
 
Mzee mwanakijiji usikasilike unapokosolewa, otherwise inabidi tukutambue kama kibalaka wa Masha.

Ningekuwa mtu ninayekasirika hivyo ningekuwa nimekunywa sumu zamani. Ukijisikia kukosoa; kosoa tu. Usijali hisia zangu. Na ukitaka kunitambua kuwa ni kibaraka wa Masha go ahead. Ningekuwa najali watu wanavyonifikiria, ningenyemaza siku nyingi kweli. Be my guest.
 
Ipo siku mungu atatuonyesha who real mengi is!!!!

Mkuu labda wewe ndio humjui, Mengi anajulikana ni nani, alitoka wapi, yuko wapi na anaelekea wapi na hatuhitaji Mungu kutuambia. Mungu is extreeeemly busy for other issues, kutuonesha Mengi ni nani wakati pembe/masikio na meno/magego yake yanaonekana ni kushusha hadhi ya Mungu!
 
Hivi ile sheria ambayo inayo mkataza mtu mmoja kutomiliki RAdio,TV na Gazeti kwa wakati mmoja itaanzishwa TAnzania..?

Nahisi ni wakati muafaka sasa kuianzisha kabla suala hili halijaleta madhara makubwa

Waache waparurane kwanza mpaka waombe msaada kwa wanyonge, ingawa ni ngumu! Kazi kubwa ni kuwapa Watanzania elimu ya kutosha waweze kupima kwa uwezo wao pumba na mchele

ndimi
Zawadi ya Ualimu
 
Mwanakijiji, nimemsikiliza kwa makini na hakuna sehemu ambayo Masha amesema anafuta agizo lake. Akiwa anaulizwa kwa woga na Mtangazaji wa TBC1 (Elisha Eliya) na yeye kujibu kwa wasi wasi kidogo, amesema kuwa wameachana nalo. Hakusema kuwa amefuta agizo lake hata kidogo. Na akaongeza kuwa Polisi wataendelea kufuatilia suala la SMS. Labda kama na wewe umekuwa na kipaji cha kusoma hisia zake. Kama ni hekima basi angekiri kuwa agizo lake halitekelezeki hivyo amaelifuta rasmi. Vingenvyo mimi (labda na wengine) namwona kama mtu ambaye hajui analofanya. Sidhani kama vitisho vyote alivyotoa awali ilikuwa ni utani au kutishia mtoto nyau! Kwa maoni yangu ameidhalilisha nafasi ya Uwaziri (ambayo tunajua ilishawahi kukaliwa na watu wenye uwezo wa kufuatilia mambo kama Mrema), Rais aliyemteua na serikali yote. Mimi sijaridhika na maelezo ya juu juu katika issue nyeti kama hii. Vinginevyo amwachie mtu mwingine ofisi afanye kazi naye arudie kazi yake ya uwakili.

Jamani siasa ina kanuni zake ambazo hajiaandikwa popote.Lakini kuna errors, mistakes and blunders.Katika haya pamoja na kupandishina munkari lazima tukubali kuwa Waziri Kijana ali err.
It could have been much worse kama Waziri Kijana angeendelea kukomalia msimamo wake usio na tija.Hivyo basi nakubaliana na Mwanakijiji kuwa kwa Waziri Kijana kuliachia suala life ni busara.
hata hivyo tumeweza kuona kuwa siasa haisomewi darasani, na uwaziri sio munkari yako.
Somo jingine ni kuwa si serikali peke yake yenye data muhimu juu ya matukio hapa nchini.Kuna watu wana data kibao, data nyingine ambazo ni embarrassing kwa wengine.
 
well.. una nguvu fulani za kiungu, itabidi nianze kukusujudia!

Bwana mkubwa usimsujudie hicho kitu hakiitaji uungu kinaitwa

psy·chol·o·gy [ sī kólləjee ] (plural psy·chol·o·gies)


noun

Definition:

1. study of human mind: the scientific study of the human mind and mental states, and of human and animal behavior

ukiwa na ujuzi huo basi yaweza kua rahisi kubashili anayoweza kufanya au kuwaza mtu kwa wakati fulani! hahahahaa
 
well.. una nguvu fulani za kiungu, itabidi nianze kukusujudia!

Bwana mkubwa usimsujudie hicho kitu hakiitaji uungu kinaitwa

psy·chol·o·gy [ sī kólləjee ] (plural psy·chol·o·gies)


noun

Definition:

1. study of human mind: the scientific study of the human mind and mental states, and of human and animal behavior

ukiwa na ujuzi huo basi yaweza kua rahisi kubashili anayoweza kufanya au kuwaza mtu kwa wakati fulani! hahahahaa

sasa hivi ninawaza nini?
 
Ndiyo mana huwa simpendi Mengi na nitasimamia hapo hapo...Mzee huyu anajidai ni msaada kwa watanzania ila hana chochote

Angalau hapa hakuna kuhisi nini kinakuongoza ni vizuri angalau kusema kama ulivyosema ili kusiwe na utata unapochangia hoja za mtu kama Mengi.
 
Masha issued a "friendly threat" which he did not follow it to its logical conlusion.
The consequences for that will come.In what way? Just wait!
 
- Mengi na Masha, hawakututendea haki wananchi na taifa zima kwa ujumla, kwa sababu watuwazima wamekuja kutishiana nyau kwa expense yetu taifa na hasa sisi wananchi walalahoi, for what hasa?

- Mengi ametuhakikishia kwamba ni very powerful na anaweza kuitikisa serikali at any of his time na Masha ametuhakikishia tu kwamba hana uhakika na either sheria au mipaka ya kazi yake, kwa sababu kwa dataz nilizonazo ni kwamba alifikia mahali aliamuru Mengi akamatwe, lakini wakulu wa polisi aliowapa amri wakamcheka sana kwamba haitakuja kutokea, what an-embarrassment kwa waziri na serikali!

- In the end wananchi walalahoi ambao wengi tulikuwa tume-invest a lot in this sagga, tume-lost maana ni majuzi tu Mengi na Masha walikuwa mahali wakioengea na kucheka as nothing happened, nilijua Mchagga Mengi sio rahisi kumdhuru kijana aliyeoa mtoto wa Mareale Chifu wa wachagga, kamwe haitakuja kutokea maana Mengi atapita wapi huko Uchaggani?

Turudi tu backo to the really ishus za taifa! maana aliyejuu labda umfuatie huko huko juu, yale ya zamani ya kumngojea chini hashuki ng'o maana anaweza kutumia parachute asianguke! Tunamuombea Mengi aendele kusaidia wananchi wanyonge kama anavyofanya, maana kwenye hilo atalipwa na Mungu tu, ingawa kwenye ishu ya Masilingi hakuwa mkweli na what real went down!.

Ndugu yangu kumdhuru kivipi? Yani akitokea mtu mwenye msimamo dhidi ya haki za wananchi kutozingatiwa basi yeye ndiyo wenye uwezo wa kumdhuru mwezie? Nani alikuwa amdhuru nani?

Nadhani madhara uliyoyazungumzia inawezekana(correct me if iam wrong) ni ya kisiasa ama kisheria,ila madai kuwa mchagga Mengi si rahisi kumdhuru Masha kwasababu kaoa uchaggani....Then kwanini hukuangalia upande wa pili wa shilingi na kusema Masha hawezi kumdhuru Mengi kwasababu kaoa uchaggani? Kwanini hukusema Masha ama mke wake watapita wapi kama wakimfilisi Mengi kwa njama?
Naelewa umekuwa dissapointed mkuu lakini still naomba ubalance ili kuweza kuleta mantiki ya haki na sense kimjadala bila unnecessary biasiness.

Ndiyo mana huwa simpendi Mengi na nitasimamia hapo hapo...Mzee huyu anajidai ni msaada kwa watanzania ila hana chochote

Gembe na wewe pia unanishangaza kwasababu saa nyingine haujulikani hata direction yako ni ipi and what you really want, kama kweli humpendi Mengi then ungetakiwa uwe upande wa MKJJ kwasababu TRUST ME mlolongo huu ukiendelea na upande wa sheria kuchukuwa mkondo wake basi Mengi will prevail dhidi ya Masha jambo ambalo litakufanya umchukie even more...Na kwasababu hiyo basi ni bora ukubaliane tu na MKJJ mambo yaishe na kijana wenu abatizwe kuwa na hekima.
 
Hii sikubaliani nayo...wamerekani wangemchangua Mcain kama kigezo ni umri!

Ushirombo, Heshima mbele,

Kwa hiyo unataka kumfananisha Masha na Obama? Hivi Masha alishawahi hata kushiriki katika kazi na uongozi wa Kijamii zaidi ya kuwa na law firm yenye Ukungu wa EPA? Ninadiriki kusema Masha hana uzoefu wa kuongoza umma,

Naomba kutokukubaliana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom