Waziri Jenista Mhagama akabidhi vifaa vya TEHAMA, Michezo, Afya na Elimu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,905
945
Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. JENISTA J. MHAGAMA Amefanya Ziara Katika Kata ya Kilagano Kijiji cha Mgazini na Kijiji cha Kilagano.

Katika Ziara hiyo Mhe. Jenista Mhagama ameambatana na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea pamoja Wakuu wa Idara.

Kijiji cha Mgazini, Waziri, Mhe. Mhagama amekagua Kituo Cha Afya; amegawa Wheel Chairs 3; T- Shirt 6 kwa Wanafunzi Shule ya Msingi Mgazini; Komputa na Printer 1 kwa Shule ya Msingi Mgazini; Chandarua kwa Wazee 10; Vifaa vya Michezo (Jezi na Mipira) Seti 4 na amefanya Mkutano wa Hadhara.

Kijiji cha Kilagano Kitongoji cha Nambarapi, Mhe. Jenista Mhagama ameweka Jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Shule ya Msingi Nambarapi na amegawa Vifaa vya Michezo ( Jezi na Mipira) Seti 4; Chandarua kwa Wazee 10 na amefanya Mkutano wa Hadhara.

Jimbo la Peramiho lipo Imara na Kazi Inaendelea.

MHE. Dkt. SAMIA SULUHU HASSAN & MH. JENISTA J. MHAGAMA.

Mama Yupo Kazini!

WhatsApp Image 2023-07-16 at 08.01.03.jpeg
WhatsApp Image 2023-07-16 at 08.01.03(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-07-16 at 08.01.04.jpeg
WhatsApp Image 2023-07-16 at 08.01.04(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-07-16 at 08.01.04(2).jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom