Waziri January Makamba hana msaada wowote kwenye Wizara ya Nishati. Tumechoka!

unadhani hizi kelele zitasaidia kumuondoa huyu waziri wa mchongo? tafuta mbadala kazi iendelee.
Kusema watu lazima waseme ndiyo maana kuna platform kama hapa jf.

Walio anzisha hili jukwaa hawakuwa wajinga maana walijua kuwa kuna mambo lazima yasemwe nje ya mfumo wa serikali.
 
Binafsi siamini kuwa ni ntu wa dili na kukatika umeme ni mpango wa kusambaza majenereta.

Naamini hatoniprove wrong na hili suala litakuwa stable. Atashinda haka kavita ninakokafikiri anapitia.
Kwanini iwe sasa baada ya waziri Kalemani kutoka wizarani?
 
Watu wapo pale Tanesco kwa mambo yao... January,Mafuru,Maharage,Nehemia ni lethal combination....
Nikuhakikishie JPM angekuwa hai hili jambo lingekuwa tofauti sana....
Personally nakubali kwenye usimamizi JPM was real deal.
Wacheni tena kuturudisha kwenye yaliyo pita yaani kila siku ange ange ange ange!!!

Hayupo sasa wacha tupambane kivyetu na huyu aliyepo asikie maana ni mzuri kwenye mitandao ya kijamii.
 
Watu wanafiki Sana.

Baadhi ya viongozi wa awamu ya5 walivyokuwa wanawawajibisha watendaji wazembe ikiwepo na Tanesco nyie nyie ndio mlikuwa mnasema kuwa wanaonewa.

Mkasema watu waachwe wafanye kazi wasiingiliwe na wanasiasa au kuacha mifumo ifanye kazi.

Mimi nnachoamini baadhi ya taasisi usipotumia nguvu Mambo hayawezi kuenda. Maana utendaji wa taasisi nyingi za Serikali ni wa taratibu na uzembe mwingi.
 
Kusema watu lazima waseme ndiyo maana kuna platform kama hapa jf.

Walio anzisha hili jukwaa hawakuwa wajinga maana walijua kuwa kuna mambo lazima yasemwe nje ya mfumo wa serikali.
upo sahihi bt pia tuandae plan B ajili ya kukabiliana na hili tatizo maana umeme kwa sasa ndo engine ya wajasiriamali alafu unazingua kishenzi na wahusika hata hawajali.
 
Back
Top Bottom