Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,898
- 943
WAZIRI DKT. ASHATU KIJAJI - SERIKALI HAIKO TAYARI KUKWAMISHA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUFIKIA MALENGO YAO
Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amesema Serikali inatekeleza jitihada mbalimbali katika kuhakikisha inaweka mazingira bora kwa wafanyabiashara na wawekezaji pamoja na kutatua changamoto walizonazo.
Dkt. Kijaji amesema hayo Agosti 1, 2023 alipotembelea Kiwanda cha Magodoro cha TANFOAM kilichopo Jijini Arusha kujionea shughuli za uzalishaji magodoro na kisikiliza changamoto walizonazo.
Aidha, Amesema Wizara yake inatekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji ambapo moja msingi yake ni kuondoa majukumu yanayofanana kati ya Taasisi ili kurahisisha ufanyaji biashara na uwekezaji nchini
Akiongea na uongozi wa kiwanda hicho, Dkt. Kijaji amezitaka Taasisi kuacha kufanya majukumu yanayofanana na kuzitaka kushirikiana katika kuwahudumia wafanyabiashara na wawekezaji ili kukuza biashara na uchumi wa Taifa
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Dkt Ashatu Kijaji (Mb.) amesema Serikali ya Awamu ya Sita haiko tayari kuwakwamisha wafanyabiashara na wawekezaji kushindwa kufikia malengo yao bali itawasaidia kukua na kuendelea kibiashara, kukaa kwa pamoja na kutatua changamoto zao ili kuhakikisha ufanyaji biashara wao unakuwa na tija na manufaa kwa Taifa .
Amesema hayo Agosti 1, 2023 alipotembelea Kiwanda cha Kutengeneza Vishikwambi cha Tanztech kilichopo jijini Arusha kwa lengo la kujionea uzalishaji huo na kusikiliza changamoto zao.
Aidha Dkt. Kijaji amesema ameridhishwa na uwekezaji huo ikiwa ni hatua ya kutatua changamoto ya matumizi ya Vishkwambi katika shule za awali na zile za sekondari ambapo vitasaidia kufundisha wanafunzi namna bora ya kutumia TEHAMA katika mitaala ya elimu.
Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) amesema Serikali inatekeleza jitihada mbalimbali katika kuhakikisha inaweka mazingira bora kwa wafanyabiashara na wawekezaji pamoja na kutatua changamoto walizonazo.
Dkt. Kijaji amesema hayo Agosti 1, 2023 alipotembelea Kiwanda cha Magodoro cha TANFOAM kilichopo Jijini Arusha kujionea shughuli za uzalishaji magodoro na kisikiliza changamoto walizonazo.
Aidha, Amesema Wizara yake inatekeleza Mpango wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji ambapo moja msingi yake ni kuondoa majukumu yanayofanana kati ya Taasisi ili kurahisisha ufanyaji biashara na uwekezaji nchini
Akiongea na uongozi wa kiwanda hicho, Dkt. Kijaji amezitaka Taasisi kuacha kufanya majukumu yanayofanana na kuzitaka kushirikiana katika kuwahudumia wafanyabiashara na wawekezaji ili kukuza biashara na uchumi wa Taifa
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Dkt Ashatu Kijaji (Mb.) amesema Serikali ya Awamu ya Sita haiko tayari kuwakwamisha wafanyabiashara na wawekezaji kushindwa kufikia malengo yao bali itawasaidia kukua na kuendelea kibiashara, kukaa kwa pamoja na kutatua changamoto zao ili kuhakikisha ufanyaji biashara wao unakuwa na tija na manufaa kwa Taifa .
Amesema hayo Agosti 1, 2023 alipotembelea Kiwanda cha Kutengeneza Vishikwambi cha Tanztech kilichopo jijini Arusha kwa lengo la kujionea uzalishaji huo na kusikiliza changamoto zao.
Aidha Dkt. Kijaji amesema ameridhishwa na uwekezaji huo ikiwa ni hatua ya kutatua changamoto ya matumizi ya Vishkwambi katika shule za awali na zile za sekondari ambapo vitasaidia kufundisha wanafunzi namna bora ya kutumia TEHAMA katika mitaala ya elimu.