benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Doto Biteko, amewahakikishia Wananchi wa Mkoa Geita kuwa, miradi yote mikubwa ya kimkakati iliyoanzishwa katika kipindi cha Serikali ya awamu ya tano, inaendelea kutekelezwa na hakuna mradi utakaosimama.
Biteko ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, ameyasema hayo kwenye wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama hicho, na kuwakutanisha wabunge wote wa mkoa huo, na ulilenga kuelezea utekelezaji wa ilani ya CCM.
“Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kupitia kauli mbiu ya kazi iendelee, amehakikisha miradi yote mikubwa ya kimkakati iliyoanzishwa katika kipindi cha Serikali ya awamu ya tano, inaenndelea kutekelezwa na hakuna mradi uliosimama wala mradi utakaosimama,” amesema Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini na kuongeza;
“Nawaomba wananchi wote na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi tuendelee kumuunga mkono Rais na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya ya kumwaga fedha za maendeleo kote nchini, na ana maono makubwa ya kufikisha nchi yetu mahala pazuri.”
Chanzo: Mwananchi
Biteko ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, ameyasema hayo kwenye wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama hicho, na kuwakutanisha wabunge wote wa mkoa huo, na ulilenga kuelezea utekelezaji wa ilani ya CCM.
“Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kupitia kauli mbiu ya kazi iendelee, amehakikisha miradi yote mikubwa ya kimkakati iliyoanzishwa katika kipindi cha Serikali ya awamu ya tano, inaenndelea kutekelezwa na hakuna mradi uliosimama wala mradi utakaosimama,” amesema Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini na kuongeza;
“Nawaomba wananchi wote na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi tuendelee kumuunga mkono Rais na Mwenyekiti wa CCM, Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya ya kumwaga fedha za maendeleo kote nchini, na ana maono makubwa ya kufikisha nchi yetu mahala pazuri.”
Chanzo: Mwananchi