Waziri apanda kizimbani: ...Kisa cha SANGAM SECURITAS!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Waziri Valentino Madusha alishtakiwa kwa kuingilia mchakato wa utoaji na upatikanaji wa tenda ya kuchapisha vitambulisho vya Raia. Katika kesi iliyovutia Taifa Waziri huyo alisimama kizimbani kuhojiwa na upande wa mashtaka kuelezea nafasi yake na hasa jinsi alivyoitetea kampuni ya SANGAM SECURITAS: Mahakamani ilikuwa hivi katika siku ya kwanza.

Waziri alikuwa amevaa suti kijivu yenye michirizi midogo sana ya rangi nyeusi, alivaa shati la rangi ya bluu nyepesi na kwenye shingo yake alitinga tai ya rangi nyekundu iliyowiva. Miwani yake yenye rangi ya redha ilimfanya aonekane kama profesa fulani wa vile vyuo vikuu vya watu weusi kule Marekani ambako alisoma. Mwendesha mashtaka alikuwa ni "mtu wa kawaida kawaida tu".

Swali- Mwendesha Mashtaka: Ni makampuni mangapi yaliyolalamika kwako kuhusu mchakato wa tenda hii ya vitambulisho?

Waziri Madusha (Jibu): Haikuwa kampuni moja bali tano.

Swali: Kwenye barua yako kwa Waziri Mkuu ulisema kampuni ngapi zimelalamika kwako?

Jibu: Sikumbuki mara moja nilisema ni ngapi hasa ila nilitolea mfano wa kampuni moja.

Swali: Ngoja nikusomee barua yako hiyo ukurasa wa nne, Naomba ipokolewe kama kizibiti namba moja. Unasema hivi "baada ya kupitia taarifa ya Kamati ya tathmini (evaluation committee) na hasa kutokana na malalamiko niliyoyapokea toka Kampuni ya SANGAM SECURITAS niliona ipo haja ya kupata ufafanuzi" na pia unarudia kwenye ukurasa huo huo na kusema kuwa "Katika kikao hicho niliwafahamisha kuwa nimepokea malalamiko kutoka kwa mojawapo ya waombaji". Je, msomaji wa barua hiyo aelewe ulikuwa umepokea malalamiko kutoka makampuni mangapi?

Jibu: Anaweza kuelewa vyovyote lakini haiondoi ukweli kuwa nilipokea malalamiko zaidi ya kampuni moja.

Swali:
Bw. Masha, wewe umesema kuwa umepokea malalamiko toka "kampuni ya" na pia umepokea malalamiko toka "mojawapo" ya waombaji, sasa mtu kwanini aelewe "vyovyote"? Ni lini neno "mojawapo" linamaa ya wingi?

Jibu:
Mimi msukuma kwetu mojawapo inaweza kumaanisha mambo mengi (ukumbi unaguna kwa kicheko).

Swali: Je umewahi kukutana na maafisa wa kampuni ya SANGAM SECURITAS wakati wowote wa mchakato huu?

Jibu: Una maana gani "kukutana"?

Swali: Kwamba umewahi kuwasiliana nao aidha ana kwa ana, kwa njia ya barua, simu, barua pepe au kwa namna yoyote kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja nao?

Jibu: Huku kukutana unakozungumzia una maana rasmi au siyo rasmi?

Swali: Haijalishi kama rasmi au siyo rasmi! Umewahi kukutana nao wakati wowote kampuni hii?

Jibu: Nilipokuwa Uswisi Mkurugenzi wa Kampuni hiyo alinialika kwa dakika chache kuangalia shughuli zao pale lakini sijui kama huko nikukutana!

Swali: Mhe. Jaji naomba mahakama irekodi kuwa mshtakiwa amekubali kukutana na maafisa wa SANGAM SECURITAS huko Hispania?

Jibu: Hapana Jaji, sijakubali! Mimi nimesema tu kuwa nilialikwa nichepukie pale mara moja wakati natoka Oman na sidhani kama ile unaweza kuiita kukutana.

Jaji: Wakili endelea na maswali, karani, hakikisha umerekodi kuwa Bw. Masha alikutana na watu wa SANGAM.

Swali:Umesema kwenye barua yako na umerudia mara kadhaa katika vyombo vya habari kuwa ulipokea malalamiko kutoka kampuni ya SANGAM SECURITAS na sasa umeongeza kuwa makampuni mengine pia yamelalamika kwako. Ni barua gani ulipokea kuhusu malalamiko hayo?

Jibu:
Sikusema nimepokea barua yoyote.

Swali: Sasa ulipokea malalamiko hayo kwa namna gani?

Jibu: SANGAM SECURITAS walilalamika kwangu, na mimi baada ya kuona kuwa malalamiko yao yana msingi niliwasiliana na Katibu Mkuu wa Wizara yangu kutaka ufafanuzi kama nilivyosema kwenye barua yangu.

Swali: Naomba nirudie tena, ulipokea malalamiko kwa njia au namna gani?

Jibu: Kwani malalamiko yanatolewa kwa namna gani?

Swali: Mhe. Jaji, naomba mshtakiwa yuko argumentative naomba umlazimishe ajibu swali.

Wakili wa Utetezi: Mhe. Jaji, tayari Mshtakiwa ametoa jibu lake kuwa amepokea malalamiko sasa Wakili anachotaka kujua sijui ni kitu gani naona anataka kuipotezea mahakama hii muda tu!

Jaji: Jongeeni hapa. (mawakili wanasogea kwenye meza ya Jaji, Mic zinazimwa na anawanong'oneza jambo huku kidole chake kikionekana kinainuliwa inuliwa juu kutilia mkazo)

Jaji: Bw. Madusha iambie mahakama hii ulipokea malalamiko ya makampuni hayo kwa njia gani, kumbuka uko chini ya kiapo.

Jibu:
Nilizungumza nao ana kwa ana.

Swali: Kwa hiyo katika wizara nzima ni wewe peke yako mwenye rekodi ya kukutana na wawakilishi wa makampuni hayo katika mazingira unayoyajua wewe ambayo unasema kuwa yalitosha kwa wewe kuandika barua?

Wakili wa Utetezi:
Objection your honor!

Swali: Withdrawn naomba nilipange upya swali langu. Bw. Madusha, umepokea malalamiko kutoka kwa kampuni moja au nne, katika mazingira ambayo siyo rasmi, kwanini watu wasiamini kuwa kulikuwa na kukiuka taratibu?

Jibu: Mimi nilifanya hayo yote kulinda maslahi ya Taifa na ni kutokana na mimi kuwasilisha malalamiko hayo mchakato ukaangaliwa upya na ndiyo maana mchakato ukaangaliwa upya, kwa hiyo mimi natakiwa kutazamwa kama shujaa na mtetezi siyo mhalifu kama unavyoashiria.

Swali: Hivyo katika kuonesha uzalendo wako uko tayari hata kuvunja sheria ili uonekane kuwa shujaa?

Wakili wa Utetezi: Objection your honor, Wakili anamhukumu mshtakiwa!

Jaji: Wakili angalia mwelekeo wa maswali yako.

Swali:Kwanini ulikubali kupokea malalamiko ya makampuni haya nje ya taratibu (informal) wakati wewe hauko kwenye mchakato wa Tenda na hakuna mahali popote ambapo ulimuita Katibu wako awe sehemu ya kusikiliza malalamiko hayo?

Jibu: (kimya)

Swali: Narudia tena, Kwanini ulikubali kupokea malalamiko ya makampuni haya nje ya taratibu (informal) wakati wewe hauko kwenye mchakato wa Tenda na hakuna mahali popote ambapo ulimuita Katibu wako awe sehemu ya kusikiliza malalamiko hayo?

Jibu: Kutokana na ushauri wa wakili wangu sitopenda kujibu swali hili nikikwepa kujichongea mwenyewe.

Swali: Kama wewe hauko katika mchakato kusimamia tenda au hata kukata rufaa, imekuwaje usikilize malalamiko ya makampuni manne badala ya kukataa kabisa kuyachukua malalamiko hayo na kuwaelekeza kwa Katibu wako Mkuu?

Jibu: Kutokana na ushauri wa wakili wangu sitopenda kujibu swali hili nikikwepa kujichongea mwenyewe.

Swali: Bw. Madusha unafikiri lolote ulilofanya kwenye hili linakaribiana na heshima ya uzalendo, utawala bora, na kuheshimu sheria?

Jibu: Mimi ni Mwanasheria, nimesoma na kukulia Marekani. Nimerudi nchini kuijenga nchi yangu. Katika kufanya hivyo nimeshiriki katika mambo mbalimbali, nimeanzisha kampuni na kutoa ajira kwa watanzania wengi, nimechaguliwa na watu wa Isamilo na kuwa Mbunge, Rais ameamini katika uwezo wangu na amenidhamini wadhifa huu wa Uwaziri.

Hivyo katika yote ambayo nimefanya hadi hivi sasa naona fahari kujiona mzalendo kitu ambacho wakosoaji wangu hawaamini. Watu wananionea wivu kwa sababu mimi ni kijana tena msomi, na wapo wanaoona natishisha maslahi yao. Kwa hiyo ndiyo mimi ni mzalendo wa kweli!

Swali: (wakili ameongeza sauti na anazungumza kwa haraka huku akimkazia macho Waziri Madusha) Kwa hiyo ni huo uzalendo ndiyo umekufanya uwe tayari hata kuvunja sheria kutetea kile unachoamini ni maslahi ya nchi hata kuingilia mchakato wa tenda za wizara?

Jibu: Mimi ni mzalendo (huku naye anaongeza sauti na uso wake uko serious na anagonga kingo ya kizimba kwa jazba). Yote niliyoyafanya hadi sasa ni kwa ajili ya nchi yangu!

Swali: Hivyo kwa ajili ya nchi yako uko tayari kuvunja sheria Mhe. Madusha? Jibu swali!

Jibu: Ndiyo!!! Niko tayari kufanya lolote kama maslahi ya nchi yangu yanatishiwa, niko tayari kukutana na mtu yeyote mahali popote na wakati wowote, niko tayari hata kuvunja sheria ya tenda na manunuzi ya serikali kama nikiona sheria hiyo ni kikwazo kwangu! Ndiyo.. now you have it!

Wakili: Sina maswali ya ziada Mhe. Jaji!

Waziri Madusha anatoka kizimbani huku akitengeneza tai, na akiiweka sawa miwani yake ya jua. Kipara chake ambacho kinaonekana kinang'ara kama kimetiwa samri kiliakisi taa za ukumbi huo. Anajipangusa mdomo huku baadhi ya watu wakinong'ona. Wanasubiri kesi hiyo itapoendelea tena kesho!!

Disclaimer:
Kisa hiki ni cha kutunga, mfanano wowote wa majina ya watu, mahali, na matukio halisi ni mambo ya kinasibu na matokeo ya ubunifu wa mtunzi.
 
Last edited:
haya Mkuu. Ngoja tusubiri hiyo kesho tuona vile itakuwa...naona kama picha kali sana hili...ngoja nivute popcorns hapa taratibu...LOL
 
Waziri alishtakiwa na nani na lini hii mbona kienyeji enyeji hakuna kwenda bungeni kuhojiwa kwa undani moja kwa moja mahakamani hii imekaaje hatutaki kujifunza kosa kwa undani na kulitungia sheria for future generation huu si mchemsho.


SAHIBA.
 
Man, This is Classic!, very beautiful indeed lol!, You've gotta make money out of it. as the matter of fact, Tanzania need a new generation of writers, Man you could be among of them!!!!!
 
Mwanakijiji, this is great man. Unajua hata kama jambo linapita hivi hivi bado tunapata nafasi ya kujifunza upande mwingine (mzuri) ungekuwaje. Congrats mpiganaji.
 
Mwanakijiji, this is great man. Unajua hata kama jambo linapita hivi hivi bado tunapata nafasi ya kujifunza upande mwingine (mzuri) ungekuwaje. Congrats mpiganaji.


asante.. the imagination of an imaginative person is sometimes very imaginary!
 
Waziri alishtakiwa kwa kuingilia mchakato wa utoaji na upatikanaji wa tenda ya kuchapisha vitambulisho. Katika kesi iliyovutia Taifa Waziri huyo alisimama kizimbani kuhojiwa na upande wa mashtaka kuelezea nafasi yake na hasa jinsi alivyoitetea kampuni ya SAGEM SECURITE: Mahakamani ilikuwa hivi katika siku ya kwanza.


Swali- Mwendesha Mashtaka: Ni makampuni mangapi yaliyolalamika kwako kuhusu mchakato wa tenda hii ya vitambulisho?

Madusha (Jibu): Haikuwa kampuni moja bali tano.

Swali: Kwenye barua yako kwa Waziri Mkuu ulisema kampuni ngapi zimelalamika kwako?

Jibu: Sikumbuki mara moja nilisema ni ngapi hasa ila nilitolea mfano wa kampuni moja.

Swali: Ngoja nikusomee barua yako hiyo ukurasa wa tatu, Naomba ipokolewe kama kizibiti namba moja. Unasema hivi "baada ya kupitia taarifa ya Kamati ya tathmini (evaluation committee) na hasa kutokana na malalamiko niliyoyapokea toka Kampuni ya SANGAM SECURITAS niliona ipo haja ya kupata ufafanuzi" na pia unarudia kwenye ukurasa huo huo na kusema kuwa "Katika kikao hicho niliwafahamisha kuwa nimepokea malalamiko kutoka kwa mojawapo ya waombaji". Je, msomaji wa barua hiyo aelewe ulikuwa umepokea malalamiko kutoka makampuni mangapi?

Jibu: Anaweza kuelewa vyovyote lakini haiondoi ukweli kuwa nilipokea malalamiko zaidi ya kampuni moja.

Swali:
Bw. Masha, wewe umesema kuwa umepokea malalamiko toka "kampuni ya" na pia umepokea malalamiko toka "mojawapo" ya waombaji, sasa mtu kwanini aelewe "vyovyote"? Ni lini neno "mojawapo" linamaa ya wingi?

Jibu:
Mimi msukuma kwetu mojawapo inaweza kumaanisha mambo mengi (ukumbi unaguna kwa kicheko).

Swali: Je umewahi kukutana na maafisa wa kampuni ya SANGAM SECURITAS wakati wowote wa mchakato huu?

Jibu: Una maana gani "kukutana"?

Swali: Kwamba umewahi kuwasiliana nao aidha ana kwa ana, kwa njia ya barua, simu, barua pepe au kwa namna yoyote kuwa na mawasiliano ya moja kwa moja nao?

Jibu: Huku kukutana unakozungumzia una maana rasmi au siyo rasmi?

Swali: Haijalishi kama rasmi au siyo rasmi! Umewahi kukutana nao wakati wowote kampuni hii?

Jibu: Nilipokuwa Uswisi Mkurugenzi wa Kampuni hiyo alinialika kwa dakika chache kuangalia shughuli zao pale lakini sijui kama huko nikukutana!

Swali: Mhe. Jaji naomba mahakama irekodi kuwa mshtakiwa amekubali kukutana na maafisa wa SANGAM SECURITAS huko Uswisi!

Jibu: Hapana Jaji, sijakubali! Mimi nimesema tu kuwa nilialikwa nichepukie pale mara moja wakati natoka Dubai na sidhani kama ile unaweza kuiita kukutana.

Jaji: Wakili endelea na maswali, karani, hakikisha umerekodi kuwa Bw. Masha alikutana na watu wa SANGAM.

Swali:Umesema kwenye barua yako na umerudia mara kadhaa katika vyombo vya habari kuwa ulipokea malalamiko kutoka kampuni ya SANGAM na sasa umeongeza kuwa makampuni mengine pia yamelalamika kwako. Ni barua gani ulipokea kuhusu malalamiko hayo?

Jibu:
Sikusema nimepokea barua yoyote.

Swali: Sasa ulipokea malalamiko hayo kwa namna gani?

Jibu: SANGAM walilalamika kwangu, na mimi baada ya kuona kuwa malalamiko yao yana msingi niliwasiliana na Katibu Mkuu wa Wizara yangu kutaka ufafanuzi kama nilivyosema kwenye barua yangu.

Swali: Naomba nirudie tena, ulipokea malalamiko kwa njia au namna gani?

Jibu: Kwani malalamiko yanatolewa kwa namna gani?

Swali: Mhe. Jaji, naomba mshtakiwa yuko argumentative naomba umlazimishe ajibu swali.

Wakili wa Utetezi: Mhe. Jaji, tayari Mshtakiwa ametoa jibu lake kuwa amepokea malalamiko sasa Wakili anachotaka kujua sijui ni kitu gani naona anataka kuipotezea mahakama hii muda tu!

Jaji: Jongeeni hapa. (mawakili wanasogea kwenye meza ya Jaji, Mic zinazimwa na anawanong'oneza jambo huku kidole chake kikionekana kinainuliwa inuliwa juu kutilia mkazo)

Jaji: Bw. Masha iambie mahakama hii ulipokea malalamiko ya makampuni hayo kwa njia gani, kumbuka uko chini ya kiapo.

Jibu:
Nilizungumza nao ana kwa ana.

Swali: Kwa hiyo katika wizara nzima ni wewe peke yako mwenye rekodi ya kukutana na wawakilishi wa makampuni hayo katika mazingira unayoyajua wewe ambayo unasema kuwa yalitosha kwa wewe kuandika barua?

Wakili wa Utetezi:
Objection your honor!

Swali: Withdrawn naomba nilipange upya swali langu. Bw. Masha, umepokea malalamiko kutoka kwa kampuni moja au nne, katika mazingira ambayo siyo rasmi, kwanini watu wasiamini kuwa kulikuwa na kukiuka taratibu?

Jibu: Mimi nilifanya hayo yote kulinda maslahi ya Taifa na ni kutokana na mimi kuwasilisha malalamiko hayo mchakato ukaangaliwa upya na ndiyo maana mchakato ukaangaliwa upya, kwa hiyo mimi natakiwa kutazamwa kama shujaa na mtetezi siyo mhalifu kama unavyoashiria.

Swali: Hivyo katika kuonesha uzalendo wako uko tayari hata kuvunja sheria ili uonekane kuwa shujaa?

Wakili wa Utetezi: Objection your honor, Wakili anamhukumu mshtakiwa!

Jaji: Wakili angalia mwelekeo wa maswali yako.

Swali:Kwanini ulikubali kupokea malalamiko ya makampuni haya nje ya taratibu (informal) wakati wewe hauko kwenye mchakato wa Tenda na hakuna mahali popote ambapo ulimuita Katibu wako awe sehemu ya kusikiliza malalamiko hayo?

Jibu: (kimya)

Swali: Narudia tena, Kwanini ulikubali kupokea malalamiko ya makampuni haya nje ya taratibu (informal) wakati wewe hauko kwenye mchakato wa Tenda na hakuna mahali popote ambapo ulimuita Katibu wako awe sehemu ya kusikiliza malalamiko hayo?

Jibu: Kutokana na ushauri wa wakili wangu sitopenda kujibu swali hili nikikwepa kujichongea mwenyewe.

Swali: Kama wewe hauko katika mchakato kusimamia tenda au hata kukata rufaa, imekuwaje usikilize malalamiko ya makampuni manne badala ya kukataa kabisa kuyachukua malalamiko hayo na kuwaelekeza kwa Katibu wako Mkuu?

Jibu: Kutokana na ushauri wa wakili wangu sitopenda kujibu swali hili nikikwepa kujichongea mwenyewe.

Swali: Bw. Masha unafikiri lolote ulilofanya kwenye hili linakaribiana na heshima ya uzalendo, utawala bora, na kuheshimu sheria?

Jibu: Mimi ni Mwanasheria, nimesoma na kukulia Marekani. Nimerudi nchini kuijenga nchi yangu. Katika kufanya hivyo nimeshiriki katika mambo mbalimbali, nimeanzisha kampuni na kutoa ajira kwa watanzania wengi, nimechaguliwa na watu wa Nyamagana na kuwa Mbunge, Rais ameamini katika uwezo wangu na amenidhamini wadhifa huu wa Uwaziri.

Hivyo katika yote ambayo nimefanya hadi hivi sasa naona fahari kujiona mzalendo kitu ambacho wakosoaji wangu hawaamini. Watu wananionea wivu kwa sababu mimi ni kijana tena msomi, na wapo wanaoona natishisha maslahi yao. Kwa hiyo ndiyo mimi ni mzalendo wa kweli!

Swali: (wakili ameongeza sauti na anazungumza kwa haraka huku akimkazia macho Waziri Masha) Kwa hiyo ni huo uzalendo ndiyo umekufanya uwe tayari hata kuvunja sheria kutetea kile unachoamini ni maslahi ya nchi hata kuingilia mchakato wa tenda za wizara?

Jibu: Mimi ni mzalendo (huku naye anaongeza sauti na uso wake uko serious na anagonga kingo ya kizimba kwa jazba). Yote niliyoyafanya hadi sasa ni kwa ajili ya nchi yangu!

Swali: Hivyo kwa ajili ya nchi yako uko tayari kuvunja sheria Mhe. Masha? Jibu swali!

Jibu: Ndiyo!!! Niko tayari kufanya lolote kama maslahi ya nchi yangu yanatishiwa, niko tayari kukutana na mtu yeyote mahali popote na wakati wowote, niko tayari hata kuvunja sheria ya tenda na manunuzi ya serikali kama nikiona sheria hiyo ni kikwazo kwangu! Ndiyo.. now you have it!

Wakili: Sina maswali ya ziada Mhe. Jaji!

Waziri Masha anatoka kizimbani huku akitengeneza tai, na akiiweka sawa miwani yake ya jua. Kipara chake ambacho kinaonekana kinang'ara kama kimetiwa samri kiliakisi taa za ukumbi huo. Anajipangusa mdomo huku baadhi ya watu wakinong'ona. Wanasubiri kesi hiyo itapoendelea tena kesho!!

Disclaimer:
Kisa hiki ni cha kutunga, mfanano wowote wa majina ya watu, mahali, na matukio halisi ni mambo ya kinasibu na matokeo ya ubunifu wa mtunzi.

Hongera sana mkuu kwa kisa hiki..natamani iwe kama ulivyoandika,ngoja tusubiri na tuone....,hope itakuwa hivi..Uzidi kubarikiwa kwa kipaji chako hiki cha kucheza na maandishi......Bravo MMK
 
Last edited by a moderator:
MMKJJ,
Siku zote nasema uandishi wako umekwenda shule. Mara nyingine ni vigumu sana wengi kukuelewa.
Hapa tena unastahili pongezi zangu za dhati kwa ubunifu wako.
Masha anatakiwa asome hapa na kuona jinsi anavyoweza kusimama mahakamani.
Kama si leo au kesho, asubiri awamu ya rafiki yake Kikwete iishe ili tumsulubu wakati wewe umegombea 2010 na kufanikiwa. LOL
 
MKJJ kwa nini usingewatumia jamaa wa Clouds FM watakapokuwa na huyu bwana live kesho?

wameshakuwa naye mapema leo, na nilijaribu lakini haikuwezekana. Nadhani, nitafanya mimi mwenyewe Masha akikubali ananikwepa kwa sababu nimeshamuandika vibaya!
 
Du, wewe Noma!!!! Motoooo!!! Naona kama kweli vile. Tusubirie hukumu tu. Hapa hachomoki mtu. Hata wakili wa utetezi ameshindwa kumtetea...amebakia kusema.."objection your honour"! kila wakati. Kwenye kesi hii, jamaa huyu hatobebeka, haka akileta staff yake nzima (Including na wale ambao wameishazawadiwa ujaji) kwenye kampuni yake kumtetea!!!! hahahahahahaha...nomaaaa...balaaaaa...motooo....
 
Mzee Mwanakijiji!
Awesome, dude!! Kumbe visa vya mawaziri wetu vinaweza kutengenezewa vitabu au movie kabisa. 'kukutana' siyo? Tunasubiri busara za jaji!
 
hii nilikuwa sijaiona......yaani hapa imebidi mpaka wanangu waniulize Baba unacheka nini..........MMKJJ....safi sana Mkuu.....keep it up
 
...Mkjj, wiki mbili hizi umekuwa na mashambulizi makali sana katika battleground-fikra. Pongezi nyingi. NN amekupatia a little portion of that hypersupernanoconcentratepimpasonic potion nini?!

...Kwenye hiki kisa, nadhani kungelileta ladha nzuri zaidi kama usingetoa jina la mhusika katika hayo majibishano. Ni kisa cha kujitungia hivyo si budi kuwa na majina ya kujitungia pia, hata kama sote tunaelewa kinachoendelea na wanaohusika. Just a little note on separation of real life characters from those on stage when pre-conceiving drama!!!!!
 
wameshakuwa naye mapema leo, na nilijaribu lakini haikuwezekana. Nadhani, nitafanya mimi mwenyewe Masha akikubali ananikwepa kwa sababu nimeshamuandika vibaya!

angekuwa msafi asingekukimbia mkuu. Thanks for the beautifull art. Tutasambaza kama kawaida mkuu.
 
Last edited:
...Mkjj, wiki mbili hizi umekuwa na mashambulizi makali sana katika battleground-fikra. Pongezi nyingi. NN amekupatia a little portion of that hypersupernanoconcentratepimpasonic potion nini?!

...Kwenye hiki kisa, nadhani kungelileta ladha nzuri zaidi kama usingetoa jina la mhusika katika hayo majibishano. Ni kisa cha kujitungia hivyo si budi kuwa na majina ya kujitungia pia, hata kama sote tunaelewa kinachoendelea na wanaohusika. Just a little note on separation of real life characters from those on stage when pre-conceiving drama!!!!!

done!
 
Back
Top Bottom