Waziri aibiwa akiwa gesti

Waziri aibiwa akiwa gesti

Usijekuta alikuwa anajaribu kufuata nyendo za MACHEMLI.
 
Ls man-19:34 Today-
Kama kuna mtu ana gazet la mtanzania(kma sikosei)habr hii imeandikwa vzr zaidi, kuwa wazr aliingia na mtu kulala, na taarifa zilipofika polic wazr akataka zisiwe puplic!! Ili kutunza hadhi yake,,, hii nchi bwana michepuo diliiii

so alijifanya baby anapenda kunyonyaaa... safi sana!
 
Mboni kicheko? Hivi umesahau ukipinda kona ukachepukia barabara yenye tope na mashimo kuna faida na hasara?Utafika haraka lakini angalia spring za gari yako!

Na pili yake amechukua haki yake yaani kodi yake na part ya keki ya Taifa,upo?

nimekupata mkuu.
 
Huwezi kupewa kazi ya umma halafu unaishi kihunihuni mabarabara yapo tele ............ By J NYERERE .My take Mheshimiwa anapaswa kujiuzulu kwa mujibu wa baba wa Taifa mwasisi wa ccm.
 
Hii ni aibu na fedhweha kwa waziri kulala guest na hata kuibiwa.

Hivi jamani huo TZ mawaziri wanalala ovyo ovyo tu bila kuwa na taarifa zao katika vyombo vya dola vya sehemu alipo?

Au alikuwa na Mchepuko akaamua kujificha. Siku nyingine wanaweza io tu kuibiwa bali kuuwawa na hiyo michepuko yao?.
 
Na Waandishi wetu
8th June 2014
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani, anadaiwa kuporwa vitu mbalimbali zikiwamo nguo pamoja na fedha, wakati akiwa amelala kwenye moja ya nyumba za kulala wageni iliyoko mjini Bariadi mkoani Simiyu.
Habari zilizoifikia NIPASHE Jumapili jana zilisema uhalifu huo dhidi ya Waziri ulifanywa usiku wa kuamkia jana.

Akithibitisha habari hizo Kamanda wa Polisi mkoani Simiyu, Charles Mkumbo, alisema Dk Kamani ambaye ni mbunge wa jimbo la Busega (CCM) pia Mwenyekiti wa chama hicho mkoani humo, aliibiwa usiku wa kuamkia jana.

" Ni kweli tukio hilo lipo. Lakini nipigie simu baadaye kwa sababu nipo kwenye kikao" alisema Kamanda Mkumbo.

Chanzo chetu ndani ya nyumba hiyo kilieleza kuwa vitu vilivyoibwa ni pamoja na nguo, kadi za benki na fedha taslimu, lakini kilikataa kutajwa gazetini.

Inadaiwa Waziri huyo alibaini kuwapo kwa wizi huo alipoamka asubuhi, na hivyo kutoa taarifa katika kituo cha polisi kwa ajili ya ufuatiliaji.

Jitihada za kumtafuta Dk Kamani hazikufanikiwa kwa vile simu yake japo iliita kwa muda mrefu lakini haikuwa na majibu.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Tusubiri utetezi
 
Hapo kwenye RED nadhani umegeuza kalenda juu chini:A S-confused1:

Hilo ni jina la gazeti mkuu

Nipashe.JPG
 
Hakujifunza kwa Adam Malima? Hawa watakuwa ndugu na Malima!!! Mnawapangisha macd wenyewe wakiwaliza mnaaza lia lia!!
 
Hakujifunza kwa Adam Malima? Hawa watakuwa ndugu na Malima!!! Mnawapangisha macd wenyewe wakiwaliza mnaaza lia lia!!

Siku ya Jumamosi Bariadi kulikuwa na Shindano la kumtafuta miss Simiyu na mh. alikuwepo kwenye show..
 
Upuuzi katika hatua ya mwisho hivi Waziri unalala guest house za uswahilini unategemea nini kwanini asingeenda Mwanza? Aibu kubwa sana bora wangemuiba nayeye.
 
Back
Top Bottom