Waziri Abdallah Ulega: Madai ya Samaki kuhifadhiwa kwa maji ya maiti ni hisia tu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Hamis Ulega amesema suala la maji ya kuoshea maiti kudaiwa kutumika kuhifadhia Samaki halina uhakika na kwamba ni hisia tu.

Akijibu swali Bungeni kuhusu taarifa hizo ambapo inadaiwa matumizi ya maji hayo yanasababisha Saratani kwa walaji, amesema “Siyo kweli na ndio maana Makamu wa Rais (Phillip Mpango) ameagiza Wizara ya Afya ifanyie utafiti ili kama kuna kitu cha aina hiyo kizuiwe mara moja.

“Niwatoe hofu Watanzania, wapo salama na hakuna shaka yoyote juu ya taarifa hizo.”

 
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Hamis Ulega amesema suala la maji ya kuoshea maiti kudaiwa kutumika kwenye Samaki halina uhakika na kwamba ni hisia tu

Amesema “Ndio maana Makamu wa Rais (Phillip Mpango) ameagiza Wizara ya Afya ifanyie utafiti ili kama kuna kitu cha aina hiyo kizuiwe mara moja.

“Hakuna kitu kama hicho cha kuhifadhi Samaki kwa maji ya maiti, wapo salama na hakuna shaka yoyote.

Afanye utafiti huru asiseme ati hakuna kitu kama jicho wakati sisi ndio wauzaji wa hizo dawa na sisi ndio wavuvi na wahifadhi samaki

Atusikilize tumwambie ukweli tupone
 
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Hamis Ulega amesema suala la maji ya kuoshea maiti kudaiwa kutumika kwenye Samaki halina uhakika na kwamba ni hisia tu

Amesema “Ndio maana Makamu wa Rais (Phillip Mpango) ameagiza Wizara ya Afya ifanyie utafiti ili kama kuna kitu cha aina hiyo kizuiwe mara moja.

“Hakuna kitu kama hicho cha kuhifadhi Samaki kwa maji ya maiti, wapo salama na hakuna shaka yoyote.
NW anamfokea VP kweli?
 
Makamu wa Rais alikurupuka kuja na habari iliyojaa hisia. Alitakiwa afanye huo utafiti kwanza, kabla ya kutamka hadharani habari yenye ukakasi.
Na wao ni miongoni mwetu tu kuna wakati wanapata Habari za Vijiweni
Wala halina mjadala
Ndio maana unaona wengi wao hukurupuka kama yule wa viti maalum kuongelea ulimaji na uvutaji wa bangi
Akidhani bangi ni kuivuta tu eti duniani wameruhusu
 
Hii ndio Taarifa rasmi iliyotolewa na Naibu Waziri Abdalla Ulega bungeni Dodoma, kwamba uvumi wa samaki kuhifadhiwa kwa kutumia dawa za Maiti hauna ukweli na ni hadithi za kufikirika.

Sasa kama huu ndio Msimamo wa Serikali basi ATAFUTWE MTU ALIYEVUMISHA ILI ATUAMBIE ALIKOTOA UZUSHI HUO .
 
Back
Top Bottom