Duh! man, hakuna kinyume cha sijambo. mimi nadhani umejaribu kutenganisha "si-jambo" ukitenganisha inaleta maana tofauti.
kama sio shwari hakuna neno moja litakaloelezea hiyo hali?
Unapoulizwa hujambo na kama huna-jambo ndio unajibu sijambo,na kama una jambo,kwa mfano unaumwa utajibu,naumwa! au wakati mwingine mtu anajibu,aah wapi bwana hivyo hivyo sijambo ya kiswahili.
Wazee wa lugha, unapoulizwa 'hujambo' huwa unajibu 'sijambo'.
Hiyo inamaanisha upo mzima hakuna tatizo.
Vipi kama kuna tatizo?
Kuna kinyume cha sijambo? Neno lenyewe naliona kama lipo kwa kinyume tayari.
Kipo kinyume chake lakini huwa kinahitaji maelezo au ufafanuo wa hilo jambo lenyewe.
kama ni kinyume tu ni hivi:-
Sijambo ---- Nijambo inamaanisha Nina jambo.
Una jambo...sina jambo
Hujambo ...Sijambo au nijambo.
Sina ujambo.Wazee wa lugha, unapoulizwa 'hujambo' huwa unajibu 'sijambo'.
Hiyo inamaanisha upo mzima hakuna tatizo.
Vipi kama kuna tatizo?
Kuna kinyume cha sijambo? Neno lenyewe naliona kama lipo kwa kinyume tayari.
Mikorogano mingine hii! Mi nimeamua kulipotezea tu hili neno!! nalitumia inapobidi lakini huwa halipambi kiswahili changu kabisa.
unatumia neno gani badala yake unapouliza hujambo?
Mkuu ebu fafanua hii kitu.hahahaha! Au shwari, barida, shkopa, mzuka, neto, shwanga!
Hapo mambo yamenyooka. Lol!
Walioliingiza neno hilo tokea mwanzo walifanya makosa kwani walitakiwa kuangalia sarufi ya kiswahili na kanuni zake. Neno lolote hata kama ni la kukopa ni lazima likubali kunyumbulika kwa kutumia viambishi awali na tamati. Pia, viambishi vikanushi kama si-jambo na hu-jambo vinaenda kinyume kabisa na unyambulikaji wa maneno ya Kiswahili.Wazee wa lugha, unapoulizwa 'hujambo' huwa unajibu 'sijambo'.
Hiyo inamaanisha upo mzima hakuna tatizo.
Vipi kama kuna tatizo?
Kuna kinyume cha sijambo? Neno lenyewe naliona kama lipo kwa kinyume tayari.