Wazazi,ndugu hawamtaki,na yeye hataki kuelewa,ushauri wako unahitajika sana hapa!!

Ndugu zangu wanaJF

Nimekuwa kwenye mahusiano na binti mmoja wa kichagga kwa mwaka mmoja sasa,na kama mjuavyo siku zote mahusiano ya watu wazima wawili yanahitimishwa na ndoa’sasa ishu yenyewe ipo hivi….
Wazazi,ndugu,marafiki kwa asilimia kubwa hakuna anayeniunga mkono katika suala la kumuoa binti huyu,na sababu yao ya msingi ni kwmba ni MCHAGGA.wamejaribu kunieleza kwa mifano hali halisi na tabia za watu wa kabila hili waliowahi kuolewa na ndugu zetu na effects walizozileta kwenye familia zao.

Ukweli ni kwamba yote niliyoelezwa ni sahihi na mifano ninaiona pamoja na matatizo yao kweli yanaonekana kwa mtu yeyote mwenye uelewa mzuri……katika kutafuta ushauri nikashauriwa kwamba ni vema nimweleze mwezangu hali halisi na kutowezekana kwa ndoa kuwepokwa manufaa yetu wote yaani mimi nay eye,

Tatizo limekuja katika kuipokea habari yenyewe,dada wa watu kaipokea negatively na anadai namzingua,ukweli ni kwamba mimi sipo tayari kuwa nae kulingana na sababu nilizomweleza ambazo ni za msingi Kabisa,sasa jamani………nahitaji ushauri wenu wa dhati jinsi gani niweze kumwelewesha dada huyu ilia aache kulia lia na kuangalia mambo yake mengine hasa shule maana ndo kwanza yupo mwaka wa pili katika moja ya vyuo vikuu hapa nchini………

Nawasilisha wakuu…


Naamini kabisa kua thinking capaacity yakoo nii zero.Wakati unaantongoza hadi ukakubaliana nae utamuoa ni wazi kua mlikaa kipindi cha mwaka na unamjua tabia zake kiundani zaidi,iweje leo mzazi na ndugu wakuambie kua hafai na wewe ukubaliane nao?akili yako itakua haipo sawa.

Hao ndugu zako watAkuchagulia mke wamtakao wao au itakuaje?maana katika dunia hii hamna mwanamke perfect inabidi ukubali mapungufu yake of wich najua ulishayakubali ndo maana mmedumu mwaka,iwaje leo umuone hafai kisa ndugu na wazazi?au ukimuoa na wao watakua wanakusaidia ku jig jig?ndo maana wanamuona hana mvuto kwao.Mapenzi ni ya wawili hayahusishi ndugu wala wazazi,wao wanatakiwa tuu wakupeni baraka kwenye ndoa yenu muishi kwa amani na upendo.

Ni dhahiri kabisa hukumpenda huyu dada na unamchezea tuu,maana kama kweli unampenda basi ungeachana na mawazo finyu ya familia na kutengeneza familia yako na huyo msichana,Maisha yA hao ndugu zako na wazazi kwa upande wao yashaishA wanakaribia kuuacha ulimwengu,huu ni wakati wako wewe sasa kuanza yako ili kutengeneza maisha yako yenye furaha na amani.Usiwe mpumbavu wakufikiri,kabila si kitu we kijana.Alafu kesho unamlalamikia MZUNGU anaku discriminate because wewe mtu mweusi!To hell with you,acha aku discriminate mjinga kama wewe ambaye una discriminate kabila tuu wakati wote weusi.Nitashangaa sana kama utakua ni msomi alafu upeo wako wakufikiria na maamuzi ndo huu.
 
Badirika ujinga mzigo kwn wazaz wako, ndugu zako na marafik ndio wataishi nae huyo bint bado unanuka maziwa.

tumia akili ndugu,ile ni ndoa sio mapenzi...........ungeijua maana ya ndoa kwa mapana zaidi usingeandika huo utumbo hapo juu,,nway......okay nimekuelewa!!
 
Naamini kabisa kua thinking capaacity yakoo nii zero.Wakati unaantongoza hadi ukakubaliana nae utamuoa ni wazi kua mlikaa kipindi cha mwaka na unamjua tabia zake kiundani zaidi,iweje leo mzazi na ndugu wakuambie kua hafai na wewe ukubaliane nao?akili yako itakua haipo sawa.

Hao ndugu zako watAkuchagulia mke wamtakao wao au itakuaje?maana katika dunia hii hamna mwanamke perfect inabidi ukubali mapungufu yake of wich najua ulishayakubali ndo maana mmedumu mwaka,iwaje leo umuone hafai kisa ndugu na wazazi?au ukimuoa na wao watakua wanakusaidia ku jig jig?ndo maana wanamuona hana mvuto kwao.Mapenzi ni ya wawili hayahusishi ndugu wala wazazi,wao wanatakiwa tuu wakupeni baraka kwenye ndoa yenu muishi kwa amani na upendo.

Ni dhahiri kabisa hukumpenda huyu dada na unamchezea tuu,maana kama kweli unampenda basi ungeachana na mawazo finyu ya familia na kutengeneza familia yako na huyo msichana,Maisha yA hao ndugu zako na wazazi kwa upande wao yashaishA wanakaribia kuuacha ulimwengu,huu ni wakati wako wewe sasa kuanza yako ili kutengeneza maisha yako yenye furaha na amani.Usiwe mpumbavu wakufikiri,kabila si kitu we kijana.Alafu kesho unamlalamikia MZUNGU anaku discriminate because wewe mtu mweusi!To hell with you,acha aku discriminate mjinga kama wewe ambaye una discriminate kabila tuu wakati wote weusi.Nitashangaa sana kama utakua ni msomi alafu upeo wako wakufikiria na maamuzi ndo huu.


kwenye grey:punguza jazba,rudi kenye hoja ya msingi
green:ungejua nilipotoka nae na vikwazo nilivyopitia pamoja nae,nimekusamehe tu najua hujui
purple:mimi sio mjinga mkuu,tafadhali sana.....sijahitaji kutukanwa hapa,nahitaji ushauri tu na wala si vinginevyo!! kuwa na busara hata kama hoja imekugusa kwa namna moja ama nyingine mkuu!!
red:ndo hakuna tena hizo baraka hapo....unafikiri hiyo ndoa itadumu??
blue:ishu ya elimu hapa haihusiki......ukiihitaji ni PM make hata nikiiweka hapa haina uhusiano na tatizo lililopo mezani

ki ujumla mkuu umetumia jazba nyingi sana kutoa hisia zako,jus cool down....nishauri jambo la msingi na sio kubwabwaja tu,hapa hatumtafuti mshindi,

by the way........................thanks!!!!
 
Si muoaji wewe! Ndoa ni ya watu wawili the rest ni washauri n a washerehekeaji wa ndoa: anayekwenda kuishi na mke ni wewe brother:
Binti kama unavijari hapa chapa lapa muuoaji hayupo hap
 
Mimi nahisi damu wa jamaa atakuwa mmachame manake wanawaogopa kama ukoma.Lakini ukiniambia mrombo au wengine atakuwa amenipa wasiwasi kidogo

huu una ukweli wake,hata wanaume wa huko wanajua. Rafiki zangu wa huko niliosoma nao chuo waliwahi kuniambia,hata wazazi wao huwa wanawaelekeza kuwa wanawake wa sehemu fulani hapana! Hilo ni kabila moja,mzazi anakwambia ni afadhali uoe ndugu yako. Sasa wazazi wetu wa huko mbali wafanyaje? Ila kwa upande mwingine they are very BEAUTIFUL,hilo lazima tukubali.
 
Tuspende kuhukumu kijiji chote kwa kosa lililofanya na mmoja wa wanakijiji...

ni zaidi ya mwanakijiji mmoja mkuu. Hawa watu tumekutana nao vyuoni,tumekaa nao sana. Kwa sisi ambao tulikuwa na interest za kujua ukweli tuliwauliza na wakakili kwamba hivyo vitu vipo. Bad enough mtu anakuambia kabisa yeye mwenyewe anatafuta mwanamke wa kabila tofauti.
 
kwa manufaa yako haya malalamiko ulitakiwa uyapeleke kwingine make hapa mkuu wa msafara huu ni shemeji yako!
 
Ndugu zangu wanaJF

Nimekuwa kwenye mahusiano na binti mmoja wa kichagga kwa mwaka mmoja sasa,na kama mjuavyo siku zote mahusiano ya watu wazima wawili yanahitimishwa na ndoa’sasa ishu yenyewe ipo hivi….
Wazazi,ndugu,marafiki kwa asilimia kubwa hakuna anayeniunga mkono katika suala la kumuoa binti huyu,na sababu yao ya msingi ni kwmba ni MCHAGGA.wamejaribu kunieleza kwa mifano hali halisi na tabia za watu wa kabila hili waliowahi kuolewa na ndugu zetu na effects walizozileta kwenye familia zao.

Ukweli ni kwamba yote niliyoelezwa ni sahihi na mifano ninaiona pamoja na matatizo yao kweli yanaonekana kwa mtu yeyote mwenye uelewa mzuri……katika kutafuta ushauri nikashauriwa kwamba ni vema nimweleze mwezangu hali halisi na kutowezekana kwa ndoa kuwepokwa manufaa yetu wote yaani mimi nay eye,

Tatizo limekuja katika kuipokea habari yenyewe,dada wa watu kaipokea negatively na anadai namzingua,ukweli ni kwamba mimi sipo tayari kuwa nae kulingana na sababu nilizomweleza ambazo ni za msingi Kabisa,sasa jamani………nahitaji ushauri wenu wa dhati jinsi gani niweze kumwelewesha dada huyu ilia aache kulia lia na kuangalia mambo yake mengine hasa shule maana ndo kwanza yupo mwaka wa pili katika moja ya vyuo vikuu hapa nchini………

Nawasilisha wakuu…

Unajua,wazazi wako na good intentions at times but ile kuprotect watoto wao too much wanashindwa kujua,one is neither a child nor wife/husband to them..hekima ni something inahitajika sana..kuna wengine tunawekewa vigezo vya pesa,dini,kabila,beauty,elimu etc,yani wao wanaona they are doing you a fever wakati they sometimes are trying to live your life(with what they perceive as good or bad).kaa chini muombe Mungu akutangulie,it's either wako wrong or wako right!.pia,hekima ya mwanaume ni muhimu sana,a man that is easily swayed by people's judgement as far as a relationship is concerned ni ngumu kuwa na stable family.. leo umepeleka mchaga,how sure are you ukipeleka mzungu watamkubali?do they have a list of what THEY desire from a woman?check the list again before hujaanza relationship ingine.. my last words are:when you choose to do something(its easier to face the regrets kama ilikua wrong)but when people help you choose,the regrets zinakua intense because you will blame yourself and wale wengine!. weka mizani kwenye advice unapata kutoka kwa watu.
 
Ckukubalianinae moja kwa moja, pamoja na kwamba ndoa ni ya wawili lkn familia inayokuzunguka ina nafasi yake kwa sababu ikitokea umeoa mwanamke ambae familia yako hawampendi hasa wazazi, hata wanaweza kua ni wa kabila moja, kuna madhara makubwa yanaweza kujitokeza badae..... 1. Unawezakua umesafiri akipata tatizo hawamsaidii kama wanaishi nyumba moja au karibu. 2. Hata wewe ukipata tatizo wanaweza wasishirikiane na wewe kwa lolote kwa sababu ya kutowasikiliza. 3. Hata mkitofautiana kidogo wao wataamini ni tabia za huyo mwanamke hata kama mkosaji ni mwanaume. 4. Hata akinyanyaswa na mme wake ana nguvu ya kushtaki upande wake tu hawezi kuwaeleza upande wa wakwe zake. 5. Kubwa zaidi endapo mme atatangulia mbele za haki watamnyanyasa sana hadi hata kufikia kumnyang'anya mali alioachiwa na mme wake. Na hili la kudharau wazazi lipo sana sasa hivi kwa sababu hatuwashirikishi wazazi au ndugu wa karibu mwanzo wa mahusiano, tukishachafuana sana ndo tunaenda kuwaambia wazazi nataka kuoa unategemea nini kama wanamjua tabia zake ambazo wewe hukuziona kwa sababu mlianzana kwa tamaa za mwili? Na hili linachangia sana ongezeko na watoto wa mitaani.
 
ha ha ha ha ha kwanza kabisa wewe unasema umeona wanaume walioa wachaga ndoa zao hazikukaa vyema ulichunguza tatizo ni nini hapo? au ulikurupuka tu? kwanza uelewe ukioa mchaga hutakiwi uwe lege lege ni maendeleo mtindo mmoja na pia hakuna habari za kimajungu majungu kama hilo kabila lako pia mnatakiwa muheshimiane ndani ya nyumba ukimletea dharau nae anakuzidishia mara kumi so unatakiwa kuishi kwa repsect we unataka mwakamke umuendeshe kama remote? hapo umechemsha na pia ujue mwanamke kwa kichaga ni mchumi ndani ya nyumba so income unayoipata kwa mwezi lazima aijue na inatumika vip wote mnapanga matumizi. baba kama hauko tayari kwa hilo mwambie mama yako akuchagulie kabinti huko kijijini kwenu ili muendelee kuishi na maisha yenu ya kimajungu majungu na kusema kwanini haumendelei eti mmelogwa. lol mwanaume gani wewe ina maana mbona wachaga kwa wachaga wameoana ina maana nyie kwenye kabila lenu ndio kuna wasichana wenye adabu tu ebo tena wala sikutaki uwe shemeji yangu tena maana naona ni mwanume suruali tu utampa shida bure dada yangu. kwanza msichana yupo chuo we una elimu gani kwanza maana naweza kuongea na mtu ambae kasaidiwa kuweka mada kwenye JF tu. jiangalie jipange uje na mada inayoridhisha hakuna hata mmoja atakekusuport na hii mada ulioitoa pole sana.
 
nimesahu kuuliza wazazi wako walichaguliana au walipendana hilo ni la msingi kuwauliza. kama baba alitafutiwa mzigo ujue mmekwishneeeeeeeeee lol jamani bado kuna mambo ya kijinga namna hii kwenye hii dunia unauliza eti kabila?.... halafu haujasema we kabila gani ningekusaidia kidogo
 
@mtoa maada unanichekesha! Wakati unamdate mpaka mwaka mzima umeisha.....haukujua kama ni mchagga? Sasa hivi ndo unajifanya una msimamo.......khaaa!
 
Kweli wachaga wengi wanatraits fulan za kijinga haswa kwenye ndoa coz nina mifano miwili mmoja wapo ni mke wa kaka yangu.
Ila cha msingi ni we ungeangalia tangu enz za uchumba wenu kuwa je huyo mpz wako ni jamii ile ya wachaga ambao wazaz na ndugu na hata mifano waliokupa anafanana nayo.POINT yangu ni kuwa usije uka generalize jamii ya wachaga wote na hiyo mifano yako kutoka kwa ndugu na ukajikuta umetupa Zahabu ili ubebe jiwe.
 
nimesahu kuuliza wazazi wako walichaguliana au walipendana hilo ni la msingi kuwauliza. kama baba alitafutiwa mzigo ujue mmekwishneeeeeeeeee lol jamani bado kuna mambo ya kijinga namna hii kwenye hii dunia unauliza eti kabila?.... halafu haujasema we kabila gani ningekusaidia kidogo

nimeamua kukuheshimu na kuyaheshimu mawazo yako,nakaa kimya.
 
ha ha ha ha ha kwanza kabisa wewe unasema umeona wanaume walioa wachaga ndoa zao hazikukaa vyema ulichunguza tatizo ni nini hapo? au ulikurupuka tu? kwanza uelewe ukioa mchaga hutakiwi uwe lege lege ni maendeleo mtindo mmoja na pia hakuna habari za kimajungu majungu kama hilo kabila lako pia mnatakiwa muheshimiane ndani ya nyumba ukimletea dharau nae anakuzidishia mara kumi so unatakiwa kuishi kwa repsect we unataka mwakamke umuendeshe kama remote? hapo umechemsha na pia ujue mwanamke kwa kichaga ni mchumi ndani ya nyumba so income unayoipata kwa mwezi lazima aijue na inatumika vip wote mnapanga matumizi. baba kama hauko tayari kwa hilo mwambie mama yako akuchagulie kabinti huko kijijini kwenu ili muendelee kuishi na maisha yenu ya kimajungu majungu na kusema kwanini haumendelei eti mmelogwa. lol mwanaume gani wewe ina maana mbona wachaga kwa wachaga wameoana ina maana nyie kwenye kabila lenu ndio kuna wasichana wenye adabu tu ebo tena wala sikutaki uwe shemeji yangu tena maana naona ni mwanume suruali tu utampa shida bure dada yangu. kwanza msichana yupo chuo we una elimu gani kwanza maana naweza kuongea na mtu ambae kasaidiwa kuweka mada kwenye JF tu. jiangalie jipange uje na mada inayoridhisha hakuna hata mmoja atakekusuport na hii mada ulioitoa pole sana.

punguza hasira,rudi kwenye hoja....huu sio uwanja wa mipasho,kuwa na busara hata kama umeguswa
 
Ndugu, ningekuwa mie ndo wewe ama ndugu yako ningejaribu kufanya analysis ya kabila letu, na kuangalia mifano ya ubaya uliopo. Nina hakika hapo kwenye kwa upande wa baba na upande wa mama ukiutafuta ubaya huwezi kuukosa. Tena kuna siri za familia ambazo ni fedheha tupu! Ukichimbua hukawii kuambiwa huyo unayemuita baba sio babako ni kakako!
Kila aliye m'baya ana uzuri wake. Ishawishi familia yako kwa kuangalia udhaifu wa ndani ya ukoo wenu na uangalie mafanikio ya couple za kichaga. Usije ukamuacha huyo dada ukajuta maisha yako yote!
Kila la kheri, kama umedhamiria mueleweshe tu. Pengine Mungu kampangia mwanaume atakaempenda na kumthamini maisha yake yote.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom