Wazamiaji wa miaka ya 90

Duuuuuuuuh walllah npo tayar kufia huko France, lazima nizamie hukoooh
 

Mmhhh huyo baharia wako amezamia miaka ya 2000?? Mie nakumbua real "STOROWAY" (STOWAWAY) walikuwa miaka ya 70's-80's.
 
Kubaniwa pua na wamama wa Libya ndiyo kutaka kuuwawa?
 
Mmhhh huyo baharia wako amezamia miaka ya 2000?? Mie nakumbua real "STOROWAY" (STOWAWAY) walikuwa miaka ya 70's-80's.
Alianza safari yake mwaka 96 na ametua Tanzania mwaka 2004 napo alikuwa depoted to Kenya from South Korea
 
inaonekana france kuna bata balaa sasa balotel nn kinamshnda mpaka anasema anataka kurud africa na atacheza ligi za africa
 
Mkuu sikutaka kukaa ulaya,,,nikuwa Italy na Spain mwaka 2015 /2016 nikarudi bongo,,nikaenda tena Swiss nikawa France 2019 kwahyo mm sikutaka kukaa kule,,,sababu ya shughuli zangu,,,.now nipo kwenye mandonga,,,,
mandonga ndo nn mzee
 

Vipi kuhusu nchi ya Canada
 
Huu uzi ungekuwa mzuri kama ndugu mhamasishaji wa mambele huko angekuja kutoa vitu vyake no matter what please mzee pita hapa Parabora
 
Reactions: amu
Mkuu hebu elezea kidogo maisha ya turkey yapoje?yaan hii nchi natamani sana kufika
Mkuu Mimi nilikaa kama miezi sita hivi,, pale maisha yanategemea kufanya kazi viwandani mfano viwanda vya nguo,,,nk,,au kuhangaika mitaani,

,ni inchi nzr kwa raia,,lakini kwa wageni ni ngumu kidogo,,, maana kuna migrants wengi wakitokea Syria,, hata Egypt kwa njia za panya,,,pesa ,,, strong hazipishani sana na dola.,,,,,,

pale nilishindwa sababu ya haraka zangu,,nikaelekea Greece,,

sababu sikuwa na viza ya Greece,,, nilikuwa na viza ya Turkey tu,,na Turkey sio inchi ya shengen ,,,ikanibidi nijiunge na migrants wanaokwenda Greece kwa njia za panya,,

Zilikuwa njia mbili za kuingia Greece,,baharini au kupitia mtoni,,,
zote ni dola 500 kila migrants mmoja,,,
nikachaguwa njia ya kuvuka mto,,
niliona ndy salama zaidi,,

Turkey ipo border na Bulgaria,, na Greece,,upande fulani,,kuna mji unaitwa Izmir,,, upo close to Greece,,,tofauti yake ni mto tu,,,

Tulifungiwa kwenye fuso moja tukiwa kama migrants 100 hivi,,,
tulitembea usiku kwa usiku toka Istanbul hadi Izmir kuanzia saa mbili usiku hadi saa sita usiku tukafika lzmir,,,

ilikuwa winter time hatari,,jinsi nilivyo vaa ni kama begi zima lipo mwilini mwangu.,,,nilikuwa nimevaa jeans tatu na track suit ndani,,na fulana tatu ,sweater na koti kubwa la ngozi,na soksi ya kuzuia baridi juu,,still bado baridi hatari.

Baada ya kufunguliwa mlango wa fuso,,,
ilikuwa baridi haswa,,
eneo lote lilikuwa jeupe kwa theluji,,,
basi haraka haraka tukaambiwa tuiname chini,,,,
pale pale wale wa Turkey wenye connection za kutuvusha,,,wakatoa boat ya kujaza kwa upepo,,
wakaijaza pale baada ya kama nusu saa wakaiweka mtoni,,ulikuwa mto wa upana kama wa mita 50 hivi,,,huo mto unatenganisha Turkey na Greece,, na huwa unalindwa pande zote wakati wa summer time,,
lakini unakuwa haulindwi wakati wa winter time...kwahyo winter ndy watu wanakatisha hapo,,basi nikaingia kwenye boat,,ikapigwa kasia hadi upande wa greece ni kama dk 10 tu nipo upande wa Greece,,,

Baada ya kumaliza kutuvusha,,tukaanza safari kuitafuta mjini,,,tulipewa maelekezo na wale jamaa kwamba tufate maandishi ya kigiriki,,,
maana maandishi ya kigiriki na maandishi ya Bulgaria ni tofauti lakini yanafanana sana,,so tufate barabara ambayo inaelekeza maandishi ya kigiriki,,,tukifata tofauti tutakuwa mikononi mwa askari wa Bulgaria,,
na wakasema lazima tukamatwe na police wa kigiriki,, ili watupeleke vituoni,,
tusipokamatwa tutatembea umbali mrefu sn kwa miguu,,,
tusihofu tukiona police,,,

basi tulitembea kuanzia saa nane usiku hadi saa mbili asubuhi,,, tukaanza kukamatwa kwa makundi na kupelekwa kituoni,,ule mji nimesahau kidogo,,, baada ya muda wakatupeleka camp,,,nika complain kama raia wa somalia,,baada ya week mbili za pale camp,,,
nikatolewa nikapelekwa kuna mji mmoja unaitwa ethlonic hapo tukapandishwa train,,,
wakatwambiya you are free to go,,,

Mwandende nikaingia Athens au Athena,,,
huo ndy ulikuwa mwanzo wangu wa kuingia ulaya,,,2011.,.hivyo tu mkuu,,,ktk harakati za mbongo,..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…