Wawindaji na nyati.

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,026
Wawindaji wanne,mmoja akiwa na torch(kurunzi).Wakiwa wanatembea msituni usiku,mwanga wa kurunzi yao ulimulika kitu kama mnyama nyati aliyekaa.Wakazima kurunzi haraka kisha wakajipanga na bunduki zao,wakahesabu 1,2,3...wakamimina risasi mfululizo kisha wakatupa bunduki chini wakapanda juu ya miti kwa usalama wao.Walikesha juu ya miti mpaka kulipokucha.Walishuka toka mitini,kwa mwendo wa mnyato wakalielekea windo lao la jana usiku.Walipofika eneo la tukio hawakuamini walichokiona,lilikuwa ni gogo kubwa la zamani lililotobolewa na risasi!
 
Back
Top Bottom