Wawekezaji Wanakimbia Ushuru. Serikali Mpo !!!!!!

Wawekezaji Wanakimbia Ushuru. Serikali Mpo !!!!!!

DMV

Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
58
Reaction score
63
Wakuu hali nchini kwetu inatisha. Kuna mwekezaji ambaye ni Mwingereza, amefungua ofisi maeneo ya Masaki. Baada ya kukodi ofisi, TRA walimfuata alimpe Ushuru kabla ya kuanza kazi na hii ikawa ni kama Millioni 1.2 corporate tax. Akalipa, baada ya muda mfupi, mwekezaji huyu akatuma vifaa vyake (container 40”) ambayo ilimgharimu $17,000 kutoka Uingereza hadi Dar.

Kufika Dar, TRA walifanya assessment ya kwanza ikawa $4000, baada ya kulipa, wakafanya assessment ya pili, na kumpa bili ya $ 8,400. Mzungu katoa vitu vyake. Baadae katuma vitu kidogo, yaani accessories kwa DHL. Alitumia $238 kuzisafirisha, lakini baada ya bidhaa hizi kufika airport, TRA wakampiga ushuru wa millioni Tsh. 1,205,000. Baada ya hapo mambo yakawa magumu sana, na wafanyakazi 6 alokuwa nao wa kitanzania, ameamua kufunga ofisi yake baada ya miezi 6 Tanzania. Hii ndio Tanzania !
 
Sio kweli

wazungu wako sensitive kwenye kodi na wanaijua kodi kuliko hayo majinga ya TRA, by the way muwekezaji anakuja na Container lenye thamani ya $17,000 alafu anakwenda kufungua ofisi Masaki?

Au ni container la ofisi furniture?

Kuhusu numbers: Bill sahihi kwa taarifa uliyoleta hapa inapaswa kuwa $8,075, hivyo wanapaswa kumpelekea ingine iliyo sahihi.
 
simtetei mzungu wala wawekezeji.
_kufanya biashara Tanzania ni ngumu sana hasa kwa sisi wazawa.
_ninafanya biashara na ninaenda sana kampala na nairobi,hizo nchi mbili ushuru ni bei rahisi sana kama unaingiza bidhaa kwenye hizo nchi na serekali ni rafiki sana wa wafanyabiashara tofauti na Tanzania ambapo uwe umelipa kodi au hujalipa huna amani na mali yako hadi uiuze!
_jiulize ni kwanini Nairobi na kampala bidhaa ni rahisi kuliko Tanzania yenye bandari na airports????
 
Mbona wengine tunalipa tunakamuliwa mpaka tone la mwisho tunajikaza kiume maana hatuna namna
 
Back
Top Bottom