mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,867
- 8,271
Jioni ya leo nimeshuhudia maelfu ya waumini wa kanisa la Mwingira hapa Mwenge wakitoka kwenye misa bila ya hata mmoja kuvaa barakoa, yaani ni kama hawajui kama kuna UVIKO 19 , pia hata kwenye vyombo vya usafiri bado msongamno ni kama zamani kabla ya kutolwa amri na abiria sehemu kubwa hawavai barakoa, hali ni hiyo hiyo hata kwenye maeneo ya biashara kama kwenye migahawa, mahoteli sokoni,madukani. Chonde chonde mkuu wa mkoa Mhsimiwa sana Amos Makalla hakuna anayezingatia maagizo yako,watu wamekuwa wagumu kubadilika, inabidi nguvu za ziada zitumike na mamlaka zisimamie uwajibikaji kwa tatizo hili ,isishie tu kuonyeshwa kuwa mnachanjwa.