Kwanini watu wakiwa Kanisani hawavai Barakoa ila wakienda Sokoni na maeneo mengine wanavaa? Kuna siri gani hapo?

The Humble Dreamer

JF-Expert Member
Oct 12, 2015
7,442
10,233
Wakuu Salaam,

Nimeamkia bucha moja huku niliko nipate nyama nitengeneze mtori, sasa hili bucha linalofungua mapema liko karibu na Kanisa na linauza sana maana watu wakitoka tu ibadani wanajazana pale.

Nilichoshangaaa watu walioko ibadani hawajavaa Barakoa..yani kuanzia muhubiri, waongoza nyimbo, kwaya, watumishi wote mle ndani hawajavaa.

Hili nimelijua kwa njia 3

Moja, bucha lilipo si mbali na kanisa, na mtu akivaa barakoa inaonekana kwa ungaaji wake mana nyingi rangi zina mng'ao. Najua ziko nyeusi pia. Hata mwitikio wa sauti za nyimbo au kujibu 'Amen' ungekua wa chini kama wamevaa barakoa. Lakini wanashangilia kabsa.

Mbili, ni kwamba Nimemuuliza muuza nyama, vipi Ibada ya kwanza watu walikua wamevaa Barakoa? Amejibu 'watu wakiwa ibadani hawavai lakini wakishatoka tu huko Ibadani ndiyo wanaanzia kuvalia hapa buchani kwangu na wengine hawana kabsa.'

Tatu, njia inayoelekea nakokaa nako kuna kanisa, na muda huu asubuhi ndiyo nyimbo za kusifu. Sasa watu wamejiachia wanacheza tu. Hili kanisa halijamaliziwa madirisha yake kwahyo unawaona moja kwa moja. Siyo muhubiri siyo muumini au waimbishaji wote hawajavaa Mask.

Na hii hali inaonekana ni kwa Ibada nyingi hapa Tz.

Watu hao hao wa Ibadani unakutana nao stendi wamevaa, sokoni wamevaa, kwenye gari wamevaa, benki wamevaa nk. Lakini Ibadani hawavai.

Huu ujasiri wa kutovaa barakoa wanautoa wapi?

Hii hali inatia huzuni maana hakuna anayejua afya ya mwenzake hasa ukizingatia hiki kirusi kinaeza kutulia tu ndani ya mtu huku kikiendelea kukutengeneza taratibu na huku ukiendelea kuambukiza wengine. Saa kikichanganya ni kimeamka kweli.

Watu wanatakiwa kuchukua hatua kwa mazingira yote.

Stay Safe.
 
Ila kuvaa barakoa nao mtihani kuna mta ilinilazimu nivae masaa mawili kabla hayajaisha kichwa kikaanza sina hamu nazo
 
Tatizo halijawa kubwa,,lingekuwa kubwa kila mtu angejipanga bila hata kushurutishwa. Sasa sijui corona inatuotea kimya kimya ama watu wengi wako na immunity kubwa.
 
Ila kuvaa barakoa nao mtihani kuna mta ilinilazimu nivae masaa mawili kabla hayajaisha kichwa kikaanza sina hamu nazo
Unakosea KING 360,
Ni lazima kila mmoja avae barakoa na kuchujua hatua nyingine stahiki ili kujikinga yeye binafsi na wengine pia.

Unaposema huwezi kuvaa ilihali unajua kabsa kuna ugonjwa hatari uliopo duniani unaohitaji hatua fln kujilinda, hueleweki.
 
Tatizo halijawa kubwa,,lingekuwa kubwa kila mtu angejipanga bila hata kushurutishwa. Sasa sijui corona inatuotea kimya kimya ama watu wengi wako na immunity kubwa.
Tatizo halijawa kubwa,,lingekuwa kubwa kila mtu angejipanga bila hata kushurutishwa.
Kitaalamu unakosea.
Katika magonjwa haya ya kuambukizana, hatua za awali ili kuzuia maambukizi ndiyo zinazohitajika ili kuzuia. Tusijiaminishe kua tatizo halipo wakati tunashuhudia kweny vyombo vya habari watu wakifa kwa ugonjwa huo.

Sasa sijui corona inatuotea kimya kimya ama watu wengi wako na immunity kubwa.
Unajichanganya..unasema corona ipo kimya kimya hlf hapo tatzo halijawa kubwa.
Kirusi cha corona kinaweza kukaa kwa mtu kikiendelea kujizalisha kila muda na mbaya zaidi kinapitia mutation hivyo usifikir kukabiliana nacho ni rahisi.

Hivyo mtu ataendelea kuambukiza wengine hlf mwishowe watu hawatatibika kwa dalili zitakazokuweko.
Saa kikianza kuchemka ni kimeanza kweli na itakua too late.
 
Hata sokoni hawavai nipo stereo hapa temeke kukulukakala kama kawa pua wazi midomo wazi tunatemeana mimate tu....

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama serikal inatumia wizara ya Afya kutoa elimu kwa watu, na bado wamezira..itafanya nini tena pale ambapo watu haohao wamezidiwa...watu wataendelea kuambukiza wengine kila uchao.

Na mbaya zaidi watu hatujijui kama tuna maambukizi ama lah
 
Inategemea unaongelwa kanisa gani mkuu.
Kanisa nnalosali kwanza sanitizer zimetapakaa kila mlango wa kuingilia. Viti vimewekwa mbali mbali. Unapoingia unapewa barakoa mlangoni.
Sadaka hamshiki kile chombo, ni mhudumu tu na zinawekwa namba za simu, account za bank na kuna mashine ya kuchanja kwa wenye kadi.
Kana kwamba haitoshi, ibada zinarushwa mtandaoni. Wahudumu kila mmoja ana mic yake, hawachangii.

Tukirudi kwenye hoja yako, nafikiri shida ya watu wengi ni imani ya woga. Anafikiri akivaa barakoa ataonekana ana imani hafifu, lakini pia kuna baadhi ya wanaojiita watumishi wanapotosha watu kwa kubeza tahadhari zinazotakiwa kuzingatiwa.
 
Wakuu Salaam,

Nimeamkia bucha moja huku niliko nipate nyama nitengeneze mtori, sasa hili bucha linalofungua mapema liko karibu na Kanisa na linauza sana maana watu wakitoka tu ibadani wanajazana pale.

Nilichoshangaaa watu walioko ibadani hawajavaa Barakoa..yani kuanzia muhubiri, waongoza nyimbo, kwaya, watumishi wote mle ndani hawajavaa.

Hili nimelijua kwa njia 3

Moja, bucha lilipo si mbali na kanisa, na mtu akivaa barakoa inaonekana kwa ungaaji wake mana nyingi rangi zina mng'ao. Najua ziko nyeusi pia. Hata mwitikio wa sauti za nyimbo au kujibu 'Amen' ungekua wa chini kama wamevaa barakoa. Lakini wanashangilia kabsa.

Mbili, ni kwamba Nimemuuliza muuza nyama, vipi Ibada ya kwanza watu walikua wamevaa Barakoa? Amejibu 'watu wakiwa ibadani hawavai lakini wakishatoka tu huko Ibadani ndiyo wanaanzia kuvalia hapa buchani kwangu na wengine hawana kabsa.'

Tatu, njia inayoelekea nakokaa nako kuna kanisa, na muda huu asubuhi ndiyo nyimbo za kusifu. Sasa watu wamejiachia wanacheza tu. Hili kanisa halijamaliziwa madirisha yake kwahyo unawaona moja kwa moja. Siyo muhubiri siyo muumini au waimbishaji wote hawajavaa Mask.

Na hii hali inaonekana ni kwa Ibada nyingi hapa Tz.

Watu hao hao wa Ibadani unakutana nao stendi wamevaa, sokoni wamevaa, kwenye gari wamevaa, benki wamevaa nk. Lakini Ibadani hawavai.

Huu ujasiri wa kutovaa barakoa wanautoa wapi?

Hii hali inatia huzuni maana hakuna anayejua afya ya mwenzake hasa ukizingatia hiki kirusi kinaeza kutulia tu ndani ya mtu huku kikiendelea kukutengeneza taratibu na huku ukiendelea kuambukiza wengine. Saa kikichanganya ni kimeamka kweli.

Watu wanatakiwa kuchukua hatua kwa mazingira yote.

Stay Safe.
nimepita karibu na kanisa asubuhi ya leo wakati naelekea kibaruani nikamsikia muongoza misa anawaambia waumini kwamba, anashangaa kwaniini wakifika kanisani wananawa mikono na maji tiririka lakini wakiingia ndani ya kanisa wanavua barakoa,naona asilimia kubwa ya watanzania wengi wameondokewa na hofu ya huu ugonjwa.
 
Inategemea unaongelwa kanisa gani mkuu.
Kanisa nnalosali kwanza sanitizer zimetapakaa kila mlango wa kuingilia. Viti vimewekwa mbali mbali. Unapoingia unapewa barakoa mlangoni.
Sadaka hamshiki kile chombo, ni mhudumu tu na zinawekwa namba za simu, account za bank na kuna mashine ya kuchanja kwa wenye kadi.
Kana kwamba haitoshi, ibada zinarushwa mtandaoni. Wahudumu kila mmoja ana mic yake, hawachangii.

Tukirudi kwenye hoja yako, nafikiri shida ya watu wengi ni imani ya woga. Anafikiri akivaa barakoa ataonekana ana imani hafifu, lakini pia kuna baadhi ya wanaojiita watumishi wanapotosha watu kwa kubeza tahadhari zinazotakiwa kuzingatiwa.
Inategemea unaongelwa kanisa gani mkuu.
Kanisa nnalosali kwanza sanitizer zimetapakaa kila mlango wa kuingilia. Viti vimewekwa mbali mbali. Unapoingia unapewa barakoa mlangoni.
Sadaka hamshiki kile chombo, ni mhudumu tu na zinawekwa namba za simu, account za bank na kuna mashine ya kuchanja kwa wenye kadi.
Kana kwamba haitoshi, ibada zinarushwa mtandaoni. Wahudumu kila mmoja ana mic yake, hawachangii.
Hapo inaonekana labda si Tz.
Au kama ni hapa Tz basi kwenye ratio yatakua ni machache.

Tukirudi kwenye hoja yako, nafikiri shida ya watu wengi ni imani ya woga. Anafikiri akivaa barakoa ataonekana ana imani hafifu, lakini pia kuna baadhi ya wanaojiita watumishi wanapotosha watu kwa kubeza tahadhari zinazotakiwa kuzingatiwa.
Hilo la imani yo woga ni dhahiri na ndiyo nadharia nafikiri ipo kwa wengi wanaoenda humo. Kirusi cha korona hakijifichi. Watu wana imani lakini bado kinawashika, cha muhimu tahadhari.

Watumishi muda mwingine kweli hawajawa mstari wa mbele kuhakikisha tahadhari inachukuliwa ipasavyo. Na wanadanganya watu corona haiwez washuka. Ref: Gwajima. Hii hali inaongeza maambukizi kanisani bila watu kujua.
 
Back
Top Bottom