richaabra

JF-Expert Member
Jul 12, 2016
1,454
3,469
Mimi ni muumini wa hili kanisa usharika wa Mbezi Louis, tokea nianze kusali nikiwa sunday school pale ni mwaka wa 18 sasa, katika vitu nlivyogundua ni kwamba haya makanisa hasa Kkkt yanaendeshwa kupitia sadaka za waumini yaani waumini wakisema wasitoe sadaka ndani ya miezi 3 tu hali ya viongozi ipo taabani

Usiposhiriki misa au kutoa Sadaka unaonekana mkosaji, ibada nzima ni michango tu kikapu kuanzia mwanzo hadi mwisho watu wanakamuliwa ni pesa kwenda mbele ila sijui kama wanajua hizo pesa zinapotokea ni wapi

Linapokuja swala la uchumi tunatakiwa tuwe kitu kimoja, kesho kama taifa tukiingia mikataba mibovu alafu kesho tukaja kuivunja nchi ikiingia kwenye madeni mazito haumii mtu mwingine tunaumia wote ndio haya matozo na kodi kubwa walizoweka huu ni mwanzo tu picha linakuja Viongozi wetu wa KKKT ikifika mahali mkaambiwa kuwa hatuna pesa sababu uchumi umeharibika muwe wasikivu maana ibada zenu ni kuomba pesa mwanzo mwisho, hajawajenga wachungaji na wainjilisti kujitegemea kiuchumi mmewajenga kuwakamua waumini kwenye kapu la sadaka.

Askofu Shoo unasema unabariki uwekezaji ni uwekezaji gani huo wa kijinga namna hii, unampa mtu Bandari kwa mkataba wa kudumu huo ni uwekezaji au uuzaji wa Bandari? Kesho akiingia kiongozi type ya Magufuli akauvunja mwishowe DP world wataenda mahakamani halafu tukidaiwa mabilioni ya pesa wanatuwekea Tozo na kodi kubwa tulipe wananchi, wananchi tukishapigika tukija makanisani mikono mitupu muwe waelewa maana kodi kubwa ni chanzo cha kufanya watu wafilisike.

Niwapongeze Roman kwa kuwa wakweli maana mmeona mbali, waumini wenu mnajua kabisa uchumi wao ukiyumba utaleta shida hadi kwenu ila uchumi ukinyooka hata kwa kanisa ni faida kubwa.

Na Mama ajue kuwa hatupingi maendeleo wala uwekezaji ila tunapinga uwekezaji wenye Dalili zote zinazoashiria uuzwaji wa mali zetu, Cha kwanza tunachotaka kujua ili Tumbariki mama kwenye Hili la Do world ni haya

1.Mkataba ni wa muda gani kwa nini kuna viashiria kuwa mkataba ni wa milele usalama uko wapi hapo, unawezaje kumpangishia mtu nyumba yako kwa mkataba wa kudumu?

2.Imekuwaje Ubinafsishe Bandari zote za Bara alafu za Zanzibar uziache Hivi Zanzibar hawapendi maendeleo? kama wanayapenda imekuwaje wao hawamo? Tukumbuke kuwa mikopo yote mikubwa Zanzibar mama hakuwasahau alihakikisha wanapata mgao wao, ila hii anayoiita Neema Zanziar hawapo maana yake ni nini?

3.Dp world kuna kipengele kuwa anapinga kuanzishwa au kuendelezwa kwa bandari mpya hadi yeye apewe taarifa na aamue yeye kubariki hilo?, Hivi fikiria kampuni ya bia ya TBL,TCC Zilipoingia ubia na wazungu wangeweka sheria kuwa hakuna kampuni yoyote ya bia itakayoruhusiwa kuanzishwa au kuzalisha bia, Ila ni TBL Pekee yao ndio mwenye hiyo kazi hebu fikiria hivi viwanda vyote pinzani vinavyoiingiza kodi kubwa serikali mfano wazee wa Serengeti Light think TBL angeweka kipengele leo Serikali ingepoteza mapato makubwa kiasi gani kwa kumlilia mtu mmoja

Endapo wazungu wa TANZANIA CIGARETTES COMPANY wangesema enzi hzo kuwa mkataba usomeke kuwa hakuna kampuni yoyote itakayoruhusiwa kufanya biashara ya kuuza sigara au kuzalisha zaidi yetu hivi think hivi viwanda pinzani visingekuwepo hali ingekuwa vipi na ni kwa nini Mkubali kusaini mkataba ambao unapinga uanzishwaji au uendelezwaji wa Bandari mpya hadi Dp ato idhini hapa ndipo shida yetu ila tukihoji mnasema tunaligawa Taifa jibuni hizi hoja.

2.a
 
Mimi ni muumini wa hili kanisa usharika wa Mbezi Louis, tokea nianze kusali nikiwa sunday school pale ni mwaka wa 18 sasa, katika vitu nlivyogundua ni kwamba haya makanisa hasa Kkkt yanaendeshwa kupitia sadaka za waumini yaani waumini wakisema wasitoe sadaka ndani ya miezi 3 tu hali ya viongozi ipo taabani

Usiposhiriki misa au kutoa Sadaka unaonekana mkosaji, ibada nzima ni michango tu kikapu kuanzia mwanzo hadi mwisho watu wanakamuliwa ni pesa kwenda mbele ila sijui kama wanajua hizo pesa zinapotokea ni wapi

Linapokuja swala la uchumi tunatakiwa tuwe kitu kimoja, kesho kama taifa tukiingia mikataba mibovu alafu kesho tukaja kuivunja nchi ikiingia kwenye madeni mazito haumii mtu mwingine tunaumia wote ndio haya matozo na kodi kubwa walizoweka huu ni mwanzo tu picha linakuja Viongozi wetu wa KKKT ikifika mahali mkaambiwa kuwa hatuna pesa sababu uchumi umeharibika muwe wasikivu maana ibada zenu ni kuomba pesa mwanzo mwisho, hajawajenga wachungaji na wainjilisti kujitegemea kiuchumi mmewajenga kuwakamua waumini kwenye kapu la sadaka.

Askofu Shoo unasema unabariki uwekezaji ni uwekezaji gani huo wa kijinga namna hii, unampa mtu Bandari kwa mkataba wa kudumu huo ni uwekezaji au uuzaji wa Bandari? Kesho akiingia kiongozi type ya Magufuli akauvunja mwishowe DP world wataenda mahakamani halafu tukidaiwa mabilioni ya pesa wanatuwekea Tozo na kodi kubwa tulipe wananchi, wananchi tukishapigika tukija makanisani mikono mitupu muwe waelewa maana kodi kubwa ni chanzo cha kufanya watu wafilisike.

Niwapongeze Roman kwa kuwa wakweli maana mmeona mbali, waumini wenu mnajua kabisa uchumi wao ukiyumba utaleta shida hadi kwenu ila uchumi ukinyooka hata kwa kanisa ni faida kubwa.
Hakuna kosa katika kubariki uwekezaji. Wote tunataka uwekezaji.
Shoo aligusia swala la bandari, ila hakutaka kuuweka msimamo hadharani kwa waumini sababu anasema walishakutana na rais na kumpatia Maoni yao.

Hivyo basi, sioni kama upo sahihi kumlaumu Askofu Shoo katika hili. Kama kuna kitu utataka umlaumu Shoo, basi ni kutowashirikisha ninyi waumini kuhusu Msimamo wao kama viongozi wenu au msimamo wa Kanisa na kupelekea mkiwa hamuelewi msimamie kipi.
 
Juzi kuna mchungaji kaingia kakuta tarazo zimewekwa akasema ziwekwe mpya material yapo tanzania akasema anaagiza yeye nnje ndio mazuri yaani ni upigaji kila kona.
Yaani unakiri upigaji upo kanisani!
Sasa kama wakanisani tu mmeshindwa kuudhibiti huu wa serikali sizani kama itawezekana
Tena chini ya CCM kwa muunganiko wa serikali viongozi wa dini na deepstate..
Anyway waliotia saini wapo kimyaaa sijui hizi kelele zetu kama zitazaa matunda sijui..
 
Ukisikiliza kwa makini Askofu Shoo hakuunga mkono mkataba wa Bandari!! Amesema walimpa ushauri Samia juu ya huo mkataba na yeye aliahidi kuwa angeyafanyia kazi mapendekezo yao.
Askofu akamalizia na kibwagizo ambacho nadhani kilimlenga mkwere kuwa " TUNAPOWAKOSOA MNATUAMBIA TUNACHANGANYA SIASA NA DINI"!
 
Yaani unakiri upigaji upo kanisani!
Sasa kama wakanisani tu mmeshindwa kuudhibiti huu wa serikali sizani kama itawezekana
Tena chini ya CCM kwa muunganiko wa serikali viongozi wa dini na deepstate..
Anyway waliotia saini wapo kimyaaa sijui hizi kelele zetu kama zitazaa matunda sijui..
kote ni upigaji
 
Vyovyote iwavyo, hoja zijibiwe...

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Vyovyote iwavyo, hoja zijibiwe...

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

Zinapotakiwa zijibiwe hizo hoja, ndio unaambiwa dini zisiingilie siasa
 
Back
Top Bottom