Watumiaji wa AliExpress, Msaada wenu tafdhali

Watumiaji wa AliExpress, Msaada wenu tafdhali

Baba Rhobi

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2020
Posts
1,846
Reaction score
3,373
Mimi nimetumia AliExpress muda kidogo umepita, mwaka 2025 nilitumia mara moja tu, tena pale mwanzoni, juzi hapa naingia nahitaji kuagiza kitu nakuta mauza uza.

Shipping method ni moja tu, "Free shipping" na hakuna option ya kuchagua na hujui nani ataleta mzigo, pia muda ni mrefu sana, mfano na angalia leo May 10, mzigo unasoma watadeliver July 15, Mbona kama ni mrefu sana, na kwa uzoefu wangu ilikua ikisoma Siku 21 maximum mwezi, leo ni miezi miwili na zaidi, aliye agizisha hivi karibuni anipe uzoefu tafadhali.
 
Hujui kama hali ya usafir wa maji sio salama? Au ndo nyinyi wapumbavu msioangalia hata taarifa za habari za kimataifa?
Matusi ya nini Ndugu yangu, AliExpress mara nyingi kama sio mara zote hutumia usafiri wa Anga ndio maana nimeuliza, na nimeandika hapo vizuri kabisa kwa walio tumia huduma zao recently anipe uzoefu, wewe hapo zoefu umeandika upi....!?
 
Matusi ya nini Ndugu yangu, AliExpress mara nyingi kama sio mara zote hutumia usafiri wa Anga ndio maana nimeuliza, na nimeandika hapo vizuri kabisa kwa walio tumia huduma zao recently anipe uzoefu, wewe hapo zoefu umeandika upi....!?
Bado huna unalolijua kwaher
 
Mimi nimetumia AliExpress muda kidogo umepita, mwaka 2025 nilitumia mara moja tu, tena pale mwanzoni, juzi hapa naingia nahitaji kuagiza kitu nakuta mauza uza.

Shipping method ni moja tu, "Free shipping" na hakuna option ya kuchagua na hujui nani ataleta mzigo, pia muda ni mrefu sana, mfano na angalia leo May 10, mzigo unasoma watadeliver July 15, Mbona kama ni mrefu sana, na kwa uzoefu wangu ilikua ikisoma Siku 21 maximum mwezi, leo ni miezi miwili na zaidi, aliye agizisha hivi karibuni anipe uzoefu tafadhali.
Free shipping mara nyingi karibia zote ni speedaf
 
Mtoa bandiko pole kwa kutokujua haya,
Kwanza huo mda ulioandikwa hapo wa siku 75 kama sikosei ni makadirio ya juu ila aliexpress now wako njema mara nyingi mizigo naipata chini ya siku 18 hivo nunua tu.
Product kua na free shiping isikufanye kusita kununua kwani mizigo inasafirishwa na inafika vizuri kabisa tu
 
Mtoa bandiko pole kwa kutokujua haya,
Kwanza huo mda ulioandikwa hapo wa siku 75 kama sikosei ni makadirio ya juu ila aliexpress now wako njema mara nyingi mizigo naipata chini ya siku 18 hivo nunua tu.
Product kua na free shiping isikufanye kusita kununua kwani mizigo inasafirishwa na inafika vizuri kabisa tu
Ila mzigo ukipitia posta kuna mawili uupate au usiupate bora kutumia wakala wa alitexpress
 
Ni kweli anachosema. Posta bado kuna njaa. Watu hawatosheki na mishahara yao.
Cha msingi atumie speedaf asiache freeshipping ipitie Posta atalia!
Acheni ujuaji usio na tija haya specific eleza kabisa ukiingia aliexpress kununua mzigo kuna sehemu umewahi kutana na shipping carrier speedaf (imetajwa before ya kufanya malipo) au automatic wao ndio wanaselekt item ije na carrier yupi? Kama hujui procedure za kununua vitu online utabaki unalaumu watu bure na kuwachafua. BORA KUULIZA UKAELEKEZWA HAO SPEEDAF UNAZIJUA KERO ZAO AU PENGINE MNANUNUA ITEM MOJA LEO MNAKAA MIEZI TISA NDIO MNA NUNUA INGINE. Posta tz ni bora mara elfu moja na wametusaidia kwa mda mrefu before hao speedaf na ufikaj wa mzigo ni asilimia mia. Pitia humu nyuzi za speedaf kulalamikiwa ziko ngapi linganisha na posta uje na ushahid hapa. Tunanunua kila siku na mizigo inafika salama tu. Sasa hao ajent wa speedaf ambao hata kulipwa kwao ni kwa kamisheni kwa kila mzigo uje ulinganishe na watumishi wa posta? Ushahidi huo, kwa mwezi mmoja nanunua bidhaa si chini ya laki 5nazote hunifikia bila kelele
 

Attachments

  • Screenshot_2026-05-27-12-07-03-416_com.android.mms-edit.jpg
    Screenshot_2026-05-27-12-07-03-416_com.android.mms-edit.jpg
    99.9 KB · Views: 17
  • Screenshot_2026-05-27-12-07-56-204_com.android.mms-edit.jpg
    Screenshot_2026-05-27-12-07-56-204_com.android.mms-edit.jpg
    90.7 KB · Views: 16
  • Screenshot_2026-05-27-12-08-57-106_com.android.mms-edit.jpg
    Screenshot_2026-05-27-12-08-57-106_com.android.mms-edit.jpg
    86.4 KB · Views: 14
Bidhaa hizo na zinafika fresh tu na unapatiwa huduma kama inavyotakikana na pia tizama ushahidi hapo wa speedaf mhusika alipokea simu akaona ajipongeze mpka leo hajatoa ushirikiano na mfumo unataja hadi namba yake ni hio na hajawahi patikana na hq speedaf majibu hovyo ngoja kikikulamba
 

Attachments

  • Screenshot_2026-05-27-12-13-19-969_com.alibaba.aliexpresshd-edit.jpg
    Screenshot_2026-05-27-12-13-19-969_com.alibaba.aliexpresshd-edit.jpg
    139.3 KB · Views: 12
  • Screenshot_2026-05-27-12-16-30-050_com.whatsapp-edit.jpg
    Screenshot_2026-05-27-12-16-30-050_com.whatsapp-edit.jpg
    83.2 KB · Views: 16
Back
Top Bottom