Naam, ninalo,
Mtoa mada amechanganya changanya vitu vingi amewaponda wacheza mpira wanawake lakini pia amewaponda waafrika kwa ujumla, naona hapo kwa waafrika ni kama na yeye anafanya kama walivyo waafrika wengine, kuona waafrika hawafai kufurahi, kumwaga mipesa, kufanya the so called dhambi kisa ni waafrika hapo tayari mindset yake imefungwa fungwa na utumwa wa fikra, kila binaadam bila kujali jinsi yake, rangi yake, utaifa wake waka sexuality yake anahaki ya kufanya chochote na akasifiwa ama kuadhibiwa kama amepitiliza
Tukija kwa wachezaji wa Africa wa kike ni kweli wengi wana utomboy na hii inachagizwa na jamii waliyopo kuona kua mpira wa miguu ni wa wanaume kwa hiyo na wao wanajikuta wanaiga ukiume ili waende sawa na kaka zao, binafsi sipendezwi na hicho kitu, hivyo hivyo kwa boxing,
Wachezaji wa Ulaya na America ni moja ya sharti zao kua kikike nilivyosikia, nadhani wasingeweka hilo sharti tungeona mabro wengi sana wakisakata kabumbu.