kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
KATIKA hali ya kuonyesha mmomonyoka wa adabu unazidi kushika kasi kwa baadhi ya watu, mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Rabia [32] amejikuta akipata aibu ya mwaka baada ya kukutwa akifanya mapenzi na mume wa mdogo wake.
Hali hiyo ilijitokeza jana huko maeneo ya Yombo Vituka, majira ya saa moja usiku baada ya mdogo wa mwanamke huyo kupiga kelele za mayowe baada ya kuwakuta mumewe na dada yake wakiwa ndani wakifanya mapenzi.
Tukio hilo lilisisimua watu na watu walimiminika eneo hilo kumshuhudia mwanamke huyo aliyekosa hata chembe ya huruma kuiba mume wa mdogo wake.
Nifahamishe ilishuhudia tukio hilo wakati ilipokuwa katika harakati za kusuka habari na ilipofika eneo hilo ilikuta watu wakimshambilia huku wengine wakitoa maneno machafu kwa mwanamke huyo huku mdogo wake akilia kwa uchungu kuhusiana na tukio hilo.
Na huku akijaribu kuwasiliana na kuwajuza wazazi wake kuhusiana na tukio hilo huku wengine wakimtia moyo kuhusiana na tukio hilo.
Imedaiwa kuwa, Fatuma [28] ambaye ni mke wa mume aliyefahamika kwa jina la Fred, asubuhi ya jana aliwaaga majirani zake kuwa anakwenda mkoani Pwani kwa mama yake mzazi akamsalimie.
Ilipofika majira ya saa 5 asubuhi walimuona dada yake alifika hapo na majirani walimjuza kuwa mdogo wake hayupo lakini cha kushangaza alionekana akifungua mlango na kuingia ndani.
Majira ya mchana waliweza kumuona mume wa Fatuma alirudi hali ambayo hawakuielewa kwa kuwa hawakuzoea mume huyo kurudi majira hayo lakini walidhani huenda alirudi mara moja
Majirani waliendelea na shughuli zao na kumuona dada huyo akijishughulisha na shuhguli za nyumbani kwa mdogo wake huyo na watu hawakupata na wasiwasi kwa kuwa walishamzoea kufika hapo mara kwa mara
Mpashaji wa habari hii ambaye anaishi chumba cha pili kutoka chumba cha Fatuma alidai majria ya saa 10 jioni walisikia sauti ya redio imefunguliwa kwa sauti ya juu lakini waliendelea na shughuli zao.
Imedaiwa Fatuma aliweza kufika nyumbani hapo majira ya saa 12:47 na aliingia ndani na ghafla alipiga kelele za mayowe na ghafla hakusikika tena akipiga kelele hizo
Ndipo majirani walipokimbilia na kumkuta ameanguka chini kwa hofu na mume wa dada huyo akiwa amevaa upande wa kitenge na kumuona tena dada yake akiwa na amevaa upande wa khanga
Hata hivyo waliachana na wawili walichofanya wamshuhulikie kwanza afya ya Fatuma na dakika chache baadae hali yake ikawa sawa ndipo alipoelezea hali aliyoikuta ndani kwake na kueleza kuwa alimkuta dada yake na mumewe wakiwa katika hali ya kufanya mapenzi na majirani walianza kumshambulia mwanamke huyo na kwa makelele na watu waliposikia tukio hilo walimiminika kushuhudia tukio hilo
Imedaiwa mwanamke huyo alitaka kuchomoka mlangoni na kukimbia lakini kuna baadhi ya watu walimzuia na walimzuia pia asivae nguo na abaki hivyo hivyo
Nifahamishe ilishuhudia mdogo wa mwanamke huyo akishikwa na majirani zake na aliomba majirani hao wampeleka kwa shangazi yake anayeishi karibu nae ili akapumnike huko na asingeweza kulala hapo
Hadi nifahamishe inaondoka eneo hilo iliacha Fatuma anaondoka nyumbani kwake hapo kuelekea kwa shangazi yake huyo akajipumnzishe na dada yake akilia kwa kujilaumu kwa aliyoyafanya huku mume huyo nae akibaki ameinama kwa aibu aliyoipata kwa majirani zake
Hali hiyo ilijitokeza jana huko maeneo ya Yombo Vituka, majira ya saa moja usiku baada ya mdogo wa mwanamke huyo kupiga kelele za mayowe baada ya kuwakuta mumewe na dada yake wakiwa ndani wakifanya mapenzi.
Tukio hilo lilisisimua watu na watu walimiminika eneo hilo kumshuhudia mwanamke huyo aliyekosa hata chembe ya huruma kuiba mume wa mdogo wake.
Nifahamishe ilishuhudia tukio hilo wakati ilipokuwa katika harakati za kusuka habari na ilipofika eneo hilo ilikuta watu wakimshambilia huku wengine wakitoa maneno machafu kwa mwanamke huyo huku mdogo wake akilia kwa uchungu kuhusiana na tukio hilo.
Na huku akijaribu kuwasiliana na kuwajuza wazazi wake kuhusiana na tukio hilo huku wengine wakimtia moyo kuhusiana na tukio hilo.
Imedaiwa kuwa, Fatuma [28] ambaye ni mke wa mume aliyefahamika kwa jina la Fred, asubuhi ya jana aliwaaga majirani zake kuwa anakwenda mkoani Pwani kwa mama yake mzazi akamsalimie.
Ilipofika majira ya saa 5 asubuhi walimuona dada yake alifika hapo na majirani walimjuza kuwa mdogo wake hayupo lakini cha kushangaza alionekana akifungua mlango na kuingia ndani.
Majira ya mchana waliweza kumuona mume wa Fatuma alirudi hali ambayo hawakuielewa kwa kuwa hawakuzoea mume huyo kurudi majira hayo lakini walidhani huenda alirudi mara moja
Majirani waliendelea na shughuli zao na kumuona dada huyo akijishughulisha na shuhguli za nyumbani kwa mdogo wake huyo na watu hawakupata na wasiwasi kwa kuwa walishamzoea kufika hapo mara kwa mara
Mpashaji wa habari hii ambaye anaishi chumba cha pili kutoka chumba cha Fatuma alidai majria ya saa 10 jioni walisikia sauti ya redio imefunguliwa kwa sauti ya juu lakini waliendelea na shughuli zao.
Imedaiwa Fatuma aliweza kufika nyumbani hapo majira ya saa 12:47 na aliingia ndani na ghafla alipiga kelele za mayowe na ghafla hakusikika tena akipiga kelele hizo
Ndipo majirani walipokimbilia na kumkuta ameanguka chini kwa hofu na mume wa dada huyo akiwa amevaa upande wa kitenge na kumuona tena dada yake akiwa na amevaa upande wa khanga
Hata hivyo waliachana na wawili walichofanya wamshuhulikie kwanza afya ya Fatuma na dakika chache baadae hali yake ikawa sawa ndipo alipoelezea hali aliyoikuta ndani kwake na kueleza kuwa alimkuta dada yake na mumewe wakiwa katika hali ya kufanya mapenzi na majirani walianza kumshambulia mwanamke huyo na kwa makelele na watu waliposikia tukio hilo walimiminika kushuhudia tukio hilo
Imedaiwa mwanamke huyo alitaka kuchomoka mlangoni na kukimbia lakini kuna baadhi ya watu walimzuia na walimzuia pia asivae nguo na abaki hivyo hivyo
Nifahamishe ilishuhudia mdogo wa mwanamke huyo akishikwa na majirani zake na aliomba majirani hao wampeleka kwa shangazi yake anayeishi karibu nae ili akapumnike huko na asingeweza kulala hapo
Hadi nifahamishe inaondoka eneo hilo iliacha Fatuma anaondoka nyumbani kwake hapo kuelekea kwa shangazi yake huyo akajipumnzishe na dada yake akilia kwa kujilaumu kwa aliyoyafanya huku mume huyo nae akibaki ameinama kwa aibu aliyoipata kwa majirani zake