Watu wa Dar acheni kuwatelekeza ndugu zenu stendi

Mhaya

JF-Expert Member
Aug 20, 2023
1,658
4,866
Watu wengi wanaoishi Dar es salaam wakipigiwa simu na ndugu zao wa mikoani, hawataki kusema ugumu wa maisha ulioko Dar es salaam badala yake wanasifu uzuri wa jiji na raha zilizoko kwenye jiji hilo namba moja nchini Tanzania. Kupelekea kuwafanya na ndugu walioko mikoani kutaka kufunga safari wakihisi Dar es salaam kuna maisha raha mstarehe.

Ndugu hao wakishafunga safari na kufika stand ya mabasi Magufuli basi wanatelekezwa, na hao ndugu zao wa Dar uwazimia simu. Jambo ambalo limesababisha watu wengi wa mitaani kuongezeka jijini, ambapo kwa siku stand ya Magufuli upokea makumi ya watu waiokuwa na pa kwenda miongoni mwao ni hao waliotelekezwa na ndugu zao.

Kama uwezi kuwa mwenyeji wa mtu, si bora umwambie tu, atafute alternative kuliko kumtia moyo ya kuja kuishi Dar es salaam na kisha kumtelekeza. Kama maisha yamekuchapa, mwambie tu ukweli kwamba maisha yangu hayako sawa. Hili abaki mkoani, kuliko kujichanga nauli alafu unamtupa stand.
 
Kuna mmoja kaniambia anakuja jumatano. Me nikakubali tu. Anzia kesho sipatikaniii.

Mnavopanga safari zenu huwa mnamshirikisha nani? Unaamua tu kwa vile flani yuko sehemu ngoja niende.unajua anapitia hali gani? Unajiamulia tu mwenyewe. Maisha yenyewe yashaharibika tukiwalaza na watoto wetu mnawaharibu.dawa yenu ndo hyo mtaishia magufuli stend hadi mkome.
 
Kuna mmoja kaniambia anakuja jumatano. Me nikakubali tu. Anzia kesho sipatikaniii.

Mnavopanga safari zenu huwa mnamshirikisha nani? Unaamua tu kwa vile flani yuko sehemu ngoja niende.unajua anapitia hali gani? Unajiamulia tu mwenyewe. Maisha yenyewe yashaharibika tukiwalaza na watoto wetu mnawaharibu.dawa yenu ndo hyo mtaishia magufuli stend hadi mkome.
Tutolee unafiki na ujinga wako hapa, .Ulitakiwa umwambie safari njema ila sina nafasi ya kufikia kwangu.
 
Mimi nafanyakazi stend ya magufuli na hizo kesi za watu kutelekezwa na ndugu zao mbona sizioni? Wanaweza kupoteana siku moja kutokana na matatizo ya mawasiliano kesho yake anapata mwenyeji wake! Ebu tupe ushaidi mkuu
Wakiwa njiani wanapiga simu kila saa .anafika kati huko simu inaisha charge. Hawatulii
Mtu anatoka mwanza hajafika hata shinyanga amepiga mara kumi kila mahali anatoa update
Hadi afike dodoma na simu ishaharibika kabisa. Anaingia dar hajui aanzie wapi.
 
Kuna mmoja kaniambia anakuja jumatano. Me nikakubali tu. Anzia kesho sipatikaniii.

Mnavopanga safari zenu huwa mnamshirikisha nani? Unaamua tu kwa vile flani yuko sehemu ngoja niende.unajua anapitia hali gani? Unajiamulia tu mwenyewe. Maisha yenyewe yashaharibika tukiwalaza na watoto wetu mnawaharibu.dawa yenu ndo hyo mtaishia magufuli stend hadi mkome.
😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 nimechekaa balaa
 
Fikiria unamwambia hivyo dada yako aliyekulea
Kuna mmoja kaniambia anakuja jumatano. Me nikakubali tu. Anzia kesho sipatikaniii.

Mnavopanga safari zenu huwa mnamshirikisha nani? Unaamua tu kwa vile flani yuko sehemu ngoja niende.unajua anapitia hali gani? Unajiamulia tu mwenyewe. Maisha yenyewe yashaharibika tukiwalaza na watoto wetu mnawaharibu.dawa yenu ndo hyo mtaishia magufuli stend hadi mkome.
 
Mimi nafanyakazi stend ya magufuli na hizo kesi za watu kutelekezwa na ndugu zao mbona sizioni? Wanaweza kupoteana siku moja kutokana na matatizo ya mawasiliano kesho yake anapata mwenyeji wake! Ebu tupe ushaidi mkuu
Wanaopotea ni wale wanaodhani Dar es salaam ni kijiji anapanda basi tu anashuka stendi analeta ujuaji wa kijijini akidhani akiulizia mtu yeyote jina la huyo ndugu yake kila mtu atakuwa anamjua

Akifika Dar ujuaji unaisha simu ya huyo nduguye hana kaja kichwa kichwa jiji anashangaa
 
Kuna mmoja kaniambia anakuja jumatano
Me nikakubali tu
Anzia kesho sipatikaniii
Mnavopanga safari zenu huwa mnamshirikisha nani?? Unaamua tu kwa vile flani yuko sehemu ngoja niende.unajua anapitia hali gani?? Unajiamulia tu mwenyewe
Maisha yenyewe yashaharibika tukiwalaza na watoto wetu mnawaharibu.dawa yenu ndo hyo mtaishia magufuli stend hadi mkome
Kuna wengine walitelekezwa.
Yaani mtu anampigia classmate waliosoma wote na hawakuwa na mazoea hata.
Anampigia classmate eti awapokee ndugu zake.

Jamaa kufika jioni ,hapatikani..
Wanahaha.
Jamaa hakupatikana hadi kesho yake,ndio anawarudia kuwa eti simu ilizima chaji.

Kuanza kututafuta kuwa tukawapokee,na wakati hata taarifa hawakutoa..
Wanafika kibaha hapo ndio wanapiga simu tuende kuwapoke..sie tulishakula na tunajiandaa kulala.

Jamani watu wa mikoani..Dar watu maisha ni magumu..
Usidhani eti sijui classmate wa mwanao aje kukuchukua na hata hawakuwa marafiki kihivyo.
Fikieni tu kwa sisi ndugu zenu,na mtupe taarifa mapema kabla hamjasafiri...Siyo mtu upo kibaha ama umeshashuka stand ,umekuwa fungu la kukosa ndio unaanza kupiga simu za ghafla tuje kukuchukua.
Hiv mtu anafika dar ndo anakupgia? Hayupo serious, toa taarifa siku mbili tatu kabla mtu ajue anakupa jibu la ndio au la!!
 
Asee Daslam na watanzania💔😅
Ni vyema kutoa taarifa mapema kama unakuja kwa jambo la msingi ili anaekupokea ajipange au akupange unipange.
Na kama unakuja kuzurura tu basi fika Daslam fanya mishe zako tenga muda kidogo wa kumsalimia umjuae ila sio kumvika majukum.
Watu wana ndugu chungu nzima na wote hufika Daslam kwa sababu zao huwezi wamaliza.
 
Watu wengi wanaoishi Dar es salaam wakipigiwa simu na ndugu zao wa mikoani, hawataki kusema ugumu wa maisha ulioko Dar es salaam badala yake wanasifu uzuri wa jiji na raha zilizoko kwenye jiji hilo namba moja nchini Tanzania. Kupelekea kuwafanya na ndugu walioko mikoani kutaka kufunga safari wakihisi Dar es salaam kuna maisha raha mstarehe.

Ndugu hao wakishafunga safari na kufika stand ya mabasi Magufuli basi wanatelekezwa, na hao ndugu zao wa Dar uwazimia simu. Jambo ambalo limesababisha watu wengi wa mitaani kuongezeka jijini, ambapo kwa siku stand ya Magufuli upokea makumi ya watu waiokuwa na pa kwenda miongoni mwao ni hao waliotelekezwa na ndugu zao.

Kama uwezi kuwa mwenyeji wa mtu, si bora umwambie tu, atafute alternative kuliko kumtia moyo ya kuja kuishi Dar es salaam na kisha kumtelekeza. Kama maisha yamekuchapa, mwambie tu ukweli kwamba maisha yangu hayako sawa. Hili abaki mkoani, kuliko kujichanga nauli alafu unamtupa stand.
Hata watz waliopo USA hawatuambii ukweli wa hali halisi ya maisha ya huko, kimbembe tukifika tunakuta mchizi analala kwenye kichumba hata kugeuka hageuki
 
Back
Top Bottom