Watu hawakumuelewa Rais Magufuli

Watu hawakumuelewa Rais Magufuli

Kuna haja ya Magufuli kushughurika na huyu Lowasa, Nadhani
bado anaweweseka, akimuacha atatuharibia nchi
 
Wewe kwanini usiende kulima? Hivi unafikiri shughuli ambayo ni dili Tanzania huwa inasukumiwa watu wa kundi fulani kwenda kuifanya au uwa inalazimishwa.
Wewe unajuaje kama silimi? Kilimo kinalipa inategemea wewe unafanya kilimo cha nini na unakiendesha je. Hivi unafahamu kama kuna ardhi hapa Tanzania haijawahi kulimwa na haiitaji mbolea za viwandani?
 
HOPO KWENYE BOLD, RAIS ALISEMA WATENDAJI WANAOWANYANYASA WANANCHI WASEKWE NDANI, WEWE UNASEMA UONEVU KWA WANANCHI TENA JAMAN AU RAIS ANAWANANCHI WAKE NA WEWE UNAO WAKWAKO????



KUNA WATENDAJI UWEZI PATA UDUMA BILA KUTOA KITU KIDOGO, AU KM WEWE NI MASKINI AKUSIKILIZI, HAWA NDIO WANONYANYASA WANANCHI NDIO MAANA RAIS KASEMA WAWEKWE NDANI

..kwanini wasichukuliwe hatua za kinidhamu kulingana na taratibu za ajira zao badala yake inahimizwa wawekwe ndani 48 hours?

..hata watendaji wa serikali nao ni wananchi. wakuu wa mikoa na wilaya wanaweza kutumia agizo hilo vibaya kunyanyasa wananchi na Raisi asiwachukulie hatua Kama ilivyotokea kwa rc mulugo na Makonda.
 
..Raisi anakosea kutoa kauli za VITISHO.

..pia kuwahimiza ma-rc na ma-dc kuwasweka mahabusu kwa masaa 48 watendaji wa serikali kunaweza kusababisha uonevu kwa wananchi wasio na hatia.

..zaidi utaratibu na pilikapilika za kukamata vijana wasio na kazi siyo jambo jipya hapa nchini. But one thing has remained constant, utaratibu huo haujawahi kutatua tatizo la uzururaji ambalo linasababishwa na ukosefu wa ajira.

..uchumi wetu, kutokana na sera mbovu za ccm, hauzalishi ajira za kutosha na zinazovutia kwa vijana wetu na hi yo kusababisha wazurure mitaani. Sijui kama unakumbuka tukio la vijana kujaa uwanja wa taifa wakati idara ya uhamiaji ilipotangaza nafasi za kazi.

..kwa hiyo Raisi na watendaji wake warudi kwenye drawing board na kuja na mikakati ya kupambana na tatizo la UKOSEFU WA AJIRA.
Ukosefu wa ajira zipi na za aina gani ndio tatizo. Vijana wengi wanaokimbilia mijini ni wale waliomaliza elimu ya msingi na wanaona kilimo ni kazi ngumu hawaiwezi wanawaachia baba na mama zao waifanye kazi hiyo. Kundi jingine ni vijana waliomaliza elimu ya sekondari na vyuo. Hawa nao wanadhani white colar jobs ndio size yao! Kwa hiyo tunajikuta taifa lina vijana wengi wenye nguvu wanaoweza kufanya kazi za kilimo na UJASIRIAMALI wenye tija lakini hawataki kufanya kazi hizo. Kilimo na UJASIRIAMALI kumeweza kuwanufaisha ama kwa kiswahili kipya KUWATOA vijana walioonyesha nia ya kujiajiri. Rais amewatuma kazi ma RC ya kuwamobilise vijana wasio na kazi na wale wanaochagua kazi wapatiwe kazi sio wacheze pool na kuzururua tu! Sioni njia nyingine yoyote inayoweza kuleta ajira kwenye mazingira tuliyonayo.
 
Habari wana JF
Jana Rais Magufuli aliwahutubia kwa muda mfupi wakuu wa mikoa baada ya kuwaapisha. Rais aliongea mambo machache lakini yaliyobeba maana kubwa kuhusu uwajibikaji na watu kufanya kazi hasa akitia msisitizo kuwa tumeshachelewakwa kuwa haya yalitakiwa kuanza miaka kumi iliyopita.
Ni ukweli uliyodhahiri kuwa tumechelewa tena sana kutokana na nchi yetu iliyojaliwa kuwa na raslimali nyingi pamoja na ardhi kubwa yenye rutuba.
Jambo la kushangaza watu wameibuka na kauli mbalimbali wakiwemo wanasiasa, ambazo zimebadili maana halisi iliyokuwa kwenye baadhi ya maneno ya Mh. Rais.

Mh. Rais aliwaambia ma-RC "kuna watendaji wengine kazi yao ni kuwanyanyasa wananchi nendeni mkawashughulikie. Nyinyi mna mamlaka ya kumweka mtu ndani masaa 48, wawekeni ndani ili wawaheshimu wananchi". Lakini kauli hii imepindishwa na watu, hata wengine wakisema wakuu wa mikoa wameagizwa waende kuwakamata vijana wasiokuwa na kazi!
Hivi kweli hawa wakuu wa mikoa ni watu wasiojitambua ambao wanaweza kuitumia sheria inayowapa mamlaka hayo kuwaonea watu wasiokuwa na hatia?

Jambo jingine ambalo linapotoshwa ni kauli ya Rais kuzuia watu kucheza pool table asubuhi na kuwataka vijana kufanya kazi badala ya kuzurura pale alipokazia kuwa ikiwezekana walazimishwe kufanya kazi kwenye kambi maalum.
Watanzania wenzangu hivi ni kutokufuatilia sheria au ni upotoshaji wa makusudi? Niwaulize wanasheria akina Tundu Lissu, sheria inasemaje kuhusu muda wa kufungua bar na sehemu mbalimbali za starehe? Sheria inasemaje kuhusu uzembe na uzurulaji?
Mimi sioni kama mh. Rais ametunga sheria mpya ya kwake bali anasimamia sheria ambazo zilikosa usimamizi ambazo leo ni matokeo yaliyozalisha makundi ya vibaka mitaani.

Hapa Tanzania haiingii akilini kwa mtu anayejua hasa kutumia zile dutu nyeupe zilizo katika fuvu la kichwa ukimwambia hakuna kitu chochote cha kufanya kukuingizia kipato. Huko ni kukosa ubunifu na kuyaacha mambo yaende kwa kudra za Mwenyezi Mungu. Katika nchi iliyo na ardhi zaidi ya 70% haijakaliwa na watu wala haimilikiwi na mtu. Ardhi ni mtaji wa kwanza kwa sababu juu ya ardhi ndipo kila kitu kinafanyika.

Kila Mtanzania aliye na akili timamu kutoka moyoni mwake ukiacha anachokisema mdomoni ili kuwahadaa, anajua kuwa sasa hivi vijana wengi wamekuwa wavivu hawataki kazi ngumu, wamekuwa ni watu wanaotaka kuvuna wasipopanda. Kiasilia hilo jambo halipo wala haliwezekani, hata Simba porini anapambana kupata mawindo.

Rai yangu kwa Watanzania wenzangu, acheni kupotosha maana halisi ya maneno ya Mh. Rais ambaye ameonesha uthubutu wa kukemea maovu yaliyokuwa yameshamiri hapa nchini. Ili Tanzania isonge mbele hata tufikie katika huo uchumi wa kati, haina budi kila Mtanzania kutimiza wajibu wake kwa moyo wa uzalendo, na si kukosoa kila jambo ilimradi kila mtu aonekane anajua kuliko mwenzie.
Wanasiasa wa vyama vya upinzani acheni kuwa na roho zilizojawa na hamu na maombi ya kuiombea serikali ishindwe mpate mashiko katika uchaguzi ujao. Hivyo mtakuwa na malengo ya kushika dola tu na si kutaka Tanzania iendelee. Kwani Nchi inaweza endelezwa na yeyote na chama chochote.

Nahitimisha kwa kusema nchi ilipofikia haitaji tena siasa wala kubembelezana, sasa twende kwa mwendo wowote ikibidi hata kukimbia ilimradi tufike.
Big up. Nipashe online wamekuwa wamekuwa wa kwanza kupotosha. Sijui ndio sera ya Ipp Media kama sio Mhariri Kwayu na wenzie wawe makini.
 
Big up. Nipashe online wamekuwa wamekuwa wa kwanza kupotosha. Sijui ndio sera ya Ipp Media kama sio Mhariri Kwayu na wenzie wawe makini.
Umakini wa Waandishi wa Habari umeanza kupotea.
 
Wewe unajuaje kama silimi? Kilimo kinalipa inategemea wewe unafanya kilimo cha nini na unakiendesha je. Hivi unafahamu kama kuna ardhi hapa Tanzania haijawahi kulimwa na haiitaji mbolea za viwandani?
Toa mifano hai na sahihi kuandika tu hakuna Tija. Hao wanaocheza pooltable wako mijini wanawezaje kufikia hayo maeneo tajwa ambayo hayajawai kulimwa, kama hayajawai kulimwa miundo mbinu yake ikoje mara baada uya kuvuna isije ikawa usafirishaji inzazidi gharama za mauzo (maeneo mengi yako ya aina hivyo). Hapo sijazungumzia gharama za uendeshaji kama pembejeo, madawa na nyenzo
 
Sasa hayo maendeleo mnayoyataka yatakuja kwa watu kucheza pool table na betting huku ardhi ikiendelea kustawisha majani?[/QUOTE
Nionueshe mkulima alitetajirika kwa kilimo cha mkono bila mtaji Wa ziada. Tunao ndugu zetu wakulima vijijini hali zao zinatisha. Kilamala wanatusumbua tulioko mjini kwa kuomba misaada wakidhani huku kuna nafuu. Sasa nikijana gani ajitose porini bila kitu eti akalime. Tumieni busara, acha siasa za majikwaani, haiwezekani
 
Habari wana JF
Jana Rais Magufuli aliwahutubia kwa muda mfupi wakuu wa mikoa baada ya kuwaapisha. Rais aliongea mambo machache lakini yaliyobeba maana kubwa kuhusu uwajibikaji na watu kufanya kazi hasa akitia msisitizo kuwa tumeshachelewakwa kuwa haya yalitakiwa kuanza miaka kumi iliyopita.
Ni ukweli uliyodhahiri kuwa tumechelewa tena sana kutokana na nchi yetu iliyojaliwa kuwa na raslimali nyingi pamoja na ardhi kubwa yenye rutuba.
Jambo la kushangaza watu wameibuka na kauli mbalimbali wakiwemo wanasiasa, ambazo zimebadili maana halisi iliyokuwa kwenye baadhi ya maneno ya Mh. Rais.

Mh. Rais aliwaambia ma-RC "kuna watendaji wengine kazi yao ni kuwanyanyasa wananchi nendeni mkawashughulikie. Nyinyi mna mamlaka ya kumweka mtu ndani masaa 48, wawekeni ndani ili wawaheshimu wananchi". Lakini kauli hii imepindishwa na watu, hata wengine wakisema wakuu wa mikoa wameagizwa waende kuwakamata vijana wasiokuwa na kazi!
Hivi kweli hawa wakuu wa mikoa ni watu wasiojitambua ambao wanaweza kuitumia sheria inayowapa mamlaka hayo kuwaonea watu wasiokuwa na hatia?

Jambo jingine ambalo linapotoshwa ni kauli ya Rais kuzuia watu kucheza pool table asubuhi na kuwataka vijana kufanya kazi badala ya kuzurura pale alipokazia kuwa ikiwezekana walazimishwe kufanya kazi kwenye kambi maalum.
Watanzania wenzangu hivi ni kutokufuatilia sheria au ni upotoshaji wa makusudi? Niwaulize wanasheria akina Tundu Lissu, sheria inasemaje kuhusu muda wa kufungua bar na sehemu mbalimbali za starehe? Sheria inasemaje kuhusu uzembe na uzurulaji?
Mimi sioni kama mh. Rais ametunga sheria mpya ya kwake bali anasimamia sheria ambazo zilikosa usimamizi ambazo leo ni matokeo yaliyozalisha makundi ya vibaka mitaani.
Kwakweli mimi nimeishia kusoma hapo nilipo-quote,ila ngoja niulize wewe mtu asiye na kazi yoyote unataka afanye kazi gani ambayo haihitaji mtaji wa fedha.
 
Toa mifano hai na sahihi kuandika tu hakuna Tija. Hao wanaocheza pooltable wako mijini wanawezaje kufikia hayo maeneo tajwa ambayo hayajawai kulimwa, kama hayajawai kulimwa miundo mbinu yake ikoje mara baada uya kuvuna isije ikawa usafirishaji inzazidi gharama za mauzo (maeneo mengi yako ya aina hivyo). Hapo sijazungumzia gharama za uendeshaji kama pembejeo, madawa na nyenzo
Mkuu hivi kweli kuna mtu atakuja tu kukupa mtaji huu hapa kalime? Sidhani hata kama ni serikali inaweza kutoa pesa kwa mtindo huo.
Hivi kweli kama mtu una malengo ya kuwa mtu fulani maishani mwako ushindwa kutafuta pesa hata kwa kuanza na shughuli ndogo, ukasave hadi milioni moja ukaenda kwa mjomba, shangazi au jamaa yako yeyote kijijini ambako ambako unaweza kupata ardhi ya bei nafuu ukanunua na kuanza shughuli yoyote ya kilimo?
Au hapo ulipo ukaona kuna fursa gani ambayo unaweza kuitumia?
 
Kwakweli mimi nimeishia kusoma hapo nilipo-quote,ila ngoja niulize wewe mtu asiye na kazi yoyote unataka afanye kazi gani ambayo haihitaji mtaji wa fedha.
Mtaji unaweza kuupata kwa kuanza na kazi za kutumia nguvu kama utakuwa umekosa namna yoyote ya kupata kianzio.
Lakini zipo njia nyingi za kupata mtaji kama mtu utaamua kushughulisha akili yako.
 
Sasa nimeamini kuwa sisi wananchi wa Tanzania ni wavivu wa kufikiri na wavivu wa miili yetu,

Baadhi ya watu wameponda maagizo ya rais na wanaponda juhudi za rais katika utendaji wake wa kazi, wakiwepo wanasisa, mfano kuna mtu eti anaenda kucheza pool table eti anasubiri viwanda vifufuliwe aajiriwe huu ni ujuha usio na kifani.

Wengi wanaolalamika wanaishi mijini kwa misheni town huku wakiwa wameacha hekari na hekari vijijini kwao wakisubiri bibi na babu zao walime wao wakale mazao tu.

Kama kwetu kutakuwa na malalamiko maana vijana wanaenda kipindi cha mavuno tu so wazee wanaolalamika sana.

Rudini vijijini mkalime na bibi zenu mpate hela, mfano mimi nalima alizeti na mahindi kwa na mwaka huu natarajia kupata gunia zaidi ya 50.

TAFAKARI hakuna serikali inayoweza kuajiri wananchi wake wote. Na pia Nafanya ufugaji wa kuku wa mayai
Hivi watu wanalima bila pesa,je hiyo miundombinu ya kilimo ipo wapi,kuna maji au mvua za uhakika na unavyopiga kelele na kilimo je masoko yameandaliwa.Unakumbuka msimu wa mavuno ulioishia mwaka jana,gunia la mahindi kule Rukwa lilikuwa likiuzwa elfu kumi na nane.Huyo mtu anatumia gharama kiasi gani na return yake ni kiasi gani.Acheni kuongea kama PM alivoshusha bei ya sukari bhana.
 
Ukosefu wa ajira zipi na za aina gani ndio tatizo. Vijana wengi wanaokimbilia mijini ni wale waliomaliza elimu ya msingi na wanaona kilimo ni kazi ngumu hawaiwezi wanawaachia baba na mama zao waifanye kazi hiyo. Kundi jingine ni vijana waliomaliza elimu ya sekondari na vyuo. Hawa nao wanadhani white colar jobs ndio size yao! Kwa hiyo tunajikuta taifa lina vijana wengi wenye nguvu wanaoweza kufanya kazi za kilimo na UJASIRIAMALI wenye tija lakini hawataki kufanya kazi hizo. Kilimo na UJASIRIAMALI kumeweza kuwanufaisha ama kwa kiswahili kipya KUWATOA vijana walioonyesha nia ya kujiajiri. Rais amewatuma kazi ma RC ya kuwamobilise vijana wasio na kazi na wale wanaochagua kazi wapatiwe kazi sio wacheze pool na kuzururua tu! Sioni njia nyingine yoyote inayoweza kuleta ajira kwenye mazingira tuliyonayo.

..kwenye nchi zilizoendelea maduka ya pombe, mabaa, na kumbi za starehe, huendeshwa kwa sharia maalum za wakati wa kufungua na kufunga biashara.

..labda nikuulize: kwanini hakuna blue collar jobs ambazo zinavutia vijana wanaozurura? Au kwanini hakuna white collar jobs za kutosha kuajiri vijana wanaomaliza form 4 , 6, na vyuo vikuu?

..hawa vijana mnawaona ni mzigo lakini kuna nchi Kama Japan wanatamani wangekuwa na vijana wengi wenye nguvu kwasababu sehemu kubwa ya population Yao wanazeeka.

..Hivi tunataka tuwe taifa lililoendelea Hulu sehemu kubwa ya population yetu ni wakulima, tena wa jembe la mkono?
 
Ile Sheria ya uzembe na uzururaji huenda ikapata nguvu tena. walifungwa wengi kwa sheria hiyo wakati wa awamu ya kwanza pale Sokoine alipoanzisha sera ya Nguvu kazi

Kama huna ajira wewe ni mzururaji na mzembe. kwa wakati huo angalau ardhi ilikuwa mali ya umma unaweza kufyeka pori ukaanzisha shamba ingawa mavuno utajua mwenyewe pa kuuzia hakukuwa na soko huria kama ilivyo leo mazao yananunuliwa hata yakiwa shambani hayajakomaa


Lakini dunia ya leo siasa zimebadilika ardhi karibu yote inawenyewe. jaribu kufyeka pori uone cha moto aidha ni hifadhi ya serikali ama ina mmiliki tena ana hati ya umiliki wa ardhi.
sasa vijana waende wapi au ile Tamzania ya viwanda haiwezekani..? mahali vijana waliweka matumaini ya mkombozi wa tatizo la ajira amepatikana kwa kuanzisha viwanda vya aina ya Dangote nchi mzima

kama ndoto hiyo imekufa sasa serikali ya Magufuli ipanuwe magereza kwa vile itawafunga vijana wengi kwa kutokuwa na ajira rasmi
 
Mtaji unaweza kuupata kwa kuanza na kazi za kutumia nguvu kama utakuwa umekosa namna yoyote ya kupata kianzio.
Lakini zipo njia nyingi za kupata mtaji kama mtu utaamua kushughulisha akili yako.
Yaani unachekesha sana.Kwani hao vijana wamekuambia wanashida na chakula kwao au unamaana gani kwa kusema.Mtu akalime jembe la mkono,hilo shamba anapewa na nani,vifaa na pembejeo zitatoka wapi.

Hizo shughuli nyingine anazoweza kutumia nguvu ni zipi.Nitajie tano tu ambazo anaweza kufanya na akapata mtaji wa kilimo.
 
Kabla ya kuanza kuwakamata wacheza pool table kwanza akamate wote waliosaini mikataba mibovu kwa nchi yetu,amkamate Jecha aliyevuruga uchaguzi kule Zanzibar,na wale waliotorosha pesa nchi za nje.
 
Pool table ni aina gani wa mchezo na unapatikana hasa wapi? Tuanzie kwanza hapo.
Hapa mtaani kwangu vijana wabacheza ukumbi wa ccm
Jirani kwenye bar kabla haijafunguliwa na baada ya kufunguliwa
Lakini rudi kwenye hoja Ni ipi sheria inayopanga muda wa kucheza pool
 
Yaani unachekesha sana.Kwani hao vijana wamekuambia wanashida na chakula kwao au unamaana gani kwa kusema.Mtu akalime jembe la mkono,hilo shamba anapewa na nani,vifaa na pembejeo zitatoka wapi.

Hizo shughuli nyingine anazoweza kutumia nguvu ni zipi.Nitajie tano tu ambazo anaweza kufanya na akapata mtaji wa kilimo.
1: Kuwachotea maji watu waliombali na huduma ya maji
2:Kubeba mizigo sehemu ya stand na maduka
3:Kuwa kibarua mashambani
4:Kusafisha na kupanga vifaa kwenye maduka
5:Kuhudumia mifugo
 
Vijana wavivu wavivu wale wasiopenda kazi, asubuhi asubuhi wanacheza Pool table kamata wote peleka mashambani. Wale wanaoshinda kwenye vibanda umiza asubuhi mpaka jioni wakiangalia filamu za kihindi kamata wote peleka mashambani. Wale wavuta bangi na vibaka wanaoshinda vijiweni kamata wote peleka mashambani. Ni amri sio ombi...hapa kazi tu!

Kiboko cha mkoloni kirudi sio :-D
 
Hapa mtaani kwangu vijana wabacheza ukumbi wa ccm
Jirani kwenye bar kabla haijafunguliwa na baada ya kufunguliwa
Lakini rudi kwenye hoja Ni ipi sheria inayopanga muda wa kucheza pool
Ni sheria ya uzembe na uzurulaji. Kwani kucheza pool table asubuhi kijana siyo uzembe?
 
Back
Top Bottom