Watoto wetu wanakula nini mashuleni?

Watoto wetu wanakula nini mashuleni?

Oohooo, kaangalieni msikute school bus driver keshafanya yake, oohooo.

Miaka 2 shule ? Si atachoka sana.

Okay kila mtu ana maamuzi na makuzi ya mwanaye, hakuna nyongeza wala punguza
Jamani acheni tu hamjui situation yetu
 
Yaani miaka 2 yuko shule?!!!.
Subiri afike 5 kama anakuboa akiwa home,tafuta housegal ili asiwe anakusumbua ukiwa unachati,kuliko kumpeleka shule umri huo
Huwa nachati na Nani sasa.yaani mngejua nilivo busy acheni tu
 
watu saiz wamechoka kulea.. nilikaona katoto kana miaka miwili kapo shule yaan ata upendo wa mamaake hajaufaidi.. wanawatesa sana.. shule hawatoweza kuwapikia watoto wengi chakula cha afya ni makande tuuu
Kwani nashinda nyumbani?
 
Mm naonekana mtata kwa mwnzng na hta mama mkwe...mfano,I told them,why are we not abiding to the exclusive breastfeeding(ebf) tunayoambiwa na wataalam wa RCH tuendako...nn Sasa umuhimu wa mm kwenda nawe clinic loooh majibu yanakuwa hapana Mana mtoto hashibi sjui Bibi yake kasema...tushazoea haya...katoto kana miez 2 miuji kibao ananyweshwa,mimaji eti ana kiu...kitumbo ndiii yaani
Nawewe ukakubali miezi miwili apewe miuji na mimaji?
 
Nawewe ukakubali miezi miwili apewe miuji na mimaji?

Banaa eee niliandamana kwa maneno wee jitu halisikii....sista duu wangu kauweka U Class pembeni na kuufuata ushauri wa mamiye....

Nimegoma siendi naye tena hyo RCH clinic 😂😂
 
Wazazi wa siku hizi wanakimbia Majukumu ya kulea kwa madai kwamba wanasomesha.
Mtoto wa 2yrs anatakiwa akae Nyumbani acheze,ale,alale,aangalie katuni.Hu

Huko shuleni Kama wako wa 2yrs 20 huyo mwalimu atawapa Matunzo vipi?
 
Mungu ni mwema shule zimefunguliwa japo wengine tulikuwa tushakula ada ,ila sio mbaya tutadanga hivo hivo watoto wasome.

Mwenzenu Nina changamoto kababy ketu kalianza shule mwaka huu kabla ya lockdown ile Jan.nikalipa ada vizuri tu .ila hakusoma sana hata mwezi akaanza kuzingua mara anaumwa .mara anachelewa kuamka ,mara mvua etc anyway wenyewe tukaona kwa vile ni mdogo just 2yrs tusiforce akaacha tu ndo kukutana na lockdown ya shule Hadi alivoanza tena shule just imagine tumelipishwa tena ada nziiima sina hamu.

Kinachoniuma toka dogo aanze shule juzi anajamba balaa.japo ni kadogo siwezi kusema anachoniambia ni kweli au lah ila nikimuuliza shule ulikula nini anasema ugali maharage na maziwa, jana makande Ugali maharage yaani kila siku maharage.

Mtoto anajambaaa Dar nzima yaani hadi tunakionea kitoto chetu huruma nataka niandamane kwa Ndalichako maana hela nalipa sasa nauliza nifanyeje wakuu na hii shule.
Unamtaka mkamjambie waziri wa elimu ?
 
Wazazi wa siku hizi wanakimbia Majukumu ya kulea kwa madai kwamba wanasomesha.
Mtoto wa 2yrs anatakiwa akae Nyumbani acheze,ale,alale,aangalie katuni.Hu

Huko shuleni Kama wako wa 2yrs 20 huyo mwalimu atawapa Matunzo vipi?
Sasa nifanyeje wakuu??
 
Facts.Mimi nligombana na huyu mwnzngu KUHUSU huohuo uzungu....aaagh yaan we acha tu...mwanamke utafkr anaishi Philladelphia...
Hahahhaaa nacheka na comments zako mkuu! Hahhaaa demu ametoka Jimbo la Philadelphia🤣🤣🤣🤣!
Ila watoto wa nyakati hiz wako bright Sana kumwacha had 5yrs ni kumdumaza tu!
 
Wazazi mna viherehere tu,mtoto miaka mitano hata utoto hajamaliza unampeleka shule,akagundue Nini?
Tafiti zinasema mtoto anaanza kuelewa akiwa na miaka sita,sasa nyie na uzungu wenu mnawapeleka na miaka mitatu mpaka mitano.
Lishe ya mtoto unatakiwa uiandae wewe mama sasa unawapa kazi hiyo waalimu?
Miaka mitano bado anakwenda kliniki Kama sikosei,kwa hiyo mtoto wa kliniki unampeleka shule?
Ndo ushangae kitoto kina miaka 2 kinapelekwa na kushindia shule kinalishwa vyakula visivyoeleweka
 
Hahahhaaa nacheka na comments zako mkuu! Hahhaaa demu ametoka Jimbo la Philadelphia🤣🤣🤣🤣!
Ila watoto wa nyakati hiz wako bright Sana kumwacha had 5yrs ni kumdumaza tu!
Naam mkuu wangu kwi kwi kwi kwi,unachosema kina ukweli,ila huyu miss mtafutaji inaonekana katoto alikanyonyesha ile miezi 6 ya mwanzo atareeee😂😂
 
Lea mtoto wako acha kukwepa majukumu kisa utumwa wa pesa.
Malezi sio kukaa tu na mwanao 24/7 jombaa...atakula Nini...ni kutenga muda na mwanao zaidi..lakini bila kutafuta pesa ndo unakuta mitoto ikisikia kwa jirani nyama innukia inahamia huko!..hapana aisee
 
Malezi sio kukaa tu na mwanao 24/7 jombaa...atakula Nini...ni kutenga muda na mwanao zaidi..lakini bila kutafuta pesa ndo unakuta mitoto ikisikia kwa jirani nyama innukia inahamia huko!..hapana aisee
Kuna mahali nimesema ukae na mtoto 24/7?
 
Back
Top Bottom