Watoto wa vigogo na ajira BoT

Samahani, naona watu walikuwa wanauliza majina. Uzuri ni kuwa majina yalishawekwa hapa siku nyingi... tatizo vyombo vyetu vya habari vingekuwa vinakuja hapa wasingeripoti hili wiki kadhaa baadaye. Hatuhitaji watuambie majina, tunawajua.

mwanakijiji you are one tricky guy ! last post kwenye hii thread ilikuwa 25th-Feb, leo umekuja kujibu. but also you didnt have tosay what you said...LAKINI NAELEWA WHY YOU DID THAT !!
 
Nadhani Kilatu alistaafu kazi miaka ya 1990. Aliendelea kwa mkataba kama Mkurugenzi wa NPS (National Payment Systems) wakati wa Balali.
Isangya alikuwa Mkurugenzi wa fedha wakati wa Balali baada ya Mama mmoja aliyekuwa na nafasi hiyo kutolewa kwa sababu asingekuwa yes, yes.
Kimela alikuwa kwenye legal dept. ya Bank.
Komu nadhani alikuwa foreign markets (sina hakika)
Watu wa Bot watueleze vizuri.
 
Mbona sijaona jina la Liumba hapa? Mimi nilijua yeye ni Director wa Finance and Administration
 
Mbona sijaona jina la Liumba hapa? Mimi nilijua yeye ni Director wa Finance and Administration

Liumba alikuwa DPA - Director of Personnel and Administration.
Huyu jamaa hakuwa na influence sana kwenye maswala ya fedha na banking. Yeye alikuwa ni mtu wa sera na maaumuzi hasa kwenye maswala ya safari, mafunzo, warsha, mikutano, n.k.
Na inasemekana alikuwa karibu sana na Gov.
 
Kwa Tabia ya watanzania ilivyo hawa jamaa waliosimamishwa kazi watarudi tu maana haki na sheria ni tofauti sana (sheria inataka asimame na haki itamtaka arudi kazini) kama watu hawa wamesimamishwa kwa kesi ya EPA au ya RICHMOND wafukuzwe kama ni kesi tofauti na hiyo basi waendelee kusimama, vinginevyo tutumie hoja ya mhesh.Ndesambulo ambae anasema watu kama hawa China wananyongwa maana china hawataki michezo ya ajabuajabu kama hii ya ufisadiufisadi.

jamani hawa jamaa ni vidagaa tuu tusidanganyike ile tuondoke kwenye focus, TUNATAKA MAJINA YA WALIORUDISHA.... MAJINA YA VIGOGO naongelea hapa... I say stop playing games now kikwete
 
Yakowapi majina ya akina PAMELA LOWASSA ambao mmetudanganya mnapoza soo.. a.k.a mnachunguza uhalali wao wa kuajiriwa?????
Mbulu mbona hufungui mdomo kutueleza kuhusu Mgonja hata baada ya malalamiko yote haya ya kuhusishwa na harufu?? ndicho ulichoambiwa ukifanye ulipokwenda kule butiama?????
 
jamani hawa jamaa ni vidagaa tuu tusidanganyike ile tuondoke kwenye focus, TUNATAKA MAJINA YA WALIORUDISHA.... MAJINA YA VIGOGO naongelea hapa... I say stop playing games now kikwete

Huyu Ndullu wakati ufisadi unafanywa yeye alikuwa kama naibu gavana hivyo alistahili na yeye kuwajibishwa. Utakuwaje naibu gavana wa BoT usijue kuna wizi wa bilioni 288 unaendelea ndani ya taasisi yako? Kama hukuhusika na wizi huo basi wewe ni incompetent hustahili wadhifa wowote mkubwa!
 
Huyu Ndullu wakati ufisadi unafanywa yeye alikuwa kama naibu gavana hivyo alistahili na yeye kuwajibishwa. Utakuwaje naibu gavana wa BoT usijue kuna wizi wa bilioni 288 unaendelea ndani ya taasisi yako? Kama hukuhusika na wizi huo basi wewe ni incompetent hustahili wadhifa wowote mkubwa!

Akkk Sante mkuu!
 
Huyu Ndullu wakati ufisadi unafanywa yeye alikuwa kama naibu gavana hivyo alistahili na yeye kuwajibishwa. Utakuwaje naibu gavana wa BoT usijue kuna wizi wa bilioni 288 unaendelea ndani ya taasisi yako? Kama hukuhusika na wizi huo basi wewe ni incompetent hustahili wadhifa wowote mkubwa!

Prof Benno Ndullu hakuwepo wakati madudu ya Richmond yanafanyika,ameteuliwa last year tena baada ya bajeti ya 2007-08 sasa huo ushirika wake wa kifisadi umeanzia wapi? BUBU plse sasa ongea maana leo nimegundua kuwa wewe umetawaliwa na hamu ya kuongea hata kama huna taarifa za kutosha,any way tujisahihishe sisi kwa sisi kama anavyojitahidi Ndullu kwa sasa.
 
UCHUNGUZI uliofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuhusu ajira za upendeleo kwa watoto, ndugu na jamaa za wakubwa ndani ya Benki Kuu (BoT), umekamilika.

Kukamilika kwa uchunguzi huo kulitangazwa mbele ya waandishi wa habari jana na Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu.

Ingawa hakuwa tayari kusema kile kilichomo ndani ya taarifa hiyo kwa maelezo kuwa TAKUKURU ni taasisi inayojitegemea, Gavana Ndulu alisema, tayari BoT imeshaanzisha uchunguzi wake mwingine kufuatilia suala hilo hilo la ajira.

Gavana Ndulu alisema kuwa katika uchunguzi wake, TAKUKURU ilikuwa ikichunguza ajira za watu 14 wanaohusishwa na viongozi waandamizi kulingana na maelezo waliyopewa na ngazi husika.

Alisema baada ya kupata taarifa hiyo ya TAKUKURU, BoT nayo ikaamua kuanzisha uchunguzi wa ajira za wafanyakazi wake wote, ili kuepusha malalamiko kutoka upande fulani pamoja na kuepuka kupelekwa mahakamani.

"Wale TAKUKURU walifanya uchunguzi wa ajira za watoto wa vigogo kulingana na maelezo waliyopewa, lakini sisi tunataka kufanya uchunguzi wa ajira za wafanyakzi wote," alisema Ndulu.

Alisema kuwa ndani ya BoT kila mfanyakazi ni sawa, awe mtoto wa kigogo au wa mkulima, ndiyo maana wameamua kuwashirikisha wafanyakazi wote kwenye uchunguzi huo.

"Unajua leo hii ukifanya uchunguzi wa ajira za watoto wa vigogo pekee, kesho unaweza kujikuta hata hao watoto wa wakulima nao walipata ajira kwa njia zisizokubalika," alisema Ndulu.

Aidha, alisema uchunguzi wao utakuwa tofauti zaidi, kwani wao watafuata sheria ya mwaka 2004 (iliyobadilika), wakati TAKUKURU walitumia sheria ya mwaka 2000.

Ndulu hakuwa tayari kufafanua utofauti wa sheria hizo, lakini alidai kuwa katika uchunguzi huo, TAKUKURU haikutumia sheria iliyotumika kuwaajiri watoto hao.

"Hapa kunaweza kutokea tofauti ya kutokuelewana na jamii ikachukulia vibaya mambo haya, kwani sheria zilizotumika kufanya uchunguzi zilishabadilishwa, sasa sijui itakuwaje," alisema Ndullu.

Aidha, alisema ni vizuri jamii ikavuta subira ya kupata matokeo ya uchunguzi wa BoT kuhusiana na ajira za wafanyakzi wake na asingependa kutoa matarajio ya kazi hiyo mapema.

"Jamani nisingependa kuwaahidi nyinyi au wananchi wengine hivi sasa matarajio ya uchunguzi wetu, bali ninawaomba tungoje hayo matokeo," alisema.

Hivi karibuni, vyombo mbalimbali vya habari vilitoa taarifa na kutaja majina ya watoto wa vigogo ambao wanafanya kazi BoT, wakisadikiwa kuwa walipata kazi hizo kutokana na ushawishi au nafasi za ndugu zao.

Taarifa hizo pia zilinukuu viongozi wa TAKUKURU wakidai wanachunguza ajira za watoto hao wa vigogo kuona kama walipata ajira BoT bila kufuata taratibu zilizotakiwa.

Juhudi za Tanzania Daima kumtafuta Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Edward Hosea, kuthibitisha kukamilika kwa uchunguzi wa ajira za watoto wa vigogo hao ziligonga mwamba baada ya simu yake kutokuwa na majibu.

Taarifa kwamba kulikuwa na ajira za upendeleo ndani ya BoT kwa mara ya kwanza zilisambazwa katika mtandao wa intaneti kabla vyombo kadhaa vya hapa nchini kuripoti taarifa hizo.


CHANZO:
Tanzania Daima
 
Jamani tukumbushane majina ya watoto wa vigogo hapo kwenye hekaru la pesa BoT...
 
tanzani ni nchi ya maajabu! kila leo kunafanywa chunguzi za kila aina, lakini matokeo ya chunguzi hizo yanawekwa kapuni! then whats the point of having uchunguzi ina the first place?
 
Lini mtajifunza kuandika habari iliyokamilika, majina ya watu 14 ndio nini? Kama huna majina hayo basi huna habari.

Msilazimishe biashara ya magazeti!
 
[watu wnazungumza kuwa eti wana sifa? sawa, lakini je taratibu zilifuatwa? je walipambanishwa na wenye sifa wengine kwa njia ya usaili? kwa kuwa kuwa na sifa ni kitu kingine na kushinda usaili ni kitu kingine, na kwa nini watoto wa akina mwinyi, mkapa, mramba etc peke yao ndo wana sifa? hivyo vyuo wamesoma peke yao?

la msingi.

10 wale wote walioajiriwa bila kufanyiwa usaili wasimamishwe mara moja, iitwe kampuni kama price water house au yenye kuheshimika, nafasi zao zitangazwe upya, wafanyiwe usaili na kama kwa kushindanishwa na wengine wtashinda, MIYE SANA NOMA

2 WALE wengine ambao itabainika kuwa wameajiriwa kwa vimemo, na kuwa hawnan sifa, wafukuzwe na kuchuliwa hatua. waLE wote waliohusika katika kufanikisha mpango huu haramu wa ajira za upendeleo, wakiwemo maafisa utumishi, nk, yaani watimuliwe bila haya na hatua kali dhidi yao.SIJAONA MAHALI GANI KATIKA HILI KUNAHITAJI UCHUNGUZI, KAMA NI MAFAILI YA INTERVIEW YAPO HAPO OFISINI, KAMA NI CV ZIPO, UCHUNGUZI WA NINI?
 
Jamani tukumbushane majina ya watoto wa vigogo hapo kwenye hekaru la pesa BoT...

Mbona hili watoto wa vigogo BOT liilishaletwa hapa jamvini likachambuliwa sana wakati suala wizi wa pesa BOT lilipofumuka kama unavyoona ishu ya balali kuvuta kamba ilivyo zungumzwa hapa kwa wiki kadhaa sasa na kuacha maswali mengi hayana majibu sahihi.Labda wairudishe tujiridhishe tena.
 
Back
Top Bottom