Watoto wa kariakoo mpo jf?

Karega nasikia ana Ualaza wa Nguvu... lol
Mitaa hiyo alikuwepo Kichaa George na Rabiya yule Mama wa Kihindi Mento..!
Mitaa hiyo karibu na Home kwa Mw. Ndossi... Krokodire Ushuzi wa Mung..




Nangatai Ulishakula wewe? inaelekea na wewe ulikuwa unapenda sana Sun Vita...
GEORGE alikuwa ni msomi baadaye aka fyatuka kutwa hutembea na magazeti.Rabiya ulikuwa ukimuuzi ukutemea mate au anakuvulia nguo lazima utoke mbio
 
GEORGE alikuwa ni msomi baadaye aka fyatuka kutwa hutembea na magazeti.Rabiya ulikuwa ukimuuzi ukutemea mate au anakuvulia nguo lazima utoke mbio
Mimate ilikuwa inanuka haswa... Huyo George Mdingi wangu alisema walishasoma nae School Moja.. Na Alikuwa akimuona Anampa Pesa na George alikuwa anawajua aliosoma nao kwa majina na Sura wacha kabisa na ndio aliokuwa anaongea anao hao dah! kuna kipindi cha miaka ya 2000 hadi 2005 hivi kama niulikuwa namuona mita ya Mawenzi Hotel akivizia marafiki zake awapige vizinga kuna mmoja yupo pale jengo la Nedco

Huyu Goerge sijui kama bado yu hai lol Nasikia walikuwa wanasafiri kwenye gari enzi zake anasoma gari likapinduka wakafa wote yeye akabaki na kuupata ukichaa wake...

Vichaa wa Upanga kuna mmoja fresh tulikuwa tunamuita Domo chenza au Chenger alikuwa anaokota makopo ukimuita Domo chenger anakukimbiza akupige... kwa watengeneza koroboi kuna Siku nilienda pale Salender Brigde maeneo ya polisi kupata viepe nikamuona jamaa wakaniambia yupo fresh na akili poa ana mke anasafisha maeneo yale hadi karibu na kituo kote anapiga usafi... Dunia hii hata Vichaa wanapona...

Unakumbuka Embe Chips!!
 
Mimate ilikuwa inanuka haswa... Huyo George Mdingi wangu alisema walishasoma nae School Moja.. Na Alikuwa akimuona Anampa Pesa na George alikuwa anawajua aliosoma nao kwa majina na Sura wacha kabisa na ndio aliokuwa anaongea anao hao dah! kuna kipindi cha miaka ya 2000 hadi 2005 hivi kama niulikuwa namuona mita ya Mawenzi Hotel akivizia marafiki zake awapige vizinga kuna mmoja yupo pale jengo la Nedco

Huyu Goerge sijui kama bado yu hai lol Nasikia walikuwa wanasafiri kwenye gari enzi zake anasoma gari likapinduka wakafa wote yeye akabaki na kuupata ukichaa wake...

Vichaa wa Upanga kuna mmoja fresh tulikuwa tunamuita Domo chenza au Chenger alikuwa anaokota makopo ukimuita Domo chenger anakukimbiza akupige... kwa watengeneza koroboi kuna Siku nilienda pale Salender Brigde maeneo ya polisi kupata viepe nikamuona jamaa wakaniambia yupo fresh na akili poa ana mke anasafisha maeneo yale hadi karibu na kituo kote anapiga usafi... Dunia hii hata Vichaa wanapona...

Unakumbuka Embe Chips!!

umenikumbusha Rabia anatoka mitaa ya Don Bosco anakuja jamatini,tunaita Rabia anafunua nguo,kuna siku alilambwa mabao alimtemea mate baba mmoja...
Huyo domo chenza si ndio domo Chawa muokota makopo? Nilikua namuogopa balaa
halafu kulikua na babu mapisto mzee mmoja anavaa makorokoro mengi,shingoni na mikononi.
Huyo George ni yule alikua na manywele mengi?
 
Embe Chips...lol
tulikua tunaita Chips keri,
mi nimekumbuka makomamanga,kama ukiwa mtoto mzuri utaishia kuyaona tu...
Tulikua tunaiba kwenye nyumba za wahindi,pia kwa kina Mama Terry Gbmemundu karibu na ubalozi wa Syria ulikuepo mkomamanga tukienda tu ni uharibifu.
Loh,nilikua mtoto mbaya kwa makomamanga ya watu jamani.
 
Leo nataka tukumbushane mji wetu mkongwe,mji maarufu wenye historia kubwa ndani ya nchi hii lakini inayoelekea kupotea.Mko wapi watoto wa kariakoo wa ukweli mtueleze tuijue kariakoo iko vipi,ilikua vipi,raha na karaha za mitaa ya kariakoo,na je kariakoo ya zamani na ya sasa zinalingana?karibu sana maskani mnaoijua kariakoo kiundani mtujuze sie wakuja maana ndo kwanza tunaishi kwenye maghorofa mapya baada ya wenye mji kuukimbia mji wao,maana tumekuwa tukiyasikia mengi kuhusu mitaa hii ilivyokua zamani.

Wewe kakwambia nani tumekimbia mji wetu, mie baba yangu ameniachia nyumba tisa na bado zipo na SIONDOKI NG'O ! hao walokimbia ndio wakuja, mzawa wa KAriakoo Kindakindaki hawezi kuukimbia mji wake !

KAriakoo ilikuwa raha sana enzi zile, kila siku ukiamka asubuhi unakutana na nyuso zle zile mitaani lakini sasa hivi Looooh! kila siku sura mpya mara zinatoka mara huko! nyingine sijui wapi kaaha tupu, basi ukienda mitaa ya Mkunguni na Jangwani wamejaa kina Mgosi na vitunguu vyao wakati huo tulikuwa tukichezacheza bila taabu, pale Msimbazi na Jangwani Wachaga kibao na mapodozi eeeh! huko ndio kabisa ! karaha mpaka basi ! ili muradi Kariakoo imevamiwa ...
 
Ah..kwetu hiyo.. Mitaa ya MkunguniSwahili,,Mafia,Masasi,Narung,ombe,Tandamti,Pemba,Kongo,Twiga,Nyamwezi,Aggrey,etc...

Misikiti,Kwa Mtoro,Idrissa,makanisa,KKKT Kariakoo..
Zahanati,kwa Dr Maro,yule wa kihindi Dr nani vile? Na pale Pan African kwa Dr Makene..Baadaye,Al Jumaa..pale Mafia na Sikukuu..

Siwezi sahau miilk shake,na ice cream za Bakhressa pale Livingstone.. Na mikate ilikuwa ya ukweli enzi hizo.. Mitamu ina ladha..

Mahoteli,Mico Hoteli,Hadhara Mount(Pemba na Msimbazi)...
Kulikuwa na askari mmoja alikuwa na mikogo miaka fulani pale Msimbazi Police.. Akiitwa Koplo Mukama Sharp!

Palikuwa na mama mmoja maarufu wa kihindi mama Songambele... Marehemu mzee Chaurembo alikuwa mjumbe wetu wa nyumba kumi.. Tulikuwa tunaenda duka la kaya kupimiwa sukari na unga...

Mambo mengi jamani..

Pale kwa Mzee PAzi mitaa ya Mkunguni ... yule Askari alikuwa anatokea mara yule Mkama Sharp , alikufa yule dah! enzi zile anawapanga foleni watu na wakimuona tu wanastuka na alikuwa akiogopwa sana yule!
 
haha Da Pretty wa zanaki unaweza kuwa sawa au si sawa wazee wengi wa kariakoo walipenda kuwasomesha watoto wao Shule ya Zanaki lakini kwa utundu wao hawakuweza kuendana na mazingira so wazazi wao waliwapeleka katika shule za mnazi mmoja lumumba na baadhi jamhuri..

Mie Sababu nimeishi Upanga na City Centre so nawafahamu kwa Sana... Tabia Za Watoto wa Karikakoo ni Wanakimbia Sana hata Sijui kwanini hakuna Wanariadha kutoka Kariakoo! Wanaongea Sana Tabia ya Udokozi ikiwemo kupapasa papasa macho hapa na pale kama kuku atafutaye chakula. Ukigombana nao cha kwanza wanakupiga mtama na walikuwa hawakosi wembe mfukoni. so unaweza kuchaniwa begi na ukifika home hakuna mkebe.

Pia Tabia zao hazikupishana na za watoto wa Magomeni na Ilala.. Watoto wa Kariakoo nilikuwa nawapenda kwene soccer tu japo walikuwa wanacheza sana rafu na mpira wanaujua

Yaani wewe ni muongo sana! mie nimekaa Kariakoo na nimesoma Zanaki na watoto wengi waliokuwa wakiishi Kariakoo, na tulikuwa tukitoka Zanaki pale Jela ya watoto tunakutana na watoto wanaotoka Mnazi Mmoja wanarudi majumbani mwao Upanga.
 
Huo Wimbo vipi mbona haujakaa kiupanga upanga? Michezo ya Watoto karibu mingi inafanana ,, Ukuti ukuti wa meme wa meme, Komborela, Tampo, Baba na Mama,Yai Bovu,Maji ya Ndimu,Ana ana ana Do, Gololi Sachi, Kidali Po, Tikbar Tik, Soccer, Karata n.k..

Hata mi wimbo wake sijaujua.
Huu haukuwa mchezo bali ni maneno yaliyosemwa na mzee mmoja aliyekuwa akikusanya mabati sehemu za katikati ya jiji. Alikuwa akiingia kwenye block anasema hayo maneno (Ilala..toto na lala). Watoto walikuwa wanamwogopa sana na kama kweli Duduwasha uliishi city center utotoni (miaka ya themanini) huwezi kumsahau huyo mzee.
 
Kariakoo ni miaka ya '70 na '80. I miss those years..

Sasa hivi imekua janga la kitaifa. Hata sehemu ya kupita kwa miguu imekuwa shida..!!!!
Shikamoo Babu.... wewe lazima utakuwa unaifahamu sana club ya Saigoni sikuhizi kabla haijapinduliwa na Iddi Simba...
 
Hadhara mount hotel pale pemba na msimbazi mdau umenikumbusha mbali kuna mtu alikua maarufu kwa kuvizia maaba(ukoko) pale jioni kwa bei poa sana anaitwa hamis mangara sijui yuko wapi yule mzee alikua anapenda sana yanga zamani akifanya kazi tanesco
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom