Watoto wa kariakoo mpo jf?

Watoto wa kariakoo mpo jf?

A. Ngdk sijasoma nae,
alikua anakaa mitaa gani?
Kamsopi kama wa Mangengesa Mdimi namfahamu hadi kesho,si walikua wanakaa sea view kwenye lile jengo lilikua refu kuliko yote miaka ile? Mule ndio tumejifunzia kupanda lift..
Pia watoto wa Upanga tulikua tunakutana sana Don Bosco na wengine mafundisho St. IMACULATE kwa Fr. Amadori.
Mi nilikaa mitaa hiyohiyo uliyoitaja ila umesahau Lugalo st. Kwa kina Ephraim Kibonde,Manase Zablon,Mtinangi.
Malik Rd kwa kina Telesphory Ndunguru,Undali kina Togani Ngota, Maria Goyayi, Ray Kasonga...
Alykhan kwa kina Koku yule alipata ajali akiwa na Kenedy Seusi akapoteza macho yote.. Unaikumbuka hiyo?
DUUH!!!!!! umenikumbusha mtu kibao-huyu kennedy yuko wapi siku hizi
 
Hata mi wimbo wake sijaujua.
Umesahau Upanga tumecheza sago pia(ule mchezo wa kurusha betri)
Ila we ulikua mtundu sana,unayajua hadi ya lumumba,mnazi mmoja,mkama sharp!
Pale jeshini mtaa wa Magore kulikua na mibuyu,basi tukitoka kanisani au mafundisho tulikua tunapita kuwaomba mabuyu yale ambayo hayajapasuliwa,wanajeshi wa miaka ile walikua wapole maana yakianguka tunawekewa,yasipoanguka wanatuambia..lol.
Sahivi mjeshi gani aokote ubuyu eti awawekee watoto watapita.
Dah! Wewe ni mkaree... unakumbukumbu Sana Wanajeshi sure Walikuwa Wapole kwa Watoto tu enzi zile fensi yao ilikuwa ni Senyenge tu sie tulikuwa Watundu acha hatuwaogopi hao wanajeshi tunawakera hadi basi wanatupatia au wanatuambia tuingie tuyaangue kabla mkuu wao hajafika tunachukua mabuyu na maembe pia Sielewi Upanga kwa nini ilikuwa na miti ta Miembe Mingi Sana hadi ndani mule Jeshini..

Magore kulikuwa na Duka la Kaya Pia na Mchine ya Kusaga Nafaka nyuma ya Duka la Kaya pia na Ndio Mtaa aliokuwa anakaa Bibi Titi.. Kipindi kile cha mGao wa kwanza wa Umeme Mtaa wa Magore ulikuwa haukatwi umeme lol
 
Kweli miembe ilikua mingi,
ile mashine tumeenda sana pale.
Bibi titi wajukuu zake walisoma UPS,nadhani na Duly Sykes pia alikaa kwa bibi Titi ila sina uhakika au kumbukumbu nzuri kwa hilo.
Jeshini pia kulikua na dispensary,nimechomwa sana sindano pale... Lol
then magore/maliki upande huu wa Diamond kulikua kiwanja kimezungushiwa fensi fupi tulikua tunaruka kwenda kuchuma mapera.
Aga khan wakati huo jengo moja tu tulikua tunaenda kuchuma maembe ng'ong'o hapo tulikua tunaenda na watoto wengine wanakaa mbali kama kinondoni,kariakoo ila wanasoma UPS.
 
Kennedy hayupo tena,
niliambiwa mdogo wake ila sikumbuki nini kilimuondoa.
Son of Alaska nawe upanga East?
West sikuwafahamu sana...
MIMI ni wa upanga west,primary nimepiga hapo UPS,mitaa ya upanga east nimeyumba sana.
 
mimi utoto nimekulia kariakoo..
Ujana nimekulia Upanga...
Ukubwa............Kijtonyama.......Kinondoni block41.......
 

....kulikuwa na mtemi mmoja anaitwa siga siga, nani anakumbuka jina hili?....halafu kuna mmoja (mlemavu) nishalisahau jina lake alikuwa anatabia ya kuandika graffiti ukutani ".....kapita hapa!" mitaa ya upanga hiyo...

...pale uwanja wa shule ya muhimbili, team ya Super Star ilikuwa inapiga zoezi kila jioni, kina Abdul na Ahmad Amasha hii ilikuwa team yao ya mtaani...

...huku karibu na klabu ya Yanga kulikuwa na mkaanga chipsi maarufu kwa jina MASALADI, ilikuwa kama transit point kwa wote wanaoelekea majumbani kuanzia saa nane usiku mpaka alfajr kwa waliotokea Gogo-Africana, Mbowe etc...enzi hizo Bagamoyo Rd vumbi tupu, ni road race na wale waarabu wenye coaster za Scaba Scuba na Sea Never Dry kuwahi chipsi moto!
 

....kulikuwa na mtemi mmoja anaitwa siga siga, nani anakumbuka jina hili?....halafu kuna mmoja (mlemavu) nishalisahau jina lake alikuwa anatabia ya kuandika graffiti ukutani ".....kapita hapa!" mitaa ya upanga hiyo...

...pale uwanja wa shule ya muhimbili, team ya Super Star ilikuwa inapiga zoezi kila jioni, kina Abdul na Ahmad Amasha hii ilikuwa team yao ya mtaani...

...huku karibu na klabu ya Yanga kulikuwa na mkaanga chipsi maarufu kwa jina MASALADI, ilikuwa kama transit point kwa wote wanaoelekea majumbani kuanzia saa nane usiku mpaka alfajr kwa waliotokea Gogo-Africana, Mbowe etc...enzi hizo Bagamoyo Rd vumbi tupu, ni road race na wale waarabu wenye coaster za Scaba Scuba na Sea Never Dry kuwahi chipsi moto!
Huyo kilema namkumbuka,jina nimemsahau
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
silver oak napajua,kijiwe cha castro ndio ilikuwa maskani kuu

....shwari, ...kwa mtaji huo shule ya muhimbili imekuhusu sana, mitaa ya duka shop kwa baba Tayyibali na potelo zake, chipsi za Arawa, four flats nk...mitaa ya home hiyo.
 
Ali gulu alikuwa mlemavu,inamaana ya kuwa akishakuiba badala ya kumkamata munamuangalia tu!dah!hii nomaa kabisa!!!
Kulikuwa na Mwizi Maarufu alikuwa anaitwa Ali Gulu.. Cha kushangaza alikuwa ana mguu mbovu anachechemea lakini ni mwizi tena yule wa kukaba na anaondoka pole pole hakimbiii alikuwa anakuja hadi mitaa a kwetu kuba na wenzake mitaa tote ya Upanga kawaliza sana wahindi na waswahili...

ukisiikia mtu anataka kwenda kariakoo unamshangaa na kumuuliza wewe humuogopi Ali Gulu
 

....shwari, ...kwa mtaji huo shule ya muhimbili imekuhusu sana, mitaa ya duka shop kwa baba Tayyibali na potelo zake, chipsi za Arawa, four flats nk...mitaa ya home hiyo.
Duka Shop,4 flats,unanikumbusha mbali sana-enzi za neema hizo-i would do anything to turn the hands of time backwards. Life imechange,whenever i am back washikaji hatuonani-kila mtu anaenda mbio
 
Duka Shop,4 flats,unanikumbusha mbali sana-enzi za neema hizo-i would do anything to turn the hands of time backwards. Life imechange,whenever i am back washikaji hatuonani-kila mtu anaenda mbio

dah.. Mimi nilisoma Muhimbili..
Ila makazi,Kariakoo.. Vijiwe vya Upanga navifahamu...
 

....shwari, ...kwa mtaji huo shule ya muhimbili imekuhusu sana, mitaa ya duka shop kwa baba Tayyibali na potelo zake, chipsi za Arawa, four flats nk...mitaa ya home hiyo.
Karega nasikia ana Ualaza wa Nguvu... lol
Mitaa hiyo alikuwepo Kichaa George na Rabiya yule Mama wa Kihindi Mento..!
Mitaa hiyo karibu na Home kwa Mw. Ndossi... Krokodire Ushuzi wa Mung....

Watoto si Manunda hawa Si hawana Akili Si Hawana Adabu.. Mw. N.



Duka Shop,4 flats,unanikumbusha mbali sana-enzi za neema hizo-i would do anything to turn the hands of time backwards. Life imechange,whenever i am back washikaji hatuonani-kila mtu anaenda mbio
Nangatai Ulishakula wewe? inaelekea na wewe ulikuwa unapenda sana Sun Vita...
 
Dudu utakuwa ulisoma Muhimbili kama mimi...
Tuna alumni yetu kule.......... Vp unaingiaga?
 
Ali gulu alikuwa mlemavu,inamaana ya kuwa akishakuiba badala ya kumkamata munamuangalia tu!dah!hii nomaa kabisa!!!
na kama Ali Guru mwenyewe wanayemzungumza ni yule wa mtaa wa Twiga....nimechoka kabisa!!!
 
Back
Top Bottom