Watoto wa kariakoo mpo jf?

Watoto wa kariakoo mpo jf?

kifilio!!!!!!!!
Hahahahahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!
Lakini pia watoto wangu wakiona avatar yako wanalia sana kwa woga mkuu!!!

Lakini ningeandika SHARPENER kusingekua na nongwa hii,acheni kupenda lugha za watu,kiswahili kinajitosheleza kabisa.
 
kifilio!!!!!!!!
Hahahahahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!
Lakini pia watoto wangu wakiona avatar yako wanalia sana kwa woga mkuu!!!

Mbona iko powa labda watoto wako umewazoesha kuona vitu vyeupe tu, halafu inaonekana picha za wale wanawake walioko kwenye simu hawajavaa nguo unawaoneshaga watoto wako
 
Amekuingilia kwenye kazi yako nini maana wewe ndo unatisha hapa town. Watu wa mbagala wakikusikia hulala na majeanz

hata wale wa tandale nao wananihanya kishenzi, sahivi nataka nianze project ya masaki na ostabey nao watie adabu.
POPOBAWA.
 
Ah..kwetu hiyo.. Mitaa ya MkunguniSwahili,,Mafia,Masasi,Narung,ombe,Tandamti,Pemba,Kongo,Twiga,Nyamwezi,Aggrey,etc...

Misikiti,Kwa Mtoro,Idrissa,makanisa,KKKT Kariakoo..
Zahanati,kwa Dr Maro,yule wa kihindi Dr nani vile? Na pale Pan African kwa Dr Makene..Baadaye,Al Jumaa..pale Mafia na Sikukuu..

Siwezi sahau miilk shake,na ice cream za Bakhressa pale Livingstone.. Na mikate ilikuwa ya ukweli enzi hizo.. Mitamu ina ladha..

Mahoteli,Mico Hoteli,Hadhara Mount(Pemba na Msimbazi)...
Kulikuwa na askari mmoja alikuwa na mikogo miaka fulani pale Msimbazi Police.. Akiitwa Koplo Mukama Sharp!

Palikuwa na mama mmoja maarufu wa kihindi mama Songambele... Marehemu mzee Chaurembo alikuwa mjumbe wetu wa nyumba kumi.. Tulikuwa tunaenda duka la kaya kupimiwa sukari na unga...

Mambo mengi jamani..
 
hata wale wa tandale nao wananihanya kishenzi, sahivi nataka nianze project ya masaki na ostabey nao watie adabu.
POPOBAWA.

Ukija masaki utanasa kwenye fensi za umeme tukukute asubuhi
 
Leo nataka tukumbushane mji wetu mkongwe,mji maarufu wenye historia kubwa ndani ya nchi hii lakini inayoelekea kupotea.Mko wapi watoto wa kariakoo wa ukweli mtueleze tuijue kariakoo iko vipi,ilikua vipi,raha na karaha za mitaa ya kariakoo,na je kariakoo ya zamani na ya sasa zinalingana?karibu sana maskani mnaoijua kariakoo kiundani mtujuze sie wakuja maana ndo kwanza tunaishi kwenye maghorofa mapya baada ya wenye mji kuukimbia mji wao,maana tumekuwa tukiyasikia mengi kuhusu mitaa hii ilivyokua zamani.
Binafsi nimeishi Kariakoo karibu miaka 10....kuanzia mwaka 1998 - 2008. Nimeishi mtaa wa Sikukuu na Kariakoo karibu na St.Benard
hospital ya zamani.
Kuna mambo mengi sana niliyojifunza wakati naishi Kariakoo (nitaorodhesha machache tu)

1. Karibu ya wakazi wake waliowengi ni jamii ya kiislaam....wakristo ni wa kupapasia kwa mbali sana.
2.Nyumba zote za zamani zinamilikiwa na Wamanyema,wangazija,wahindi na waarabu....haya magorofa ya kisasa sijui wamiliki wake.
3.Wafanyabiashara waliowengi ni Wapemba,wahindi,waarabu na waswahili (hasa wakinga na wachaga)
4.Wazawa wa Kariakoo (dark skin) ni waswahili wa kutupwa! yaani wanamaneno ya kejeli na misemo ya maudhi sijapata kuona!.
5.Vijana wengi wa kariakoo (hasa wazawa) hawataki kufanya kazi yeyote....wanalala saa moja asubuhi na wanaamka saa moja jioni.
wengi wao wanajishughulisha na mambo ya madawa ya kulevya,kula milaa na dili za hapa na pale ili wapate pesa ya kwenda kula chips kwa Dullah pale mtaa wa Sikukuu na kwenda kwenye ma night clubs.
MWISHO:
6.Kariakoo na Ilala zitakuwa ni sehemu za mwisho sana katika ukombozi wa nchi yetu kwa mara ya pili....maana wakazi wa maeneo haya wanaipenda CCM sijapata ona! yaani wao na ccm na ccm na wao!. Haya ndiyo machache niliyoyashuhudia kwa macho yangu
wakati naishi kariakoo
 
Ah..kwetu hiyo.. Mitaa ya MkunguniSwahili,,Mafia,Masasi,Narung,ombe,Tandamti,Pemba,Kongo,Twiga,Nyamwezi,Aggrey,etc...

Misikiti,Kwa Mtoro,Idrissa,makanisa,KKKT Kariakoo..
Zahanati,kwa Dr Maro,yule wa kihindi Dr nani vile? Na pale Pan African kwa Dr Makene..

Siwezi sahau miilk shake,na ice cream za Bakhressa pale Livingstone.. Na mikate ilikuwa ya ukweli enzi hizo.. Mitamu ina ladha..

Mahoteli,Mico Hoteli,Hadhara Mount(Pemba na Msimbazi)...
Kulikuwa na askari mmoja alikuwa na mikogo miaka fulani pale Msimbazi Police.. Akiitwa Koplo Mukama Sharp!

Palikuwa na mama mmoja maarufu wa kihindi mama Songambele... Marehemu mzee Chaurembo alikuwa mjumbe wetu wa nyumba kumi.. Tulikuwa tunaenda duka la kaya kupimiwa sukari na unga...

Mambo mengi jamani..

afande mkama sharp alikua noma,nasikia alidedi bwana,du jamaa alikua mashuhuri sana kariakoo,kuna kipindi alikua na kikundi cha mchiriku,kariakoo yetu ilikua raha sana sio siri,enzi zile pasaka pasaka kweli,ndugu zetu wazanzibar tulishirikiana nao kushereka pasaka,yanga,simba red star zote zilipokea wageni marafiki toka zenj,mimi ni mtu wa red star sisi tulikua tukiwaalika malindi wakija pale usiku raha mbaya...pale kongo,red star mpaka leo kautamaduni kapo kidogo japo timu hamna!
 
Binafsi nimeishi Kariakoo karibu miaka 10....kuanzia mwaka 1998 - 2008. Nimeishi mtaa wa Sikukuu na Kariakoo karibu na St.Benard
hospital ya zamani.
Kuna mambo mengi sana niliyojifunza wakati naishi Kariakoo (nitaorodhesha machache tu)

1. Karibu ya wakazi wake waliowengi ni jamii ya kiislaam....wakristo ni wa kupapasia kwa mbali sana.
2.Nyumba zote za zamani zinamilikiwa na Wamanyema,wangazija,wahindi na waarabu....haya magorofa ya kisasa sijui wamiliki wake.
3.Wafanyabiashara waliowengi ni Wapemba,wahindi,waarabu na waswahili (hasa wakinga na wachaga)
4.Wazawa wa Kariakoo (dark skin) ni waswahili wa kutupwa! yaani wanamaneno ya kejeli na misemo ya maudhi sijapata kuona!.
5.Vijana wengi wa kariakoo (hasa wazawa) hawataki kufanya kazi yeyote....wanalala saa moja asubuhi na wanaamka saa moja jioni.
wengi wao wanajishughulisha na mambo ya madawa ya kulevya,kula milaa na dili za hapa na pale ili wapate pesa ya kwenda kula chips kwa Dullah pale mtaa wa Sikukuu na kwenda kwenye ma night clubs.
MWISHO:
6.Kariakoo na Ilala zitakuwa ni sehemu za mwisho sana katika ukombozi wa nchi yetu kwa mara ya pili....maana wakazi wa maeneo haya wanaipenda CCM sijapata ona! yaani wao na ccm na ccm na wao!. Haya ndiyo machache niliyoyashuhudia kwa macho yangu
wakati naishi kariakoo

Hii ya kuipenda ccm inatokana na historia zaidi,mababu zao ndio walioanzisha harakati za uhuru zilizozaa tanu-ccm,hivyo japo ccm ilikuja kuvamiwa na wakuja baadae bado wanafeel kwa connected na chama hicho japo inaenda ikipungua taratibu kutokana na kushamiri kwa wapemba na ujio wa cuf.

Chips kwa dulla sikukuu sio,kweli kabisa bila kusahau kwa muchacho gerezani chips za kufa mtu.Vijana wengi enzi hizo walikua watu wa kuwaza safri za ugiriki na ulaya kiujumla,na wengi ndio walikua watu wamwanzo kuondoka tanzania kukimbia hali ngumu ya maisha kutokana na kibano cha nyerere,watu wengine wengine hasa wa bara walikua wakienda ulaya basi ulaya yao ni urusi kusoma!
 
We mkinga nini manake mnavyojazana kkoo mpaka mnatisha
 
Leo umenichekesha sana. Kweli kuna jamaa nilikuwa namfahamu amezaliwa na kukulia pale kariakoo alikuwa anasoma Old Moshi Sec .Tabia ulizosema za watoto wa kariakoo nikamkumbuka sana yule jamaa kwa sababu ni kama ulikuwa unanitajia sifa zake. Maneno maneno haswaa matusi yenye maudhi ndio jadi yao.
 
kwanini nyumba nyingi za kariakoo ni wabibi wa kimanyema?

sababu kubwa ni wazee wa kizaramo,kindenge na wengine wa jamii hizo za pwani kuchanganyikiwa kimapenzi na bibi zetu hao wa kimanyema ambao kiasili walikua ni wafanyabiashara wazuri wakija pwani mpaka zanzibar kibiashara.Wazee wa kizaramo wakawa wanachanganyikiwa sana na bibi zetu hao kutokana na maumbile yao,kujishughulisha kumsaidia bwana,mapishi n.k hivyo ikawa ni fahari kuwa na bibi wa kimanyema,jambo hili liliwafanya wazaramo kwa kuzidiwa na mapenzi kuwaandika wabibi wa kimanyema kwenye milki ya nyumba walizojenga na wao kuhamia mbagala na bi mkubwa na kumuacha bi mdogo na nyumba kariakoo.kimaumbile wanawake wa kizaramo ni watu wadogo wadogo tofauti na bibi zetu wa kimanyema.
 
kaangalie kwenye kamusi ya kiswahili utaona maana yake halisi...mzee,usikurupuke.

watoto wa mitaa ya swahili hili jina maanake la kumegwa vp kijana unapakatwa nini?
 
watoto wa mitaa ya swahili hili jina maanake la kumegwa vp kijana unapakatwa nini?

La hasha,unless uwe sio mswahili....ni jina mujarab la kiswahili fasaha sema nyie wavivu tu wa kujifunza maneno mapya ya lugha yenu,mko busy ni kidhungu ili muonekane wasomi eti!

Hiyo swahili yako namba ngapi?
 
Muulize swahili na nini ndio utamjua kama kweli ni wa kariakoo,hiyo huwa inawababaisha sana wasiokulia kariakoo hata kama wana maduka kariakoo,bado inawazingua!
 
wapendwa kuna tofauti ya r na l
lakini hata hivyo itakuwa taaab sana iwapo jina kifilio akikutana nalo afande chacha mwita nazile ''arooooo utarara rokap''
 
Back
Top Bottom