Watoto wa geti kali mko wapi siku hizi?

Watoto wa geti kali mko wapi siku hizi?

pureman2

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2019
Posts
1,491
Reaction score
2,563
Context izingatiwe

Nivilio kila Kona, wanaume wakiuliza yako wapi mapenzi tuliosimuliwa na Babu zetu. Waliotuhadithia kuwa mapenzi si pesa bali hisia za wawili waliopendana na kuamua kuishi bila kuathiliwa na Hali ya mtu kiuchumi, kijamii, na ata kielimu.

Waliotusimulia simulizi hizi wakifufuka na warudi kwenye ulimwengu wa Leo, si ajabu watajikuta chama watakachoweza kujiunga ni CHAPUTA tu kwani mapenzi imekua bidhaa aghali sana .

Almost girls wote wamekua ombaomba, wote wana njaa, wote hawana Kodi, wote hawana uwezo wa kuhudumia simu , wote hawana nauli kuudhulia makwao kipindi matatizo yanapotoke, wote wanahitaji kwenda salon, wote wanahitaji nguo na vifaa lukuki vya urembo. Bila pesa ukidate nao hutayafurahia mapenzi. Na hata ukijitutumua uwe na uhakika makasiriko hayatakuisha.


Mimi nauliza watoto wa geti kali ambao sifa yenu ilikua ni upendo wa dhati Leo mmeenda wapi???

wanawake wanaotokea familia bora wao walikua wakipenda ndo shughuli imeisha. Atafanya visa vyote ili kupambania penzi la roho. Kitu hiki kimekua hadimu kama kupata bikra uswahilini. Jamani watoto wa geti Kali mpo ?

Nauliza hivi coz ukifanya utalii wa ndani ya nchi hii utaona maendeleo ya vitu. Watu wanaishi nyumba Bora za kisasa , wanatembelea magari makali, wanasoma kwenye shule aghali toka kindergarten hadi elimu ya chuo. Cha kushangaza watoto wa geti Kali hawapo Tena mtaani Ili kuendeleza sifa Yao ya mapenzi ya dhati. Badala yake wote wamekua wadangaji na makuwadi.


Najua mtavamia Uzi huu na kusema acha kulialia tafuta pesa, but I stand with my point ....wako wapi wanawake wenye mapenzi ya kweli ?

Wengine tumejaliwa pesa ,ila tunatamani kuzitumia na wanawake wenye mapenzi ya kweli , Cha kushangaza tunaambulia wadangaji.

Tunahitaji mapenzi na sio utelezi na kumwaga. Ndio maana malaya hawezi ku replace mpenzi. Malaya wako kila mahala ila wanashindwa kutambua hitaji la binadamu ni mahusiano zaidi ya sex.

Mmetugeuza wanaume kuwa kama mateja wa sex. Daily tunafanya mambo mengi hatarishi Ili tupate pesa ya kutafuta mapenzi na badala yake tunaambulia mbunye tu. Mbususu sio mapenzi, mapenzi ni furaha, amani, utulivu, maelewano, mshikamano, urafiki, na mapenzi teletele.

Na kwa sababu mapenzi yamekosekana kilichopo sokoni ni sex tu. Nimasikitiko kuona tunaishi kwenye jamii ambayo wanawake hawana kingine to offer than SEX. This is too sad.

Shime shime watoto wa geti Kali mjitokeze muokoe jamii. Kwa mkutadha wa uzi huu mtoto wa geti kali ni yeyote mwenye mapenzi ya kweli na sio njaa ya PESA. Anaeweza kuthubutu kuingia kwenye mahusiano na ukapita mwezi hajatangaza njaa na shida zake bali kipindi chote hicho lugha yake iwe UPENDO
 
Inabidi tukubaliane na matokeo tu maana kuna mistakes zilisha tokea na ndio matokeo yake haya sasa.

Ikibidi tuachane na mapenzi tutafute uzazi tu ili kuendeleza maisha, maana wenzetu wanachotufanya hata hamu ya maisha hatuna tena.
 
Wengine tumejaliwa pesa ,ila tunatamani kuzitumia na wanawake wenye mapenzi ya kweli , Cha kushangaza tunaambulia wadangaji.
Nafikiri hii ndio point ya msingi. Kifupi mkuu bado haujapata anayekupenda kikweli

Demu kama hajakuelewa atakachokuwa anataka ni pesa yako tu na ndio kilio chako kwenye huu uzi uliondika. Na hii ndiyo hali unayopitia kwa sasa
 
Ati mtoto wa geti kali ambae hana njaa ya pesa? Kwa maana nyingine unataka mwanamke kwao mboga saba afu wewe pesa huna una mapenzi tu?

Kwani akiwa sio wa geti kali na kwao wana maisha ya kawaida hawezi kuwa na mapenzi ya dhati?

Wadogo zangu ambao mko humu kwenu pesa haisumbuwi musiolewe na wanaume wenye maisha duni wana wivu kupindukia.

Shoga yangu sasa hivi ni marehemu kisa kuolewa na mwanaume njaa. Na kila mtu alimzuia ila alisema atapambana mme akae sawa.

Baada ya ndoa wivu wa kipumbavu ukaanza. kwao na shoga yangu magari yapo kibao so alikuwa akienda nyumbani kutembea muda wa kurudi kwa mme wake anapewa dereva ampeleke asipande daladala.

Deleva akimfikisha mme akaona walivyoletwa yesuuu anavimba maneno yanaanza oh unajidai kwenu kuna hela maneno kibao.

Kingine tangu amuoe hakuwahi kununua chakula humo ndani anasubili shoga aagize kwao vyakula. Na huyo mwanaume sio kwamba hakuwa na hela hata ya chakula, no alikuwa na kikazi so vipesa vidogo alikuwa navyo.
Shoga yangu alikuwa akipambana bila kujali kwao pesa ipo lakini yule mme hapana.

Hakuwahi mnunulia hata kitenge kisa eti kwao hela ipo? Kilichomkuta ndani ya muda mfupi ni mauti.

Mwanaume tafuta pesa zako wacha kuwaza kuoa wenye nazo wakati wewe una 1200.
 
Noo,sio kweli la huwa mnakurupuka,mfn. Yan Unahela then unadate na mwanamke ambaye hata kujinunulia bando hawez sasa ataweza kukupa mapenz ya kweli?
Nionyeshe wasiotangaza njaa na shida zao . Hao ndo nawatafuta mm
 
Ndio uboya tunaoukataa yan mtu mzma kabisa ushndwe kung`amua yupi ni GOLD DIGGER na yupi KUKU WA KIENYEJI...
Mkuu sio vyepesi hivyo. Ukiwaona usoni kama watu , ingiza mguu TU ,hakuna shida utaacha kuisikia.
 
Back
Top Bottom