DOKEZO Watoa huduma wa Zahanati ya Mianzini ni jipu. Wizara ya Afya ikaangalie wanachofanyiwa Wajawazito

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Kuna hii Zahanati ya Serikali ipo Mburahati hapa Dar es Salaam, inafahamika zaidi kwa jina la Zahanati ya Mianzini, kiukweli huduma zao ni mbovu sana hasa kwa hawa mama zetu Wajawazito.

Awali nilikuwa nasikia tu taarifa hizo kuhusu madai hayo lakini nimeshuhudia mimi mwenyewe, nilienda kumpeleka mgonjwa katika Zahanati hiyo nikashuhudia Wauguzi hasa wa kike ni wa kali muda wote, wananyanyaswa sana Wajawazito na kuwaambia kama wanataka huduma nzuri waende ‘private’.

Kwa ufupi Wajawazito wanaoenda hapo hawapati huduma stahiki, wahudumu wamekuwa sugu, ukitaka ugomvi nao anza kuhoji chochote tu ambacho unaona hakipo sawa utapata cha moto.

Inamaana Serikali nayo imeridhia taasisi zake za Afya kama hii ya Mianzini kuwadharau wagonjwa kwa kuwa tu wanaoenda hapo ni wa kipato cha chini?

============== =================

UFAFANUZI WA MGANGA MKUU WA DAR
Alipoulizwa, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Rashid Mfaume amesema “Tulielekezwa na Wizara ya Afya kuwa namba za simu za Mganga Mkuu wa Mkoa ziwepo kwenye vituo vya afya vya Serikali, kwa ajili ya kutoa taarifa mbalimbali kama kero za aina hiyo.

Pia kama kuna mwananchi ambaye anapata changamoto au kero yoyote kwenye vituo vya Afya afya tunasisitiza kuwasiliana na Mganga Mkuu tena ikiwezekana muda huohuo wakati wa keri ili iwe rahisi kuitatua.

“Kuhusu changamoto hiyo ya wauguzi wa Zahanati ya Mianzini bado sijapata hizo taarifa lakini tutafuatilia na kwa kuwa ni changamoto yenye mwendelezo tunaweza kutuma watu wetu au kupandikiza ili kuona kama kuna changamoto ya aina hiyo.”
 
Shida kubwa ni Kazi zinakuwa nyingi Ila stahiki zinakuwa chache, watumishi wanakosa morali ya kazi, Hivyo wanafanya kazi ili tu kibarua kisiote nyasi wasikose pa kujifichia ili kupata mkate wa kila siku....

Fanya tafiti mkuu sio hapo tu nenda kokote kule hasa hawa waliochini ya Tamisemi,, watumishi wamechoka walichoahidiwa na walichopata sio wanakazi nyingi wanafnya ila malipo machache.

Fikiria huyo Nurse kwa mfano kazalisha watu Sita usiku na wakati huo huo lazma asubuhi aende tena kazini kwwnye majukumu yake....

Bado anatakiwa afanye kazi zingine tofauti na kuzalisha na wakati huo kachoka anakuja mgonjwa anamuuliza maswali..bhasi hata angekuwa analipwa vizuri ila trust me Wengi wanachukua TGHS A ambayo kwa sasa Baada ya ongezeko ni Tsh 492k kama basic wakati huo makato na mikopo aliyonayo unakuta anaweza kubakiwa na 200k kwa mwezi haitoshi kwa matumizi ya nyumbani yey kama yeye....

Posho nyingi siku hizi zimeminywa,Seminar na warsha zimezimwa unafukiri mtumishi huyo atakuwa na hali gani kimawazo...

Ndo maana wengine wanaingia katika kuuza dawa za hospitali na kufanya magendo mengine kwa sababu akili na roho zao wanziweka rehani angalau waepuke aibu...

Mkuu ninakuambia kwa sababu najua na nimedanya tafiti nyingi kuhusu hilo kama u a swali uliza
 
Kuna hii Zahanati ya Serikali ipo Mburahati hapa Dar es Salaam, inafahamika zaidi kwa jina la Zahanati ya Mianzini, kiukweli huduma zao ni mbovu sana hasa kwa hawa mama zetu Wajawazito.

Awali nilikuwa nasikia tu taarifa hizo kuhusu madai hayo lakini nimeshuhudia mimi mwenyewe, nilienda kumpeleka mgonjwa katika Zahanati hiyo nikashuhudia Wauguzi hasa wa kike ni wa kali muda wote, wananyanyaswa sana Wajawazito na kuwaambia kama wanataka huduma nzuri waende ‘private’.

Kwa ufupi Wajawazito wanaoenda hapo hawapati huduma stahiki, wahudumu wamekuwa sugu, ukitaka ugomvi nao anza kuhoji chochote tu ambacho unaona hakipo sawa utapata cha moto.

Inamaana Serikali nayo imeridhia taasisi zake za Afya kama hii ya Mianzini kuwadharau wagonjwa kwa kuwa tu wanaoenda hapo ni wa kipato cha chini?
Ifike wakati warekodiwe warushwe kwa mitandao tunao wengine wanaotafuta ajira kila siku
 
Ifike wakati warekodiwe warushwe kwa mitandao tunao wengine wanaotafuta ajira kila siku
Kuchukua video na kurusha haisaidii kutatua tatizo cha msingi kufanya utafuti kujua,chanzo ni nini ila kwa kifupi watumishi wote sio afya wala ualimu wala Utawala wamekosa morali
 
Kuchukua video na kurusha haisaidii kutatua tatizo cha msingi kufanya utafuti kujua,chanzo ni nini ila kwa kifupi watumishi wote sio afya wala ualimu wala Utawala wamekosa morali
Kila mmoja ana wajibika kwa matendo na kauli zake, na tabia zake, kuna uwajibikaji binafsi na jumuishi katika utumishi. Zingatia hilo utiisho wa kanuni za adhabu ni sehemu ya kazi. Mtumishi anapaswa kuwa humble, kutawala hisia zake wakati wote.
 
Kila mmoja ana wajibika kwa matendo na kauli zake, na tabia zake, kuna uwajibikaji binafsi na jumuishi katika utumishi. Zingatia hilo utiisho wa kanuni za adhabu ni sehemu ya kazi. Mtumishi anapaswa kuwa humble, kutawala hisia zake wakati wote.
Yaah nakuelewa mkuu na ndivyo inavyotakiwa ila soma comments ya #4 niliyoandika halafu urudi na hoja kwa mtumishi kama huyo
 
Yaah nakuelewa mkuu na ndivyo inavyotakiwa ila soma comments ya #4 niliyoandika halafu urudi na hoja kwa mtumishi kama huyo
Utumishi wa umma ni utumishi wa Mungu na ni utumishi wa kunyenyekea ikibidi hata kinafiki, disillusionment ni internal matters not to the customers.

Am using business perspective kwenye service delivery, iwe profit bound or not ni sharti la huduma.

Hideouts kiutumishi hazipo katika kumkera mteja
 
Mwaka fulani mwanza pale nilienda hospital (.............) baada ya vipimo nikaandikiwa sindano. Aseeee yule mama (nurse) aliyetakiwa kunichoma sindano sura yake na alivokuwa kanuna nilikataa nikarudi kwa daktari nikamwelezea akacheka kisha akanipangia mlimbwende mmoja charming halafu ana lugha ya kidaktari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utumishi wa umma ni utumishi wa Mungu na ni utumishi wa kunyenyekea ikibidi hata kinafiki, disillusionment ni internal matters not to the customers.

Am using business perspective kwenye service delivery, iwe profit bound or not ni sharti la huduma.

Hideouts kiutumishi hazipo katika kumkera mteja
Mkuu nakuelewa sana na nasimama upande wako kwamba utumishi wa umma ni unyeyekevu kama utumishi wa Mungu

sitaki nimsemee huyu kwa sababu simjui ila nataka niseme kero hii ambayo imekuwa kama tatizo la muda saasa kwa hawa manesi huenda wanawasilisha ujumbe ambao wanaotakiwa kuuchukua ujumbe huo wamefunga masikio...

kwanini kwa sababu ukimsikia hata huyo anavyosema kuwa ungetaka huduma nzuri ungeenda private...
unafikir kwanini Private....

private wanajali hali za watumishi wao hawawatumii watumishi to the extent mpaka wakashindwa kuacha ubongo upate kufanya kazi vizuri...private wanapata muda mwingi kupumzika na pia kingine...private kila kitengo kina Mhudumu wake ila tofauti na serikali...

serikali zahanati moja inakuwa na Mganga(Tabibu),Huyo nurse na Mhudumu wa afya unakuta wanatibu wagonjwa wengi sana....
na wakati huo huo wanafanya kazi nyingi za ziada zikiwa tofauti na kutibu lkini zisizokuwa na maslahi kwao wanachoka wanaahidiwa kulipwa stahiki wanakosa mtetezi...

(KWA mfano mtumishi huyo aingie siku nzima ya kazi lakini kuna wagonjwa wa dharura inabidi awa attend,Kuna wajawazito usiku inabdi awazalishe pengine mpaka saa kumi usiku,Lakini kumbuka asubuhi saa moja na nusu inatakiwa awe amefika kazini na kuhudumia wagonjwa pia na hii routine huenda kwa muda wowote na non stop wanapumzika pale wajawazito na wagonjwa wa dharura watakapokuwa wamepungua?)

kwa sababu hata waliowaamini wanageuka watetezi wa sehemu wanayopaswa kupeleka malalamiko..

wanahifadhi machungu mengi ya Walichokosa na walichotakiwa kupata...Usione wanacheka mkuu wanaumia na ndo maana wwngi wanafanya kwa maksudi misconduct ili angalau wapate kupata sehemu ya kuitwa kusema hizo shida zao...

nimefanya utafuti na nina uhakika wa ninachokuambia
najua sheria nyingi haziruhusu kama STANDING ORDER FOR PUBLIC SERVICE YA MWAKA 2009,KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA MWAKA 2003 ....Kanuni za maadili za utumishi wa umma ...

lakini kuna vipengele vinavyowaruhusu kufanya mgomo au mgomo baridi ambao ndo kama huo wanaofanya....
 
Back
Top Bottom