wanzagitalewa
Senior Member
- Jan 25, 2018
- 128
- 84
Kabla sijaanza kueleza ni kwa namna gani Watanzania watanufaika na mkopo wa shilingi trilioni 2.4 kutoka Shirika la Fedha Duniani, kwanza ifahamike kwamba hakuna nchi duniani ambayo haikopi, nchi zinatofautiana kiwango na sababu za kukopa.
Baada ya hilo, nielekeza kwamba mkopo ambao Tanzania imepata, sio mkopo uliochukuliwa ili kuja kulipa mishahara, bali ni mkopo utakaowezesha utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo na huduma za kijamii.
Fedha hizo zitaleta unafuu kwenye mfumuko wa bei kwa kushusha bei ya mafuta na kuwezesha uchumi jumuishi, uchumi ambao utakugusa maisha ya Watanzania wote.
Pia, zitatumika kusisimua uchumi ambao umeathiriwa na janga la UVIKO19 na vita vya Urusi na Ukaine ambavyo vimeathiri uzalishaji na usambazaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo ngano na mafuta duniani.
Aidha, sekta binafsi ambayo imeajiri idadi kubwa sana ya Watanzania nayo itapata unafuu, zitatumika kuwezesha utoaji wa pembejeo za kilimo zenye ruzuku na zitasaidia vijana, wanawake na makundi mbalimbali.
Mkopo huo wa masharti nafuu utatolewa katika kipindi cha miezi 40 kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa Tanzania.
Baada ya hilo, nielekeza kwamba mkopo ambao Tanzania imepata, sio mkopo uliochukuliwa ili kuja kulipa mishahara, bali ni mkopo utakaowezesha utekelezaji wa miradi ya kimaendeleo na huduma za kijamii.
Fedha hizo zitaleta unafuu kwenye mfumuko wa bei kwa kushusha bei ya mafuta na kuwezesha uchumi jumuishi, uchumi ambao utakugusa maisha ya Watanzania wote.
Pia, zitatumika kusisimua uchumi ambao umeathiriwa na janga la UVIKO19 na vita vya Urusi na Ukaine ambavyo vimeathiri uzalishaji na usambazaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo ngano na mafuta duniani.
Aidha, sekta binafsi ambayo imeajiri idadi kubwa sana ya Watanzania nayo itapata unafuu, zitatumika kuwezesha utoaji wa pembejeo za kilimo zenye ruzuku na zitasaidia vijana, wanawake na makundi mbalimbali.
Mkopo huo wa masharti nafuu utatolewa katika kipindi cha miezi 40 kwa ajili ya kuimarisha uchumi wa Tanzania.