Watanzania wanataka nini kwa CHADEMA?

Chadema-Mwanza.jpg


Swali hili labda ni swali kubwa na la msingi ambalo watu wanahitaji kuona linajibiwa wanavyoona CDM inajipanga kushika madaraka. Haitoshi kuunga mkono CDM kwa sababu ya kuchukia CCM au kutokubaliana na sera za CCM. Watu wanapounga mkono CDM au kujiunga na CDM ni kwa sababu wana matarajio fulani au matumaini fulani. Matumaini hayo yanawafanya wawe tayari kuunga mkono CDM na hata kujitolea kwa mambo mbalimbali. Ni nini basi Watanzania wanataka?

Kisheria: NI sheria gani ambazo CDM itafanyia mabadiliko au inapaswa kufanyia mabadiliko? Yaani, Sheria ambazo CCM imeshindwa kuzifanyia mabadiliko au imefanyia mabadiliko ya juu kwa juu. Au sheria za hivi sasa ndizo zitaendelea kutumika chini ya CDM?

Kimfumo: Mfumo wote wa utawala uliopo sasa umetengenezwa na serikali ya CCM na matokeo yake tunayaona. Je chini ya CDM ni vitu gani vitabadilika? Jeshi la Polisi, Jeshi, usalama, wizara n.k vitakuwaje?

Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?

Na mambo mengine mengi. Ndio hapa nauliza kwa wale wapenzi na wanachama wa CDM wanatarajia nini kutoka kwa utawala wa CDM tofauti na yale yanayofanywa au kufanyika chini ya utawala wa CCM? Au labda niulize kivingine ; ni mambo gani ambayo ukiyajua sasa kuwa CDM itayatekeleza ikishika madaraka yatakutia hamasa zaidi kuunga mkono, kujiunga au kuwa sehemu ya M4C?

mzee mwana kijiji I salute you!

Kimsingi wanacho takiwa CDM kufanya ni kutulia na kujiandaa ku manage people's expectations! and they are so many!

watu wanatarajia miujiza baada ya CDM kuchukua nchi, na CDM hawajawaanda watu kukubaliana na hali itakavyo kuwa baada ya ya CDM kuchukua nchi! wakati huo huo, haijajulikana CDM iko mrengo gani, kijamaa, kibepari au ukomunisti, dhana ya peoples power, haita-apply kwenye kungoza nchi, ni applicable kwenye pressure groups tu kwa political parties si rahisi ku-work, lazima wasomi wa CDM waanze kuleta maandiko yakionyesha vision na mission yao juu ya Tanzania baada ya CCM, yasiwe ya falsafa ya CDM bali watumie model mbali mbali ili kuunda serkali ya karne hii ya sayansi na Technolojia.

kwa maana hiyo, ni CDM wanapaswa kusoma alama za nyakati na kujianda ili rais wa CDM asije kuwa kama yule wa Madagascar (the former DJ), aliingia madarakani kwa mbwembe kilichofuata baadae ni aibu.

halafu kitu kingine ambacho cdm wanaanza nacho vibaya ni kufikiri watapendwa daima! wajifunze kutokana na makosa ya CCM, hali iliyopo CCM kwa muda huu ni very likely CDM ikafika huko and very soon! why? kwa sababu CDM wana tabia ya kutopenda kukosolewa au kupokea mawazo mbadala (rejea humu JF) na kuamini wako soo perfect! wakumbuke wana CCM ni wabongo, and wana CDM ni wabongo pia! and whatever goes around, very well, comes arround!

so ku, sum up maswali yako, unge ya address moja kwa moja kwa CDM rather than wananchi, and if you ask me, CDM should prepare and be ready to manage the "People's Expectations" after using the People's power to go to Ikulu! and as you and me know, they are a mountain!

I am out.
 
nadhani ni kitu kirahisi sana wakitakacho watanzania toka kwa chama kipya kitakachochukua madaraka badala ya CCM. Ni 'people's power' in the real sense ya maana ya hilo neno. Madaraka yaende kwa watu. Umma uwe na uwezo wa kuwawajibisha wasiotimiza matarajio yao. Mfumo huu ukikaa madhubuti, hata kije chama cha aina yoyote ile, bado kitatekeleza matakwa ya umma, vinginevyo umma utakitoa madarakani. Uwajibikaji kwa umma utasaidia kutibu mirija yote ya unyonyaji na wizi vinavyotuweka ktk rindi la umasikini.
 
Watanzania tunataka serikali madhubuti inayoweza kusimamia nidhamu na uwajibikaji wa watendaji wake. Serikali isiyowaonea aibu wezi, wabadhilifu wa mali za umma na inayochukia rushwa!

Watanzania tunataka serikali inayoona uchungu kwa wananchi wake kuwa katika lindi la umaskini, inawapenda na kuwaheshimu wananchi wake na kutenda haki kwa wote!

Watanzania tunataka serikali isiyoyumbishwa na mabepari na makabaila wa ndani na nje ya nchi.
 
Hivi swali sahihi ni Watanzania wanataka nini kutoka kwa Serikali yao au wanataka nini kutoka CHADEMA (Chama cha Siasa),Naogopa sana sana kwamba sasa tunaweka mategemeo makubwa sana kwenye vyama vya siasa badala ya serikali yetu. Au sielewi vizuri tofauti kati ya Chama cha Siasa na Serikali??
 
huenda nisiwe na lolote ninalolitegemea kutoka cdm zaidi ya kutaka tu kuona mabadiliko that ccm is out and cdm comes in, real what i need is changes full stop.................
 
Ndugu mwanakijiji, swali laku ni zuri sana. Kumbuka hata wakati wa TANU mwalimu aliweka mbele vitu viwili, yaani watu na haki, akajenga falsafa. Ukiangalia kiundani utaona CDM waliweza kuchukua falsafa hii na kutumia neno nguvu ya umma. Umma ukishakuwa na nguvu, umma unapata haki. Sasa hivi umma wa Tanzania umepokwa haki, inajidhihirisha katika mchakato wa katiba unavyokwenda, bunge lilivyovurunda, ahueni ikapatikana kutoka kwa Raisi, lakini bado kuna vitisho NK. Uizi wa epa, NK. Mlima wa Kiwira. CDM inatuhakikishia nguvu ya umma, ikitugeuka tunaigeuka. Nafikiri tukianza kwenda ndani katika kuchambua dhana ya nguvu ya umma, lazima mwenye akili timamu akimbilie CDM. CCM ni ya kuogopwa kama ukoma, Kolimba aliwaambia, wamepoteza dira, na mpaka leo hawajui duka la dira lilipo. Chama kisichokuwa na Dira! Duhhhh.
 
watanzania wengi tuna stress za maisha sababu ya kukosa huduma za kijamii na uhakika wa kesho. kurudi kwenye mada mimi ninachokitaka CDM ihakikishe hii nchi na watendaji wanafuata na kuogopa mfumo wa sheria na taratibu zilizopo.

Hili wanalitekeleza vipi? Unaweza vipi kufanya watu waheshimu sheria na taratibu zilizopo.. ?
 
huenda nisiwe na lolote ninalolitegemea kutoka cdm zaidi ya kutaka tu kuona mabadiliko that ccm is out and cdm comes in, real what i need is changes full stop.................

ukisema hivyo inaonekana wewe ni rahisi sana kuridhishwa; kama CCM itatoka na CDM ikaingia wewe hilo linatosha kushangilia. Chiluba alipomuonda Kaunda na chama chake Wazambia wengi walishangilia hata kwa wanamageuzi wa Tanzania Chiluba akawa kama shujaa wa aina fulani hivi.. well u know the rest of the story...
 
Ningependa kuona CHADEMA kinakuja na mkakati wa kuondokana na utegemezi wa mataifa ya nje na mfumo wa kinyonyaji wa IMF/WB. Hilo ningependa nione linaenda sambamba na upanuaji wa wigo wa makusanyo ya kodi; kwani kwa kuna na wigo mpana katika kukusanya kodi, ndiyo taifa litaweza kuondokana na mfumo tegemezi.
 
Mada inauliza Watanzania wanataka nini kwa CHADEMA. Ndani ya maudhui mwandishi anawauliza CHADEMA watawafanya nini kwa Watanzania!

He is among the most dedicated and foremost opinion leaders of the day but he is also a terribly shambolic and incoherent commentator.

Tatizo liko wapi? One is a converse of the other.

Newton's third law of motion talks about action and reaction, the relationship is deeply entrenched in nature. How dare you enforce an arbitrary requirement that we have to examine issues from a narrow minded, one sided outlook, and castigate a fuller examination that accommodates action and reaction as lackadaisical? Who is "shambolic and incoherent" now? The one who sees and accommodates action and reaction or the one who wouldn't see the one from the other if they were dangled in front of his nose?

If the objective is to examine Tanzanian politics in order to see that Tanzanians do not flock to CHADEMA simply because they don't want CCM - a dangerous thing indeed-, then both questions "What do Tanzanians want from CHADEMA?" and "What can CHADEMA do for Tanzanians" are relevant.

And in fact, the two questions, despite your arduously pedantic and quite sedentary hair splitting, are but two sides of the same coin.

More important than understanding the disparate points in this vagary of planes called Tanzanian politics, is understanding the connection between these said points. Your almost autistic formalism seems to blind you when it comes to making a connection of even the likes, comparable and congruently juxtaposable, forget the unlike, incomparable and singular .

Is this the best critique you could come up with? Because if it is, then it tells us more about your lack of depth and penchant for nitpicking than it shows us how Mwanakijiji's analysis is lacking.
 
@Mzee Mwanakijiji Watanzania wanacho taka kwa CHADEMA ni kuwa Chadema wajifunze makosa yanayofanywa na chama tawala CCM. Endapo Chadema watakapo pata uongozi wa kutawala nchi chadema wawe mfano bora kwa wananchi na uongozi ulio bora.Na Kurekebisha Makosa yaliyofanywa na Viongozi wa CCM katika uongozi wao chadema itabidi warekebishe ili Wananchi wapate kuwa na imani nao katika kuongoza nchi.

Hili nalo jambo.

Wananchi tunapoona CHADEMA kinayumbishwa na watu kama kina Shibuda, kinashindwa kumchukulia hatua kutuonyesha principle, na zaidi ya hapo viongozi wacho wanaotumainiwa na kutajwa kama wasomi kina Dr. Kitila Mkumbo wanakuja hapa kutuambia "tumpuuze" mbunge wao wenyewe, tunapata mashaka kuhusu ukomavu wa chama.

Tunapata mashaka kama chama kina michujio ya kuwachuja watu wanaofaa viongozi ama kinapokea mtu yeyote anayeweza kuongeza viti bungeni bila kuangalia principles.

CHADEMA bila ya ku deal na matatizo yake ya ndani haiwezi kutuaminisha kwamba inaweza ku deal na matatizo ya nje yake ambayo ni makubwa zaidi.
 
Kimoja ni kwamba wana mpango wa kufuta nafasi za Ukuu wa wilaya hapa nahisi patakuwa na Savings kwasababu wakuu wa wilaya nchi nzima kwa mwaka wanatumia mabillioni ya Shiringi ilihali output yao kwa mwananchi haipo na kama ipo ni kidogo sana na ingeweza kuwepo hata kama shughuli za mkuu wa wilaya zikaachwa ziwe chini ya mkurugenzi........ Kwa kifupi nina vitu kibao vya kuisapoti M4C nitarudi baadaye kidogo naona Boss wangu anaingia asije akaicheki ID yangu.
Ezan,
Ulichofanya hapo nacho ndiyo kati ya yale yanayoturudisha nyuma. TZ tumepoteza hata na maadili ya kazi. Unapokuwa kazini unatakiwa kuwajibika na majukumu yako ya kazi halafu muda wa kazi ukiisha ndio uje humu ukumbini kwa wakati wako binafsi. Makampuni ya kigeni mara nyingine hupenda kuajiri wageni kwa visababu kama hivi. Jamani tubadilike, ukilipwa mshahara wa kufanya kazi kwa masaa 8 kwa siku, ni wajibu wako kuwa unawajibika na kazi uliyoajiriwa kwayo kwa masaa yasiyopungua hayo 8. Kama tunawachambua wabunge, mawaziri n.k. nasi tujiangalie kwenye kioo kama tunawajibikaje.
 
Kwa kweli katika vitu Anna yo vinanipa wasi wasi wa uezo wa CDM Kutaraja ni suala la Shibuda. Yaaani Ina maana imeshindikana kumuwajibisha Shibuda?

Dr. Mkumbo naye anakuja na maneno yake! Mkjj, huu ndo wakati CDM Ituonyeshe...
 
ni mabadiliko yenye maslai kwa mwananchi wa kawaida na maisha yake ya kila siku. Kiuchumi,kijamii,siasa na utawala bora.
 
ukisema hivyo inaonekana wewe ni rahisi sana kuridhishwa; kama CCM itatoka na CDM ikaingia wewe hilo linatosha kushangilia. Chiluba alipomuonda Kaunda na chama chake Wazambia wengi walishangilia hata kwa wanamageuzi wa Tanzania Chiluba akawa kama shujaa wa aina fulani hivi.. well u know the rest of the story...
wanchoma kumoyo
 
Ezan,
Ulichofanya hapo nacho ndiyo kati ya yale yanayoturudisha nyuma. TZ tumepoteza hata na maadili ya kazi. Unapokuwa kazini unatakiwa kuwajibika na majukumu yako ya kazi halafu muda wa kazi ukiisha ndio uje humu ukumbini kwa wakati wako binafsi. Makampuni ya kigeni mara nyingine hupenda kuajiri wageni kwa visababu kama hivi. Jamani tubadilike, ukilipwa mshahara wa kufanya kazi kwa masaa 8 kwa siku, ni wajibu wako kuwa unawajibika na kazi uliyoajiriwa kwayo kwa masaa yasiyopungua hayo 8. Kama tunawachambua wabunge, mawaziri n.k. nasi tujiangalie kwenye kioo kama tunawajibikaje.
Kubwajinga nature ya kazi yangu unaijua? mimi nipo mapokezi nafanya kazi mpaka pawe na mgeni au simu ikiingia, mda uliobaki nacheza game na kukaa humu Jamvini na hata nikikutwa nacheza game siyo ishu. Ishu nikikutwa kwamba mimi ni mwanajamvi
 
Kama kuna jambo ambalo WATANZANIA wanalitaka/wanalitarajia kulipata kutoka CHADEMA wafanye mapitio kidogo juu ya haya yafuatayo:
-CHADEMA na CCM wote wanatafuna kodi zetu wakiita RUZUKU;
-CHADEMA na CCM wote wanafukuza WANACHAMA wao;
-CHADEMA na CCM wote wana WANACHAMA wenye nguvu kuliko vyama vyenyewe!;
-CHADEMA na CCM wana VIONGOZI wapenda PESA na MADARAKA kupindukia;
-CHADEMA na CCM wote wana WAMILIKI wa vyama hivi. Na sasa wameanza kurithishana vyeo;
-Kwa kiwango kikubwa CHADEMA imeundwa na waliokuwa wanaCCM.
Kama Mtanzania sitarajii lolote JIPYA toka kwa CHADEMA. Wangekwisha lisema hilo jipya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom