Watanzania wanataka nini kwa CHADEMA?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Chadema-Mwanza.jpg


Swali hili labda ni swali kubwa na la msingi ambalo watu wanahitaji kuona linajibiwa wanavyoona CDM inajipanga kushika madaraka. Haitoshi kuunga mkono CDM kwa sababu ya kuchukia CCM au kutokubaliana na sera za CCM. Watu wanapounga mkono CDM au kujiunga na CDM ni kwa sababu wana matarajio fulani au matumaini fulani. Matumaini hayo yanawafanya wawe tayari kuunga mkono CDM na hata kujitolea kwa mambo mbalimbali. Ni nini basi Watanzania wanataka?

Kisheria: NI sheria gani ambazo CDM itafanyia mabadiliko au inapaswa kufanyia mabadiliko? Yaani, Sheria ambazo CCM imeshindwa kuzifanyia mabadiliko au imefanyia mabadiliko ya juu kwa juu. Au sheria za hivi sasa ndizo zitaendelea kutumika chini ya CDM?

Kimfumo: Mfumo wote wa utawala uliopo sasa umetengenezwa na serikali ya CCM na matokeo yake tunayaona. Je chini ya CDM ni vitu gani vitabadilika? Jeshi la Polisi, Jeshi, usalama, wizara n.k vitakuwaje?

Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?

Na mambo mengine mengi. Ndio hapa nauliza kwa wale wapenzi na wanachama wa CDM wanatarajia nini kutoka kwa utawala wa CDM tofauti na yale yanayofanywa au kufanyika chini ya utawala wa CCM? Au labda niulize kivingine ; ni mambo gani ambayo ukiyajua sasa kuwa CDM itayatekeleza ikishika madaraka yatakutia hamasa zaidi kuunga mkono, kujiunga au kuwa sehemu ya M4C?
 
Mzee wangu hiyo yote ni reflections ya yote na maisha magumu na watu sasa wanataka mabadiliko ya kweli na watanzania wote wanaona CHADEMA kama chama chao cha mbadala na hivyo umefika kipindi cha kuwaunga mkono. Hivyo kuna haya hata fikra zetu za kufikiria nazo zibadilike na kuona kuwa wanakuwa na kujenga utadamuni mzuri na kutoogopa kitu na kuhoji kila kitu kwa ajili ya kupata ground nzuri Tanzania
 
Chadema-Mwanza.jpg


Swali hili labda ni swali kubwa na la msingi ambalo watu wanahitaji kuona linajibiwa wanavyoona CDM inajipanga kushika madaraka. Haitoshi kuunga mkono CDM kwa sababu ya kuchukia CCM au kutokubaliana na sera za CCM. Watu wanapounga mkono CDM au kujiunga na CDM ni kwa sababu wana matarajio fulani au matumaini fulani. Matumaini hayo yanawafanya wawe tayari kuunga mkono CDM na hata kujitolea kwa mambo mbalimbali. Ni nini basi Watanzania wanataka?

Kisheria: NI sheria gani ambazo CDM itafanyia mabadiliko au inapaswa kufanyia mabadiliko? Yaani, Sheria ambazo CCM imeshindwa kuzifanyia mabadiliko au imefanyia mabadiliko ya juu kwa juu. Au sheria za hivi sasa ndizo zitaendelea kutumika chini ya CDM?

Kimfumo: Mfumo wote wa utawala uliopo sasa umetengenezwa na serikali ya CCM na matokeo yake tunayaona. Je chini ya CDM ni vitu gani vitabadilika? Jeshi la Polisi, Jeshi, usalama, wizara n.k vitakuwaje?

Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?

Na mambo mengine mengi. Ndio hapa nauliza kwa wale wapenzi na wanachama wa CDM wanatarajia nini kutoka kwa utawala wa CDM tofauti na yale yanayofanywa au kufanyika chini ya utawala wa CCM? Au labda niulize kivingine ; ni mambo gani ambayo ukiyajua sasa kuwa CDM itayatekeleza ikishika madaraka yatakutia hamasa zaidi kuunga mkono, kujiunga au kuwa sehemu ya M4C?
wadanganyika wanataka haki na matumaini ya maisha dhidi ya mgawanyo sawa wa rasilimali zao zinazozurumiwa na utawala wa ccm kama ardhi,madini,hifadhi za wanyama n.k
 
Mzee mwanakijiji,

Nafikiri kwa kiasi kikubwa swali lako linajibiwa kwenye ile post ya marehemu Regia ya "[h=2]Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA". Kama CDM watayatilia mkazo na kutekeleza yale yaliyosemwa mule, tutasonga mbele.[/h]
 
Mada inauliza Watanzania wanataka nini kwa CHADEMA. Ndani ya maudhui mwandishi anawauliza CHADEMA watawafanya nini kwa Watanzania!

He is among the most dedicated and foremost opinion leaders of the day but he is also a terribly shambolic and incoherent commentator.
 
Swali hili labda ni swali kubwa na la msingi ambalo watu wanahitaji kuona linajibiwa wanavyoona CDM inajipanga kushika madaraka. Haitoshi kuunga mkono CDM kwa sababu ya kuchukia CCM au kutokubaliana na sera za CCM. Watu wanapounga mkono CDM au kujiunga na CDM ni kwa sababu wana matarajio fulani au matumaini fulani. Matumaini hayo yanawafanya wawe tayari kuunga mkono CDM na hata kujitolea kwa mambo mbalimbali. Ni nini basi Watanzania wanataka?

Kisheria: NI sheria gani ambazo CDM itafanyia mabadiliko au inapaswa kufanyia mabadiliko? Yaani, Sheria ambazo CCM imeshindwa kuzifanyia mabadiliko au imefanyia mabadiliko ya juu kwa juu. Au sheria za hivi sasa ndizo zitaendelea kutumika chini ya CDM?

Kimfumo: Mfumo wote wa utawala uliopo sasa umetengenezwa na serikali ya CCM na matokeo yake tunayaona. Je chini ya CDM ni vitu gani vitabadilika? Jeshi la Polisi, Jeshi, usalama, wizara n.k vitakuwaje?

Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?

Na mambo mengine mengi. Ndio hapa nauliza kwa wale wapenzi na wanachama wa CDM wanatarajia nini kutoka kwa utawala wa CDM tofauti na yale yanayofanywa au kufanyika chini ya utawala wa CCM? Au labda niulize kivingine ; ni mambo gani ambayo ukiyajua sasa kuwa CDM itayatekeleza ikishika madaraka yatakutia hamasa zaidi kuunga mkono, kujiunga au kuwa sehemu ya M4C?

What they want is not neccesary. What they need must come from CHADEMA's party Manifesto (ILANI). Hivyo wananchi wakasome ILANI na SERA za CHADEMA.
 
  • Utawala bora unaofuata sheria
  • Kuhakikisha rasilimali mbali mbali nchini zinainufaisha Tanzania na Watanzania
  • Maisha bora kwa kila Mtanzania
  • Huduma bora katika upatikanaji huduma muhimu (Maji, Umeme, Matibabu)
  • Shule zenye hadhi ya kuitwa shule
  • Kulimaliza kabisa tatizo la Wanafunzi wetu kukaa chini au kukalia matofali
  • Kuwaheshimu Walimu kwa kuwapatia mafunzo muhimu ili kuboresha Elimu yetu kuanzia shule za msingi hadi Vyuoni
  • Kuwaheshimu Walimu kwa kuwalipa mishahara na marupurupu mazuri ili kukidhi gharama za maisha
  • Kupandisha kiwango cha chini cha mshahara na kufikia shilingi 300,000 kwa mwezi
  • Kuhakikisha mikataba mbali mbali ya nchi inakuwa na maslahi kwa Tanzania na Watanzania
  • Kuhakikisha Watanzania wanapata ajira kabla ya mgeni yoyote yule na kama waajiri waonyeshe sababu zilizowafanya kushindwa kumuajiri Mtanzania na kumuajiri mgeni. Hii ni kuanzia kazi za ngazi za chini hadi juu
  • Kuhakikisha Bunge letu linaweka mbele maslahi ya nchi na siyo kama hili Bunge uchwara lililoweka mbele maslahi ya magamba
  • Kuboresha mashirika yetu mbali mbali ikiwemo TANESCO, Bandari na mengineyo ili kuhakikisha huduma bora kwa Watanzania na hata majirani zetu

Haya yote yanawezekana kabisa ikiwa kuna nia ya kweli ya kuhakikisha maisha bora kwa kila Mtanzania.
 
Ni nini basi Watanzania wanataka?

Kisheria: NI sheria gani ambazo CDM itafanyia mabadiliko au inapaswa kufanyia mabadiliko? Yaani, Sheria ambazo CCM imeshindwa kuzifanyia mabadiliko au imefanyia mabadiliko ya juu kwa juu. Au sheria za hivi sasa ndizo zitaendelea kutumika chini ya CDM?

Kimfumo: Mfumo wote wa utawala uliopo sasa umetengenezwa na serikali ya CCM na matokeo yake tunayaona. Je chini ya CDM ni vitu gani vitabadilika? Jeshi la Polisi, Jeshi, usalama, wizara n.k vitakuwaje?

Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?

MMJJ,
Wananchi watakachotaka toka kwa CHADEMA ni viongozi wenye kuona mbele na walio safi, full stop.

Sheria, Mfumo na Kuwajibika, haya yote hayatakiwi yawe mambo ya chama chochote, bali yanatakiwa yawe fixed character za nchi yetu. Tutengeneze katiba ambayo itayafanya haya yote yawe ni sehemu ya muundo wa nchi yetu.

  1. Sheria isitumiwe tofauti hata kama vyama vilivyo madarakani vinabadilika.
  2. Uwajibikaji uweze kusimamiwa na sheria na sio maamuzi ya raisi
  3. Mfumo wa utawala usiwe wa kubadilika hata kama vyama vitabadilika. Isiwe ikawa CHADEMA wanajenga majimbo halafu wakiondolewa madarakani anayefuata anaamua kujenga kitu kingine tena.
 
Mzee Mwanakijiji;3923864]Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?
Wakati natafakari maswali yako nikakutana na hicho nilichokinukuu cha uwajibikaji na naomba nikielezee kwa ufupi kwasababu kipo katika wakati muafaka.

Wananchi wanataraji kwajinsi CDM wanavyoibana serikali katika uwajibikaji huenda huo ndio ukawa ukombozi wao. Wamechoka na kubebena kunakowaumiza. Wananchi wanataraji kuwa serikali ya CDM itakuwa makini, kwamba mtu akitajwa tu bila ushahidi basi kwanza awajibike halafu sheria ichukue mkondo kumsafisha au kumtuhumu mhusika.

Utamaduni wa kutowajibika ni wa CCM, na sina haja ya kurudia. CDM walishupalia Dr Mwinyi kama kiongozi wa serikali wajibike kwa mabomu. Mkuchika awajibike, Pinda awajibike n.k.

Wananchi wanaona vijana waliopo CDM wakipikwa kuanzia sasa huenda tukawa na matumaini mapya.
Matumaini hayo ya uwajibikaji sasa naona yameingia doa, tena doa kubwa sana.

Nimeshangaa Mwenyekiti Mbowe akisema mgogoro wa Heche na Juliana ni mdogo sana.
Mwenyekiti ameangalia watu na si mazingira yaliyopo yanayotoa mwashirio wa siku za usoni.
Nimesikitika kwasababu nilitegemea Mbowe angeanza kuwapika vijana katika uwajibikaji.
Sikutegemea kuwa hadi leo uongozi wa CDM ungekuwa unamlinda Juliana Shonzo kama CCM wanavyobebana.

Nilitaraji Mbowe amshauri Juliana Shonzo aombe radhi, au awajibike na ikishindikana awajibishwe.
Kinachoonekana ni utamaduni ule ule wa kulindana na ambao unaanza kufundishwa vijana wanaotegemewa mwaka 2015 nakuendelea.

Mbowe alitakiwa atende kama kiongozi na siyo siasa zile zile tulizozoea za maneno matamu kama mkakati, tunajipanga, tumeliona hilo na sasa mbowe anaongezea 'ni mgogoro mdogo tu'

Tukio la BAVICHA ni dogo kama watu watapenda kuiona hivyo, lakini linatoa picha ya jinsi gani uwabikaji ulivyo katika chama kama CHADEMA. Ni mtihani mdogo wenye majibu makubwa. Kwa uwajibikaji sina uhakika CDM wanajipya!
 
Wananchi wanachokitaka kwa CDM ni walivyovitegemea toka kwa CCM 2005 wakaamini kwamba mgombea wao atawapatia na wao wakampatia 82% ya kura. Lakini bahati mbaya hawakipata na matokeo yake wakaegemea kwa CDM wakidhani watayapata yale. Sioni kama watu wanafuata sera za CDM na sijui kama wanazijua bali watu wamechoshwa tu na ahadi ambazo hazikutekelezwa. Vijana kwa mamia walidhani kuanzia mwak 2005 woote watatoka vijiweni ama wataacha kuwa machinga na badala yake kujipatia ajira vivulini zenye vipato vinono; hiyo haikuwa basi vijana wengi wana chuki na CCM wanadhani CDM ikiingia madarakani watapata hizo ajira nono.

Sheria za kurekebisha ziko nyingi. Kuna zile 40 za tume ya Nyalali hazikuwahi kurekebishwa. Lakini hapa pia wananchi tuna fursa kwenye huu mchakato wa kiandika katiba mpya; fursa hii ikitumika vizuri suala la sheria litakuwa taken care of.

Mifumo pia inategemea katiba na sheria: Mambo ya kujilimbikizia
madaraka, oversight institutions kutokuwa huru (PCCB, DPP, nk), nk. Tukiwa makini pia haya yote yatashughulikiwa na Katiba Mpya. Hivyo CDM itabakiwa na utekelezaji wa ahadi zake na kuongoza kwa mifumo na taratibu mpya zitakazokuwepo kwenye katiba mpya (kama watafanikiwa kukamata dola).
 
@Mzee Mwanakijiji Watanzania wanacho taka kwa CHADEMA ni kuwa Chadema wajifunze makosa yanayofanywa na chama tawala CCM. Endapo Chadema watakapo pata uongozi wa kutawala nchi chadema wawe mfano bora kwa wananchi na uongozi ulio bora.Na Kurekebisha Makosa yaliyofanywa na Viongozi wa CCM katika uongozi wao chadema itabidi warekebishe ili Wananchi wapate kuwa na imani nao katika kuongoza nchi.
 
Mada inauliza Watanzania wanataka nini kwa CHADEMA. Ndani ya maudhui mwandishi anawauliza CHADEMA watawafanya nini kwa Watanzania!

He is among the most dedicated and foremost opinion leaders of the day but he is also a terribly shambolic and incoherent commentator.

ad hominem! swali laweza kuwa na sehemu mbili ya kitu hicho hicho au kama ni gumu kuingia kichwani unaweza kuomba kueleweshwa kina cha hilo swali.
 
CHADEMA Wana advantage kubwa moja kama wataingia madarakani 2015. Nayo ni katiba mpya. Infact watu lazima wata-feel changes almost katika kila eneo endapo Katiba itakuwa nzuri ambayo watanzania wanaitaka. Hapo ndipo kile walichokikosa Watanzania kwa 50 yrs watakuwa wamekipata hata kama sio kwa utimilifu wake.
 
Mada inauliza Watanzania wanataka nini kwa CHADEMA. Ndani ya maudhui mwandishi anawauliza CHADEMA watawafanya nini kwa Watanzania!

He is among the most dedicated and foremost opinion leaders of the day but he is also a terribly shambolic and incoherent commentator.

Oh my God!! Yu are terribly wrong and coherent in exhibiting your IQ!

we are the employer we are asking employee what he will do for us and you are saying we are wrong??? if u belong to CDM please feel free to respond to this question convince him and other citizen! ulichojibu ni kukwepa swali na kushambulia

Kuna watu sehemu fulani, mahali fulani humu! niliwauliza kuwa tatizo la CCM ni kuwa kina wafanyabiahsara walio kwenye position kubwa kisiasa na hivyo wanajisukumia tenda na ku-influence decision kwenye kila kitu

Nikauliza, Mbowe ni mfanyabiashara, Ndesamburo au Komu...Je wakishika nchi, say Slaa ni rais Mbowe ni waziri mkuu

Mechanism gani au kitu gani kitafanyika kuzuia wafanyabiashara hawa wasifanye yale yale ya CCM given lawas and regulations will still be there before them to change!!

Hili swali nikiuliza.....nitakuwa 'shambolic and incoherent asker''??
 
Chadema-Mwanza.jpg


Swali hili labda ni swali kubwa na la msingi ambalo watu wanahitaji kuona linajibiwa wanavyoona CDM inajipanga kushika madaraka. Haitoshi kuunga mkono CDM kwa sababu ya kuchukia CCM au kutokubaliana na sera za CCM. Watu wanapounga mkono CDM au kujiunga na CDM ni kwa sababu wana matarajio fulani au matumaini fulani. Matumaini hayo yanawafanya wawe tayari kuunga mkono CDM na hata kujitolea kwa mambo mbalimbali. Ni nini basi Watanzania wanataka?

Kisheria: NI sheria gani ambazo CDM itafanyia mabadiliko au inapaswa kufanyia mabadiliko? Yaani, Sheria ambazo CCM imeshindwa kuzifanyia mabadiliko au imefanyia mabadiliko ya juu kwa juu. Au sheria za hivi sasa ndizo zitaendelea kutumika chini ya CDM?

Kimfumo: Mfumo wote wa utawala uliopo sasa umetengenezwa na serikali ya CCM na matokeo yake tunayaona. Je chini ya CDM ni vitu gani vitabadilika? Jeshi la Polisi, Jeshi, usalama, wizara n.k vitakuwaje?

Kuwajibishana: Mojawapo ya matatizo ambayo tunayaona sana - na hasa siku za karibuni - ni jinsi gani CCM iko goigoi katika kuwajibisha serikali yake na hata huko serikalini utamaduni wa kubebana ulivyozoeleka. Je chini ya CDM watu watarajie nini?

Na mambo mengine mengi. Ndio hapa nauliza kwa wale wapenzi na wanachama wa CDM wanatarajia nini kutoka kwa utawala wa CDM tofauti na yale yanayofanywa au kufanyika chini ya utawala wa CCM? Au labda niulize kivingine ; ni mambo gani ambayo ukiyajua sasa kuwa CDM itayatekeleza ikishika madaraka yatakutia hamasa zaidi kuunga mkono, kujiunga au kuwa sehemu ya M4C?

Kimoja ni kwamba wana mpango wa kufuta nafasi za Ukuu wa wilaya hapa nahisi patakuwa na Savings kwasababu wakuu wa wilaya nchi nzima kwa mwaka wanatumia mabillioni ya Shiringi ilihali output yao kwa mwananchi haipo na kama ipo ni kidogo sana na ingeweza kuwepo hata kama shughuli za mkuu wa wilaya zikaachwa ziwe chini ya mkurugenzi........ Kwa kifupi nina vitu kibao vya kuisapoti M4C nitarudi baadaye kidogo naona Boss wangu anaingia asije akaicheki ID yangu.
 
Honestly speaking, Ninachokitaka nimabadiriko tu, CCM iondoke kiingie Chama kingine, this time CHADEMA, Naamini hii italeta displine katika uongozi,na itakuwa imeanzisha desturi mpya kwenye nchi yetu ambayo ni bora kuliko hii ya sasa, lakini kila nikikumbuka jinsi binaadamu walivyokuwa corrupted + the corruption of democratic politics nakuwa mdogooooooo.
 
Cdm ni kikundi cha watu wenye stress za maisha.
watanzania wengi tuna stress za maisha sababu ya kukosa huduma za kijamii na uhakika wa kesho. kurudi kwenye mada mimi ninachokitaka CDM ihakikishe hii nchi na watendaji wanafuata na kuogopa mfumo wa sheria na taratibu zilizopo. mambo ya ahadi nzuri za elimu bora na maisha mazuri hata CCM wanezitoa sana sema hawakufuata sheria na taratibu katika kuzitekeleza. mfano mikataba mibovu ya madini inaingiwa sababu sheria za uwazi zinakiukwa mambo yanafanyika kisirisiri pia sheria za ardhi zinakiukwa na kuteletea migogoro vivyo hivyo sheria za tenda. yote hayo yanawezekana iwapo viongozi hawatakuwa waoga katika kuwajibishana
 
Nataka cdm ilinde mali za uma, lasilimali za nchi zitumike vyema si kuwauzia mateja wakizungu kama ifanyavyo ccm!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom