Bakyaitaki
Member
- Apr 6, 2012
- 65
- 44
Kwa hili nakuunga mkuno saana. Mimi huwa ninashangazwa pia. Yaani unakuta sehemu zenye msongamano kama Kariakoo yaani mtu anatembea utafikiri tayari ameshafika. Huwa nawapush na wengine nawambia hodi napita zangu haraka nafanya yangu fasta naomdoka.Kwa waliosoma life skills kutembea haraka ni moja ya vigezo muhimu vya kustaarabika na uchapakazi .Tanzania utamaduni wa kutembea haraka haupo yaani watu wanatembea kama waliochoka ndo maana hata nchi yetu ina sifa ya watu wasiokuwa na furaha kadri ya takwimu kwa sababu ya watu kutembea kama vile wamekula sijui nini,ukitembelea mitaa mingi ya dar hata mwanza watu wanatembea kama hawana kazi za kufanya yaani wengi wanatembea sijui kusharobaro wengine wakinengua hasa mademu halafu tunasema nchi ya uchumi wa kati kufikia 2025 .hebu tazama nchi za wazungu watu wanatembea haraka hata baadhi nchi za Africa kama Kenya na south Africa movement zao zina uharaka tofauti ilivyo bongo.utamaduni wa kutembea haraka unapaswa uwepo kwenye nchi inayotaka kupiga hatua