Watanzania tupaze sauti zetu kunusuru uhai wa maelfu ya vifaranga visivyo na hatia vinavyoenda kuangamia

Tz kuna baadhi ya sheria za hovyo sana,kwenye mambo kama haya huwa namkumbuka sana Jakaya, siku moja wakati wa utawala wake nakumbuka walishawahi kupishana na hayati Magu cha roho mbaya kwenye mambo ya bomoa bomoa.

Jakaya aliuliza,"hivi kwa mfano mkakuta jengo lakihistoria limejengwa kwenye hifadhi ya tanroad hata kama sheria inawataka mlibomoe,nalo mtalibomoa?"

Hii sheria katili kwa wanyama lazima ibadilishwe, hivi kama vifaranga havina maradhi kwanini vichomwe moto?kwanini msipige faini?

Lakini pia serikali ijue tunawachokoza wakenya kuchoma vifaranga badae wakigomea mahindi yetu msisingizie vita yakiuchumi.
 
Haya mambo yatatokea tuu pale ambapo umempa mamlaka mtu
Aliyekulia kwenye njaa,
Mwenye roho mbaya,
Wivu ulioingia mpk kwenye mifupa.
Matumizi ya akili na busara ni nukta.

Unateketeza 40mil kwa kitu halali kwa kigezo cha upatikanaji usio halali?

Oky achana na uhalali au haramu, unashindwa kua na roho hata ya kua huo ni uhai wa kiumbe? Unaongea as if unateketeza misokoto ya bangi?

Huyu mama ana kazi sana, Mijitu yenye roho mbaya imetapakaa kila mahali.
 
Atozwe kodi na faini kwanza alafu TBS nao wampige faini yani kila mamlaka inayomuhusu imlambe fain.
 
Sheria ndio inasema hivyo ?
Sheria za miswada ya hati ya dharula bungeni ni tatizo sana,hii nchi inasheria za hovyo sana kama hujui,kunawatu wamenasa mahabusu miaka mitano sasa kwa amri ya hayati hawapelekwi mahakamani kwakuwa wanajuwa wakipelekwa mahakamani watashinda kesi.

Hizo ndio sheria unazozipigia chapuo.Kuanzia leo unapaswa kujua hii ichi inasheria nyingi sana za hovyo.
 
Matumizi ya nguvu kuliko akili.

Wapime kama vina vimelea vya magonjwa hatarishi, kama havina basi wapige fine (siyo ya kukomoa) halafu wampe akafuge.

1. Hapo serikali itakuwa imeingiza mapato kupitia fine.
2. Chakula cha hao kuku kinaingiza mapato kwa muuzaji na kodi kwa serikali.
3. Dawa na chanjo ni mapato kwa serikali na muuzaji.
4. Watakapouzwa muuzaji atapata kipato na atalipa kodi.
5. Hata muuza chips wa mwisho atajipatia kipato na kulipia indirect tax kupitia manunuzi.
 
Sidhani kama umefikiria kuhusiana na Afya ya watanzania ambayo iko hatarini??

Tutajuaje kama hao wanyama wanafaa kwa matumizi ya binadamu wakati hawajaingizwa kwa kufuata taratibu.

Si umeona Kenya walivyo ban mahindi yetu kwa kigezo cha afya za wananchi wake??

Badala ya kufanyia siasa kila jambo, tumia akili pia.
 
Sidhani kama umefikiria kuhusiana na Afya ya watanzania ambayo iko hatarini??

Tutajuaje kama hao wanyama wanafaa kwa matumizi ya binadamu wakati hawajaingizwa kwa kufuata taratibu.

Si umeona Kenya walivyo ban mahindi yetu kwa kigezo cha afya za wananchi wake??

Badala ya kufanyia siasa kila jambo, tumia akili pia.
Swali mtajuaje jibu lake ni kupima.Na ndio maana hata kwa Covid watu wakiingia wanapimwa kwanza au angalau kupiga marufuku wasiingie na hata wakiingia kwa njia za panya wakikamatwa hawauwawi hao watu watakamatwa watapimwa kwa lazima kwa gharama zao kisha wanafungwa.
Kwa wanyama ni kutokuwatendea haki kabisa sijui hapa Tanzania lile shirika la kutetea haki za wanyama nakumbuka linaitwa TSPCA(Tanzania Society for Prevention of Cruelty to Animals) linasemaje nakumbuka zamani niliona ofisi yao pale karibu na Muhimbili.
Mbona hata askari polisi traffick wanajua hii sheria?.Siku moja nilimpakiza Mbuzi kwenye pikipiki nikawa nimembeba vibaya nikapita tukakutana na Traffick japo ilikuwa kijijini alitusimamisha akatuambia mnamtesa bure huyu mnyama kwa njia hii tumieni njia nyingine nilitii maagizo hayo nikaamua kumswaga na tulifika tunakokwenda.
 
MZUNGU HTA PANYA AUWI HTA AKIKERWA VIPI.! HKU WAMETUKERA MAJIRANI TUU KISA MAHINDI TUNACHOMA VIFARANGA DAH! KAMA KUNA UTARATIBU WA KUVIRUDISHA VIRUDISHWE VIKIWA SALAMA VILIPOTOKA BAS.
 
Huo muda wa kutetea vifaranga nitautoa wap niache kupambana na maisha yangu mzee
 
Tatizo katika hii Dunia mwanadamu anajiamisha yeye yupo katikati ya kila kitu na hivyo kujikabidhi umungu mtu.
Kuna mambo ya ajabu sana wanadamu tunajifanya na yanatia laana kwenye maisha ya jamii pana kwa mfano katika Nchi ya Utahi waliwahi kuchimba shimo na kuangamiza maelfu ya nguruwe kutikana na mlipuko wa ugonjwa ulihusushwa na viumbe hao...mbona sisi leo tunasambaziana UUVIKO-19na tunaendelea na maisha. Unaonaje wanyama nao wangekuwa na utashi ma wao watupige moto?".

" Bina damu ni kiumbe mwenye ukichaa mwingi sana chininya mwamvuli wa utashi na akili".


Life is one but in different forms.....Luna watu tunaabdamwa na karma za ajabu ajabu sana kutokana matendo ya ajabu, tusiliingize Taifa kwenye laana.
....mbona wakimbizi wanaingia Nchini kwa njia haramu tunawakamata na kuwahoji kisha kuwapeleka kwenye Balozi zao au hatua nyingine za kisheria na hatimaye tubawarehesha makwao?...

Narudia tena uhai wetu viumbe wote ni kitu kilekile licha ya kuwa na maumbile tofauti tofauti. Binadamu hayupo katikati ya kila kitu tujaribu kuuona muunganiko wetu na vitu vyote kwenye cosmos.
 
Huo muda wa kutetea vifaranga nitautoa wap niache kupambana na maisha yangu mzee, maisha yalivyo magumu hivi hizo tabia za kizungu sina maisha yamenipa moyo wa kibedui
chukulia ni mtoto wako anachomwa moto utasema mambo ya kizungu? najua utasema mtoto wako ni binadamu ila kumbuka tu hata kifaranga ni kiumbe hai kama mwanao.Najua utasema mbona tunachinja kuku na ngombe jibu ni kwamba mungu alihalalisha tuwatawale lakini sio kuwatesa kwa kuwachoma moto.
 
Hata km vina magonjwa vinapaswa kukabidhiwa kwa madaktari wa mifugo ili vitibiwe.
Mtu akiugua anauliwa? Inasikitisha sana. Afrika mpaka ifike hatua ya maendeleo itachukumia miaka mingi sana. Njia rahisi wanaona ni kuchoma moto.
Ningekuwa kiongozi mkubwa, huyo jamaa ningemfuta kazi maana hana mchango wwte kwenye jamii.
Wawapime na kama hawana magonjwa wapige mnada kama mwenye mali hana hela ya Kodi, tuache kutumia nguvu kila siku wakati tunahitaji pesa. Hii hata tukiwachoma haitusaidii kitu. Halafu najiuliza kuna nini Kenya mbona watu wanapenda mbegu ya vifaranga vya huko?
 
Hata km vina magonjwa vinapaswa kukabidhiwa kwa madaktari wa mifugo ili vitibiwe.
Mtu akiugua anauliwa? Inasikitisha sana. Afrika mpaka ifike hatua ya maendeleo itachukumia miaka mingi sana. Njia rahisi wanaona ni kuchoma moto.
Ningekuwa kiongozi mkubwa, huyo jamaa ningemfuta kazi maana hana mchango wwte kwenye jamii.
Kuna mahali nilifanya kazi kampuni flani hivi boss wetu alikuwa mzungu sasa mlinzi wake siku moja aliingia nyoka boss akiwa hayupo getini kwake yule mlinzi akamuua.Kwa misifa yake akamchukua hakumzika akaona ili apate misifa ngoja amuweke boss akija amuonyeshe huenda atapewa sifa.
Mzungu alivyoonyeshwa alibadilika rangi akawa mwekundu kwa hasira.Akamuuliza mlinzi how many days to reach end of your month nikatafsiri umeulizwa imebaki siku ngapi mwisho wako wa mwezi ufike? .Mzungu akamuambia ok i pay you the whole of your salary inspite of you working only for 10 days for this month.Alivyomlipa hela yake akamuambia tell him to go out of gate i don't like him he cant be cruel to innocent animals snakes deserve to live afterall we have encroached his habitat.Yaani hawezi kuwa mkatili kwa wanyama namna hii kwanza pamoja na hayo ukiona hivyo sisi tumejenga sehemu ambapo ni makazi yake yule jamaa kibarua kiliota majani.
Sasa sisi vifaranga? tunazidi kuitia nchi kwenye mikosi na laana ya mungu vifaranga nawachukulia kwama watoto wachanga duuhhh
 
Kuna watu wanataka kutia doa tena kwenye uongozi huu.... Nyie watumishi wa serikali jifunzeni kutatua changamoto kama hizi kwa akili na sio nguvu...
Hapa mnamaanisha TFDA hawana kazi ya kufanya... au hizo maabara mnazo kwaajili ya kupigia selfie
Au hiyo SUA kazi yake ni nini... Si kuna wataalamu wa mifugo pale.. pelekeni wakachunguzwe Kwanza..
 
Leo katika taarifa ya habari ya ITV saa 08:00pm wametoa taarifa ya mfanya biashara huko Morogoro kukamatwa na mabox 200 yenye vifaranga vyenye thamani ya TZS 40M vilivyoingizwa nchini kinyemela kutoka Kenya.

Mwandishi amemhoji mtaalam husika wa serikali Ni nini kitafuata baada ya ukamataji huu, mtaalam akawa na jibu moja tu "Tutaviteketeza kwa mujibu wa sheria"

Ningekuwa mimi ndio nmeulizwa hilo swali ningejibu "Tutachukua hatua mbalimbali ikiwemo kuvipima kuangalia Kama vimebeba vimelea vya magonjwa then mamlaka husika itaona Ni hatua gani zaidi zichukuliwe baada ya kushauriana.

Hii ni kwa sababu, endapo vitachomwa na ikaja kutthibitika havina magonjwa, kwanza ni kukiuka haki ya ya kuishi kwa viumbe hai, pili kupotezea nchi mapato ambayo yangeweza kupatikana endapo muingizaji angetozwa faini, tatu kupoteza Kodi ya mapato kutoka kwa muingizaji na mwisho wa siku kuua uchumi wa wafanyabiashara.


Kuliko vichomwe Kama itathibitika havina ugonjwa bora vigawiwe bure hata kwenye majeshi yetu kuongeza tija.

Kwa sababu tajwa hapo juu, nawaomba wana jf wote na watanzania kwa ujumla tuungane kwa pamoja kupinga kitendo hichi kisitekelezwa kwa Hawa viumbe hai wenye Tina kubwa kiuchumi.

Roho inaniuma Sana kwa kweli!
Unataka tupate mafua ya ndege.....
wacha viteketezwe kwa speed
 
hao vifaranga ni wa kienyeji ama ni wa kidhungu???

kama jibu ni wa kidhungu basi wateketezwa ila kama ni kinyume chake, basi ni vyema wakabaki hai...
 
Back
Top Bottom