Dsecky
Member
- Dec 11, 2020
- 15
- 19
Binafsi naichukia Kenya kutokana na wivu wao na chuki zao kwetu. Hakuna zuri tutafanya likawapendeza wakenya. Muda mwingi wanatubeza sana watz ktk blog zao mbalimbali. Iwe ni wasanii wetu, maendeleo yetu kiuchumi,siasa zetu,rasilimali zetu hadi vivutio vyetu. Sawa wanatubeza hatujui kiingereza kwa kupima wasanii wetu wa muziki na filamu kitu ambacho sio kipimo halisi kwa maana ukiangalia wasanii wengi hapa nchini sio wasomi, na wengi wao wametoa historia zao kisanaa kuanza baada ya kuacha shule,kufeli kidato au mazingira magumu yaloyopelekea kuacha elimu na kugeukia sanaa. Sawa tumekubali hatujui kiingereza lakn tukikazana na kiswahili chetu na ikitokea filamu au wimbo unaotumia maneno ya Kiswahili ukatamba kimataifa na kuimbwa na mtu mashuhuri wa kimataifa basi haohao wakenya ndio wa kwanza ku claim lugha kuwa ni yao hivyo credit ziende kwao. Not to mention namna wanaovyoutangaza mlima Klm kama wa kwao na kuvutia wageni kutua kwao na kuarrange wageni hao kutembelea mlima kupitia makampuni ya tours ya Kenya. Everything nice and perfect about Tanzania is theirs na wana claim publicly kabisa, ni vingi wanafanya ila kwa hayo machache yanatosha,mengine nitaongeza badae.







