Watalaam wa hesabu naomba msaada

wakurochi

JF-Expert Member
Dec 4, 2017
2,647
2,938
Nataka kupanda miche shimo mpaka shimo mita 2.0 halafu nikipata hiyo miche kwenye mistari ya 2.0 nitatenganishwa kwa upana wa mita 2.5. Nahitaji kujua kwenye ekari moja nitaweka miche mingapi.

Natungiliza shukrani kwa ataketumia kichwa chake.
 
Njia nyingine chukua urefu na mapana ya shamba lako, upana gawanya kwa 2.5m kupata idadi ya mistari/matuta shambani kwako, kisha chukua urefu gawanya kwa 2.0 kupata idadi ya mashimo kwa kila mstari. Sasa zidisha idadi ya mashimo kwenye mstari kwa idadi ya mistari jibu utapata tena miche 800
 
Njia nyingine chukua urefu na mapana ya shamba lako, upana gawanya kwa 2.5m kupata idadi ya mistari/matuta shambani kwako, kisha chukua urefu gawanya kwa 2.0 kupata idadi ya mashimo kwa kila mstari. Sasa zidisha idadi ya mashimo kwenye mstari kwa idadi ya mistari jibu utapata tena miche 800
Kwa kweli wakuu nashukuru sana sana. Hii JF.ni kisima cha maarifa,kidumu,kimejaa watalaam.
 
Itakugomea endapo tu eneo sio ekari moja ya kupima kwa futi au kwa gps, njoo na maelezo zaidi
Mkuu nadhani kanuni uliyotoa namna ya kukokotoa idadi ya miche kwenye eneo husika inajieleza vizuri sana. Maelezo yangu ya ziada ni haya. Kwanza nimetoa mfano wa eneo husika kwa kutumia alama na herufi(rejea chini), pili nimetoa ufafanuzi wa herufi na alama, tatu nimeonyesha namna ya kukokotoa eneo lote na spacing, nne nimetumia kanuni yako kukokotoa idadi ya miche kwenye eneo la mfano na mwisho nimeonyesha ni namna gani idadi ya miche kwenye iliyopatikana kwa kutumia kanuni inatofautiana na idadi ya miche iliyoko kwenye mfano.

Karibu ufuatilie maelezo yangu kwa kina.
-------

o -o -o - o
I - I - I - I
o - o- o - o
I - I - I - I
o -o -o -o
=====
Rejea umbo la mstatiri wa herufi 'I', 'o', na alama '-' hapo juu. Alama '-' inawakilisha 2 m kati ya mche na mche, na 'I' inawakilisha 2.5 m kati ya stari wa miche na mstari mwingine wakati 'o' inawakilisha shimo la mche (mmoja).
Ukijumlisha idadi ya alama '-' kwenye mstari wa kwanza tu unapata alama 3 ambazo zinawakilisha upana wa mstatiri wa 6 m wakati ukijumlisha 'I' kwenye nguzo(column in an above rectangle) ya mstatiri huo hapo juu unapata 2 ambazo zinawakilisha urefu wa mstatiri ambao ni 5 m.

Kwa kanuni zetu za eneo, mstatiri huo una eneo la (upana X urefu)= 5 x 6 = 30 sq-m
Spacing (eneo linalotenga mche na mstari) ni sawa na [nafasi kati ya mche na mche (2 m) X nafasi kati ya mstari na mstari(2.5 m)] = 5 sq-m.
Tumeambiwa shimo lina mche mmoja (1)
Kanuni yako inatuelekeza kuwa Idadi ya miche =(Eneo lote /spacing) x idadi ya miche kwenye shimo.....eqn(i)

Nikiweka takwimu zangu hapo juu kwenye kanuni yako hapo kwenye eqn(i) ninapata kifuatacho:
Idadi ya miche = (30 sq-m / 5 sq-m) X 1 = 6. Napata miche 6. Lakini ukiangalia mstatiri wetu hapo juu utakuta idadi ya miche ni 12.

Kwa maelezo yangu hapo juu, nimekwama namna ya kutumia kanuni yako. Ebu, Mkuu, fafanua zaidi.
 
Nataka kupanda miche shimo mpaka shimo mita 2.0 halafu nikipata hiyo miche kwenye mistari ya 2.0 nitatenganishwa kwa upana wa mita 2.5. Nahitaji kujua kwenye ekari moja nitaweka miche mingapi.

Natungiliza shukrani kwa ataketumia kichwa chake.
Urefu,
Mita 64/Mita 2.0 kwa mstari = Mistari 32

Upana,
Mita 63/ Mita 2.5 kwa mstari = Mistari 25.2 (Aprox 25)

Jumla mashimo 32 ya Urefu x mashimo 25 ya upana
= Mashimo/Miche 800

Altenatively,
Eneo la Heka 1/ eneo la mche mmoja
= 4,046 Sqm / 2x2.5
= 4,046 Sqm / 5sqm
= Mashimo/Mistari 809

NB
Hii 9 imeongezeka sababu hapa hakuna estimation, so tumia ile ya pale juu kwa uhakika zaidi.
 
wakuu napenda kwanza tukumbushane kuwa heka ni ukubwa gani? mi nafahamu heka ni 70 kwa 70, sasa nashangaa hesabu zenu vile zimekaaa yani majibu mlompa huyo sijui yamekaaaje,

ufafanuzi sasa unachukua urefu * upana
70m *70m=4900msqr
2m*2.5m=5msq
4900msq/5msq=980 ndo idadi ya miche au mashimo utakayopiga


Au unachukua urefu wa shamba{70m/2m ambayo ni shimo to shimo} *upana wa shamba{70m/2.5m upana tota shimo to shimo}
jibu litakupeleka kulekule kwa miche 980.

Nakubali kurekebishwa
 
JF kuna watu wana mioyo ya kipekee mno mno !!!!
Ushidwe wewe tu kujituma
 
Mi Mkulima wa Papai jamani napatinana kiluvya gogoni dsm pia nauza Miche ya Papai hybrid f1 bei 2000
0756404226
Ila kwa hesabu mmetishaaaa
 
Back
Top Bottom