Wataalamu wa kodi na payroll, msaada wenu unahitajika

Wataalamu wa kodi na payroll, msaada wenu unahitajika

omoghaka

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
293
Reaction score
167
Ninaomba msaada kwa yeyote anayeelewa anasaidie kuelewa yafuatayo:-

1. Mwajiriwa anastahili kukatwa Kodi yoyote au Michango ya Mfuko wa Jamii wakati was Probation Period?

2. Posho anayolipwa mwajiriwa mfano Extra duty allowance inastahili kukatwa Kodi?

3. Wafanyakazi wanaolipwa kwa Siku na kuondoka, wanatakiwa walipe kodi?

4. Mstaafu aliyepata Mkataba baada ya kulipwa Mafao take, anastahili kuendelea kukatwa mchango wa mifuko ya kijamii mfano NSSF?

Nitashukuru sana kama nitapatiwa majibu ya maswali haya maana yananisumbua sana.
 
Mimi nijibie hiyo namba #2.

Posho hazikatwi kodi.
 
Ninaomba msaada kwa yeyote anayeelewa anasaidie kuelewa yafuatayo:-

1. Mwajiriwa anastahili kukatwa Kodi yoyote au Michango ya Mfuko wa Jamii wakati was Probation Period?

2. Posho anayolipwa mwajiriwa mfano Extra duty allowance inastahili kukatwa Kodi?

3. Wafanyakazi wanaolipwa kwa Siku na kuondoka, wanatakiwa walipe kodi?

4. Mstaafu aliyepata Mkataba baada ya kulipwa Mafao take, anastahili kuendelea kukatwa mchango wa mifuko ya kijamii mfano NSSF?

Nitashukuru sana kama nitapatiwa majibu ya maswali haya maana yananisumbua sana.
1. Anastahili kukatwa
 
1. Anastahili kukatwa kodi na nssf kwa mujibu wa taratibu.
Ila kwa taasisi binafsi mara nyingi hawakati kwani upo kipindi cha majaribio.
2. Zinakatwa

3. Kukatwa au kutokukatwa inategemea mambo yafuatayo.
Mosi, kiasi anacholipwa ,
Pili, kibarua au mkataba,
Inategemea.

Mwisho na 1 na 2 wote watatozwa kodi kwa kuangalia kipato,kama kinakidhi unafyekwa.
 
Kwa mfano zile posho za walimu wakuu, wakuu wa shule na Maafisa elimu kata mbona hazikatwi kodi ilhali zinalipwa na serikali.
Mambo ya serikali usilinganishe na private.
Tra akikutana na taasisi ya serikali ni tofauti akikutana na taasisi binafsi. Fanya uchunguzi.
 
Mambo ya serikali usilinganishe na private.
Tra akikutana na taasisi ya serikali ni tofauti akikutana na taasisi binafsi. Fanya uchunguzi.
Kimsingi hauna hoja(fact) yoyote inayotoa majibu ya wazi kwenye maelezo yako.

Mimi nimejaribu kukupa mfano hai kiasi, lakini pia huku private zipo posho nyingi zinazotolewa na wala sijawahi ona wala kusikia zinakatwa kodi.
 
Nimejaribu kutafuta kifungu cha TRA kinachobainisha makato ya posho kwa private sector na si public sector. Na sababu yao ni nyepesi tu hela inayotoka hazina kuwalipa posho wafanyakaz wa umma haikatwi kodi.

Mimi uzuri nimetumikia pande zote mbili, nilipokuwa government sikuwa nakatwa posho but nilipoingia private wanafyeka kama kawaida kabisa mkuu.. Ni hayo tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kimsingi hauna hoja(fact) yoyote inayotoa majibu ya wazi kwenye maelezo yako.

Mimi nimejaribu kukupa mfano hai kiasi, lakini pia huku private zipo posho nyingi zinazotolewa na wala sijawahi ona wala kusikia zinakatwa kodi.
Pamoja na kuwa sina hoja. Zitaje hizo posho wanazolipwa private.
 
Pamoja na kuwa sina hoja. Zitaje hizo posho wanazolipwa private.
Kwa walimu kuna posho za overtime, mwl wa zamu, posho za madaraka, pango, lunch, usafi Nk

Sector zingine wana posho nyingi overtime, seating allowance za vikao na semina

Hadi madereva wa magari truck wanalipwa mishahara, wanakula milage na posho zingine.

Watu wanalipwa gratuity nk.

Zipo taasisi binafsi zina utaratibu wa posho mzuri sana kuliko hata baadhi ya taasisi za serikali.
 
Nimejaribu kutafuta kifungu cha TRA kinachobainisha makato ya posho kwa private sector na si public sector. Na sababu yao ni nyepesi tu hela inayotoka hazina kuwalipa posho wafanyakaz wa umma haikatwi kodi.

Mimi uzuri nimetumikia pande zote mbili, nilipokuwa government sikuwa nakatwa posho but nilipoingia private wanafyeka kama kawaida kabisa mkuu.. Ni hayo tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nakushukuru kwa kunitoa tongotongo.
Nilikuwa sipo hewani kwa siku mbili kwa sababu za kimawasiliano.
Unaweza kunisaidia kujua kifungu kinachoelezea hizi Posho?
Maana nakutana na changamoto sana kwenye utendaji.
 
Nimejaribu kutafuta kifungu cha TRA kinachobainisha makato ya posho kwa private sector na si public sector. Na sababu yao ni nyepesi tu hela inayotoka hazina kuwalipa posho wafanyakaz wa umma haikatwi kodi.

Mimi uzuri nimetumikia pande zote mbili, nilipokuwa government sikuwa nakatwa posho but nilipoingia private wanafyeka kama kawaida kabisa mkuu.. Ni hayo tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndicho hiki nimeandika hapo juu taasisi binafsi na ya serikali ni tofauti katika treatment.
 
Ndicho hiki nimeandika hapo juu taasisi binafsi na ya serikali ni tofauti katika treatment.
Mkuu,Nisaidie Kifungu kwenye Income Tax,Tax Regulations au sehemu yoyote ili niitumie kama reference.
Naomba sana.
 
Back
Top Bottom