Usitumie nguvu zako bure huyo kashakataliwa ndio maana nyumbani kwake wamechukuwa wapinzani. Eti raisi akienda nyumbani ofisi ya kijiji ni ukawa ataripotije. Alafu kingine huyo ni mchumia tumbo hafai ccm wakimtosa anaenda act-tz
Nyerere aliwahi kumteua Wassira kuwa RC wa Mara... Kwa kutumia wadhifa wake alimwandikia barua GM wa Mutex kumtaka kiwanda kiwaajiri watu wa Mara pekee!!! GM alikasirika sana kiasi cha kupeleka ile barua kwa JKN! ... JKN alimwita wassira Butiama! Katika Mazungumzo Wassira alijikojolea baada ya kugundua kuwa Barua yake ilimfikia JKN aliekuwa anapinga Ukabila kwa nguvu zote... Baada ya hapo, wassira alipotezewa hadi Rostam alipompa fedha kwaajili ya Kampeni ya JK 2005 ... Huyu Mkabila, Mdini na Mkanda Gaidi mwenye kuabudu nguvu dhidi ya wapinzani Hastahili kamwe kuongoza hata Tarafa ndani ya nchi yetu ... Kama mnampenda sana Mpelekeni akawe msimamizi wa Mapori ya Gombe ...
Wassira amekuwa mtetezi wa Wakulima, anaamini Uchumi unajengwa kwa kuimarisha Viwanda na anaamini Wakulima kama Tabaka kubwa wanatakiwa waunganishwe kwa Kilimo Cha Kisasa na soko la uhakika, Viwanda na kuboresha Viwanda vtasaidia sekta za Serikali na Binafsi kukuza Mitaji na kutoa Suluhu la Ajira kwa Vijana.
HATABIRIKI:
Wasira hajajipambanua yeye anaamini katika njia zipi za uchumi. Japo hili ni tatizo la karibu watu wote ambao wameonesha nia ya kuutaka Urais mwaka 2015. Tupo kwenye ulimwengu wa gesi na Tanzania kuna ugunduzi mkubwa umeshafanyika, ni vizuri tukajua au kuhisi kuwa Rais mtarajiwa ana makusudio yapi.
Kuna kasoro kubwa sana hapa! Wanasiasa wengi hawana hulka ya kuandika, kwa hiyo inakuwa vigumu kupata mawazo yao ya namna wanavyoutazama uchumi wa nchi, tafsiri na majibu yao. Mawaziri wengi kwa vile wao wana wizara zao, jukumu la uchumi na bajeti ya nchi, humwachia Waziri wa Fedha.
Jukumu la gesi asilia, linaachwa kwa Waziri wa Nishati na Madini. Kwa maana hiyo, ni vigumu kumtabiri Wasira na mbinu zake za kuujenga uchumi wa nchi kwa sababu hajawahi kuyapambanua mawazo yake japo kwa maandishi. Kwa hapa japo ni msomi wa uchumi, ila hatabiriki.
Kilimo ndiyo uti wa mgongo wa taifa hili. Ni wakati mwafaka wa kuwa na viwanda vingi, vilivyokufa vifufuliwe, mchezo wa kuuza malighafi ufe, serikali iwajengee uwezo wananchi na kuwawezesha kuuza bidhaa zilizopita kiwandani badala ya mazao. Hapa pia hatabiriki.
By Luqman Maloto
Na arudishe haraka kabla mwenyewe hajasoma andiko lake maana kuna mengine yatamkumbusha machungu, baada ya kushinda ubunge mwaka 1995 kwa ticket ya NCCR- Mageuzi alipingwa mahakamani akavuliwa ubunge na kupigwa marufuku asigombee ubunge kwa kipindi cha miaka mitano hivyo kipindi chote cha awamu ya tatu, 1995-2005 hakuwa mbunge wala hakuwa katika utumishi wa umma alikuwa mwambao wa ziwa victoria akivua sangara, hivyo mheshimiwa mpambe uwe mwangalifu na upambe wako kuna watu wanaoijua historia yake kuliko wewe; na awamu ya JK ndiyo iliyomrudisha serikalini mwaka 2006 alipoteuliwa kuwa waziri, usimpambe kihivyo mchango wake kwenye taifa ni wa kawaida kabisa hauna uzoefu mkubwa kuwazidi Sitta, Lowassa, Lukuvi na hata mama Nagu.Rockspider umetumwa wewe rudisha bahasha ya watu, haya mutex sasa umetoa wapi??? Unazusha uongo hadi unaonekana mwehu.
wapendwa msipoamini maneno yangu hata neno la mungu basi mtakuwa hamuamini kwa kifupi ni kwamba akili za kuambiwa changanya na zako.. mzee wasira ndiye anayeandaliwa kumrithi kiwete na ukijaribu kuchunguza kwa umakini utaona kuwa mh wasira amekuwa chachu kubwa kwa prof kikwete kiasi kwamba hata kwenye maadhimisho ya CCM mkoani ruvuma bado alisema kuwa chagueni kiongozi asiyetiliwa shaka nikiamini kuwa wasira hatiliwi shaka hata kidogo na kikubwa zaidi ni kidogo kwani amekuwa ni mmoja wa viongozi wenye mfano wa uadilufu... Wasira ndiye rais wengine mnajisumbua
for sure iwill fight till death for wssira kwakweli ukiacha hoja za kishabiki wasira ni kiongozi mzuri na muadilifu wewe unayezungumzia sura bado huna uchungu na taifa hili
Kafanye kampeni zako Gombe