Kama lipo la KUSEMA
View attachment 225722lisemwe kwa sababu wanazozijua wao. Ni wazi kwamba wagombea wote watakaojitokeza kuomba nafasi hiyo ya juu zaidi watakuwa na mapungufu yao kama binadamu lakini kama Taifa linalohitaji kujikomboa kiuchumi, kijamii na kisiasa; ni vema tuwaepuke wote wenye sifa hizi ambazo kwa maoni yangu zinazidi kiwango cha mapungufu ya kibinadamu;
1. Wala rushwa: Hawa watahalalisha rushwa ili waweze kufaidi keki ya nchi yetu wao, marafiki zao, wapambe wao na familia zao. Nchi itazidi kudidimia katika lindi la umaskini. Kama wao watafanya madudu huko juu, walio chini pia wataiga. Wanyonge na maskini watazidi kutokomea kwenye tope hilo.
2. Mafisadi/ watuhumiwa wa ufisadi: Hawa wataifisadi nchi na wote waliomo. Namaanisha nchi itazidi kuuzwa na vyote vilivyomo ikiwa ni pamoja na wananchi. Wataingia kwenye mikataba ya kifisadi ili mradi wao wananufaika binafsi. Hapa tutashuhudia maandamano kila kona ya nchi. si wanachuo, Madaktari, walimu, bodaboda nk.
3. Wanaotumia udini na ukabila: Hawa wanaweza kusababisha machafuko nchini.
4. Wanafiki/ Wasanii: wazuri wa kuongea na kupanga mikakati mitamu na mizuri kusikia lakini ndani yake usanii mtupuu.
#WANYONGE WAMEPATA MTETEZI
#2015
#WASIRA MTETEZI WAO